SIRI YA MUUAJI EPISODE 1

Emmanuel Lee
By -
0
JABA PLANET.

SIRI YA MUUAJI EPISODE  1

NA.

K-FANI J.RUMAMBO.

Kwenye kituo cha polisi cha nchi ya china kulionekana waandishi wa habari wa kila aina ya televisheni huku wakijitahidi kutaka kuingia ndani ya kituo cha polisi ili kupata picha ikiwezekana na video pia kuhusu kukamatwa kwa muuaji hatari sana aliyekuwa anasumbua serikali ya china na dunia kiujumla kutokana na matukio yake aliyokuwa anayafanya kwenye kila nchi atakayoenda. Walipata vikwazo kutoka kwa maaskari wa kituo kikuu cha shanghai, waliokuwa wanawazuia kutoingia ndani kwa usalama wa mtuhumiwa kwani. Walijua kutakuwa na watu wanaoshirikiana na muuaji huyo. Wanaweza kumuua ili kuondoa ushahidi na kuepuka kutojulikana maficho yao.

Ndani ya chumba cha mahojiano, alionekana kijana mmoja mwenye asili ya kiafrika akiwa kafungwa kwenye kiti na kamba ngumu ili kumzuia kutojinasua kama atataka kufanya hivyo. Kijana yule aliyekuwa kapoteza fahamu kutokana na kupigwa sana, haikujulikana ni kipi hasa kilichomfanya kuwa pale na kwanini taarifa zake za kukamatwa zimesambaa kama mvua... Akiwa hana ufahamu wa kujua sehemu alipo, mlango wa kuingilia ndani ya chumba cha mahojiano. Ulifunguliwa na maafisa wa C.I.A.  wapatao watatu waliingia ndani wakiongozana na maaskari kutoka katika jeshi la nchi ya china.

 

''Mfungueni hapo na mmpeleke kwenye gari. Atatakiwa kuhukumiwa kwenye nchi ya marekani huyu''. Afisa mmoja wa C.I.A  alitoa agizo na maaskari wawili wa china wakishirikiana na wale wa C.I.A. Walimfuata yule kijana ambaye mpaka sasa bado haijafahamika ni kwanini yupo pale. Walimfungua mtuhumiwa kwenye kiti na kumbeba kwa kusaidizana, mmoja alimshika na kupitisha mkono wake wa kushoto kwenye bega la kulia la mtuhumiwa..... Na yule mwingine akapitisha mkono wake kwenye bega la kushoto la mtuhumiwa na kuanza kumtoa nnje huku nyuma wengine wakiwasindikiza kwa silaha kama ulinzi.

Kutokana na kutokuwa na fahamu, ilimfanya yule kijana mwenye asili ya kiafrika kushindwa kufanya jambo la kujitetea na kukubali kubebwa msobemsobe kama gunia la taka, walitumia njia za chini kwa chini kumsafirisha mtuhumiwa wakihofia kupita njia za juu kwaajili ya usalama zaidi, njia za chini ziliwaraisishia kufika mpaka kwenye uwanja wa ndege wa nchi ya china ambapo walimpakiza mtuhumiwa kwenye ndege tayari kwa safari.

 

''Agent Gibson, nadhani biashara baina ya nchi yako na yangu itakuwa imeishia hapa. Mtuhumiwa wenu ndio huyo hapo na sisi kuanzia sasa tutakuwa hatuhusiki kwa chochote kile kinachohusiana na huyu mtu.''. Kamanda wa jeshi la polisi nchini china. Kamishna Wuen Lee, alizungumza hayo baada ya kuwafikisha maafisa usalama kutoka kwenye kitengo maalumu cha C.I.A kwenye uwanja wa ndege wa nchi ya china na kuongea juu ya nchi yao kujiangua kwenye suala la muuaji yule aliyetakiwa akahukumiwe kwenye nchi yake ya marekani.

 

''Ahsante sana. Wuen Lee. Hakika wewe pamoja na nchi yako ni marafiki wema sana, msaada mliotupatia unatosha sana na.... Mpaka hapa tulipofika tunaweza kusema asanteni! Sana.''. Agent Gibson alizungumza hayo na kupeana mikono kama ishara ya kushukuru kwa kile walichofanyiwa na nchi ya china.

Baada ya makabidhiano ya mtuhumiwa na kuweka sign nyaraka kadhaa. Maagent kutoka kwenye kituo kinachojishughulisha na maswala ya kiupelelezi. C.I.A,walipanda kwenye ndege yao binafsi na kuiacha ardhi ya china.

 

Ndani ya ndege kijana yule mwenye asili ya kiafrika au unaweza kumuita mmarekani mweusi, alikuwa kafungwa kwenye cage maalumu yenye nondo imara ili kutompa moyo wala mawazo kama anaweza kujinasua kwenye mikono ya maagent wale. Taratiibu kijana yule akiwa ndani ya cage ambayo mara nyingi hutumika kuhifadhia au kubebea wanyama kama, chui,simba na wengineo.

Fahamu zilimrejea na kuanza kuona nuru iliyohafifu kwenye macho yake yaliyovimba kwa damu kuvilia ndani yake.

Alitikisa kichwa kulia na kushoto huku akilazimisha kufumbua macho yake ili ajue yupo wapi.... Lakini ilishindikana kutokana na maumivu kumzidi na kujikuta tena anapoteza fahamu akiwa ndani ya cage, baada ya safari ndefu...... Hatimae ndege binafsi yenye nembo ya shirika la kijasusi la C.I.A. Iliweza kuwasili nnje ya jengo kubwa la shirika hilo ambapo baada tu. Yakutua juu ya ardhi, maaskari waliizunguka ndege hiyo wakiwa wameshika mitutu iliyotayari kwa lolote lile. Kitanda maalumu cha kubebea wagonjwa. Alimaarufu kama machela, kililetwa na mtuhumiwa akalazwa juu yake ili kumuwahisha kwanza hospital kwaajili ya kuokoa maisha yake. Maana hali ya kiafya kwa upande wake haikuwa nzuri sana kutokana na kupigwa sana.

Matibabu ya awali yalianza huku wauguzi wakipewa tahadhari juu ya uzima wa kijana yule aliyeonekana ni wamuhimu sana kwenye mikono ya maafisa wale wa C.I.A.

 

Taarifa za kijana yule kukamatwa nchini china na kurudishwa kwenye nchi yake ya marekani. Ziliweza kuwafikia kikundi kimoja hatari sana kilichokuwa kinamtafuta kijana huyo kwa udi na uvumba.

Kikundi cha kigaidi cha the brothers kinachomilikiwa na mwanamama mmoja tajiri sana, kilikuwa kinamtafuta kijana huyo kwasababu zao binafsi ambazo wanazijua wao na kijana yule.

Madam's Aretha Franklin ndio mmiliki wa kundi la the brother's, kundi lenye kuhusika na wizi na unyang'anyi wa vito vya thamani.

 

''Vijana. Nadhani taarifa juu ya aliyekuwa ndugu yetu ila kwasasa ni adui namba moja kwetu. Juu ya kukamatwa kwake zimewafikia... Huu ndio mda wa kumrejesha nyumbani ili aje kuhumiwa huku maana tulishakula kiapo kwamba tutazikwa sehemu moja, anatakiwa apatikane akiwa hai maana kuna nyaraka muhimu sana anazo na zinatakiwa na boss. Hivyo jiandaeni ili jioni twende tukamchukue kwenye hospital ya ST.MARCIA HOSPITAL.''. Miongoni mwa mwanachama wa the brother's aliongea akiwa juu ya jukwaa kuwaambia vijana au wanajeshi wa the brother's waliokuwa wamesimama kwa kupanga mstari kama wapo kwenye gwaride wakimsikiliza kamanda wao.

Baada ya kutangaziwa taarifa ile. Kila kijana wa kundi la the brothers alijiandaa na kujiweka sawa kwaajili ya kazi moja tu. Iliyopo mbele yao ya kumkamata mwanakikundi mwenzao aliyeasi na kujitafutia uhuru wake,

 

''Nadhani hii ndio nafasi ya kipekee ya mimi kuonesha ubora wangu, ALEXIS huu ndio mda wako wa kufa maana unajiona bora kushinda Mimi.''. Kijana aliyetambulika kwa jina la LUCAS. Aliongea mwenyewe akiwa kwenye chumba chake  cha kubadirishia mavazi na kuchana picha yake aliyopiga enzii hizo wakiwa watoto na ALEXIS.

Mdaa ulipofika. Vijana wapatao ishirini walipanda gari ya ambulance kama vile wauguzi wanaoenda kumchukua mgonjwa sehemu na kuingia barabarani kwaajili ya kufika kwenye hospital ya ST.MARCIA HOSPITAL anapotibiwa kijana mwenzao aliyekimbia kikosi.

 

''Kumbukeni tunaeenda kumfuata ni zaidi ya hatari, kila mmoja wetu hapa anautambua uwezo wake wa kutumia silaha pia wa kupigana jinsi ulivyo.... Umakini unahitajika sana maana ni kiumbe mwenye kila aina ya mbinu za kujinasua kwenye mikono hatari, inastaajabisha kukamatwa kizembe na maaskari tena wa shanghai ambao uwezo wao ni robo ya uwezo wake.''. Kiongozi wa msafara akiwa mbele kwenye kiti cha kushoto, aligeuka nyuma na kuwaangalia vijana wake waliokuwa wamekaa nyuma kabisa huku wakiwa wamevalia mavazi ya kitabibu. Aliongea na kurudisha kichwa chake mbele baada ya kuona vijana wake wamemuelewa kwa kile alichokiongea.

