JESTINA 6

Emmanuel Lee
By -
0


RIWAYA: JESTINA

MTUNZI: Tariq Haji

CONTACT: +255624065911


SEHEMU YA SITA.


"hawezi kunifanya mimi nionekane bwege kiasi chote hichi, tokea tuingie katika mahusiano hajawahi kunipa penzi" Matt alikuwa akiongea peke yake huku akionekana mwenye hasira sana "lakini subiri atatoa tu, anadhani mi kaka yake". Siku ya safari ilifika na mapema asubuhi wanafunzi waliondoka na kuelekea Mashvile National Park (M.N.P), walifka saa sita mchana kwa sababu kulikuwa mbali sana. Muda mwingi Alwin alikuwa na Miryam na walionekana kufurahi sana, upande wa Jestina alikuwa hana amani kabisa hasa baada kugundua kuwa aliingia woga na kukubali kudhalilishwa na Alwin ambae kwa alivyotafsiri yeye ni kwamba "sina haja ya kuwa na mwenza kama wewe hata peke yangu naweza kushinda". Hivyo ndivyo alivokuwa akitafisiri Jestina, basi walindelea kufurahia safari hiyo huku wakitembezwa maeneo mbali mbali, jioni lipofika walikwenda kuogelea katika mto.

 


 Usiku uliingia na wote waliambiwa wapumzike katika mahema yao. "Jestina....Jestina amka mpenzi" Matt alikuwa akimuamsha Jestna, "unataka nini bwana" Jestina aliongea kwa uvivu "twende nje tukaangalie mwezi". Basi waliinuka na kutoka lakini wakati wanatoka Alwin aliwoana na alihisi kuna kitu hakipo sawa kwa jinsi Matt alivyokuwa akimvuta Jestina, Hivyo aliamua kufwatilia kimyakimya. "Jestina kwa kweli nimevumilia muda mrefu na sasa nimechoka, naomba unipe penzi" Matt aliongea kwa macho makavu. "si nimekwambia tusubiri nikishakutambulisha nyumbani nitakupa" Jestina alijibu huku akijaribu kujitoa mikononi mwa Matt. "we nipe saa hivi ukishanitambulisha ndio itakuwa kawaida yetu" Matt aliendelea kusisitiza na alipoona Jestina hakubaliani nae alipiga mruzi wakatokea wenzake wengi wakiwemo waschana, kwa haraka idadi yao ilifika kama ishirini hivi.

  


Basi akatoa ishara watu wanne wakamvamia Jestina na kumlaza chini "mpumbavu wewe unajifanya unajua kubana si ndio sasa leo nataka nikuoneyeshe mimi ni nani" Matt aliongea huku akivua mkanda. Baada Alwin kuona vile alichomoka alipokaa na kutaka kutoa msaada lakini aliwahiwa na kupigwa gongo la kichwa lilimfanya aanguke chini. "we boya shuhudia ninavokata utepe wa genius mwenzako" Matt aliongea bila kuchelewa alimuinamia Jestina na kuanza kufanya uchafu mbele ya Alwin Jestina alijaribu kupiga kelele lakini mschana mmoja alimuwahi na kumtia kitambaa cha mdomo. Damu nyingi zilianza kumtoka lakini Matt hakujali hilo aliendelea kufanya yake mpaka aliporidhika alimuacha na kunyanyuka "oya anaetaka kujisevia na ajisevie tu mimi nishaafungua dimba" baada kutamka hivo vijana kadha walitaka nao kuonja utamu wa genius, jambo hilo lilimuumiza sana Alwin lakini hakuwa na la kufanya kwa sababu alikuwa ameshikwa kisawasawa. 

 


Waliendelea kupokezana lakini waliingia wasiwasi baada kuona kuwa Jestina alitulia kimya chini huku damu nyingi ikimtoka sehemu za siri. Mmoja alijaribu kumtikisa lakini hakushtuka "toba kashakufa" mmoja wao aliropokwa na kila mmoja alitimua upande wake wakamuacha Alwin peke yake ambae alijivuta mpaka alipokuwa amelala Jestina. Alimuinua na kumuweka mapajani kwake. "Jestina... Jestina amka nakuomba" Alwin aliita huku akimpiga vibao vidogo vidogo mashavuni, "Alwin najua kama unanichukie sana kwa nilokufanyia" Jestina aliongea kwa sauti ya chini yenye maumivu makali ndani yake, "hapana sijawahi kukuchukia hata kidogo, nilikuwa nakupa muda tu ugundue tu njia ulochagua sio salama lakini ukweli nakupenda sana kuliko kitu chchote kile katika maisha yangu" Alwin alijibu huku machozi yakimtoka. "we unadhani kwanini nimeenedelea na mashindano hata baada ya wewe kutofanikiwa kushiriki, nilitaka ujue tu kama sikuwa tayari kukubebesha lawama za kushindwa, nilitaka ujue tu kama bado nakujali japo mengi yametokea" aliendelea kuongea kwa kwikwi. 

