NAISMA 3

Emmanuel Lee
By -
0

 NAISMA. 3

Mtunzi: Zamrata mbwana.


+255698095257


Haidary Frut aliludi kwake akiwa hana Raha Aya kidogo alimkuta mdogo wake Fahadi ameanda ugali na dagaa wakulumagia na kachumbali 

"Oooh! Bora umeludi mda muafaka Bro !

Haidary Frut alijibwaga Pale chini na kunyoosha miguu uku akijishika kichwani

"Yani sitaki ata kula uwo ugali wako sina hata amu yakula !


"Khe ! Kaka Kuna msiba ? Mbona ivo ! Tena 


Fahadi alikuwa anatenga maji ya kunawa na ya kunywa aliyaweka chini na kubaki kumshangaa Haidary . Haidary Alichukua Yale maji ya kunawa akajimwagia kichwani yote 


"Kheeeeee!!!!!!!!!!!!!

Fahadi alibaki kushangaa

"Naisma ! Naisma why ! Aaaaaah!


"Naisma ??? Amefanya Nini ? Kimemkuta Nini ?


"Fahadi mdogo wangu ! Naisma amenikataa live bila chenga !


Haidary Frut alimaliza kuongea Ivo na kuangua kilio 


"Khaaa ! Kumbe ndo Ivo tu ! 😄 ! Halooo Ila wewe Rafiki angu ukaoge tu maji ya bahari aiwezekani kila Demu akukatae wewe tu ! 


💦💦💦💦💦💦💦💦💦💦


Masiku yalikatika na Lamek alionekana Gest (Nyumba za wageni) za Bei rahisi  mtaani alimkumbuka mpenzi wake Warda na hakukata tamaa kila siku alikuwa anamuomba msamaha  na Warudiane.


Maisha ya Lamek yakawa magumu zaidi hakuitwa popote kwenye kazi zake za fashion wala video . Kulipia Gest kulimshinda na kuhamia kwa Rafiki ake Uswazi nakuanza Ayo maisha alimkumbuka Sana Warda wake ambae alikuwa anamlea na kumtimizia kila kitu cha Ndani  na kumpa ela ya matumizi 


Alipata tabu maisha ya mswahilini na alijiona kabisa kuludi mkoani kwao mtwara kunamuita kabisa Tena na miguu jiji lishamshinda ndipo alipokumbuka Kama Kuna mtu anaitwa Naisma na alipanga amtafute Tena kwani aliamini Naisma angemsamehe tu kwani Anampenda Sana


💦💦💦💦💦💦💦💦💦💦


Masiku yalikata na Haidary Frut alikata tamaa kabisa ya kuendelea kunisumbua Naisma ambae hakujali kabisa kuhusu upendo wake na aliamua kuendelea na maisha yake ya kila siku


Siku iyo Naisma aliingia Ofsini kwake na kukuta maua 💐 juu ya meza yake


"Novoooo!!!!


Naisma aliita kwa hasila mno


"Kuna Nini ? Boss Naisma


"Nilikwambiaje ? Kuhusu uyo Haidary ?


" Amefanyaje Tena ?


"Uoni Ayo maua ! Naomba uya toe Sasa ivo kabla sijachafukwa !


"Du !  Ayo maua nikweli kaleta Haidary Frut mbona Mimi sina Taarifa !


Naisma aliyafata Ayo maua na kuyashika kwa hasila mno na kutaka kuyatupa nje kabla ajayatupa alishangaa kuona kadi ilioandikwa (I'm sorry Baby . Lamek)


"Lamek !!!!!!!!!!!!!!!


Moyo wa Naisma ulilipuka baada ya kugundua alietuma maua alikuwa ni Lamek 


"Lamek !!! 

Novo alisema kwa mshangao baada ya kumuona Lamek akiingia Ofsini . Apo Apo mlinzi alikuja huku akihema 

"Samahani Boss ! Nilijalibu kumzuia lakini nimeshindwa !