******

Upande wa kijana ALEXIS akiwa hospital. Alikuwa kashamalizwa kufanyiwa huduma ya kwanza na hapo alipo alikuwa juu ya kitanda akiwa kalazwa juu huku madripu ya maji na damu yakiwa yamening'inia juu.

Akiwa kwenye usingizi wa kifo kijana ALEXIS... Alitokewa na watu wawili wakiwa kwenye mavazi meupe huku kwenye nyuso zao wakiwa wamepambwa kwa tabasamu lenye kusindikizwa kwa michirizi ya machozi kutoka kwenye macho yao.

 

''Mama!!! Babaa.''. ALEXIS alijikuta anawaita wale watu baada ya kuwafahamu ni wakina nani.

 

''Ni mda wa kuamka na kupambana na maumivu maana maadui wapo mbele yako kijana wangu. Unatakiwa kuyashinda maumivu ili uipiganie ile haki iliyopotea kwaajili ya faida za watu, wewe ni shujaa usiyeshindwa na kitu...... Amka uendeleze pale nilipopaacha. Amkaaaa ALEXIS... Amkaaaaaaa!!!!''".

 

''Babaaaaaaaaaaaa!!!!!!!'' Kijana ALEXIS alijikuta anaamka kutoka kwenye usingizi wa kifo na kupiga ukunga kumuita baba ake ambaye alimtokea ndotoni akiwa na mama ake.

Alishtuka na kujaribu kuinyanyua mikono yake ili aweze kushika kichwa chake alichohisi kinamuuma. Lakini alishindwa kufanya hivyo baada ya mikono kugoma kunyanyuka yote na kunyanyuka mmoja tu... Alizungusha shingo yake kulia kwenye mkono ulioshindwa kunyanyuka, alishangaa baada ya kuona kafungwa pingu kwenye chuma cha kitanda.

Akiwa bado anajiuliza na kukumbuka tukio la mwisho lilomfanya kuwa pale , mara ghafla kwa mbali alianza kusikia sauti za viatu vikitembea kuelekea upande kilipo chumba chake. Alijitupa kwenye kitanda na kukaa kama alivyokuwa mwanzo, hatua zilizokuwa zinasikika kwenye masikio ya kijana ALEXIS, ziliweza kufika tamati kwenye mlango wa chumba alichohifadhiwa.

Hawakuwa watu wabaya wala wazuri kwa upande wa kijana ALEXIS maana kwenye maisha yake kila mtu ni mbaya. Walikuwa ni wale maafisa usalama kutoka kwenye kitengo cha kipelelezi C.I.A wakiwa na mganga mkuu aliyehusika kumfanyia matibabu ALEXIS, waliingia mpaka ndani ya chumba na kumkuta ALEXIS akiwa kalala kana kwamba hajapata fahamu kumbe alikuwa kashazinduka mda sana ila aliamua kufanya vile kuwaaminisha madaktari kwamba yeye bado hajazinduka.

 

Mganga mkuu alipofika kwenye kitanda alicholala ALEXIS. Alianza kumpima mapigo yake ya moyo kisha akahamia kuchomoa dripu zilizokuwa zimeisha na  kuita manesi waje kubadirisha dripu kwa mgonjwa, yote hayo yakiwa yanaendelea ALEXIS alikuwa anasikilia kinachozungumzwa baina ya mganga mkuu na maafisa wa C.I.A lakini alishindwa kuona kinachoendelea kutokana na kujifanya kama hana fahamu hivyo aliishia kusikia sauti tu. Bila kuwaona wahusika wa zile sauti

''Hali ya mgonjwa ndo kama mnavyoiona.. Tumefanikisha kutoa risasi iliyokuwa kwenye mwili wake baada ya masaa mawili anaweza kupata fahamu.''. Mganga mkuu alizungumza baada ya kumpima ALEXIS na kuona maendeleo yake. Aliwaambia maafisa wa C.I.A waliokuwa wamesimama pembeni ya kitanda alicholala ALEXIS wakimuangalia kijana huyo ambae kwa macho yao na maelezo ya mganga mkuu.. Waliamini kijana huyo atapata fahamu zake baada ya masaa yapatayo  mawili bila kujua kama mwenzao alishapata fahamu zake muda sio mrefu kabla ya wao kuingia.

Baada ya kukaa kwa kitambo kidogo kwenye chumba alicholazwa ALEXIS, walitoka nnje ili kupisha manesi walioingia kumbadirisha dripu kijana huyo. Waifanye kazi yao.

Agent GIBSON alikuwa wa mwisho kutoka kwenye kile chumba, wakati akiwa anapishana na manesi wawili waliokuwa wanaingia mle na kimkokoteni chenye dripu na mashuka... Kuna nesi mmoja aliyekuwa anasukuma kile kimkokoteni, alimtilia mashaka baada ya kukutanisha mboni za macho yao.

Lakini alipotezea na kutoka nnje walipo wenzake wawili.

 

''Ulinzi unahitajika sana hapa. Nina mashaka na usalama uliopo hapa, hakikisheni haingii mtu wala kukatiza maeneo haya bila ridhaa yangu... Nahisi kuna watu wamejipandikiza humu na lengo lao sio zuri.'' Agent GIBSON aliwaachia maagizo maaskari wake na yeye akashika njia ya kutokea nnje. Alifika nnje na kuwapa ishara vijana wake wasogee upande alipo.

Vijana walijisogeza kwaajili ya kumsikiliza mkubwa wao ni kipi anachotaka kuwaambia.

 

''Nahitaji umakini maeneo haya maana hatupo wenyewe kwenye hii hospitali... Hakikisha hakuna mtu anaeweza kuingia ndani bila ruksa, mtu yeyote mnaemwona haeleweki ruksa kumpiga risasi. Natoka mara moja kuna kitu naenda kufuatilia..''. Agent GIBSON alitoa maagizo kwa vijana wake na kuingia kwenye gari yake iliyoondoshwa kwa kasi maeneo ya hospital baada ya kuwashwa na kutii amri ya dereva.

Vijana walijigawa kwa makundi kama walivyopewa maagizo na mkubwa wao wa kazi... Wakati wao wakiwa wanapeana majukumu ya kulinda, kwenye ghorofa ya pembeni iliyoumbali wa kilomita zipatazo hamsini. Kuna mtu alikuwa anawaangilia kwa kutumia kifaa chake alimaarufu kama. Miwani ya shetani ambayo ni darubini zenye uwezo wa kuangalia kwenye giza nene na mtumiaji akaona vizuri sana kama aonavyo mchana.

Yule mtu akiwa kasimama juu kabisa ya ghorofa ile yenye rufu zipatazo ishirini kwenda juu, alipeleka mkono wake wa kulia uliokuwa ndani ya gropsi iliyokatwa kwenye vidole na kuacha uwazi upande wa vidole huku juu ya kiganja kukiwa na nembo ya fuvu lenye bunduki zikiwa zimejiweka kwa mtindo wa x.. Alipeleka juu ya sikio na kubonyeza kitu kilichokuwa ndani ya sikio lake mfano wa earphone zinazotumikaga mara nyingi kusikilizia mziki  kisha akaurudisha mkono wake kwenye miwani ya shetani...

 

''Huku nnje naona sio salama kwa kumpitisha... Naona hawa wapuuzi wa C.I.A wametapakaa kila sehemu... Embu ngoja kwanza naona kuna gari ya wagonjwa inaingia hapa....... Ooooh shit. MONA LISA fanya haraka kidogo naona the brothers na wao wameingia hapa na itakuwa ni hatari kama watakukuta ndani..'' Baada ya kubonyeza kile kitu mfano wa earphone, kijana yule alizungumza kumwambia mtu aliyemwita kwa jina la MONA LISSA afanye haraka baada ya kuona gari ya ambulance ikiingia kwenye hospital ile na alipofuta taswira kwenye darubini yake. Aliwaona na kuwatambua waliokuwa kwenye gari ile ya kubebea wagonjwa ni wakina nani.

Upande wa ndani kwenye chumba alicholazwa kijana ALEXIS... Wale manesi wawili walikuwa wanamfanyia mabadirisho ALEXIS lakini mmoja wapo alipokea simu kutoka mahala, punde tu. Baada ya kupokea simu hiyo, alionekana kuchanganyikiwa mpaka mwenzake akashangaa.

 

''The brothers wanakujaa.''. Yule nesi aliyepokea simu bila shaka huyu ndie MONA LISA yule aliyepigiwa simu na yule kijana wa nnje aliyekaa juu ya ghorofa iliyo jirani na hospital ya ST.MARICIA HOSPITAL.

Kitendo cha kutamka kwamba the brothers wanakuja... Kilimfanya hata kijana ALEXIS kushtuka na kunyanyuka kutoka kwenye igizo lake la kutopata fahamu, lakini alijikuta anarudi tena kwenye kitanda baada ya kitu chenye ncha kali kikiwa cha baridi kupita kwenye mishipa yake ya mikono huku baada kitu hicho kupita kwenye mishipa yake ya mikono... Ikafuatiwa na vitu vya baridi kupenya kwenye mishipa yake ya damu na kuanza kusambaa kwa kasi.

