PENDO LAKO SUZAN

Emmanuel Lee
By -
0

  PENDO LAKO SUZAN


Pendo lako Suzana, Linanijaza furaha

unanipenda ja mwana, kwa mamaye nafuraha,

Jadi nayona ja jana,, u'vyokuwa na madaha,

Pendo lako Suzana, talinyonya hadi kifo.


Talinyonya hadi kifo, nahidi sitokuacha

takukumbata ja pillo , mpaka ifike macha

'lifanya tumbo lako, libebe watoto pacha

Pendo lako suzana, lanitia uwazimu


Lanitia uwazimu, mwana wa Mkamba

nilokujia ilimu, Luo naacha Mimba

Ugunja sio Kisumu, napaona Kama Pemba

Pendo lako suzana, limenipofua macho


Limenipofua macho, mpaka mbele sioni

kibe nimelala nacho, nimetafuta sioni

'me'ndika kuta za choo, Jina lako Suu zani

Pendo lako suzana, ndilo 'menitoa Chonyi.


Ndilo 'menitoa Chonyi, nahisi Mungu kapanga

nitakulinda kwa Usunyi, kwa manati na Upanga

'tanizalia Akinyi , babaye akiwa Chonga

Pendo lako suzana, nipe hadi uzeeni


Nipe hadi uzeeni, nikunywe yako maziwa

juu ata paka uzeeni, hunyweshwa hata maziwa 

nami nakusihi jamani, 'sininyime 'go maziwa

pendo lako suzana, lanikosesha usemi.


Lanikosesha usemi, yanibidi nitamatishe

wajua wewe na mimi, hata tujijumulishe

'takula chakula "yummy", tuachane tsalakushe

pendo lako suzana 💋💋❣️❣️ only God knows.



Created by

                       Chonga@254✌️

Tags:

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)