NAISMA 5

Emmanuel Lee
By -
0

 NAISMA 5

Mtunzi: Zamrata Mbwana

No.+255698095257 


Tulipo 🌷 ishia nipale Naisma alivyo ondoka bila kuaga baada ya kuona Zalau zimezidi kwa Recho.alianza kuondoka uku wapambe Wake walimfata nyuma Novo berry pamoja na Tina...


Songa nayo 🍊...

Naisma aliludi kwao akiwa Ana Raha kabisa alifika chumbani na kwenda adi kwenye kabati lake la nguo la milango mitatu mlango wa Kati ulikuwa unakioo kikubwa alianza kujiangalia kwa makini na kujigeuza geuza 


"Ivi Kale kasichana kanajikuta Nani ? Rihana ama ! Yani ! "Eti usiondoke Haidary ! Yani mume Wangu na ampangie pangie Yani sikipendi kile kabinti ata kidogo !


Naisma alimaliza kuongea na kubadili nguo za kazi na kwenda sebleni na kula chakula cha usiku alikaa kwa mda aliangalia TV lakini Haidary akuludi hatimae saa 4 inaendea saa 5 Haidary akuludi, watu wote walienda kulala 


Naisma aliamua Aende kulala Adi saa 5 bado Haidary Frut ajaludi na Naisma akaamua ampigie Novo berry


"Hello ! Novo berry?


"Khe ! Shosti kulikoni usikuu Kuna shida gani!???


"Mh ! Novo Haidary ajaludi Adi saizi uku ! Naomba unitumie namba yake !


"Khe ! Khe 😄 makubwa haya ndo kwanza naona mtu Ana namba ya mumewe!


"Acha maneno yako Basi na Wewe !


"Okey ! Nakutumia !


Naisma alitumiwa namba na alimtesti Haidary Frut "nambie Kama uludi nifunge mlango Wangu " 

Naisma alituma SMS iyo kwa Haidary Frut akijifanya hajali chochote na Haidary Frut akajibu 

"Naludi mkewangu nipo njiani ni foreni tu "


"Opsuuu!!!!! 


Naisma alishusha pumzi na kulala zake baada ya mda kidogo . Haidary Frut aliingia Ndani alimkuta Naisma ashalala alimsogelea na kumfunika shuka na kumbusu kwenye paji la uso kwa hisia Kali "I love you "

Haidary alienda kwenye Sofa na kulala zake.Kumbe Naisma akulala usingizi alifumbua macho na kutabasamu.....


🌷🌷🌷🌷🌷

Asubuhi na mapema Haidary Frut aliwahi kuamka na kumuandalia  mkewe Naisma Chai ☕🍞🍵🥄

Naisma alivyo amka alimkuta Haidary Frut kamuandalia Chai ya Nguvu . Haidary Frut alikuwa kashaoga na kashavaa alikuwa katulia tu akimsubili Naisma amke . Naisma aliamshwa na harufu mzuri ya Supu. Mchemsho wa Supu ya samaki mbichi


"Kalibu Chai mke Wangu !


Naisma hakujibu kitu alimtizama tu Haidary Frut ambae alikuwa kapendeza Sana siku iyo alikata nywele zake na kupaka super black na kuvaa shati lake la dog dog na jinzi yake mpya na saa yake mpya alipendeza Sana Haidary siku iyo chini akiwa na laba nyeupe mpyaa


Naisma aliingia bafuni na kuanza kuoga uku akiwa kabeba nguo zake za kubadilisha kabisa


"Mh ! Ivi Yule ni Haidary Frut kweli ! Mbona anaonekana Handsome Sana leo sijui anaenda wapi !


Naisma alijiwazia Baada ya mda kidogo alikuwa kashavaa na Alifika chumbani na kujipodoa na wakati haikuwa kawaida yake alijiangalia kwenye kioo 


"Mh ! Apa kidogo nimemfikia Recho ! 


Alijisemea moyoni nakukaa chini nakuanza kunywa Chai walikula wote yeye na Haidary Frut


"Umependeza kweli ! Leo mke Wangu !


"Asante! Mh ulisema Recho Ni Rafiki ako uliesoma nae !??


"Ndiyo ! Ni zaidi ya Rafiki ! 


"Okay ! Ni mpenzi wako si ndiyo ! 