"Lamek umefata Nini we ! Msaliti Toka ! Kabla sijakuumiza Hapa!

Novo aliongea kwa hasila mno na kutaka kumpiga Lamek lakini wafanyakazi wengine walimshika 

"Naisma mpenzi wangu ! Naomba tuyaongee yaishe ! Mimi bado Nakupenda Please!



"Nakuomba ! Naisma tuongee bado Nakupenda !


"Toka ! Toka ! Lamek !


Lamek akamkimbilia Naisma na kumkumbatia kwa Nguvu 


"Please Baby ! I'm sorry !


Aisee kweli mapenzi ayaingiliwi  wapendanao wakigombana kaa pembeni wakielewana wape hai!

Ndo hii. Naisma alilegea na kumkumbatia Lameck na yeye kitendo ambacho Novo alichukia Sana nakuondoka moja kwa moja Kwao hakukaa Tena Ofsini siku iyo


Naisma waliyamaliza yeye Pamoja na Lamek na siku iyo walitoka na kwenda mgahawani Pamoja . Siku iyo penzi lilikuwa la Moto Kama ndo kwanza wanajuana waliongea kwa mda 


"Naisma Baby . nashida Sina trend yeyote mjini nipo nipo tu ! Sina pakukaa Yani inabidi tu unisaidie unipangie ili nisiludi Tena kwa Yule shetani Warda 👺! Na pia unipe Ela ya matumizi ! Yani Baby nanikipata tu Ela katika kazi zangu  zote nakupa wewe !


Lamek aliongea uku akimuangalia Naisma kwa jicho la wizi akiwa hana uhakika Kama Naisma atakubali lile swala


"Opsuuu!!!! Mh ! Na vipi ? Kuhusu kunioa !


"Ata saivi nipo tayari Baby !


"Okay Wiki ijayo nitafanya Ivo ulivyo Nambia na Mchakato wa Ndoa utaanza!


"Mh ! Sasa Baby ! Mimi Sina hela  ya kukuoa kwasasa ! Labda Adi kazi iingie !


"Wewe upo tayari kubadili Dini iliunioe Mimi ????


"Ndiyo Naisma . ni.ni.nipo.t.a.ya.ri!


"Okay ! Basi kila kitu niachie Mimi !


🌿☘️☘️☘️☘️🌿☘️☘️☘️☘️🌿🥥


Baada ya Wiki kupita kila kitu kilikuwa kwenye mstari mapenzi Yao yalikuwa Moto Moto 


Naisma alimpeleka Lamek Kwao kumtambulisha kwa Baba yake lakini Baba mtu akupendezwa na Lamek ila kwa kuwa mwanae alimpenda Basi aliamua kutomuingilia maamuzi yake 


💮💮💮💮💮💮


"Oooh ! Jamani leo mnafuraha Tena sio kidogo !


Naisma aliongea akiwa na marafiki zake Novo pamoja na Tina wakiwa wanapata chakula cha mchana


"Furaha gani ? Iyo shosti !


"Oooh ! Tina furaha yenyewe ni Mimi na mpenzi wangu Lamek tumepanga tuvalishane pete 💍

Kesho Hapa Hapa Ofsini !


"Oooh ! Waoooo ! Kweli shosti ?!!!


"Ndiyo ! Nikweli Tina 


"Oooh ! Hongera Sana jamani !


"Asante !


Novo alivyosikia Ivo akutaka kuongea kitu aliinuka nakuondoka zake !


"Khe ! 😄 Novo mbona unaondoka Gafla kulikoni !


Naisma alimuuliza Novo Ila alijua tu kuwa Novo ampendi Lamek


"Naenda kwa Haidary Frut kula matunda !


"Kheee!!!! Jamani kumbe uyo mtu bado yupo kweli 😄 ! Twendeni wote tukale matunda buarusi wawatu niongezee supu supu mwilini !


