DADA MDUNGUAJI EPIDODE 11

Emmanuel Lee
By -
0

DADA MDUNGUAJI


EPISODE 11


STORY NA Mbogo Edgar


ILIPOISHIA EPISODE 10  : huku mlango ukifunguka, “kumekucha” aliongea Eva akijibanza pembeni ya mlango akiwaza namna ya kufanya tukio bila Denis kuona, nyumba nyingine zote zilikuwa na umeme, kasolo yakwao tu, Jackline akatuliza akili akasikiliza kwa umakini, akasikia michacho ya nyayo za watu toka ndani, hapo Jackline akaona bola aingie ndani akawamalize huko huko, pasipo Denis kuona, lakini kabla ajapiga hatua kuingia ndani, ENDELEA ........

Akasikia sauti za watu wakinong’onezana “mbona unachelewa bwana” ilikuwa sauti ya kike, ambayo ilifwatiwa na sauti ya nyayo za kunyatia, kisha ika sikika switch ya taa ya sebuleni iki to mlio, ikionyesha kuwa imebonyezwa, hapo Jackline Mcheale Nyati akajuwa kuwa kitafwatia kitendo cha gari kushambuliwa, kwa hiyo anatakiwa awai haraka sana, hivyo Jackline au mama France kwa kitendoo cha haraka sana, akiwa na uakika akuna anae mwona kutokana na giza akajivilingisha kwa mtindo wa sarakasi, na kuji toma ndani kisha aka jibanza pembeni ya sofa akizungusha macho yake kwa haraka sana, ndipo alipo ona taswala ya mtu aliesimama karibu na ilipo switch ya taa za sebuleni, hapo akajisemea kimoyo moyo , “karibu kuzimu” wakati anajiandaa kwenda kuchomoa roho ya yule mtu, mala ghafla akasikia switch kubwa ya umeme (main switch) ikitoa sauti ya kuwashwa, ikifwatiwa na mwanga wataa za nje kuwaka, sambamba na sauti ya music, “surprise” hapo Jackline akatulia na kuusikiliza ule music, ulikuwa ni ‘happy born day’ hapo Eva akahisi kunauwezekano wa kuharibu mambo, akatulia kiya akitafuta jinsi ya kuinuka toka mafichoni, “akaskikia minongono mingine, “bado wapo nje ebu washa taa” hapo haraka sana Eva akasimama, toka mafichoni, na taa zika washwa, akajifanya kustuka na kujishika kifuani, hapo Jackline alitazama ndani nakuona watu zaidi ya ishilini ambao walipiiga kelele za kushangilia, ndani ya nyumb mlikuwa mmepambwa kwa taa kama zile za chriss mass, pia yalionekna mabox mengi sana ya zawadi, pamoja vitu vya kuchezea mtoto, huku mezani kukiwa kumetapaa vinywaji mbali mbali, pombe zikiwa nyingi zaidi  Jackline usoni akiwa ameachia tabasamu, aliwatazama kwa awamu, watu wengi, wake kwa waume waliojaa ndani ya nyumba yao, huku nyuso zao zikionekana kutawaliwa na furaha iliyo changanyika na ulevi, kati ya watu wale Jackline aliwaona boss wa mume wake Mahadhi na Janeth,  ‘mnabahati mngekufa bila hatia’ alijisemea kimoyo moyo Jackline, “he! umeingia saa ngapi?” aliuliza Janet kwa mshanngao huku akimsogelea Jackline, na kumsalimia kwakumkumbati, huku anamwambia, “hongera mwaya umekuza” hapo watuwengine waliopo mle ndani, nao wakasanuka kumshangaa Jackline, maana awakumwona wakati anaingia, Jackline aikumtisha sana maana walionekana tayari wamesha anza kunywa pombe, “engineer yupo wapi?” aliuliza mtu mmoja mwenye hasiri ya kihindi, na wakati huo huo Denis akaingia ndani akiwa amembeba mwanae Fransis, pamoja na mtu alie valia jacket jeusi na mkononi alikuwa amebeba kofia ngumu ya kuendeshea pikipiki “naomba nmiambie kitu kimoja, funguo mmepata