"Apana ! Siwezi kufanya Ivo Naisma 


"Okay ! Twende kazini ! Utatumia usafili Wangu !


Baada ya Mda Naisma na Haidary Frut walifika sehemu zao za kazi 

Na kila mtu aliendelea na kazi yake  . Mda wa Runchi ulifika Kama kawaida Yao Naisma pamoja na kampani yake Novo pamoja na Tina walienda kwa Haidary Frut. Lakini walishangaa hawakumkuta Haidary Frut Bali walimkuta Fahadi . Walipomuuliza Fahadi aliwaambia Haidary Frut aliondoka na Recho Toka Asubuhi 


"Ohoooo ! Umekwisha shosti 🙊!


Novo berry alidakia nakusema Ivo 


"Wameenda wapi ?


"Khe ! Yeye atajuaje Tena !


Tina alimuuliza Fahadi na Novo berry akamjibu


"Wewe Kama unajua tuambie tumfate uko uko uyo Haidary Frut na Recho Wake tukamchambe uwo uchotala wake umuishe Leo wa kudandia waume za watu 👌 ! Loh! Mwanamke Hana haya Yule Yani naona mnanichelewesha !


Tina aliongea kwa hasila uku akipiga piga mikono kishari 


"Apana Tina !!! Acha haina haja tondokeni ! 


"Khe ! Yani ! Khe !!! Shosti 


✨✨✨✨


Hatimae jioni ilifika Naisma alikuwa na mawazo Sana siku iyo

Adi mdogo wake Na wazazi Wake walimuuliza Kama anaumwa lakini alisema haumwi Mda wa chakula cha usiku ulifika na wote walikuwa wanakula ndipo Baba Naisma alipoanza kumuulizia Haidary Frut

"Kwani mkwe Wangu ! Haidary bado ajaludi kazini !


"Ndi.ndiyo ! Baba


"Kwani ! Leo hamkuongozana wakati wa kuludi ?


"Ndi.ndi.ndiyo Baba !


Mda huo huo Haidary Frut aliingia akiwa kabeba mfuko mkononi na alisalimia na kumsalimia mkewe ambae alitikia Kama ataki. Haidary Frut alienda chumbani na kuweka mzigo Wake na kwenda kula Na yeye . 

🍀☘️


Mda wa kulala ulifika na watu wote walienda kulala .✨


Naisma alifika chumbani na kukaa kwenye Sofa . Haidary nae alimfata na kukaa pia 


"Nambie malkia wa moyo wangu !


"Ulikuwa wapi ? Leo kutwa mzima ?


"Nilitoka na Recho !


"Yaani kilahisi rahisi tu unanijibu Ivo kwamba ulikuwa na Recho na hivi ndo vitu alivyokununulia !???


"Ndiyo ! 


Naisma alivimwaga vile vitu vyote Pale chini na kukuta Adi boxer za Ndani 


"Huu ni ulafiki wa Aina gani Haidary Frut mbona sikuelewi kabisa ? Ulafiki wakununuliana Adi nguo za Ndani !


Naisma aliongea kwa hasila uku akimwangalia Haidary 


"Unanionea wivu Naisma eee ! Nambie nipo tayari kuvunja ulafiki wa Mimi na Recho Kama utasema unanipenda ?


"Khaaa ! Yani Mimi nikuonee wivu wewe !


Naisma aliongea Ivo kwa Dharau Apo Apo Haidary Frut alimshika uso nakumpiga busu Naisma na wakaanza kuromance ......🔥


Naisma alimsukuma Haidary Frut kwa nguvu "Chizi Wewe ! 

Naisma aliongea Ivo nakukimbilia kitandani na kujifunika shuka gubi gubi Adi usoni . Haidary alibaki akitabasamu tu uku akimuangalia Naisma 


.........🦋🦋🦋.......


Hatimae ni siku nyingine Tena katika ofisi na ulikuwa Ni Mda wa Runchi Naisma akiwa na Rafiki zake Novo pamoja na Tina.....🔥


"We !!!!! Alikuja Hadi na Boska Haidary 😳!!!!!!


Novo berry aliuliza kwa mshangao mno


"Ndiyo jamani !


"Ivi Naisma kwa Nini usimkubali tu Haidary Frut Kama mumeo unajua Kama Recho anaweza akamchukua mazima Haidary Frut !


