SIKU ISIYO NA JINA

Emmanuel Lee
By -
0
Ni siku ya mwisho ya uhalisia maishani mwake, ni siku ya mwisho kuishi katika maisha ya ulimwengu huru na kuishi kwenye ulimwengu wa ndoto. Kila siku akilala au kufanya jambo lolote anadhani atazinduka na kukuta siku ni ya ishirini na tano mwezi ni wa oktoba mwaka wa elfu mbili na kumi na Tisa, na aendelee na maisha yake ya kawaida.
Lakini sivyo siku zinaenda lakini kwake ni kama ndoto haamini kila jambo linalofanyika mbele ya macho yake Yuko katika ulimwengu wake kivyake akiwa anamatarajio ipo siku atazinduka na kujikuta yuko siku ile; siku hiyo si nyingine bali ni siku ya ishirini na tano mwezi ni wa kumi mwaka wa elfu mbili kumi na tisa.
Ni ndoto yake kuwa ndoto hiyo itaisha!

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)