Naisma alikuwa anaongea kwa malingo adi anakela Yani alikuwa na furaha iliyo pitiliza 


Walielekea moja kwa moja kwa Haidary Frut ambae alikuwa bize na kumenya zake machungwa 🍊🔪🍊 akiwa na mdogo wake Fahadi


"Mambo ! Haidary Frut !


"Paaaaaa! Moyo wa Haidary ulishtuka Baada ya kusikia sauti ya Naisma ambae aliachia Tabasamu Pana usoni mwake 😄

Akiwa kaongozana na Novo berry pamoja na Tina


"Po.po. poa ! Mrembo Naisma sijui wewe!


"Mimi nipo poa kabisa !


Haidary Frut alimuona Naisma akija kwake na kumkumbatia na kumbusu na kumwambia "Mimi pia Nakupenda Haidary Frut na nipo tayari kuolewa na wewe "


"Oya ! We Haidary Frut mbona umeganda tu unamshangaa Naisma! 


Kumbe Haidary Frut Alikuwa anawaza tu.Naisma hakuwa na habari na Haidary Frut atakidogo


"Haidary kesho Naveshwa Pete 💍

Jioni Kama hutojali naomba uzurie !!!


"Naisma aliongea kwa malingo uku akimuangalia Haidary Frut usoni kwa dharau . Haidary Frut alishindwa kuzuia hisia zake na alishindwa kuzuia machozi yalioloanisha mashavu yake na alijikata mkono mda huo na kutoka damu 🔪🩸  


"Kaka ! Pole !


Fahadi anamkimbilia Haidary Frut na kumpa leso 


"Oooh !!! No jamani ! Hahahaha Taarifa za kuveshwa Mimi Pete 💍

Ila wanajikata wengine jamani !


"Inatosha Naisma !


"Kheee ! Nimefanyaje jamani !


Novo aliongea kwa jazba na kumkataza Naisma Ache anachokifanya 


"Yani wewe mzalau tu ! Uyu kaka lakini ndo mwanaume pekee mwenye mapenzi ya dhati kwako ! Kushinda uyo Lamek wako ! Na ndomana anatumia kwa ajiri yako !


"Msiuuuuu !!!!


Naisma alisonya nakuondoka zake  na kuwaacha wenzie Pale 


🌺🌺🌺🌺🌺


Siku ya pili ulifika na kweli Novo alimvesha Pete 💍 Naisma na Ndoa ilianza kutangazika lasmi kila Kona Naisma na Lamek


📷📷📷📷📷


Masiku yalikata na siku iyo Naisma aliingia Ofsini kwake alishangaa wafanyakazi wake wakinong'onezana uku wakimuangalia yeye 


Wengine walikuwa wakiangalia kwenye Simu walivyomuona walizuga 


"Mh ! Ofisi hii Leo imepatwa na Nini sijui !


Naisma alijiwazia na alipoangalia pembeni aliwaona Rafiki zake Novo pamoja na Tina wakiangalia kitu kwenye Simu na aliposogelea alitambua ni video hakuamini macho yake baada ya kumuona Lamek kwenye Ile video Tena akiwa na Warda wakiwa Wana Romance kwa mahaba mazito


Paaaaaa! Moyo wa Naisma ulilipuka mda huo huo  akijishika kichwani 🤦 


Wenzie walibaki kumuangalia tu alijihisi kizungu zungu mda huo huo 


"Naisma vipi Tena 😳 !


"Ni Lamek huyu  anaetaka kumuoa Boss Naisma ! 


"Ndiyo ! Kweli ni yeye !


Wafanyakazi wengine waliokuwa pembeni walisema Ivo mda huo huo Naisma alidondoka chini na kupoteza Fahamu.