"Aaah!!! Tina ushaanza Mimi Sina haja na uyo Haidary Frut namuisabia miez 3 tu tuachane na Aende kwa uyo Recho Wake !!!!


"Khe 😄 shosti gaidi we ! Yani humpendi ata kidogo Haidary wawatu ! 


Tina aliongea Ivo uku akicheka 


"Apana simpendi !


"Mh ! Usije ukatulilia tu apa !


🦋....🌺..🦋


"Yes ! Dady ni Nyumba namba 2️⃣0️⃣5️⃣ ? Okay nishaiyona dady Thanks !


Alikuwa Ni Recho ambaye alikuwa na Gari yake ya kukodi ambayo alipakiza mabegi yake ya Nguo na alikuwa anaelekezwa Nyumba ambayo anatakiwa afikie . Recho alifunguliwa geti na akaingia Ndani na alishuka na kuingia Ndani "oooh ! Kalibu Binti yangu na jisikie uko Nyumbani "


Alikuwa Ni Mzee Kazumali Baba yake na Naisma ndo alikuwa anamkalibisha Recho kwake. . 

Mzee John alikuwa Ni Baba yake Recho pia ni mfanya biashara nwenzie Baba Naisma walishilikiana Mara nyingi Na Mzee Kazumali . Na Recho alikuja kwajili us Biashara ya Baba yake Kama ilivyo kwa Naisma na Recho alitokea mkoani Mwanza alisomaa Dar ila baadae waliamia Mwanza na Baba yake aliamishia biashara zake uko 


Recho alikabiziwa chumba ambacho kilikuwa na kitanda umo umo Alitoka sebleni akiwa na kompyuta yake 💻 nakuanza kuseti maswala yake ya kazi Mda kidogo alijisikia kiu na kwenda kunywa Maji jikoni .


Ndo mda huo huo Haidary Frut alipita pale sebleni nakuelekea chumbani . Walikwepana na Recho hawakuonana 

Recho aliludi sebleni nakuendelea na kazi yake . 🔥 Mda huo huo alingia Naisma 

Uso kwa uso na Recho "Naisma !!!!!!!!


Recho alishangaa kumuona Pale Naisma ambae alijua moja kwa moja Ni mke wa Rafiki yake Haidary . Paaaaaa !


Naisma alishtuka kumuona Pale Recho moja kwa moja alienda chumbani na kumkuta Haidary Frut kajilalia zake kitandani uku akiwa anachezea kiswaswadu chake 


"Okay ! Imetosha ! Sasa Haidary ! Mmeona kufanyia uko nje haitoshi Sasa umeona bora umlete umu umu Ndani ! Uyo kahaba wako !


"Kheeeeee !!!!!! Umekuaje Naisma mbona sikuelewi unaongea kuhusu Nini ?


"Okay ! Si unajifanya uelewi ! Nifate !


Haidary Frut aliinuka nakumfata mkewe Naisma ambae aliongea kwa hasila mno na alitibuka kweli siku iyo 


Walvyo fika sebleni walimkuta Recho akiwa anachezea Kompyuta yake . Recho aliachia Tabasamu Pana Baada ya kumuona Haidary Frut


"Khe ! 😳 Recho umefata Nini !!?? Hapa !


"Haiii!!!! Haidary 🥰


"Shenzi ! Kabisa ! 👉 Kamleta Nani uyu Kama sio Wewe ! Haidary 


"Oooh ! Wanangu mmeludi sangapi !? Kutaneni na Recho Ni mshilika katika kampuni yetu na tutakaa nae apa kwa kipindi chote atakacho kuwepo apa dar mumchukulie Kama mwana familia mwenzenu !!!


"Kheee !!!!! Ba.ba.baab. so Recho ataishi Hapa 😳 ?


"Ndiyo ! Mwanangu Naisma!!!


🔥🔥🔥🔥🔥


Naisma aliludi chumbani akiwa ana Raha kabisa moja haikai mbili haikai 


Mda wa chakula ulifika na Recho alikuwa amakaa meza ya kalibu na Haidary walikuwa wanaongea na kucheka . Naisma alifika Pale Alivyo waona Roho ilimuuma Sana 


"Oooh ! Naisma kalibu japo Mimi Ndo mgeni Hapa ! Haidary jaribu haya mayai 🍳 yametiwa pili pili ya unga naamini utayapenda Sana !


"Okay !