wapi?” aliuliza Denis kwa sauti ya mshangao iliyo ambatana na ulevi, hapo Jackiline akakumbuka swala hilo, la kmba watu awa wameingiaje ndani, lakini kikalipuka kicheko, kabla boss wa akina Denis ajajibu, “jiangalie mfukoni” huku kicheko kina endelea, hapo Jackline akamwona Denis akijikagua mifukoni, kisha akaonekana kukumbuka jambo, alafu akaangua chekeo, nikwamba wakati akiongea na boss wake kule ofisini, akimweleza juu ya kuomba luksa akafanye manunuzi ya familia yake, alikuwa ameshika fungu za gari na nyumba mkononi, na kunakipindi aliziweka mezani, hap ndipo boss wake ambae alsha panga kumfanyia surprise  Denis ya kumpa hongera ya kupata mchumba na mtoto, akaichukuwa na kuanza mipango ya kumfanya surprise, akiwa julisha wateja wao na marafiki ambao aliwai kuwajulisha azma yake ya kumpongeza kijana huyu, ambae utendaji wake ni mkubwa na mzuri sana, na wao ndio walio mpigia simu Denis, ili kumchelewesha, siku hiyo mambo yaliuwa ni shamla shamla, mpaka saa nane za usiku, ndipo walipo tawanyika na kuelekea makwao, wakitumia magari yao, ambayo mwanzo waliya gesha mbali kidogo, ili kufanikisha surprise yao, kwa Denis na familia yao, kiukweli Jackline alifarijika sana kwa upendo walio uonyesha rafiki zake Denis, ambao licha ya kujumuika nao usiku ule pia wali leta zawadi nyingi sana za kwake na zamtoto Fransis, ambae ata siku zilizo fwata Fransis alikuwa na vitu vingi sana ya kuchezea, vilivyo chania apate marafiki wengi sana toka nyumba za jirani, na kusababisha ata wa mama wajirani nao waanze mazowea madogo madogo na mama France, lakini Jackline alijitaidi kuwakwepa, maana akutaka rafiki kwa mda huu, mpaka amalize kazi yake, japo maneno yaikuwa mengi toka kwa wamama wamtaani, wapo waliosema kuwa mama Frnce anajidai, wengine anajisikia sana, lakini Jackline akujari wala kuya sikiliza maneno hayo, yeye aliendelea na ratiba yake ya kila siku, ambapo asubuhi, baada ya kuandaa chai au supu ya mume wake, na kuakikisha mume wake ameenda kazini, alifanya mazoezi ya nguvu kisha kuanza shuguli za nyumbani kama mama, huku upande wa Denis nae, japo maisha yalikuwa ni yenye amani na furaha, lakini ilimshangaza tabia ya mke wake yakuto kumkubaria swala la kupeleka barua kwa wazazi wake, ili waweze kufunga ndoa, kila siku akimwambia, asiwe na haraka, kiukwei Denis alikuwa na wasi wasi sana juu ya jambo hilo, akiofia kuwa pengine Jackline angebadiri mawazo yake na kuolewa na mtu mwingine, japo alifarijika na tabia ya mke wake huyo, ya upole na unyenyekevu mwingi juu yake, ulio tawaliwa na upendo mkubwa na uaminifu, ukizingatia kuwa alimkuta bikira, na akuoneka kuonyesha dalili yoyote, ya kusaliti penzi lao, ambapo muda mwingi sana mama France alishinda nyumbani pasipo kudhurula, ***** huku nako kwa Insp Johnson pamoja na kikundi chake maalumu alicho kiunda, kwaajili ya kumsaka muuwaji wakike anae sadikiwa kuwa ni mtoto wa mzee Nyati, amba mpaka sasa wanachi walikuwa wanafahamu kuwa amesha kufa, huku askari wapelelezi wakizagaa kwenye centre mbali mbali za jiji la dar, kumsaka muuwaji ambae idadi kubwa ya polisi hao, awakuwa wana mfahamu, ndani ya miezi mitatu ya