Ni Ndani ya Hospital 🏥 ambako alilazwa Naisma ambaye alikuwa kalazwa na kutundikiwa dripu  


Familia ya Mzee Kazumali ilipata habari  na kuja kumuona Naisma Pale Hospital 🏥 


"Samahani ! Mzee tunajua Kama unataka kumuona Binti yako lakini uluhusiwi kwa Sasa !


Alikuwa ni Daktari ambaye alikuwa anamwambia  Mzee Kazumali ambaye alivulugwa baada  ya kusikia mwanae kalazwa Baada ya kuona video ya Lamek 


Walikaa adi jioni ndo akazinduka wakaenda kumuona 


"Baba ! Lamek ame .....


"Najua Binti yangu ! Nyamaza tu 


"Jasmini ! Lamek amekuja ?


"Msiuu ! Ivi Dada bado unamtaja  uyo mtu apa !


"Mnaruhusiwa  kuondoka na mgonjwa wenu ! 


Aliingia Daktari na kuwapa maelezo na baada ya mda kidogo walikuwa washafika Nyumbani kwao 


Walivyofika Naisma alienda moja kwa moja chumbani kwao ambako alilala yeye na Mdogo wake Jasmini  . Alivyofika tu akachukua Simu yake na kumpigia mpenzi wake Lamek 


"Hello! Lamek !


"Eeeheee ! Unasemaje ? 


"Eti? Unanijibuje Lamek mwenzio natoka hospital eti ! Nililazwa kisa wewe !


"Khe ! Kisa Mimi ? Nimefanyaje tena jamani !


"Unajifanya hujui? Si ile  video  yenu wewe na Warda unafikili ningekuwa kwenye Hali gani ?


"Enhe ! Kwaiyo ?


"Lamek ndo unanijibu Ivo  ! Embu jioni Naomba tuonane !


"Sawa ! Haina shida !


☘️☘️☘️☘️☘️☘️


Hatimae jioni ilifika na Naisma alijiandaa na kujipodoa kwa jili ya kwenda kuonana na Lamek 


"Khe ! 😄 Dada mbona umekwatuka Ivo  wapi ?


"Mh ! Naenda kuonana na Lamek !


" Eti unaenda kuonana na Lamek ? Yani Dada angu! Yeye hajaja kukuona na bado unatoa miguu unamfata ! 


"Eee! Sijakuomba ushauli !


"Dada ni wewe tu ! Utaki kuelewa ila kila kitu kipo wazi Lamek Hana mapenzi na wewe !


"Mimi na Lamek atuwezi kuachana ata iweje tunapendana Sana ! 


☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️


Baada ya mda kidogo waliokuwa Bar Naisma pamoja na Lamek


"Mh ! Nakusikiliza Naisma ?


"Lamek ! Mpenzi wangu mbona umebadilika Sana ! Sikuelewi siku izi !


"Naisma bola tu nikwambie ukweli sitaki kukuongopea ni hivi ! Warda nimetoka nae mbali kabla yako Ivo  kuwa na wewe niliteleza tu na Sasa Ameamua kunisamehe sitaki  Tena kuludia makosa ya mwanzo !


"Jamani mbona nilikubali kila kitu ambacho ulinambia si nimefanya kama Warda jamani !


"Naisma jalibu kunielewa Nampenda Sana Warda na sio wewe !


"Apana ! Lamek unanitania unataka kuniumiza tu makusudi Mimi sindo unanipenda zaidi kuliko uyo Warda shetani ?


"We ! We Dada unawazimu Yani mpenzi wangu Mimi anaeniweka mjini umuuite Shetani ! Tena usiludie iyo kauli yako !


Naisma aliongea uku akiwa kamshika mikono Lamek uku akiwa analia 😭


"We ! Dada naona atuelewani ! Kwaheli !


Lamek aliinuka na kuanza kuondoka zake na Naisma alimkimbilia na kumshika miguu kwa Nguvu uku akiwa analia


"Apana Lamek Mimi siwezi kukuacha Nakupenda ! Angalia ! Angalia! Watu watanichukuliaje Mimi ni Aibu jamani sema kiasi chochote cha pesa mtakupa !