ALEXIS alijaribu kukaza mishipa yake ili kitu alichochomwa kisiendelee kuingia ndani zaidi ya mwili wake.. Alishindwa kuizuia dawa iliyokuwa inasafiri kwenye mwili wake kwa kasi kubwa huku kila sehemu ya mwili ikikosa nguvu baada ya dawa hiyo kupita, alijikuta anaanza kuweweseka kama mgonjwa mwenye degedege huku mapovu yakimtoka mdomoni.

 

''Msaada jamani... Anakufaaaaa.''. MONA LISA baada ya kuona  mwenzake kashamchoma sindano itakayomfanya ALEXIS kulala......  Alipiga kelele ili wale walinzi waliokuwa nnje ya wodi aliyolazwa kijana ALEXIS waweze kuja ili adhma yao ya kumtoa ALEXIS itimie.

Maafisa wa C.I.A wawili walioachwa kama ulinzi kwenye chumba alichomo ALEXIS... Waliposikia sauti za nesi akiomba msaada, bila kupoteza mda waliingia ndani kichwa kichwa.. C.I.A wa mbele aliyetangulia, alikutana na teke la shingo lilompeleka chini na kupoteza fahamu kwani mpigaji wa teke lile alikuwa mtaalamu na anazifahamu vyema sehemu ambazo akikupiga lazima upoteze fahamu... Yule mwingine nae katika harakati za kushtuka ni kitu gani kilichomfanya mwenzake kuanguka kama mzigo, alijikuta na yeye anapigwa na vidole laini katikati ya mfereji wa uti wa mgongo na kupoteza nae fahamu.

Baada ya mwili wake kuanguka, nyuma alionekana yule nesi aliyekuja na MONA LISA akiwa kanyoosha mkono wake wa kulia huku mbele akiwa kanyoosha vidole viwili kuonesha ndie aliyefanya tukio lile kwenye mwili wa afisa yule aliyekuwa kageuka upande alipo MONA LISA aliyempiga teke la shingo yule afisa mwingine aliyekuwa wa kwanza kuingia ndani kutaka kujua kunanii lakini alizimishwa baada ya MONA LISA kuzunguka  kwa nyuma na  kuachia teke la nyuma lilompata vyema yule afisa huku kisigino cha kiatu alichovaa kikifanya kazi ya kugusa sehemu yenye mshipa mkubwa wa fahamu.

Waliingiza ndani ya chumba wale maafisa na kufunga mlango ili isijulikane kama kuna tukio limetokea, walimchukua kijana ALEXIS aliyekuwa katepweta kutokana na kuchomwa na sindano yenye dawa za usingizi ndani yake... Nesi yule aliyekuja na MONA LISA alimbeba kijana ALEXIS huku MONA LISA yeye akiwa nyuma kwaajili ya ulinzi.

Kijana ALEXIS akiwa kwenye usingizi wa nusu kaputi, alianza kukumbuka mambo kadhaa yaliyotokea nyuma.

 

 

‘’Wewe ni nani.?’’ 

 

‘’Mimi ni muaaji.’’ 

 

‘’Wewe ni nani.?’’ 

 

‘’Mimi ni muuaji’’ 

 

 

‘’Sheria na kanuni za muuaji ni ninii.?’’ 

 

 

‘’Kuua bila kuacha ushahidi,’’.  

 

‘’Sheria na kanuni za muuaji ni nini.?''

 

’Kuua bila kuacha ushahidi,’’ 

 

 

‘’Msaliti yoyote atakejitokeza, adhabu yake nini.?’’ 

 

 

‘’Kuuwawa’’ 

 

 

‘’Sijasikia. Msaliti yoyote atakaejitokeza adhabu yake ni nini.?’’ 

 

‘’Kuuwawa’’ 

 

‘’Sisi ni..?’’ 

 

‘’Familia moja’’ 

 

‘’Sisi ni..?’’ 

 

‘’Familia moja’’ 

 

‘’Kutengana kwetu..?’’ 

 

‘’Mwiko mpaka tunakufa’’ 

 

‘’Kila mmoja aweke akilini, hakuna uhuru kwenye hii dunia ila uhuru uliopo kwenye dunia ya sasa ni 

kuua ili uwe huru na maumivu kwenu mwiko, inatakiwa maumivu yawaogope na sio nyinyi myaogope 

na kudhihirisha kwamba sisi ni familia moja, kila mmoja wetu atapita hapa na kuwekwa tatoo mbili 

kiashirio cha sisi ni ndugu na ndugu milele hawatengani na ikitokea mmoja wetu kajitenga na sisi. 

Basi hukumu yake kifo, kwenye familia yetu hatuhitaji mtu mlegevu. Familia yetu hakuna mtu 

anaeshindwa’’ 

Yalikuwa ni moja ya matukio mengi anayoyakumbuka kijana ALEXIS akiwa kabebwa juu ya mgongo... Alizidi kukumbuka mambo kadha wa kadha yaliyopita...

 

''Nakufundisha hivi kwaajili ya maisha yako ya baadae na ulinzi kwenye maisha yako... Najua kwasasa utachukulia kama nakutesa ila  baadae utajua umuhimu wa haya mazoezi. Haya ingiza mikono yako kwenye huo mchanga na upige vidole ndani yake huku ukivizungusha kama unakoroga maji au kukanda ngano...''

 

''Lakini mwalimu kwanini mazoezi haya unanipa mimi tu. Wenzangu huwapii...?''

 

''Utajua mbele  utakapokua mtu mzima na ukajua maana ya neno Uhuru.''.

Ni matukio ya nyuma kipindi angali mdogo.... Aliyakumbuka yote akiwa kwenye usingizi mzito...

 

 MONA LISA akiwa na mwenzie wakiwa wamembeba kijana ALEXIS... Walipita njia za chini kwenye maji na uchafu wote unaotupwa na hospital ile maana juu kulikuwa hakupitiki jinsi ulinzi ulivyokuwa mkubwa na kikundi cha the brothers kilikuwa kimewasili nnje ya hospital kikitaka kuingia ndani kwa kigezo cha kumleta mgonjwa.

 

''DENNY tupo underground way... Tukukute kwenye mataa.''. MONA LISA aliongea kupitia simu maalumu iliyokuwa imepita kwenye sikio lake la kulia na kuonekana kama earphone

''Usijali... Dakika kumi nitakuwa eneo husika.'' DENNY ambae ndio yule kijana aliyopo juu ya ghorofa lililopo karibu na hospital ya ST. MARCIA HOSPITAL.... Alizungumza hivyo baada ya kupokea simu kutoka kwa MONA LISA...aliinama chini na kuirudisha silaha yake yenye uwezo wa kulenga masafa marefu ndani ya begi lake...

Baada ya kufanya hivyo, alinyoosha mkono wake na kubofya namba kadhaa kwenye saa aliyokuwa ameivaa mkononi, kuanzia mwanzo wa kiganja mpaka yalipo makutano ya mkono na kuonekana kama mtu aliyefungwa bandeji au kitambaa... Baada ya kubofya zile namba kwenye kioo cha saa, alivaa begi lake mgongoni na kuliweka sawa kisha akageuka upande wa pili wa lile ghorofa na kuanza kukimbia kuelekea ukingoni mwa lile ghorofa, alikimbia kwa spidi kama yupo ardhini na alipofika kwenye engo za mwisho wa lile ghorofa... Aliibana miguu yake na kudunda kwenye ncha za kuta na kujirusha juu kama samaki aingiavyo kwenye maji, akiwa juu alijibetua na kutanguliza kichwa chini huku miguu akiiacha juu tena ikiwa kaibana vilevile kama alivyoruka.

Lau kama ungebahatika kumuona jinsi alivyokuwa anashuka kutoka kule juu ya ghorofa, ungeweza kusema na kumfananisha na spider man au super man kama sio batman jinsi alivyokuwa anashuka kwa spidi kama ya roketi huku akiwa hana parachuti lenye uwezo wa kumsaidia asije kutua chini vibaya.

Macho ya DENNY mara kwa mara yalikuwa yanaangalia saa iliyokuwa inatoa sauti kama za alarm ikiwa inalia, alifika mpaka katikati ya ghorofa na kubakiza rufu kadhaa tu. Afike chini,, aliangalia tena saa yake na kutabasamu kisha akajibetua kwa kichwa chake kuangalia juu na ule mkono wenye saa akiunyoosha juu.... Kuna kitu kilitoka kwa kasi kwenye vijitundu fulani vilivyokuwa pembeni ya saa yake upande wa mbele na kwenda juu kwa kasi kama risasi itokapo kwenye bunduki, kile kitu kilikuja kufika tamati baada ya kutoboa pembe ya ukuta wa ile ghorofa na kutokea upande wa juu kabisa wa ile ghorofa. Kilipofika juu kilijitanua na kuweka pembe tatu na kunata kwenye ukuta.

Mkono wa DENNY uliokuwa na ile saa, ulikaza na kufanya DENNY ajivute chini kwa nguvu hali iliyofanya kutua kwa ustadi wa hali ya juu... Mguu wake wa kulia ulipinda kidogo na kupiga goti huku ule wa kushoto ukiwa kama kisaidizi cha mkono wa kushoto uliokuwa juu yake na ule wa kulia ulibaki ukiwa umenyooka juu kutokana na ile kamba.