mwanzo mabo yalikuwa ni magumu sana kwa wanchi wanao penda kudhurula usiku, maana licha ya kuzagaa kwa polisi wapelelezi, pia usiku kulikuwa na doria kali sana, ya polisi, hivyo kwa alie onekana na zulula usiku alikuwa na hali mbaya, hapo ange pewa kipigo cha kue;eweka, kisha angeenda kujieleza kituoni, ambako atakama ungekuwa na vielelezo gani, basi ungeachiwa asubuhi, hali hiyo iliyodumu kwa miei mitatu, akuwa na mafanikio yoyote, na hali ilikuwa shwali kabisa, akukuwa na tukio jingine la mauwaji lililo tokea linalo fanana na matukio yanayo, sadikiwa kufanywa na mwanamke hatari, ndani ya miezi mitatu, insp Johnson aliangaika sana kumtafuta Jackline, huku akiangaika kumwuliza baba yake, jambo ambalo alilifanya nchini congo, mwaka 1988, alitumia mbinu nyingi sana, ikiwa pamoja na siku ambayo alikaa na baba yake wakinywa pombe nyingi sana, kiasi cha mzee Masinde kulewa sana, lakini alipo jaribu kumwuliza juu ya swala hilo, lakini mzee Masinde alijibu, kwa mkato “hachana na nahuyo mjinga” Insp ambae alikuwa anania thabiti, ya kumwokoa baba yake, akukata tamaa, alirudi mala kadhaa kwa mzee Soud, ambae safari hii akutaka kutoa ushirikiano kwa insp Johnson, zaidi ya ushauri “kijana unapo mfwatilia mzee Nyati kuwa makini sana” maneno ambayo insp aliyaona ya kinafiki, na kwamba yana lengo la kumtisha na kumkatisha tamaha, insp akiwa na tegeo kwa askari wake aliowaweka kumlinda baba yake pasipo mwenyewe kujuwa, na pc busungu alie kuwa akishinda, maeneo ya mbezi mpaka kibamba, aliendelea uongoza kikundi chake kipya, chenye watu zaidi ya sitini, wenye mafunzo mazuri na silaha za kisasa, pamoja na vazi maalumu la kuzuwia risasi (bullet proof) ambalo walikuwa wakivaa muda wote wakiwa kazini, siku zilisonga, mambo yakwa kimya kabisa, ata baada ya miezi mitatu aliyopewa Insp Johnson kupita, mambo yaliendelea kuwa kimya, licha ya insp kuwa tayari kupokea simu, toka kwa Jackline, huku akitega askari kila kona ya mtaa anao kaa, kule mbezi, akitarajia kumkata Jackline endapo angeingia nyumbani kwake, kuulizia kwanini akutekeleza shariti la wakina mzee Masinde, ujitangaza makosa waliyo fanya miaka hiyo, lakini akaona kimya kabisa, ***** mzee Masinde na mwinzie bwana Kaijage waliendelea na maisha yao, huku siku zikizidi kuendelea kusonga, wakiamini kuwa mzee Nyati ameshindwa kuwa kabili kutokana na msakako unaoendelea, hivyo wazee awa walifanya shughuli zao, za kibiashara kama kawaida, shulizao kwakiasi kikubwa azikuwa halali, wakati mzee masinde akeajiri vijana wengine wanne, baada ya wale wanne wa kwanza kupoteza maisha, aliendelea ku fanya biashara zake za kuvusha magendo kwa kutumi ameli yake, huku mala nyingine wakivamia na kupola kwenye meli kubwa, zinazo safirisha mizigo, huku lunten mstaafu Kaijage akindeleza biashara yake ya usafirishaji wanchi kavu, kwa kutumia magari yake makubwa, mna licha ya kusafirisha mizigo kutoa na kupeleka nje ya nchi, pia kama ilivyo kuwa kawaida yake ya kusafirisha meno ya tembo na ngozi za chui, ambavyo vilimwingizia pesa nyingi sana, ***** ilsha timia miezi sita toka Jackline aingie Dar es salaam tokea Songea, ilikuwa alahamisi