Lamek alimpush Naisma na kuondoka zake Naisma akabaki analia kwa uchungu 


Naisma alianza kuagiza bia nakulewa Sana aliludishwa tu na boda boda anaemjua akiwa ajitambui hata kidogo . Baba yake Naisma alichukia Sana 


"Yani huyu Lamek anamtesa Binti yangu Naisma !


"Anataka mwenyewe Baba uyo mwanao ! 


"Sasa Basi nikiwa Kama Baba kea haibu tulioipata katika Familia yetu ! Naisma ataolewa na Haidary Frut maana ndo mwenye mapenzi ya dhati na Binti yangu ...


"Eee! 😳 ! Eti unasemaje Baba


Tulipo 🌷 ishia nipale Naisma alivyo kataliwa na Lamek Live na Naisma alichanganyikiwa na kwenda kuzifakamia bia na hatimae alilewa Adi kushindwa kujitambua  na kuludishwa na boda boda kwao kitendo ambacho Baba yake Naisma Mzee Kazumali alikasirika Sana . Nakuchukua maamuzi mwanae Naisma aolewe na Haidary Frut atake asitake ..


Songa nayo 🍊......


Naisma alipata Fahamu Asubuhi na aliamka na kujihisi mwili wote ukiwa mchovu "aaaaaah"  Naisma alijinyoosha na kutoka kitandani na kaenda kuoga na alivaa vizuli na kwenda sebleni kwaajili ya Chai ☕🍞 

Alikuta Familia yake yote ipo sebleni kuanzia Baba yake, Mama yake na mdogo wake ambaye alikuwa na mwanae ambae alianza jutembea kilikuwa kimekua kua.Walivyo muona Naisma wote walikaa kimya kwa mda


"Mwanangu Naisma ! Unaendeleaje ? Saivi 


"Sijambo Mama !


Mama Naisma alimuliza mwanae kwa unyenyekevu mkubwa


"Utaenda kazini leo ? 


Naisma aliulizwa na Baba yake mzee kazumali huku akimkazia mwanae Naisma macho. Naisma alikataa kwa kichwa kwamba haendi 


"Anha ! Unaona Aibu sasa ? Si ndiyo ? Unafikiria utaangaliaje watu usoni baada ya Ayo yote aliokufanyia uyo mpuuuzi wako ? 


Mzee Kazumali aliongea kwa hasila mno. Naisma hakuwa na lakuongea zaidi ya kukaa kimya 


"Samahani ! Baba !


"Okay ! Mimi na wewe ukitaka tuelewane kuna Jambo moja tu ukikubali sawa !


"Jambo gani Baba ! 


"Ni wewe kufunga Ndoa na Haidary Frut !


"Eeee !!!!!! 😳 Ni masikio yangu au sijakuelewa ! Unasemaje Baba 


"Ni hivi ukitaka Mimi na wewe tuelewane uolewe na Haidary Frut !


"Kheee !!!!! 😳 Ba.ba.ba. unamjua huyo ! Ni . ni . Umemjuaje. Oooh !


"Ndiyo nilimfahamu ile siku nilivyokuja kukagua Ofisi ! Ndo siku niliyomuona nilimuona nikijana mwenye heshima na adabu Ivo nikamuuliza Novo berry akanielezea kila kitu kuhusu wewe ! Na yule kijana !


"Oohooo ! Halooo !😳 Yani Novo kalibu ! Tobaaa ! Wee !


Naisma alinuka kwenye kile kiti na kuweka mikono kichwani na kuanza kupiga piga miguu alivulugwa Mara moja 


"Aaa! aaaa! Apana hiyo sio haki Baba ! Sipo tayari kuolewa na Haidary Frut ! Mimi na mpenzi wangu Lamek tu !


