KOSA LANGU UTANGULIZI

Emmanuel Lee
By -
3
JABA PLANET.

KOSA LANGU

MTUNZI: Emmanuel Kahindi
WhatsApp:+254796273110
Website: jabaplanet.blogspot.com

Sehemu 1
Nilikuwa nawaza itakuaje siku hiyo, somo la Kiswahili tunalofunzwa na madam Nasra, mie humuita tu Nasra Kwa nini nitangulize Jina madam? Kwa kiumbe huyu.
Nasra ni mzuri kivyake, kifua chake kimebeba matiti ya wastani ya mviringo yalo simama dede, nyuma amebeba makalio ya wastani akitembea hutikisika si haba na mashaka kama Nasra huvaa chupi kweli si Kwa  mtikisiko huo! Kasura kama mtoto hivi na mweupeee ndiyo maana Mimi hupata ugumu wa kumuita Madam Nasra. Uzuriwe unakamilishwa na kasauti kake dah!

Hakika ni mwalimu mzuri aliyekamilika kila idara si uzuriwe ; urembo eti. Darasani hata usiseme wanafunzi wake hulipasi somo lake kasoro mimi tu Hadi nashangaa kosa langu lipi mbona nifeli somo rahisi kama Kiswahili na linalofunzwa na mwalimu shupavu kama huyu? Kusema kweli Nasra ni mkali akiwa darasani hataki masihara kamwe utasema Simba aliyepokonywa windo lake.
Ukweli alikuwa ana nitatiza akiwa mbele yangu akifunza nilikuwa si kamati kitu uzuriwe uliniweka pabaya

Siku ya Leo nikawa na Raha maana kwa mara ya kwanza tangu niingie shule hii ya Mtakatifu George hapa nchini Tanzania kutokea nchini Kenya shule ya Mtakatifu George pia sadfa ilioje, eti Nami nimekamilisha kazi ya Madam Nasra. Nayo ilikuwa kutunga shairi kichwa WOSIA ndio maana nilikuwa nikiwaza itakuaje madam aone Niko na shairi ataamini kweli?

"Hamjambo"
ni sauti nyororo isiyokera Bali kufurahisha masikio ya wengi, haikuwa mwengine alotoa sauti hiyo zaidi ya Madam Nasra.
"Hatujambo mwalimu, shikamoo"
tulimujibu mwalimu
"Marahaba, haya natumai m'memaliza kazi niliyowaachia juzi lakini kuna mtu mmoja najua hajamaliza au nakosea Hezron"
Nasra alipotaja jina Hezron aligeuza shingo yake nakutizama upande niliokuwa, macho yangu yalipogongana na yake moyo wangu ulienda mbio sio kawaida, niliganda kama nusu dakika hivi nikiwa namtazama Tu bila kusema chochote kile
"Mnaona siku Tatu bado hajamaliza huyu nimfanye nini, nambieni"
"Wewe"
Mmmh niliishtuka siyo kawaida Nasra alipoanza kufoka nilijua ni viboko vinakuja Kwa mgongo
"Pia mimi nimemaliza mwalimu" nilimujibu Kwa upole
"Hehe hehe , pia Mimi nimemaliza mwalimu"
Nasra alirudia kauli yangu.
"Haya leta kitabu chako hapa"
Nilijiinua kivivu na kuelekea mbele alipokuwa mwalimu
Nilimpa kitabu changu Kisha kuyaelekeza macho yangu kwa kifua chake dah acheni tu Nasra amebarikiwa sana
"Nenda kakae" alifanya kama kuninong'onezea
"Yusra njoo utuimbie shairi la huyu cha uvivu"
Wanafunzi wenzangu walipasua kicheko.

Yusra ni mrembo si haba, wadau Tanzania imejaa warembo
Yusra alianza kulikariri shairi langu lenye kichwa WOSIA
  "Usidanganywe na dunia, ndugu yangu nakuusia,
    wangapi waloipenda na leo washaangamia,
     Usidanganywe na mababu, ibilisi ashawapambia
    Swali kabla hujaswaliwa leo nakuusia,
    
     "Pumzi unazovuta ni neema zake jalia
       Masaa yanavyosonga kifo...

"Yusra nenda kakae"
Nilishangaa madam akimwambia Yusra akae ilihali shairi halijaisha ndio hata anaanza ubeti wa pili shairi la beti kumi hili, au Kesha gundua nimelikopi mahali ama muda umeenda nilijipa matumaini.
"Baada ya somo hili Hezron nione tafadhali"
Atakuwa ashajua nimekopi huyu si bure muda wote simalizi kazi zake hajawahi niita hata mara moja mbona Leo au ana zawadi mmmh mbona asingenizawadia mbele ya wanafunzi wenzangu.

Somo lile lilikuwa la mwisho siku hiyo alhamisi katika shule hiyo ya Mtakatifu George
Somo lile lilienda mbio hata sikuelewa liliisha Vipi
"Hezron nifwate" nilishutushwa na sauti ya madam
Niliinuka kinyonge kufuata madam Nasra nili enjoy safari Ile fupi kutoka darasani kwetu Hadi ofisi ya Madam Nasra
"Ingia ndani!" aliniamrisha madam

Itaendelea


Post a Comment

3Comments

Your Thoughts

  1. Duh!! Hongera sana...nataka mwendelezo wake...ni nzuri.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nataka mwendelezo jamani ,,,mko poa madam hr❤️

      Delete
  2. Hata usiende mbali muendelezo unakuja si kitambo

    ReplyDelete
Post a Comment