saa mbili usiku, akiwa sebuleni na mume wake wana pata chakula cha jioni, huku wakitazama taharifa ya habari kwenye television ya taifa, ndpo alipo vutiwa na habari moja iliyo kuwa inasomwa, ilikuwa ni habari ya hajari, iliyo toke kongowe mkoani pwani, gari kubwa aina ya scania la mizigo, lililo gongana na bus la abiria, nakusabisha vifo vya watu wengi sana zaidi ya ishirini, huku wengine wote wakiwa maututi hospital ya Tumbi, mkoa wapwani, kitu kilicho vutia kwenye habari hiyo, nikupatikana kwa nyala za serikali kwenye gari hilo la mizigo ambalo, kwa mujibu wa mashuhuda, ndilo lililo sababisha hajari, wakati Jackline na mume wake wanaanglia habari hiyo, waliona ikionyesha tukio la kukamatwa kwa mmili wa gari la mizigo ambalo gari lake limesababisha hajari na kukutwa na pembe za ndovu na ngozi kadha za chui, na kwamba jumatatu anafikishwa mahakamani,  “kama na mfahamu huyu mzee” aliongea Jackline akimtazama Denis, “sijuwi kama unamfahamu, huyu tajiri sana anaitwa Kaijage, kumbe dili zake ni noma” aljibu Denis akishangaa kidogo, wakati huo huo simu ya Jackline ikaita Jackline akaitazama simu yake, akaona jina lime andikwa baba, akaipokea na kuweka sikioni, hapo Denis akusikia kitu chochote zaidi ya shikamoo, kisha ikafwata ndiyo ndiyo ndiyo, mwishoni kabisa ikawa sawa, alafu simu ikakatwa, alafu Jackline akasema “kazi imeanza” maneno hayo yali mstua Denis akamtazama mkewake kwa mshangao, 


 “Kuna nini tena kimetokea?” aliuliza Denis kwa mshangao mkubwa, akijuwa kuwa kuna tatizo nyumbani, maana Jackline au mama France uwa anapigiwa simu kutoka nyumbani kwao Songea tu, kwa baba yake, “baba anasema, mama anaumwa” alijibu Jackline kwa sauti ya chini, kama vile amenyongea flani hivi, “kwa hiyo unafanyaje, tutaenda au inabidi utatuma fedha?” hapo Jackline akamtazama mume wake kwa macho yakipekee, yaliyo jaa upendo na shukurani, huku anasogeza mkno wake wakushoto na kuushika mkoni wakushoto wa Denis, “nashukuru sana mume wangu, kwa kuwajali wazazi wangu, nazani tuwatumie fedha tu!, iwapo atazidiwa sana tutaenda kuwaona” hapo Denis alijikuta akitaasamu “usijali mke wangu, ilo nijukumu langu kuakikisha wazazi wetu wana pata tiba na maitaji mmuhimu, kwani wazazi wako ni wazazi wangu, ila sijuwi nikiasi gani kitaitajika kwenda kutuma?” aliuliza Denis, “nazani nifedha kidogo tu za dawa” alisema Jackline huku wanaendelea kula, “hapana Jack, nazani wanaitaji fedha za kutosha, sababu atuja watumia fedha toka ulipo kuja kutoka Songea” aliongea Denis na Jackline akuwa na kipingamizi, ila wakakubariana kuwa kesho waende pamoja mjini kisha Jackline aende kutuma fedha hizo, ambazo nikiasi cha shilingi  laki tatu za kitanzania, **** taalifa ya kukamatwa kwa KAIJAGE, ilitapakaa sana nchini, ukiachilia mzee Nati na insp Johnson pia ilimfikia rafiki yake mzee David Masinde, baada yakuipata taalifa hii bwana masinde akamkubuka mkuu wakitengo cha upelelezi wakosa ya jinai alie msaidia kumtoa bwana Mathayo sikule aliyo uwawa, hivyo akampigia simu kuitaji msaada wake, baada yakupokea simu mkuu wakitengo cha upelelezi , mzee Masinde  alimweleza shida yake, na wakakubariana