"Mh ! Kho ! Kho ! Samahani Binti yangu Recho kwani Wewe Na Haidary Frut mnajuana kabla ?


Baba Naisma aliuliza 


"Oooh ! Ndiyo Baba kumbe sikuuwambia ! Ni Rafiki angu wa shule sekondari tumesoma wote form 1_4 darasa moja .!


"Oooh ! Wow inapendeza ! 😄 


"Ndo ! Yani tulipoteana....... Haidary alikuwa na akili Sana nimeshangaa kumkuta anauza matunda alafu wanamuita Haidary Frut 😄 


Stori ziliendelea Naisma aliinuka nakuelekea chumbani


Songa nayo 🍊


Naisma alifika chumbani na kujilaza chumbani uku akiwa na mawazo kuhusu Recho kuja kukaa Kwao . Yani aliwaza Sana .


Haidary Frut aliingia chumbani na kumkuta Naisma akiwa bado ajalala . "Khe ! Mke Wangu bado ujalala kumbe ! 


Naisma akujibu kitu alichukua shuka lake nakujifunika gubi gubi Kama kawaida yake


🦋🦋☘️🍀


Siku iyo Naisma alifika kazini akiwa anaraha kabisa hata kidogo mda wote alimuwaza Recho na Haidary "sijui hata kimenipata Nini Mimi ? 

Naisma aliongea Ivo na kuinuka kwenda Dirishani kumchungulia Haidary Frut lakini alishangaa kutokumuona na alimuona Fahadi tu.aliangalia saa yake ya mkononi ambayo alikuwa ameivaa aliona ni saa 7 na Alichukua Simu yake na kumpigia mumewe Haidary Frut 


"Hallo ! Wewe ! Mbona leo ujaja kazini ?


"Aaah ! Naisma ? Leo Kuna Mambo nafatilia ! Ndo Mana sijaja kazini !!!


"Upo wapi ?


"Aaanhaaa ! Kuna sehemu nipo ! Baadae nipo bize kidogo !


Naisma kabla ajakata Simu akasikia sauti ya Mwanamke "bhna ! Haidary hii Ndo mzuri " sauti ambayo iliongea kwa madeko akajua moja kwa moja atakuwa ni Recho . Mapigo ya moyo yalianza kwenda mbio 


🌿


Hatimae ni mda wa Runchi 


"Khe 😄 Naisma mbona ! Leo upo mnyonge Sana ! Unaumwa !


Novo berry alimuuliza Naisma uku wakiendelea kula chakula cha mchana Apo kazini kwao ni mda wa Runchi 🍛


"Yaani Novo berry yaliyonitoke mwenzenu mpaka Sasa ata siamini ! 


"Kheee !!! Yapi Tena Ayo ! 


"Yaani Yule Recho lafiki wa Haidary Frut ameamia Nyumbani kwetu ! 


"Eeeheee !!!!! Umepigaje Apo ? 😳


Tina na Novo berry walibaki na mshangao 


"Ndo Ivo Yani .(...........)!


Naisma aliwasimulia ilivyo kuwa Recho alivyo kuja Kwao


"Yani Apo ! Kuwa kalibu Ivo lazima atampata tu ! Haidary Frut Yani Recho anampenda Haidary tokea shule! Mimi si namjua Yule Binti tumesoma nae ni king'ang'a 👌 !


"Mh! Pole shosti ! Na unavyojitia umtaki Haidary Basi mwisho wa siku atabaki na Recho tu Apo !


Tina alimaliza kuongea Ivo nakuchukua glasi ya juisi 🍷 nakunywa . Naisma alibaki kimya 


🌿


Hatimae jioni Naisma aliludi kwao  na kwenda chumbani kwao ambako alilala yeye na Haidary alimkuta Haidary Frut akiwa chumbani amelala alifika na kwenda kuoga Na. Kuvaa night dress 👗 yake na suluali yake ya gauni .

Alimuamsha Haidary Frut "Aaah ! Najisikia kuchoka mkewangu mtatoka baadae nyie kaleni tu !