Alikaa style kama ya watu wa marathon wakiwa wanataka kukimbia, alinyanyuka na kubonyeza batani iliyokuwa chini ya saa na ile kamba kule juu ikajifungua na kurudi kwa kasi na kuingia ndani ya vitundu vilivyokuwa kwenye saa ile... Alitabasamu na kutoka mbio kuelekea upande wa kushoto kulipokuwa na njia za watu wa miguu na baiskeli, alikimbia mpaka akaja kutokea sehemu moja kulipokuwa na gari aina ya hiace yenye nembo za mikate kuonesha ni gari inayohusika na usambazaji wa mikate... Aliingia kwenye gari hiyo na kuitoa kwa spidi kiasi cha tairi kulalama kwenye rami na kuacha moshi tu.

Upande wa pili kwenye njia za chini ambapo kulikuwepo na watu watatu, MONA LISA na yule nesi ambae mpaka sasa hajatambulika jina ni nani wakiwa na kijana ALEXIS... Walizidi kukata kona za Chemba zile za maji machafu na kufanikiwa kufika sehemu moja walipoona kuna mwangaza unapenya kutoka juu kuingia mle ndani, moja kwa moja bila kuchelewa walianza kusogezana sehemu ile kwani ndio walikuwa wanaitafuta kwaajili ya kuwatoa nnje, MONA LISA alikuwa mbele akiwa na toji huku nyuma yule nesi akija akiwa na ALEXIS.

MONA LISA alipofika pale , aliangalia juu na kuona mfuniko wa chemba kuonesha wakiutoa mfuniko huo watakuwa wamepata njia ya kutokea juu... Haraka aliibumba toji yake mdomoni na kuanza kupanda juu kutumia ngazi zilizowekwa kwenye kila chemba, alipanda kwa kasi na kufanikiwa kufika juu kiasi cha kichwa chake kugusa nondo za mfuniko.

Alitumia mikono yake kupitisha kwenye matundu ya mfuniko na kufanikiwa kuusogeza pembeni huku yeye mwenyewe akijivuta juu kwa tahadhari kubwa maana aliibukia kwenye mataa ya magari na ilikuwa ni katikati ya barabara, alipofika juu aliangaza huku na kule kabla ya kuyatuliza macho yake kwenye gari moja iliyokuwa inakuja upande alipo kwa kasi, alijikuta anaachia tabasamu baada ya kujua ni nani anaekuja na ile gari. Hakuwa mwingine zaidi ya kijana DENNY ndie aliyekuwa anakuja upande alipo MONA LISA na alipofika karibu yake, alifunga breaki za ghafla na kufanya tairi kuburuzika kwenye rami.

Gari ilikuja kusimama kwenye miguu ya MONA LISA yaani ilibakia kidogo tu kama angeachia breaki angemgonga, alishuka akiwa na kamba na kuiviringa kwenye mkono wake.

Alifika mpaka pale kwenye ile chemba na kuirusha ile kamba ndani ambapo yule nesi aliipokea na kumfunga kiunoni ALEXIS na kuivuta ishara ya kuwataka walioko juu waivute. Kamba ilianza kuvutwa kwa watu wawili kushirikiana huku wakipata msaada mwingine kutoka ndani kwa yule nesi Ambae nae alikuwa anapanda juu.... Walifanikiwa kumtoa ALEXIS na yule nesi akatoka na kuingia ndani ya gari iliyoondoka kwa kasi na kutokomea barabarani huku nyuma wakiacha ushahidi wa moshi mdogo uliotokana na tairi kuburuzika kwenye rami.

Upande wa pili kwenye hospitali ya ST.MARCIA HOSPITAL... Hali ya maaskari walioachwa kama ulinzi haikuwa nzuri baada ya kukutana na dhahama kutoka kwa kundi la the brothers waloingia kwenye hospitali hiyo kwania ya kumchukua kijana ALEXIS lakini wakakuta tayari ameshachukuliwa.... Kilichofuata ni kuua kila mtu atakae wazuia na kujifanya anajua kuliko wao.

Miili iliyokuwa haina uhai ya maafisa wanaotoka kwenye kitengo cha kipelelezi cha C.I.A ilikuwa imezagaa kila kona ya hospitali ile ikiwa haina uhai tena huku wahusika waliofanya hivyo wakiwa wameshaondoka baada ya kutimizia mauaji kwa maafisa hao.

Agent GIBSON alihisi kuchanganyikiwa baada ya kuona hali ile kwa maafisa wake, breaki ya kwanza ilikuwa ni kwenye chumba alichomuacha kijana ALEXIS akiwa kalazwa.... Alitahamaki baada ya kukuta kitanda kikiwa kitupu huku pingu zikiwa zinaning’inia upande mmoja.

Aliangaza kwenye kila kona ya kile chumba na kubahatika kuona miili ya maafisa wake wawili ikiwa imelala huku ikiwa na matundu ya risasi kila sehemu ya mwili... Aliuma meno kwa hasira na kutoka nnje ambapo waandishi wa habari walikuwa wameshajazana nnje kutaka kufahamu kipi kilichotokea.

*********

Wiki moja iliweza kukatika pasina taarifa zozote za kupatikana au kuonekana kwa kijana ALEXIS.

Nnje ya ofisi moja iliyopo kwenye mitaa ya jiji la newYork, kulionekana kuna gari moja ndogo yenye kutumika sana kwenye mbio za masafa marefu ikiwa imepaki nnje ya ofisi hizo zenye kushughulika na utoaji huduma za mikate na vyakula mbalimbali.... Tunamuona msichana mmoja akiwa counte akihitaji huduma na baada ya dakika kadhaa kupita, akatoka nnje mkononi akiwa na furushi la mikate..... Alienda kufungua buti ya gari na akahifadhi vitu Vyake huko kisha yeye mwenyewe akaingia ndani ya gari hiyo na kutekenya funguo ambapo bila ubishi engine ilitii amri na kuwaka.

Alitoa gari yake sehemu aliyopaki na kuingia barabara kubwa ya jiji la NewYork,wakati akimalizia kuingia kwenye barabara kubwa... Kuna gari nayo ilikuwa inamfuatilia kwa nyuma, ndani ya gari ile ya nyuma kulikuwa na maafisa kutoka kwenye kitengo cha C.I.A .

Msichana akiwa hana hili wala lile, yeye alizidi kukanyaga mafuta na kubadirisha gia bila kufahamu kama nyuma kuna watu wanamfuatilia.... maafisa wale walikuwa kwenye mwendo mdogo lakini hawakutaka kumpoteza mlengwa wao aliyekuwa anazidi kukata mitaa ya jiji hilo.

‘’Kuna watu wanakufatilia nyuma... Kuwa makini sana.’’ . Msichana yule akiwa kwenye gari yake yenye kioo kinachoonesha ramani ya jiji na dunia kiujumla, alisikia sauti ikimweleza kipi kilichopo nyuma yake na yeye kwa kuzibitisha, aligeuka nyuma na kuwaona maafisa wa C.I.A wakiwa kwenye mwendo wa wastani.

Alitabasamu na kuvaa miwani kisha akajifunga mkanda vizuri na kubadirisha gia kitendo kilichofanya gari yake kuongezeka mwendo na kuwaacha maafisa wale nyuma kwa umbali kidogo ambapo nao baada ya kuona mlengwa wao kaongeza mwendo ilibidi nao waongeze..... Patashika nguo kuchanika ikaanza kwenye barabara ya NewYork baina ya yule msichana na maafisa wale. Mkimbizano ulikuwa mkubwa lakini maafisa wale walikuwa hawaligusi wala kulisogelea gari la binti yule liliokuwa linatembea kwa spidi kubwa, walifika sehemu ya mataa ambapo magari yalisimamishwa na kuruhusiwa wavuka kwa miguu wapite... Yule msichana alitabasamu na kuongeza mwendo kitu ambacho maafisa C.I.A nao waliongeza mwendo bila kujua mbele kuna nini.

Kuna mwanamama mmoja alikuwa ndio wa mwisho kuvuka akiwa na mwanae mchanga aliyemweka kwenye kigari kidogo chenye matairi nane, ile anafika katikati ya barabara na yule msichana alikuwa ndo anafika na gari yake.... Binti yule alifanya kukanyaga breaki za nyuma huku mguu wake mwingine ukiwa bado upo kwenye mafuta, gari yake iliseleleka kutumia tairi za nyuma na kumzunguka yule mama aliyeishiwa nguvu na kubaki akiwa kasimama wima..

Alimzunguka karibia mara tatu kabla ya kuachia breaki na kumpita kama upepo... Mama yule pamoja na mwanae waliwekwa katikati ya O iliyochorwa na msichana yule huku moshi ukiwa umechukua nafasi... Maafisa C.I.A walipofika pale walifunga breaki za ghafla ilihali gari yao ipo kwenye mwendo kasi, walipinduka na kwenda kuangukia kwenye gari moja iliyokuwa imesimama kusubiri wapita na miguu wamalize kupita.

Yule msichana aliachia tabasamu baada ya kuona tukio lile kupitia kioo chake cha mbele.... Alikanyaga mafuta na kutokomea barabarani

Nnje ya jiji la New York city, tunaliona lile gari la yule msichana likiingia kwenye moja ya mashamba ya mahindi huku ndani yake akionekana yule msichana aliyekuwa anakimbizana na maafisa wa kipelelezi kutoka kwenye kitengo cha C.I.A...... Alionekana ni mwenyeji kwenye mashamba yale maana alikuwa anapita kwenye njia ambazo kwa mtu ambae hajui eneo lile anaweza kupata ajali.