"Lamek ! ? Lamek yupi ? Uyo aliekukataa Dada angu Naisma 


"Yani uyo ! Lamek wake! Anaemtaja Apo ndo atutaki hata kumuona kwenye Familia yetu ! 


"Kheee ! Hata wewe Mama ndo unasema Ivo 😳 na Naisma ? Kumbe lenu moja eee !!!!


"Ndiyo mwanangu Naisma sipendi kuona unazalilika kila siku Kama Baba yako kamchagua Haidary ! Sawa Kama ndo anamuona ndo sahihi olewa nae ! 


"Nihivi kama utaki kuolewa na Haidary Frut Basi katafute Familia yako ! 


Baba Naisma aliongea uku akiwa anagonga meza kuonyesha msisitizo . Naisma alimuangalia Mama yake na mdogo wake Jasmini nao walikaa kimya kuashiria msimamo wao na wao ndiyo uwo


"Apana Baba siwezi kufanya Ivo na Nyie ndo Familia yangu ! Siwezi kuwa na Familia nyingine !


"Sawa ngoja tumpigie Sasa hivi Haidary Frut aje tumwambie na akiwa tayari taratibu za Ndoa zifuate !


Baba Naisma Alichukua Simu yake na kumpigia Novo berry aje na Haidary Frut....


🍃🍃🍃🍃


Novo alivulugwa  mda huo huo na akaenda kwa Haidary Frut Alimkuta ndo anafungua biashara yake ya matunda 🍉🍉🍊🍊🥝🍏🍈🍒🍎🍓🍌🍍🥭🍊🍑🍐🍇


"Ooh ! Rafiki angu Novo berry kalibu !


"Asante ! Mambo !


"Poa ! Kalibu Matunda Novo berry kila aina na Ndizi unazopenda ndo zimejaa kibao


"Aaah ! Unajua Haidary ! Aaah ! Yani ! Ni.ni.aaa...


Haidary Frut aliacha kupanga matunda na kumgeukia Novo berry


"Mh ! Mbona sikuelewi Rafiki angu Novo ! Kuna shida gani ? Kwani 


"Samahani Haidary Rafiki angu sikutegemea Kama Mambo yangekuwa makubwa ivi !


Novo aliongea uku akifinya finya mikono ishara ya kuvulugwa 

Na kumuacha Haidary Frut akibaki na alama ya mshangao


"Mh! Mambo gani Tena? Ayo makubwa !


"Yani ni hivi ! Sikuelewi ulivyokuja Ofsini...................) Kwaiyo Baba Naisma anakuita kwake 


"Kheee ! 😳 Ndo ilivyo kuwa Rafiki angu !?


"Ndi.ndi.ndi.yo Samahani ! Haidary !


"Da ! Ushaniuza Rafiki angu ! Lakini Mimi nilishakata tamaa kabisa ya kumpata mwanae Naisma ! Du ! Sawa twende 


Haidary Frut alimuachia mdogo wake Fahadi biashara na yeye na Novo walielekea kwa kina Naisma 

Na Haidary Frut alitembea Kama anapelekwa machinjioni

🔥🔥🔥🔥


Walifika na kukalibishwa Ndani walikuta Familia ipo pale Naisma alishtuka alivyomuona Haidary Pale na Novo.Haidary alikaa kimya na Mzee Kazumali alimueleza Haidary alichomuitia na Haidary Frut alishindwa kuzuia hisia zake za furaha na kutabasamu kwa furaha 


"Je upo Tayari kumuoa Binti yangu Naisma ? Haidary Frut 


Haidary Frut kabla ajajibu alimgeuzia macho Naisma ambae alikaa kwenye kiti cha pembeni na Alivyo muona Haidary Frut anamuangalia akimkazia macho na kutikisa kichwa ishara kwamba Haidary Frut asikubali....🔥🔥💥


Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)