ISTILAHI ZA USHAIRI

Emmanuel Lee
By -
0
JABA PLANET. USHAIRI

2.Istilahi za Ushairi

¶ Istilahi ni maneno yanayotumiwa katika uwanja fulani maalumu;

MASHAIRI YA ARUDHI_ni yale ambayo hutungwa kwa kufuata sheria, kanuni au kaida za utunzi
*ARUDHI_ni sheria au kanuni za kimapokeo, jadi au kiutamaduni zinazoongoza utunzi wa mashairi. Arudhi za mashairi ni kama vile uzingatiaji wa vina, idadi fulani ya mishororo, vipande na kadhalika.

MASHAIRI HURU_ni mashairi ambayo hayazingatii arudhi za kiutunzi ; hukiuka Arudhi au kaida za utunzi wa mashairi na walah hayajifungi kwenye mtindo fulani maalumu wa uandishi.

FALSAFA YA MWANDISHI_ni msimamo wa mshairi kuhusu suala linalorejelewa katika shairi.
Ni maoni yake kuhusu jambo fulani.

VINA_ni silabi za mwisho katika Kila kipande cha ubeti.

MSHORORO_ni mstari katika ubeti.

MIZANI_ni jumla ya silabi katika kila mshororo wa ubeti

UBETI_ni kifungu cha mishororo kadha

VIPANDE_ni sehemu ya mshororo iliyogawanyika aghalabu kwa koma(,).

UKWAPI_ni kipande cha kwanza cha mshororo.

UTAO_ni kipande cha pili cha mshororo.

MWANDAMIZI_ni kipande cha tatu cha mshororo.

UKINGO_ni kipande cha nne cha mshororo.

MWANZO_ni mshororo wa kwanza katika ubeti.

MLOTO_ni mshororo wa pili katika ubeti.

MLEO_mshororo wa tatu katika ubeti.

KITUO/KIISHIO/KIMALIZIO_ni mshororo wa mwisho katika ubeti.

KIBWAGIZO_ni mshororo wa mwisho katika ubeti unaorudiwarudiwa katika kila ubeti pia huitwa kikara au kikomo.

SABILIA_shairi ambalo halina kibwagizo.

KIANGIKO_ni mshororo wa kwanza unaorudiwarudiwa.

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)