Alitembea kwa mwendo kasi mpaka alipokuja kutokea kwenye ukuta mrefu uliokuwa umetenganisha lile shamba na upande wa pili ambapo kuna bahari... Alisimama kwa dakika kumi kabla ya kuruhusu gari yake kutembea kuelekea sehemu moja iliyokuwa inajifungua kwenye ule ukuta, ulikuwa ni mlango wa kuingia ndani au upande wa pili wa ule ukuta ambapo kuna bahari.. Aliingiza gari ndani na ule mlango ukajifunga kama mwanzo na kufanya kutoonekana kama kuna mlango wa siri maeneo yale, ndani ya ukuta ule.... Kulikuwa na barabara kama nyingine ila isipokuwa barabara iliyokuwepo mle ndani ilikuwa imetengenezwa kwa vitu maalumu vyenye uwezo wa kuzuia silaha ya aina yeyote ile,

Binti yule alizidi kukanyaga mafuta mpaka alipofika kwenye geti kubwa la kuingia ndani zaidi, alisimama na baada ya dakika tano akaendelea kukanyaga mafuta na kuingia ndani zaidi ambapo kulikuwa na mji mdogo huku kukionekana kuna kila aina ya dhana za jeshi.

Alisimamisha gari yake sehemu yenye magari kama yake na kushuka...

‘’Naona umeivaa kwenye udereva.’’. Kuna mtu alikuwa anashuka kutoka kwenye ndege moja ya kivita iliyokuwa ndio inapooza engine kuonesha ilikuwa inafanya kazi muda sio mrefu.. Alizungumza vile na kusogea mpaka sehemu alipo yule binti ambae anafanana na yule nesi aliyekuwa na MONA LISA kule hospitalini walipoenda kumchukua kijana ALEXIS.

‘’Kawaida sana.’’. Yule binti alijibu na kutabasamu huku akitoa vitu vyake alivyotoka navyo mjini.

‘’Naweza kukusaidia bibiye..?’’. Yule kijana aliyeshuka kwenye ndege aina ya chopa, aliuliza swali kwa yule binti na kuweka mkono wake wa kushoto chini ya buti huku ule wa kulia akishikilia mfuniko wa buti uliokuwa juu.

‘’Ningehitaji msaada ningekwambia... Nipishe.’’. Yule binti alijibu kwa sauti kidogo na kufunga buti kwa nguvu bila kujali kama yule kijana kaweka mkono chini.

‘’Aaaaauuuuu!!! Shit..’’. Yule kijana alitoa mkono wake baada ya kukandamizwa na buti.

Yule binti hakujali kama kamuumiza yule kijana... Alishika njia mpaka kwenye rifti na kuiruhusu kupanda juu huku chini akimuacha kijana wa watu akiugulia maumivu ya kidole.

‘’MIKEL... Pole sana ila usikate tamaa ipo siku CHRISTINA atakuelewa na kuzikubali hisia zako, usife moyo.’’. Kuna kijana mwingine alikuja na kumshika bega MIKEL aliyekuwa anamuangalia yule binti ambae ni yule nesi aliyekuwepo kule hospitalini kipindi kile walichoenda kumtorosha kijana ALEXIS.. Kumbe anaitwa CHRISTINA.

‘’Aaah!!! Sidhani kama ipo siku huyu binti atakuja kuzielewa hisia zangu.. Ila poa twende ndani maana nasikia kuna vitu vimeharibika..’’. MIKEL aliongea na kuongoza njia kwenda ndani zaidi ya kambi hiyo ambapo alidai kuna vitu vimeharibika.

Ndani ya chumba kimoja hivi kwenye kambi hiyo, kulionekana madaktari wakipishana huku mbele yao kukiwa na mwili wa mtu ukiwa umelala kwenye incubator ambacho ni chombo cha kisayansi chenye kuhusika na kuhifadhia watoto walioazaliwa kabla ya siku zao au mara nyingine hutumika kutengenezea watoto wanaotokana na mbegu za mwanaume kuchukuliwa na za mwanamke kisha zinachanganywa sehemu moja na kutengenezwa mtoto.

Nnje ya chumba kile kilichokuwa na vioo tu. Alionekana mtu mmoja wa makamo akiwa kavaa suti huku pembeni yake kukiwa na watu wawili.. MONA LISA na kijana DENNY, walikuwa makini sana kuangalia kile kinachoendelea ndani ya maabara juu ya mwili wa kijana ALEXIS uliokuwa unafanyiwa vitu fulani vya kutoa kumbukumbu za kijana huyo.

Madaktari waliokuwepo mle ndani baada ya kumaliza kumpachika mirija fula kwenye mwili wa kijana ALEXIS... Walitoa alama ya dole gumba nnje ya chumba kile upande wa kulia ambapo kulikuwa na makompyuta mengi yakiwa yanaonesha mfumo mzima wa mwili wa kijana ALEXIS na mapigo yake ya moyo... Madaktari waliokuwepo kwenye kompyuta zile baada ya kuona wenzao wa ndani wamewapa taarifa, walianza kuchezea keyboard za computer zao huku wakiwa makini kwa kile wakitendacho.

Walizidi kupoteza kumbukumbu za kijana yule mwenye asili ya kiafrika.. Kadri muda ulivyokuwa unakwenda na ndio mwili wa ALEXIS ulivyoanza kujitingisha kama anapinga kitu fulani .

Walizidi kuzipoteza kumbukumbu za kijana yule huku mhusika mwenyewe akionekana kupingana na kitu fulani kisitoke kwenye mwili wake...Walifanikiwa kiasi fulani lakini kuna kumbukumbu zilikataa kufutika kwenye kichwa cha kijana ALEXIS.

‘’Kuna matukio kadhaa yamekataa kufutika kwenye ubongo wake na tukilazimisha tunaweza kumpotezea uhai wake...’’. Kuna daktari aliongea kuwaambia wakina MONA LISA na yule mtu aliyeonekana ni mkubwa wa kambi nzima.

Yule mtu alitoa ishara ya kuwataka waache maana alishajua ni kumbukumbu gani hizo zilizokataa kufutika...

‘’Hapo inatosha najua kumbukumbu zilizokuwepo kwenye ubongo wake zitazidisha chachu kwenye kazi... Mpelekeni chumbani tusubiri apate fahamu zake..’’ Yule mtu alizungumza hivyo na kunyanyuka kutoka pale alipokaa na kwenda nnje.

Walifanya kama walivyoambiwa, walimtoa kijana ALEXIS aliyekuwa kalegea kutokana na shughuli aliyokuwa anafanyiwa na kumpeleka kwenye chumba kimoja chenye rangi nyeupe kote mpaka kitanda... Walipofika walimlaza na kutoka nnje.

Masaa yalizidi kukatika pasipo kijana ALEXIS kupata fahamu zake.... Chumba alicholazwa kijana huyo, kilikuwa kimewekwa camera kila pembe za ukuta lakini haikuwa kazi rahisi kwa mtu kugundua kama mle ndani kuna camera.... Kutokana na rangi ya chumba kuwa nyeupe na camera zenyewe zilifungwa kitaalamu.

ALEXIS akiwa kwenye usingizi wa madawa na kunyong’onyeshwa ubongo wake baada ya kupotezewa kumbukumbu zake... Kuna ndoto aliweza kuota akiwa pale kitandani.

Aliota yupo katikati ya pori lilofungamana huku yeye akiwa katikati ya pori hilo...Mwili wake ulikuwa umetapakaa damu kuonesha kuna tukio amelifanya nyuma, akiwa pale akijishangaa jinsi alivyo.. Ghafla kuna kitu kilikuja na kumkumba pale alipo, alihangaika kujitoa kwenye mikono au himaya ya kitu kikichomkumba, lakini ilimuwia ugumu kutokana na hali yake kuwa mbaya na kukubali kuchanwa na kucha za yule kiumbe....

Kiumbe yule alikuwa ni aina mpya ya chui wapatikanao kwenye nchi ya india.. Jinsi walivyo na wanavyoonekana hawakuwa na utofauti na wale chui wa bengali lakini aina ya chui huyu ni wepesi na weredi kwenye kufanya maamuzi dhidi ya adui.... ALEXIS alitupwa mbali na kujibamiza kwenye shina la mti na kuanguka chini kama mzigo, akiwa pale chini akijaribu kujizoazoa... Pembeni yake aliweza kuona kuna mtu akiwa kasimama akimuangalia kwa masikitiko makubwa kuonesha hajapendezwa na tukio lile. ALEXIS alijaribu kunyanyua mkono wake kutaka msaada kutoka kwa mtu yule, lakini alishindwa na kujikuta akianguka chini na kupoteza fahamu.

‘’Mheshimiwa... Ameamka!!’’. Kwenye chumba kimoja kinachotumika kuongozea camera.. Mlinzi aliyekuwa anaangalia camera za kambi hiyo hususani ni camera zilizopo kwenye chumba alicholala kijana ALEXIS, alizungumza hivyo kuwaambia watu waliokuwepo nyuma wakingojea kijana ALEXIS apate fahamu zake.....