kusaidiana kwa kuficha ushaidi, huku wakitumia unja kama ule wa mwanzo, wa kutengeneza nyaraka fake ya kuibiwa kwa gari, huku wakipanga kutoa uhai wa dereva, ambae mpaka sasa alikuwa yupo hospital akitibiwa majalaha aliyo yapata kwenye hajari, natukio hilo lilipngwa lifanyike usiku ule, “andaa millon ishilini kwangu, na kumi kwa mtu atakae fanya kazi hiyo, njoo nayo kesho asubuhi , ofisini kwangu” alimaliza mkuu wa upelelezi, na mzee Masinde akaubaliana nae, *** ijumaa saa mbili asubuhi, insp Johnson alikuwa ndani ya ofisi yake katika jengo kubwa la kituo kikuu, akimalizia kukagua report ya siku iliyotoka, kisha akainuka na kuelekea ofisini kwa mkuu wakitengo cha upelelezi, akatoe report ya sikuile, kisha aende kumwona mzee Kaijage kule mahabusu, laikini wakati anatakakuingia ofisini kwa mkuu wake, akazuiliwa, akiambiwa kuwa kuna mgeni ndani ya ofisi hiyo, hivyo alitakiwa asubiri kidogo, mgeni huyo atoke, insp alikaa kwenye kiti kimoja kati ya vitatu vilivyo kuwepo maalipale, huku akiwaza juu ya mzee Kaijage, ambae ni rafiki mkubwa wa baba yake, na apakuwa na shaka kuwa, mzee huyu ni mmoja kati ya wale waliotakiwa kuuwawa, “lazima nimshawishi ani eleze kitu ambacho walikifanya huko congo” aliwaza insp Johnson ambae alikuwa ana amini kuwa endapo atajuwa siri hiyo, itakuwa lahisi kwake kumaliza swala hili, wakati Johnson anaendelea kuwaza mahari pale mala akaona mlango wa ofisi ya mkuu wa upelelezi, unafunguliwa, na akamwona baba yake mzee Masinde, akitoka ndani ya ofisi hiyo Johnson akaduwaa, “ba..... ha! mzee umefwata nini hapa” aliongea kwa sauti ya chini insp Johnson, huku anainuka toka kwenye kiti alicho kuwa amekalia, na kumwafwata baba yake, “usijari Johnson, nilikuwa na maongezi kidogo, na mkubwa hapa” aliongea mzee Masinde, kisha akaanza kutembea kuelekea nje ya jengo lile, insp alimtazama baba yake mpaka alipopotea nje yajengo, insp akaingia ndani ya ofisi ya mkuu wa upelelezi, akamkuta boss wake akiwa anaifadhi fedha kwenye begi lake dogo la mkononi, “hooo! insp karibu, tena nilikuwa nataka niagize uitwe haraka, maana kunajambo lakushngaza limetokea huko hospital” alisema mkuu wa kitengo cha upelelezi, ambae akuwa anafahamu kuwa mzee Masinde ni baba wa Johnson, Johnson nae akasalimia kwa kupiga salut, kisha akiwa bado amesimama mbele ya meza kubwa mle ofisini, akauliza, “samahani afande, huyu mzee alietok mna fahamiana,?” hapo Johnson akamwona afande wake akibabaika kujibu “haaaaa! mh!!!! huyu bwana ni mwana siasa, ni rafiki yangu wamda refu sana, toka tupo chuo cha magogoni, wakati huo tuna somea siasa, alikuja kunisalimia tu!” aliongea mkuu hyu akimdanganya Johnson, huku akiwa na uakika Johnso atokuwa na uwezo wakufahamu uongo huo, wakati Johnson akiwa anashangaa jibu la afande wake, mzee huyu aka muwai, “insp kunatukio lilitokea jana, kuna hajari ilitokea huko kibaha” alianza kuongea mkuu waupelelezi wa makosa ya jinai, akimweleza Johnson kuhu kifo cha dereva wa gari lililo sababisha hajari na kukutwa na nyara za serikali, huku akiwa anasikitika sana juu ya kifo cha dereva, mkuu wakitengo cha upelelezi alisema kuwa derva huyo alikuwa mtu