 


 "Alwin kwanini unanipenda kiasi chote hicho na wakatii nilishaakwambia zamani kuwa sina hisia za kimapenzi juu yako" Jestina aliongea japo kwa tabu sana. "Jestina kukupenda mimi haikuwa na maana na wewe unipende, penzi la upande mmoja lilitosha kabisa kuishi na wewe" Alwin aliendelea kuongea huku machozi yakimchuruzika ka maji machoni mwake. "Alwin nakuomba unyamaze na uniache nipumzike kwa amani, nakuahidi kuwa nitazaliwa tena kwa ajili yako iwe katika maisha haya au yoyote yale..... tafadhali niache niende kwa amani" alimaliza kuongea maneno hayo na kukaa kimya, Alwin alijaribu kumtingisha lakini hakushtuka, alipeleka kidole kwenye pua na hapo ndio akagundua kuwa tayari Jestina alishaamuacha peke yake duniani. "no...n.o...no ple...ase Jestina...Jestina... Jestinaaaaaa" alipiga kelele na papo hapo akapoteza fahamu.

*************************************************************

(miaka kumi baadae)

 


"Jestina amka" iliskika sauti laini ikimuamsha Jestina, alikurupuka kutoka kwenye usingizi huo akihema. "karibu katika ulimwengu wa waliodhulumiwa" alisikia tena sauti ikiongea lakini aliongea hakumuona. Na alipoangalia vizuri aligundua kuwa alikuwemo ndani ya jeneza, alitoka mbio huku akijaribu kutafuta njia lakini hakuiona kutokana na kiza kizito kilichokuwepo katika macho yake. "niko wapi" aliuliza, "khah! kwani hujui uko wapi" alijibiwa ,"sasa ningekuwa najua ningeuliza" alijibu Jestina kwa hasira kidogo. "wewe upo katika dunia ya wafu kwa maana nyingine tayari umeshakufa" alijibiwa lakini alionekana kutokubaliana na jibu hilo "haiwezekani mara ya mwisho nilikuwa mikononi mwa..." hakumalizia picha za tukio la yeye kubakwa na Matt halafu akaruhusu wenzake wajisevie zilianza kurudi kichwani mwaka. Akajikuta anaanza kupiga kelele huku machozi yakianza kumotoka lakini alipojaribu kuyafuta aligundua kuwa hayakuwa machozi bali ilikuwa ni damu iliokuwa ikitiririka machoni mwake.

  


"Kweli Matt ni wa kunifanyia vile, kumpenda kote kule ameamua kunifanyia unyama wa aina ile" alijikuta akijesemea mwenyewe huku hasira zikianza kumpanda. "usijali hapa upo kwa sababu wewe umedhulumiwa na hukupaswa kufa siku ile lakini Matt na wenzake wamekuhujumu na kusababisha kifo chako na matatizo mengine mengi sana ambayo ukiyaona lazima machozi yatakutoka". Ghafla mandhari ilianza kubadilika, muangaza mkali ulitokea mbele yake na kumfanya afunge macho yake. Alipoyafungua alijikuta yuko mbele ya watu wengi sana tena walikuwa wanatisha sana. Wapo waliokuwa hawana vichwa na wengine walikuwa wakivuja damu mwili mzima. "karibu katika ullimwengu wa mpito wa watu waliodhulumiwa" aliongea mwanamke mmoja alionekana kama kiongozi wa sehemu hiyo. "hapa upo kwa ajili ya kuwalipa wale waliosababisha kifo chako na kusababisha watu wako wa karibu kufarakana, kifo chako kimeacha utata mkubwa sana duniani na haki haiwezi kutendeka kwa sababu mtu mmoja tu ndie anaujua ukweli juu ya kifo chako lakini hawezi kutoa ushahidi kwa sababu amepata matatizo ya akili" alizidi kufafanua mwanamke huyo ambae alionekana ni Malikia.