Baada ya taarifa ile, kuna mtu mmoja aliyeonekana ndio kioongozi wa kambi ile... Alitoka sehemu alipokuwa ameketi na kwenda kwenye luninga iliyokuwa inamuonesha kijana ALEXIS akiwa kakaa kwenye kitanda akionekana kufikiri jambo.

‘’Hatimae amezinduka... Mpelekeeni nguo, nadhani anajishangaa kujikuta hapo na hakumbuki tukio lolote hapo alipo... Huu ni muda wetu wa kuifanya hii kazi juu ya ushenzi unaoendelea kwenye hii dunia na mtu mwenye uwezo wa kumaliza mambo yote hayo ni huyu kijana..’’. Mtu yule aliongea hayo na kuonesha furaha aliyokuwa nayo baada ya kijana ALEXIS kuzinduka.

Walitoka vijana wapatao watatu na kwenda kwenye chumba alichopo ALEXIS.

*****

ALEXIS baada ya kuota ile ndoto ambayo kwa upande wake ilikuwa yakutisha na wala hakuelewa nini maana ya ile ndoto.. Alizinduka na kujikuta akiwa kwenye mazingira ambayo hakuyaelewa...

Alijaribu kuangaza macho yake kwenye kile chumba kama anaweza kukijua. Lakini hakuweza kukumbuka kitu hata alipojaribu kushika kichwa chake na kufumba macho kujaribu kukumbuka, hakuweza kukumbuka kitu zaidi ya kusikia maumivu kwenye kichwa chake, alifunua shuka aliyokuwa kafunikwa na kujishusha kutoka kwenye kile kitanda na kujaribu kukichunguza kile chumba.... Alikuwa na nguo ya ndani tuu. Alitembea huku na kule akijaribu kutafuta mlango wa kutokea nnje lakini hakufanikiwa kuona dalili zozote za kumjulisha kama mle ndani kuna mlango, ilibidi arudi na kukaa kwenye kitanda.. Akiwa anataka kukaa, mara alianza kuhisi kuna sehemu zinafunguka kwenye ukuta... Ilibidi ageuke na kukaa tayari kwa kukabiliana na kitu chochote kile ambacho ni kibaya kwa upande wake, aliona mlango ukiwa unafunguka wenyewe na baada ya kumalizika.... Waliingia vijana watatu ambao kwenye macho yake walikuwa ni wageni, vijana wale baada ya kuingia mle ndani... Wawili walikaa nyuma na mmoja aliyekuwa kabeba nguo kwenye mikono yake, akaenda mbele ya ALEXIS na kumnyooshea mikono mbele ikiwa na nguo juu yake ishara ya kumtaka azipokeee..

ALEXIS hakuelewa ni mambo gani yanajitokeza kwenye maisha yake maana hakuwa na kumbukumbu kama watu waliopo mbele yake alishawahi kuwaona kabla... Ilibidi azipokee zile nguo lakini kwa kusitasita...

‘’Karibu sana nyumbani.’’. Yule kijana ambae ni DENNY baada ya kumpatia nguo ALEXIS... Alimkaribisha na kutabasamu kitu ambacho kijana ALEXIS hakukielewa... Alilazimisha tabasamu usoni kuashiria kakubaliana na yale aliyozungumza DENNY.

DENNY baada ya kuona vile... Alitoka nnje na wale wengine wawili na kumuacha ALEXIS mwenyewe..

‘’Mbona sielewi mambo yanayotokea kwenye maisha yangu... Mara ya mwisho nilikuwa wapiiiiiii!!!! Aaaaah. Hata sikumbuki alafu nimejikuta nipo hapa na hawa watu wanaonesha tabasamu usoni mwao ilihali mimi siwatambui, hii sinema gani sasa.’’. Alijiuluza maswali bila kupata majibu sahihi... Mwisho akaamua kuvaa yale mavazi aliyoletewa na wale watu ambao kwake walikuwa ni wageni.

‘’N.I.S.A.... Hii inamaana gani.?’’. Baada ya kuvaa na kuona maneno yaliyoandikwa upande wa kushoto wa shati alilovaa, alijaribu kuyasoma na kujiuliza nini maana ya neno N.I.S.A lakini hakupata jibu sahihi.

‘’Karibu sana nyumbani... DAMIAN, ni muda umepita hatujaonana... Naitwa General JEFF ukiniita the ghost utakuwa hujakosea, aaaah!!! Najua unajaribu kujiuliza kwanini upo hapa? Twende kwanza nikakutembeze nnje ya hii kambi na nitakujulisha kidogo kidogo maana najua ni muda mrefu sana hujafika hapa na ulishasahau mazingira ya hapa..’’. Akiwa anajiuliza maana ya neno aliloliona kwenye t-shirt aliyoivaa... Ghafla kuna mtu aliingia kwenye chumba alichokuwepo na kujitambulisha huku akimuomba watoke nnje ili akamkumbushe vitu kadhaa ambavyo atakuwa amevisahamu na kumpachika jina jipya badala ya lile la mwanzo.

‘’DAMIAN? Inamaana mimi naitwa DAMIAN.?’’. ALEXIS aliuliza swali na kujishangaa kisha akamuangalia mtu aliyesimama mbele yake.

‘’Ndio.. Inamaana hata jina lako mwenyewe umelisahau!! Aaaaaah. DAMIAN.. Embu acha masikhara yako najua lile tukio la kurushwa na bomu ndio limekufanya usahau hata jina lako... Inamaana hata mimi hunikumbuki..’’. General JEFF The Ghost alijibu na kumuuliza huku akimshangaa kijana ALEXIS kwa kulisahau hata jina lake.

‘’Aaaanhaaa.!!! Ndomaana kichwa changu kinaniumaa aaah.. Basi kumbukumbu zimenitoka kidogo nadhani zitarejea polepole...’’. ALEXIS baada ya kupewa maneno matamu na kuaminishwa na General JEFF The Ghost, alijikuta anakubali na kuonesha kweli yeye ni DAMIAN ila alipitiwa tu.

Waliongea mengi kiasi cha kuzoeana kwa muda wa lisaa limoja na dakika zake.. ALEXIS ambae kwasasa anatambulika kama DAMIAN... Alimzoea General JEFF kama walishawahi kukutana kabla kumbe ni kutokana na kumbukumbu zake kufutwa na kubaki na kumbukumbu chache ambazo nazo zitakuwa zinakuja kwenye kichwa chake na kupotea..

Maisha mapya yalianza kwa kijana ALEXIS ambae kwenye ile kambi ya siri anajulikana kama Leader DAMIAN.. Kambi ile iliyokuwa chini ya General JEFF THE GHOST.. Ambae alishawahi kufanya mambo makubwa kwenye nchi ya marekani na kupewa cheo cha the one and only kabla ya kupewa uongozi wa General ambapo kwenye cheo hicho hakukaa sana kutokana na kuwa na maadui wengi sana... Hivyo alitengeneza kifo cha bandia na kuwaaminisha watu kuwa amekufa lakini ukweli aliujua yeye na kuamua kuanzisha kitengo chake mwenyewe kilichokuwa kinatambulika na raisi wa nchi tu. Huku kambi yake akiitoa nnje kabisa ya mji wa New York.

Huku wanajeshi wake akiwafunza kuua na sio kukamata maana wasaliti wengi sana walikuwa serikalini.... Kitengo chake alichokipa jina la NATIONAL INTELLEGENCY SECURITY AGENT (N.I.S.A).. Kilikuwa ni kitengo chenye uwezo wa kivita kutokana na wengi wao kupitia mafunzo magumu sana... Walikuwa wanajishughulisha na mambo ya kupambana na uharifu huku serikali kikitambua kitengo kile ni moja ya makundi ya kigaidi na kuingia kwenye upelelezi.

General JEFF mara nyingi sana na kwa ungwe nyingi alikuwa anatamani kufanya kazi na kijana ALEXIS ambae historia yake anaifahamu vyema na uwezo aliokuwa nao pia na miongoni mwa kundi ambalo analitafuta ni kundi ambalo ALEXIS analifahamu vyema kutokana na kukulia kwenye kundi hilo ambalo mmiliki wake hajulikani kwa sura zaidi ya jina tu. Huku mtandano wake ukiwa mkubwa duniani kutokana na washirika wake kuwa kwenye vyeo mbalimbali serikalini... Hivyo iliwawia vigumu kuungamiza mtandano wasiojua hata chimbuko lake.

Waliitumia nafasi ya kumpata kijana ALEXIS ili awasaidie kuuangamiza mtandao huo baada ya kuona ndio kijana wa pekee anaepigana kwaajili ya kutafuta uhuru wake... Walitumia njia za kumtoa kumbukumbuku kijana huyo kwasababu wanamfahamu vyema na wangeacha awe na kumbukumbu zake, ingewaletea shida kutokana na kijana huyo kutoamini mtu mwingine awe mzuri au mbaya kwake hakutaka kumuamini kiumbe wa aina yeyote ile zaidi yake mwenyewe.