muhimu sana kwa upelelezi wa tukio hilo, sababu gari hilo lilikuwa limerepotiwa kuibiwa siku chache zilizo pita, taalifa hiyo ilimstua sana insp ambae kengere ya tahadhari iligonga kichwani mwake, huku likimjia tukio lililo tokea mwaka mmoja uliopita, kwa mzee Mathayo, “kwahiyo afande, huyu alie kamatwa inabidi aachiwe?” aliuliza Johnson kwa mshangao, “hapana insp, huyu bwana ataachiwa jumatatu mahakamani, baada ya kuwakirisha report ya upotevu” aliongea mkuu wakitengo cha upelelezi, huku akimruhusu insp kuwakilisha report yake, **** baada ya kufika ofisini, na kuomba luksa Denis na mke wake wakiwa na mtoto wao France wakaondka na kuelekea mjini kutuma fedha, “unajuwa baba France mimi sizijuwi sehemu nyingi hapa mjini?” aliongea Jackline huku, wakati wakiwa wana katiza maeneo ya fire, “kama wapi mke wangu?” aliuliza Johnson huku akipunguza mwendo, “huko wanakosemaga poster, bandalini ata maakama siijuwi yani nakujuwa hospital tu!?” aliongea kwa mtindo wa kulalamika Jackline, “ok! inabidi twende kwanza tukatumefedha, kisha nikuzungushe mpaka ikulu, ukakuone” alisema Denis huku akikata kna kuingia kaliakoo, “alafu inabidi week end hii nikufundishe kuendesha gari, ikiwezekana tutafute gari jingine liwe linakusaidia katika miznguko midogo midogo” aliongea Denis huku akiendelea kuendesha gari kuelekea ofisi za zamani za kamata (kampuni ya mabasi Tanzania) , ambapo sasa zilikuwa zina milikiwa na kampuni moja ya mabasi ya mtu binafsi, “mh! nitaweza kweli baba France?” aliongea Jackline nakumfanya Denis acheke kidogo, “kwanini usiweze mama France, nikitu lahisi tu, nitakufundisha kuanzia kesho” aliongea Denis akimwondoa wasi wasi, mke wake, “mh! sizani kama nitaweza” aliongea Jackline wakati huo waikuwa wameshafika, na kusimama nje ya ofisi za kamata yazamani, “utaweza tu! wala usiwe na wasiwasi” Jackline akashuka kwenda kutuma fedha, huku Denis akibakia ndani yagari na France, ***** baada yakutoka ofisini kwa mkuu wakitengo cha upelelezi, insp Johnson akiwa na mawazo tele, akaondoka peke yake, akielekea kibaha hospital ya Tumbi, akitumia gari lake binafsi aina ya Toyota wish, insp Johnson akiwa anahisi hatari ikikaribia siku za karibuni, maana alionganisha matukio ya vifo hivi, vyote vilitanguliwa na flani linalomweka muusika adharani, ilionyesha kuwa muuwaji alisha wasahau mawind yake, hivyo alitumia nafasi kama hizi kuwa ng’amua, na kuwamaliza, insp alipofika maeneo ya mbezi maeneo ya magari saba, akamchukuwa Busungu, kisha wakaenda pamoja Tumbi kufwatilia kilicho msibu dereva, mpaka kupelekea kifo chake, dakika kumi natano insp alikuwa ndani ya Hosptali teule ya tumbi waki jaribu kuulizia kilicho sabisha kifo cha dereva huyu, ambapo waliamabiwa kuwa dereva huyu amepoteeza maisha isha baada ya kuvuja damu nyingi, lakini walipoomba taalifazake za mwanzo, waligunduwa kuwepo na utata, maana zilionyesha kuwa marehemu ni mmoja kati ya watu wachace walio umia kidogo katika hiyo hajari, hapo Johnson na busungu wakatazamana, “kuna mchezo mchafu unachezwa” alisema Johnson huku wanaelekea kwenye gari lao na kundoka zao, kurudi mjini, **** ilikuwa ni safari fupi sana