 


"oh samahani Jina langu naitwa Malkia Alina" aliongea mwanamkwe huyo baada kugundua kuwa hakujitambulisha. "na utakaa katika ulimwengu huu mpaka pale kazi yako itakapo kamilika" aliendelea kuongea. Jestina alianza kujiangalia kwa makini sana na kugundua kuwa kucha zake zilikuwa kubwa sana tena ngumu huku macho yake yakiwa meupe bila kuonesha kiini, nguo alioivaa ilikuwa imetapakaa damu iliokuwa ikiendelea kutoka katika sehemu zake za siri. Sura yake ilikuwa imeharibika kabisa na ilikuwa ni vigumu hata yeye mwenyewe kujitambua. "najua utakuwa na maswali mengi sana, lakini ukiachilia damu inayokutoka sehemu zako za siri mabadiliko mengine yametokea kwa sababu hata wewe ulimdhulumu mtu haki yake wakati ukiwa hai na si mwingine bali ni Alwin" aliongea mwanamke huyo na kumfanya Jestina atoe macho akijiuliza amemjuaje Alwin. 

 


"mimi mbona sijamdhulumu Alwin" alijaribu kujitetea lakini ghafla aliskia maumivu makali sana sehemu zake za majeraha, alipiga kelele akiomba msaada lakini yule malkia akamwambia "huku hakuna kusema uongo, na ukifanya hivo maumivu yatakuwa yanazidi kila saa". "kwani mi nilimdhulumu vipi Alwin" aliuliza kwa sauti iliojaa maumivu, "kwanza inabidi ukubali kama ulikuwa ukimpenda Alwin lakini kutokana na kuwa alikuzidi kiuwezo wa akili uliapa kutokuwa nae kama mpenzi wako, unakumbuka siku ya kwanza kukutana na Alwin nyumbani kwenu". "Ndio nakumbuka" alijibu Jestina. "siku ile Alwin alikushunda katika kitu ambacho uliamini hakuna anaekuweza hivyo tokea siku hiyo uliacha wivu wako wa kimasomo ukutawale lakini unajua alichijisemea Alwin baada kukuona unalia siku ile". "hapana sijui" alijibu Jestina, "sasa ni hivi baada Alwin kugundua kuwa ulikuwa ukilia kwa sababu amekushinda, aliapa kutokukuliza tena na kuahidi kuwa daima atakupa furaha". Jestina baada kusikia hivo alihisi maumivu makali sana moyoni mwake, huku akijisemea "kwanini Alwin".

**************************************

 Kelele ziliendelea kusikika huku kila kichaa akiongea na kuimba anachokijua yeye isipokuwa mmoja tu ambae alikuwa kimya huku akiuwangalia ukuta alioandikwa kwa maandishi fulani kwa damu, maandishi hayo hayakufahamika kabisa isipokuwa jina moja tu ambalo lilikuwa juu kabisa na jina lenyewe lilikuwa ni JESTINA. Naam chizi huyo hakuwa mwingine bali ni Alwin ambae ubongo wake uliingia ufa baada ya kifo cha mwanamke aliempenda. Yeye pekee ndie aliewajuwa wahusika lakini alishindwa kusema kutokana na kuwa hakukuwa na mawasiliano kati ya akili na mdomo wake hivo hakuweza kuongea chochote kile. "inspecta Hans hapo utajisumbua tu, huyo hawezi kuongea" dokta alikuwa akimwambia inspecta huyo ambae ameifufua kesi ya mauaji ya Jestina iliotokea miaka kumi iliopita. "Asante dokta mimi sitaki kuongea nae bali nataka kujua tu kile alichokiandika kwenye ukuta, kivipi kinahusiana na kifo cha Jestina". 

 


Alitoa camera ndogo na kupiga picha yale maneno, aliporidhika aliondoka na kurudi kituoni kwa ajili ya kuendelea na upelelezi. Inspector Hans ni afande machachari sana na ni kawaida yake kuona kila mtu anapata haki yake. Hivyo baada kuhamishiwa Mashvile alikutana na kesi hiyo ambayo ilishaafungwa muda mrefu. Lakini kutokana na ukaribu wake na profesa Alexander Harison aliombwa aifungue upya kwa kile alichoambiwa na profesa huyo kuwa "ili kumrudisha Alwin kama alivyokuwa zamani ni lazima kesi hii itatuliwe". Aliayakumbuka maneno hayo alioambiwa na rafiki yake huyo. Profesa Alexander alifanya kwa sababu ya mwanae Miryam ambae ilibidi amhamishe mji baada matatizo yaliotokea lakini pia alihofia mwanae kuchizika. Hivyo akaamua kuvalia njuga kesi hiyo ambayo ni ngumu kupita maelezo kutokana na kuwa mwenye ushahidi hawezi kuutoa.


ITAENDELEA

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)