‘’DAMIAN... Unajua hapa duniani kuna watu wanajifanya miungu watu na kumkufuru mungu, biashara ya ushoga duniani imekuwa kubwa sana na vijana wengi wanaharibika kupitia hii biashara... Wazazi wanalia kila siku kwa kuwapoteza watoto ambao waliwazaa kwa kutumainia ni wakombozi wao wa baadae. Lakini kuna watu wasiojua uchungu wa kuzaa wanawafanya mashoga na vijana wa watu, wengine ni watu wazima na pesa zao ila nao wapo kwenye michezo hii ya kufanya mapenzi jinsia moja.... Nimeangalia ni nani wa kumpatia hii kazi na akaifanya vizuri, nimeona ni wewe kwasababu unauwezo na ni mzoefu kwenye mapambano, naomba uifanye hii kazi kwaajili ya vizazi vijavyo..’’. General JEFF aliongea hayo siku moja akiwa sehemu fulani kwenye kamgahawa kilichopo kwenye mitaa fulani pale New York city....

DAMIAN alimsikiliza kwa umakini kabla ya kutua glass yake ya juice na kumuangalia JEFF usoni kabla ya kupelekea tena glass kinywani.

‘’Aaa..Unajua watu wanaoiharibu dunia sio wakuishi sayari moja na watu wema.. Hilo jambo ni zuri na nipo tayari kuipokea hiyo kazi ila kwa sharti maalumu.’’

‘’Sharti gani tena..?’’.

‘’Sihitaji kuingiliwa kwenye kazi yangu..’’

 

‘’Wala usiwe na shaka juu ya suala hilo... Hakuna atakaechumpa mipaka na kuinga kwenye tawala yako.! Jeff alimwambia Damian huku akiruhusu koo lake kupita radha ya juice iliyotengenezwa kiustadi wa hali ya juu..

‘’Kazi itaanza wiki ijayo, mtandao wa biashara hii haramu ni mkubwa mno, yakupasa utulie na ufanye upekuzi kabla ya kutenda jambo!’’. Jeff alimsisitiza na kumtaka kuweka umakini kwamaana mtandao anaoenda kuuchokoza ni mpana sana na ni hatari endapo ataingia kichwa kichwa..

Walizungumza mambo kadha wa kadhaa kabla ya kujinyanyua kutoka kwenye viti vya mgahawa huo na kutoka nnje.. Waliingia kwenye usafiri wao waliokuja nao na kuuondoa kwa ustadi mkubwa sana, ndani ya gari ukimya ndio ulitawala huku kila mmoja akionekana kutafakari jambo..

Umri wa General Jeff alimaarufu kama The Ghost, ulikuwa umemtupa mkono na kutokuwa na makali yale ya enzi zake za ukamanda, walitembea kila engo za jiji la NewYork city kama watalii lakini kuna mambo yao binafsi walikuwa wanayafanya kwenye utembeaji wao.

Muda ulitamaraki na kusababisha majira kupinduka, usiku walitafuta hotel yenye hadhi ili wajihifadhi ikiwa ni katika mikakati yao ya kupembua jinsi watakavyoifanya kazi iliyombele yao.

Kutokana na Jeff kutambulika kama ni marehemu aliyekufa kitambo kilichopita, ilifanya kutoingia ndani ya hoteli ile na kumpatia maelezo pamoja na vifaa muhimu kwenye kazi kijana Damian ambae jina lake la awali ni Alexis kisha yeye akaingia kwenye gari na kuliondoa maeneo yale akimuacha Damian akimsindikiza kwa macho mpaka alipopotea kwenye upeo wake nd’o nae akaingia ndani ya hoteli ambapo alipitiwa na kisachio ikiwa ni sehemu moja wapo ya ulinzi uliopo kwenye hoteli ile yenye vyumba vya wageni ndani yake... Baada ya kutambulika hana kitu chenye kuhatarisha usalama, alipatiwa ruksa ya kuingia ndani mpaka sehemu ya mapokezi..

‘’Habari yako bibie! Naweza kupata chumba kinachoendana na mimi?’’ Damian baada ya kufika mapokezi aliachia madaha yaliyomfanya mhudumu wa pale kuachia tabasamu na kuonesha uzuri wake ulivyo, baada ya kuuliza suali Damian alihitimisha mboni zake kwenye sura ya mrimbwende huyo ambae nae alimtizama kijana aliyopo mbele yake kabla ya kujibu swali la kijana huyo.

‘’Vyumba vipo, unahitaji chumba cha aina gani labda? Kuna vyumba vya V.I.P ambavyo ndani kuna kila kitu na ni salama kwa mambo yako mbalimbali pia kuna vyumba vya kawaida..’’. Mrimbwende yule alijibu na kutazama uso wa kijana mtanashati mwenye uchangamfu kupita maelezo.

‘’Nahitaji chumba cha V.I.P nadhani kitanifaa zaidi.’’. Kijana Damian alitoa chaguzi yake na kuingiza mkono kwenye mfuko wake wa ndani ya koti na kutoa mfuko mdogo wa kaki ambao Mara nyingi hutumika kuhifadhia nyaraka na fedha pia, aliweka juu ya meza ambapo msichana yule aliuchukua na kutoa noti za dola kadhaa na kuziweka kwenye mashine ya kuhesabia fedha.

‘’Ni kiasi cha miezi mitatu na wiki mbili, naomba pasipoti yako tafadhali.’’. Msichana yule aliongea baada ya mashine yake ya kuhesabu hundi kutoa takwimu za fedha ile iliyotolewa na kijana Damian. Bila hiyana kijana Damian aliingiza mkono nyuma ya mfuko wa suruali aliyoiva siku hiyo na kutoa waleti na kuifungua ambapo alichambua vitu kadhaa na kutoa pasipoti yake iliyotengenezwa kwa masiku kadhaa yaliyopita nyuma na kumpatia yule kimwana ambae aliipokea na kuiweka kwenye mashine maalum. Na baada ya dakika kadhaa kukatika akaitoa na kuandika maelezo kwenye kompyuta yake na kuonesha sehemu moja ya kuweka sahihi na kijana Damian bila kusita akaweka sahihi yake.

‘’Karibu sana bwana Damian Lewis kwenye hotel yetu, jisikie huru kwa kila kitu utakacho utakipata, twende nikakuoneshe kilipo chumba chako.... Wewe njoo mara moja ubebe mizigo ya mteja.!’’. Kimwana yule mwenye sauti nyororo yenye kupendeza masikioni mwa kila amsikiae na kuwafanya watu wengi kupenda kumsikia akiongea, alitoa maelezo kwa kijana Damian na kumuomba aongozane nae akamuoneshe kilipo chumba chake na kuita mfanyakazi anaehusika na ubebaji wa mabegi ama! Mizigo ya mteja na kumpelekea ndani.

‘’Aaah. Hapana usijali nitabeba mwenyewe nisikupe tabu..’’. Damian aliomba asibebewe mizigo yake na kudai atabeba yeye, bila hiyana kijana yule akarudi sehemu yake ya awali kungojea mtu mwingine wa kumbebea mzigo.

Walipanda lift na kutokea ghorofa ya juu kabisa ambapo nd'o sehemu ya vyumba vya watu wenye heshma zao wanapokaa.

‘’Njia hii tafadhali..!!’’. Kigoli yule alimuonesha njia kijana Damian baada ya kufika juu na kijana huyo akataka kupita kuliani kwake kulipokuwa na watu wenye suti nyeusi wakiwa wamesimama kwenye milango kadhaa kuonesha ni walindaji wanaomlinda mtu, alijiuliza upande ule kunani? Lakini hakupata majibu sahihi kwenye kichwa chake na kuamua kupuuza na kuongoza kule alipotakiwa kwenda.

‘’Chumba chako ni hiki, kama kutakuwa kuna vitu vingine unahitaji usisite kutujuza kwa nambari zilizopo kwenye simu ya mkonge iliyopo pale mezani. Nikutakie siku njema na upumzikaji mwema.’’. Msichana yule baada ya kumfikisha sehemu husika kijana Damian alimkabidhi funguo na kumtakia mapumziko mema na yeye akaondoka kwa mwendo wa maringo kama wa twiga, miguu yake ya bia, mwendo wake wa kinyonga, shingo yake ya twiga, vilimvutia kijana Damian na kutamani kumuita kimwana huyo lakini alikwisha chelewa maana bibie alikuwa kashakata kona na kwenda sehemu ya lift na kuondoka akimuacha kijana Damian akitumbua macho pima kama aliona kitu cha kustaajabisha mbele ya macho yake.

Aliugeukia mlango wa chumba chake na kusoma namba za chumba na kuufungua na kujitosa ndani yake, chumba kilikuwa ni kizuri na chenye kupendeza kwenye macho ya kila mtu. Kijana Damian alitupia begi kwenye sofa lililopo mule ndani na kupunguza uzito kwa kuvua koti lake na kulegeza tai kisha akaanza kutalii kwenye kile chumba, alitembea kila sehemu na kujihakikishia usalama na kurudi kwenye sebule ndogo na kutazama nnje kupitia dirisha la kioo na kuona man’dhali ya jiji la New York city lilivyo.

Kwakua ilikuwa ni usiku na mchana kutwa hakupata nafasi ya kujisafisha, ilibidi aingie maliwatoni kidogo kujifanyia usafi wa mwili, punde baada ya kumaliza kujifanyia usafi allitoka maliwatoni akiwa kajifunga tauro kiunoni huku jingine akijifutia maji. Alipofika sebuleni alifikia kwenye mkonga wa simu na kubofya nambari kadhaa zilizoandikwa kwenye kikaratasi kilichonatishwa juu ya simu ile na kuweka mkonga sikioni..