Haidary alikataa kula Naisma pia alishangaa kutokumuona Recho pia kwani na yeye alikataa mda ule . Walikula na baada ya mda wote walienda kulala 


🌿🌹


Baadae kidogo Haidary Frut aliamka na kwenda kuoga aliludi nakuvaa pensi yake pamoja na tisheti lake na kutoka kwenda kula alikaa nakupakua chakula 🍛 nakuanza kula ile anaanza kula tu . Alihisi Kama Kuna mtu anakuja Nyuma yake aligeuka na walikutana macho kwa macho na Recho ambae alikua kajipodoa usiku uwo na alibusti maziwa yake na kuyaacha yakiwa yanavutia uku akiwa kavaa night dress 👗 yake ya pink ambayo ilikuwa ina melemeta na kuvutia mno ilikuwa ni fupi na kuachia mapaja yake myeupe na laini yakionekana


Haidary Frut alimeza mate Baada ya kumuangalia juu Hadi chini Recho 


"Hai !!! Haidary Frut 🥰 kumbe na Wewe ! Ujala Kama Mimi ?


"Ndi.ndi.ndiyo.!!!!


Recho alivuta kiti nakukaa uku akikunja mne na kumfanya Mapaja yake yazidi kuonekana na kumtamanisha zaidi Haidary Frut  . Baada ya mda walimaliza kula 


"Mh! Haidary Mimi sijisikii usingizi mwenzio ! Nakuomba tutembee tembee nje kwenye bostani alafu Kuna kitu nataka nikwambie  Ido !


"Mh ! Mbona mda umenda Sana Recho saa 6 kasolo hii kwanini usiende kulala na siulisema kesho tutanza kazi wote alafu sijamjulisha mke Wangu Naisma!


Recho alichukia kusikia jina la Naisma Pale . Hapo Hapo wivu ulimshika 


"Please ! Nakuomba Haidary ! Okay Kama utaki !😔


" Basi twende ! 


Recho na Haidary Frut walitoka nje  nakwenda Kwenye Bostani na walifika Apo na kukaa kwenye kiti cha mbao kirefu refu ivi walikaa wote walipiga stori kwa mda Adi saa 6 na nusu 


"Mh ! Recho Mimi naenda kulala  ! 


"Subili bhna Haidary ! 


Recho aliongea kwa kudeka na kumshika Haidary Frut mkono ili asiinuke .

Naisma alilala alivyo kulupuka alishangaa kutokumuona mumewe Haidary Frut . Aliwaza na akakumbuka maneno ya Rafiki zake Novo pamoja na Tina kwamba Recho atahakikisha anamchukua Haidary Frut .


Apo Apo Naisma aliinuka nakuanza kumtafuta Haidary Frut

🥰🥰🥰🥰


"Najisikia Baridi mwenzio Haidary!


Recho aliongea kwa kudeka na kumshika Haidary Frut mkono uku akitaka kumlalia kifuani lakini Haidary Frut alimkwepa 


"Basi Kama unajisikia Baridi kalale mda umeenda !


"Yaani Haidary unajifanya ujui mnacho kitaka Mimi Ni miaka mingi imepita na Ndo mda sahihi Mimi kuwa na wewe 🥰 Nakupenda sana Haidary I love you so much !🥰 


Recho aliongea na kumsogelea Haidary mdomoni mwake ili waromance . Haidary Frut alitulia tu alikuwa kaloa mtoto alikuwa mashalah Recho alikuwa kaumbika 


"Haidary !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! 


Naisma aliita na Recho na Haidary Frut walishtuka 


Songa nayo 🔥🔥🔥🔥


Wote walishtuka na Haidary Frut aliinuka mda huo huo . Naisma alijisikia wivu wa Hali ya juu na alishindwa kuzuia hisia zake 


"Mnafanya Nini ? Apo wewe Na Recho !


"Tunaongea Mambo ya kazi kesho tutanza kazi Mimi na Haidary katika kampuni yako , Haidary akiwa Kama mshirika Wangu !


Recho alijibu kwa hasila . Pia Naisma alitibuka mda huo huo . Haidary Frut alimshika mkono Naisma na kumwambia waendoke . Haidary alitangulia chumbani na kuwaacha . 


"Oooh! Vizuli 👏 so kuongea na waume za watu ! Usiku wa saa, 6 ndo biashara yako inataka Ivo si ndiyo?


"Hahahaha ! Nicheke kwanza ! Enhe kwa Ndoa gani ? Iyo ya mchongo ? Au Mimi Ndo mwanamke wake wa maisha Haidary na si wewe ! 


"Okay ! Vizuri na Kama Wewe Ndo wake wa maisha mbona hakukuoa Wewe na akaja kunipigia mie goti ?