yenye mzunguko mfupi, wa njia moja, maana baada ya kumaliza kutuma fedha kwenye kampuni ya bus, Denis akiwa anamtembeza mke wake, waliingia mnazi mmoja, wakaelekea pster na kunyoosha ocean road akiiita hospital na kutokea ikulu, kisha kwa maombi ya Jackline, wakasimama maeneo ya bandarini, kwenye kituo cha poster ya zamani, mita mia nne kutoka mahakama kuu, hapo wakashuka na nakuanza kutazama mandhari ya bahari, ambapo walitumia kama nusu saaa hivi kutazama eneo hilo, pasipo Denis kujuwa Jackline alikuwa analengo lake jingine kabisa, baada yakulizika wamesha tazama vyakutosha wanafamilia hao, waliingia ndani yagari, nakuondoka zao, safari yao ilitumia nusu saa nyine mpaka Denis aiposimamisha gari mbezi akienda kununua cartoon la bia na mvinyo mwekundu kwaajili ya mke wake, Denis aishuka kwenye gari na kuelekea ndani ya full dose, akiliacha gari karibu na sehemu ya kuingilia na kutokea, akiamini atatoka mda siyo mrefu, **** “ebwanae nasikia njaa kari sana” aliongea insp Johnson wakati wanapita mbezi kwa Yusuph, “kuna pub moja hapo, wanachakula kizuri sana, kwasikuzote nilizo shinda huku ndio na kula ga hapo” aliongea Busungu, na kumwelekeza Johnson, sehemu aliyo itaja, dakika tano baadae walikuwa wanaingia sehemu hiyo, lakini wakakuta kuna gari aina ya Toyota noah, ikiwa imeegeshwa kwenye sehemu ya kuingilia, “watuwengine bwana sasa ndio kupakigani huku” aliongea kwa Johnson huku anapiga honi kwanguvu, akilipigia lile gari mbele yake, lakini akuna alie stuka zaidi waliona kama kuna mtu ndani yagari, tena mwanamke, ambae alikaa upande wa abiria, na akuonyesha kujari honi ile, “ngoja kwanza” aliongea Busungu huku akishuka toka kwenye gari na kulifwata gari lile, **** Jackline aliliona gari la insp Johnson likiingia pale Full dose pub, kwanza alilifananisha, maana aliliona siku moja tu! tena nyumbani kwa insp Johnson, siku ile alipoenda, hivyo akatulia na kulitazama kwa kutumia back vew, na bahati mbaya gari hilo likaja na kusimsms nyuma ya gari lao, ambalo liliziba njia, Jackline akatazama vizuri, akawaona watu waliokuwa ndani ya gari hilo, akawatambua mala moja, ni insp Johnson a busungu, akimtambua kuwa nikijana ae mwona miezi sita iliyopita pale kweny canteen kaliakoo,  Jackline akaumiza kichwa afanye nini, ili wakina busungu wasimwone, mala akasikia honi kaari ikitokea kwenye gari la kina busungu, wakionyesha kuwa wanaitaji nafasi ya kupitisha gari lao, ukweli nikwamba Jackline asingeweza kusogeza gari, akiofia kubainika uongo wake kwa Denis, “nifanye je hapa?” aliwaza Jackline, huku anatazaama kwenye side mirror na kumwona Busungu anashuka toka kwenye gari lile na kulifwata gari lao, “mungu wangu nimekwisha” 