‘’Nahitaji chakula na wine moja, naomba viletwe chumba namba 291 muda huu.. Haya nashukuru..’’. Baada ya upande wa pili kupokea simu, kijana Damian alitoa maagizo ya maang,’akuli na kurejesha mkonga sehemu husika baada ya kumalizana na mtu aliyempa oda, aliendelea kujikausha maji na tauro dogo kabla ya kushtushwa na mlango ukigongwa.

‘’Ngo! Ngo! Ngo! Ngo!’’. Mlango uligongwa kiustaarabu na mgongaji na kufanya kijana Damian kunyanyuka alipokuwa ameketi na kuuendea mlango maana alishajua ni nani anaegonga... Alizungusha kitasa na kikakubali na mlango ukafunguka, alikuwa ni mhudumu akiwa na kimkokoteni chake cha kubebea vyakuka na vinywaji alikaribishwa ndani na kijana Damian.

Alisukuma kimkokoteni chake mpaka mezani na kuweka vitu alivyoagizwa juu ya meza kisha akaaga na kutoka. Baada ya mhudumu kutoka nyuma kijana Damian alikaa mezani na kupata msosi na kushushia na wine kidogo na baada ya kumaliza kupata chakula, alichukua begi lake na kutoa kompyuta ndogo alimaarufu kama laptop na kuikunjua kisha akaiweka mezani na kuichomeka waya wake kwenye soketi kwaajili ya kuilinda isije ikazima kwa kukosa chaji.

Alifungua na kutakiwa kuweka msimbo wa siri ili ifunguke, alifanya hivyo na kuweka tarakimu kadhaa kisha akasubiri dakika kadhaa ili mfumo mzima wa mashine ukae sawa, baada ya kuona umekaa sawa, alianza kuichezea na kutoa kifaa kinachotumika kuhifadhia laini kwaajili ya kuingia mitandaoni na kukiweka sehemu inayopaswa kuwekwa kisha akaingia kwenye mtandao na kuingiza kitambulishi cha tovuti aliyoitaka na baada ya sekunde kadhaa tovuti ikafunguka na yeye akaanza kufanya kile alichokusudia kukifanya ndani ya mtandao.

‘’Inamaana hii biashara inafanywa mpaka kwenye bara la afrika? Mbona hawa watu ni waharibifu namna hii.? Kuna kitu natakiwa kukifanya hapa ngoja niangalie maagent wao na ikiwezekana nitafute njia ya kuuvamia mtandao wao ili nipate wepesi kwenye suala hili laasivyo nitakuwa natwanga maji kwenye kinu.’’. Kijana Damian alijiuliza masuali mengi na kukosa majibu sahihi baada ya kufungua moja ya tovuti na kuona takwimu za ushoga dunia na kuangalia bara liloathirika ni bara la afrika ingawaje watu wa bara hilo wanaonekana kipaombele kwenye kupinga mambo ya ushoga lakini ndio bara lenye uathirika mkubwa sana wa biashara za ushoga.

Aliuma meno kwa hasira na misuri ya shingo na kifua kupanuka na kutuna mithiri ya simba awapo hasirani, alichukia sana baada ya kuona vijana wadogo wakijihusisha na biashara ya ngono za jinsia moja ilhali kwa umri wao na maumbile yao hawakupaswa kufanya ujinga kama ule.

Alizidi kuchambua na kuandika maandiko kadha wa kadhaa aliyoona yatampa muongozo kwenye upekuzi wake, masaa hayakuganda sehemu moja yalizidi kukumbia mithiri ya barafu liwapo juani, kuja kutahamaki saa kumi alfajiri ilimkutia kwenye laptop akifanya upembuzi wa mambo ya ushoga na kutafuta mawakala wanaohusika na ununuzi na usambazaji wa biashara hiyo.

Usingizi ulikuwa unasumbua mboni zake za macho na kufanya macho kumuomba yapumzike kwamaana yamechoka kusoma na kuangalia mwangaza wa laptop lakini yeye hakutaka kuyasikia wala kulala angalau kidogo nd’o kwanza alizidi kuingia ndani kabisa ya mtandao na kuchimba siri nzito za mashoga.... Kitu kilichomshangaza zaidi ni pale alipoona si. Vijana pekee wanaofanya kazi hizo hata wazee nao walikuwa wanafanya kazi hizo kwa kuwanunua vijana mashababi kwaajili ya kuwashughulikia kinyume na maumbile yao yanavyowataka wawe, alizidi kupata hasira baada ya kuona orodha fupi ya viongozi wakubwa ambao nao ni mashoga na wanawanunua vijana mashababi waliojazia kimazoezi kwaajili ya kufanya nao mapenzi ya jinsia moja.

‘’Wanahidhaya wakubwa hawa, yaani hadi wazeee? Hii siwezi kulifumbia macho lazima niikomeshe hii biashara kwa njia yeyote hata ikinibidi kuutoa uhai wangu, naua kila mmoja si. Mnunuzi wa vijana kwaajili ya kufanya nao ngono wala anaenunuliwa ni lazima wote wafe ili isitokee tena ushetani kama huu.. Oooopsssss.’’. Kijana Damian alichoka hoi baada ya kuona mambo yanayoendelea juu ya biashara iliyokithiri duniani... Aliiacha laptop yake on na yeye akajitupa kwenye kitanda baada ya kuona kapata angalau kidogo kati ya kingi alichokitaka.

******

‘’Bado hamjapata taarifa zozote kuhusu Alexis? Kwanini sasa wakati mnatambua ni kijana pekee mwenye uwezo wa kuja na kuiangusha biashara yetu..’’. Kuna mzee mmoja wa makamo alikuwa anazungumza na mtu kwenye simu huku akifoka kweli juu ya uzembe walioufanya vijana wake.

Baada ya kuzungumza vile hakusubiri maelezo kutoka upande wa pili wa ile simu, yeye alikata na kubofya nambari kadhaa na kuirudisha tena sikioni ile simu.

‘’Madam's Aretha, kijana Alexis imekuwa ni ngumu kumpata kutokana na kundi jingine kujitokeza na kumchukua kule hospitalini..’’. Mzee yule alizungumza kwa adabu kuu na mtu wa upande wa pili wa simu aliyemtamka kwa jina la Madam’s Aretha .

‘’Kwasasa inatakiwa kuangalia biashara jinsi inavyoenda kuhusu huyo kijana achaneni nae.’’. Sauti ya kike ilisikika upande wa pili wa simu ikizungumza na ukimya ukachukua nafasi kuonesha simu ilishakatwa.

Yule mzee alishusha pumzi ndefu na kuondoka sehemu alipokuwa kasimama na kushuka mpaka chini, alikuwa kwenye hotel moja iliyopo Miami Florida akifanya mambo ya biashara.

Ni miongoni mwa mawakala wa ushoga ambao ndio mashina makubwa makubwa yanayotafutwa na kijana Damian.

Alitoka nnje ya hotel hiyo na kuingia kwenye gari moja ya kifahari na kuamuru dereva aiondoshe pahala pale.... Alikuwa na msafara mkubwa sana kama wa raisi ama mbuge zote hizo ni fedha wanazozichuma kiharamu kwa kuuza na kusambaza mashoga duniani na kuua matajiri na kuwanyang’anya vito vyao vya thamani, msafara wake ulikuja mpaka maeneo ya bandalini ambapo kwenye bahari kulionekana kuna meri kubwa inaingizana sehemu ile tena kwenye usiku ule wa manane.

Meri baada ya kutia nanga kwenye bandali ile wafanyakazi walianza kushusha maboksi kadhaa yaliyomo mule ndani huku makontena yakishushwa na kifaa maalumu. Baada ya nusu saa kukatika makontena yalikuwa yameshushwa kwa wingi na yale maboksi yule mzee alishuka na kwenda kukagua vitu vilivyomo ndani ya makontena yale na maboksi, lahaula!!! Kwenye makontena yapatayo kumi na moja yalikuwa yamehifadhi ndani yake vijana wakike kwa waume waliokuwa chini ya miaka kumi na minane huku wengi wao wakionekana kutokea kwenye bara la afrika.

Walikuwa wanatia huruma jinsi walivyokuwa wamefungwa kamba kwa miguu na mikono huku wakionekana wamedhoofika kutokana na njaa, mzee yule alitabasamu na kuwataka vijana wayaweke makontena hayo kwenye magari yanayohusika kubeba makontena na wayasafirishe mpaka Las Vegas kwaajili ya kuwafanyia biashara vijana wale huku yeye akitangulia uwanja wa ndege wa kibinafsi na kukwea pipa kuelekea Las Vegas kuandaa soko.

Magari yaliyobeba makontena ambayo ndani yake kuna binadamu yalianza kusafirishwa usiku huo wa manane huku maasikari wengi wakiliokuwemo ndani ya bandali na kwengineko, wakikingia kifua biashara ile na kuyaruhusu magari hayo kuvuka kwenye kila kizuizi, pesa nd’o iliongea kwa kipindi kile na hakukuwa na askari wa kukataa kupokea mlungura mrefu ilhali kwa mwezi analipwa kiasi cha hundi kidogo, viongozi wa nyanja za ulinzi wa nchi ya marekani walikuwa chini ya mwanamama mwenye kuindesha biashara ile na hakukua na vikwazo kwenye biashara yake hiyo ya haramu

ITAENDELEA


Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)