"Haijalishi yote yaliotokea Wewe jua Mimi mwenyewe nimeludi Sasa na nakuhakikishia ilo Haidary ataludi kwangu ! Na iyo Ndoa yako ya mchongo mtaifutilia mbali ! Na nakuahidi nitambadilisha Haidary maana Wewe huku weza kufanya Ivo !


Recho aliongea Ivo uku akilinga Naisma alinyamaza kimya nakuludi zake chumbani alimkuta Haidary Frut kalala kwenye Sofa anapo lalaga 


"Okay ! Ido now umeamua kunizalilisha kwa uyo Malaya wako si ndiyo !


"Kwanini ? Mke Wangu !


"Umemwambia Nini !!?? Recho kuhusu Mimi na wewe! Amenambia Ndoa yangu ya mchongo !


"Samahani ! Mke Wangu Ni kweli aliniuliza nilikupataje nikamuadisia siku tegemea Kama angefanya Ivo !Asaivi  Unanipenda Naisma ?


"Msiuuuuu !!!  Yaani sahau msimamo Wangu ule ule siwezi kukupenda Ng'o !


"Sasa Kama unipendi mbona ulikuja kule bostanini ?


"Oooh ! Ni hivi nilikuja kwa sababu ya nataka heshima katika nyumba yetu haijalishi na Ndoa yetu ya mchongo lakini ndugu zangu wanajua  Wewe Ni mumewangu kwaiyo heshima ifate mkondo Wake ! 


"Nikweli aunipendi hata kidogo Naisma?


"Ndiyo sikupendi hata kidogo na sitakaa nikupende huu mwezi wa 3 Hadi wa 5 tunapeana talaka ! Nishasema na huo Ndo msimamo Wangu !


Haidary alimwangalia Naisma Hapo Hapo machozi yalianza kumtoka na kuanza kulia 


"Sawa ! Najitaidi kukupenda lakini hupendeki Naisma ! Unataka nikufanyie Nini ? Ili upendeke Wewe mwanamke !


"Acha unafki apa kujiliza Liza ! Usinichulie mie !


🌹🌿


Naisma alifika Ofsini na alikuwa anaongea na wafanyakazi wengine wa Pale Ofsini. Akiwa anaendelea kuongea alishtuka Baada ya kumuona Haidary Frut akiwa kavalia suti akiwa kapendeza Sana uku akiwa kaongozana na Recho . Wafanyakazi wote walishangaa nakuanza mining'ono 


Naisma alibaki kushangaa 


"Hai!!! Naisma kutana na Mimi Hapa Naitwa Recho nipo na mshilika mwenzangu anaitwa Haidary ! Tutakuwepo Hapa katika kampuni yako tukifanya kazi pamoja kwa kushirikiana na kampuni yetu ili kukuza biashara !!!


"Na.na.na.na..!


Recho aliongea kwa jeuri na kumfanya Naisma abaki nakigugumizu asijue Nini Cha kusema na mda huo huo . Baba yake Naisma alimpigia Simu Binti yake na kumueleza juu ya ujio wa Recho na Haidary Ivo awaelekeze Ofisi zao. Pozi lilimuisha Naisma 


Baada ya mda kazi ziliendelea na mda wa Runchi ulifika na wafanyakazi wote walienda Runchi . Naisma akiwa na Wenzie wanakula wakaja Haidary Frut pamoja na Recho nawakakaa meza Yao Pamoja wakaanza kula.


Novo berry pamoja na Tina Ndo waliwaona mda huo na walibaki kuwashangaa na ndipo Novo berry akaanza kuuliza  


"Ivi jamani nikweli nachokiona au macho yangu ! 


"Kumbe umeona Novo ndiyo Yule ni shemeji yetu Haidary na Yule ni Recho !!!!  Sasa imekuaje ?


Wote walimuangalia Naisma na aliwaelezea jinsi ulivyo kuwa Na wote walishangaa 


Wakiwa wanaendelea kula . Mda wa Runchi uliisha na walitakiwa kuludi Ofsini ndipo Recho alipojifanya kajikwa na Haidary akamdaka . Mda huo Naisma na Wenzie walikuwa kwa Nyuma 


"Ooohooo !!!!!!!


Novo aliongea Ivo uku akimuangalia Naisma .....


ITAENDELEA...

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)