Aliongea Jackline kwa sauti ya kunong’ona, huku mwanae France akigeuza geuza shingo kushangaa, asijuwe anacho zungumza mama yake, hapo Jackline aka papas mle ndani kama angepata kitu chenye ncha kali, ambacho kinge faa kutumuika kutoa roho ya Busungu, akapata crew drive (bisibisi) ndefu, wakati Busungu akiwa amebakiza atuwa chache kuufikia mlango wagari la kina Jackline upande aliokaa Jackline mwenyewe, mala Jackline akamwona Denis akitokea ndani ya bar huku amebeba cartoon la bia na chupa moja ya wine, akija upande ule ule ambao busungu alikuwa anakaribia, “hallow wewe ndie mwenye hili gari?” aiuliza Busungu, huku akisimama na kumtazama Denis, ambae alisha likaribia gari, “ndio kaka samahani naona nime wagandisha kidogo” aliongea Denis huku akiungua mlango wa gari wanyuma na kuweka mizigo aliyo kuwa nayo mkononi, “mbona na unafanya mambo ya kibwege, sasa wengine wapite wapi?” aliongea Busungu kama mtu aie panic, Jackline alimwona Denis akitazama kwenye gari la kina busungu, akamwona Johnson akiwa ametulia anawatazama, kumbuka kuwa Johnson alikuwa amevalia sale za polisi, na busungu alikuwa katika mavazi ya kiraia, “maneno machafu yanatokea wapi kaka, niliweka gari hapa nikijuwa kuwa sikai muda mrefu” aliongea Denis ambae alikuwa ameonekana kukosa nguvu, baada ya kuambiwa bwege mbele ya mke wake, na mwanae jpo alikuwa anaamni kuwa France akuwa anajuwa kitu japo kwasasa alikuwa anajitaidi kutaja baadhi ya maneno, Jackline alichukuwa simu yake n kuandika namba yagari, la wakina Busungu, kisha akaisave ‘insp’ “tatizo ujitambui wewe ebu toa debe ilo sisi tuingie bwana” alikroma Busungu, kwa sauti yakibabe, Denis auwa na lakufanya akaweka funga mlango wanyuma wagari lake na kuingia ndani ya gari upande wa dereva, kisha akasogeza gari mbele kidogo, kuliacha gari lile lipite, lilipo ingia yeye akaondoa gari, mda wote busungu alikuwa amesimama akilitazama gari la Denis, “siku nyingine utajikuta hupo kituoni, mjinga wewe” alisikika Busungu akiongea maneno hayo, Denis alimtazama mke wake kwa macho ya huruma, yaliyo changanyika na aibu nyingi sana, “vipi mume wangu mbona kama umenongea?” aliuliza Jackline huku akimpapasa mgongoni Denis, “wale jamaa sijuwi wanajivunia sababu ni polisi” alilalamika Denis huku akiendelea kuendesha gari, kuelekea nyumbani, “eti ananiita bwege?” aliendelea kulalamika Denis, “sema kwasababu nipolisi tu, ila nge mtandika makofi, mpaka angesahau rangi ya gari lao” aliongea Denis kwa msisitizo, kiasi cha kumfanya Jackline acheke sana, huku akisaidiwa na France asie juwa lolote, “unacheka mama France, mpaka dakika hii ningekuwa kituoni” aliongea Denis huku nayeye akiunga kicheko, ***** insp Johnson na Busungu, wakiwa pale Full Dose pub, waliendelea kupata chakula ca mchana huku waki jadilina juu ya swala la kifo cha dereva wa loli, “mpaka hapo mkuu amesha chukuwa chake, na jumatatu Kaijage ana shinda kesi kiulahini kabisa” alisema insp Johnson, akiwa na uakika wajambo analo liongea, “kwahiyo lile gari lili ibiwa week iliyo pita?” aliulliza kwamshangao bwana Busungu, “ndio maana yake, na mimi nilikua na mpango wa kumbana huyu mzee mpaka aniambie kilichotoke huko congo” waliongea mengi sana wawli awa mpaka saa nane walipo achana, na insp kuondoka zake kuelekea mjini akimwacha busungu anaendelea na kazi yake, insp alifika nyumbani kwake na kubadirsha nguo akivalia nguo za kiraia, kisha akaelekea kwa baba yake kinyelezi, huko kinyelezi insp na baba yake walikuwa katika mabishano makubwa na juu ya kitndo cha mzee Masinde kwenda ku fanya mpango wa kupindisha sheria, ili kumtoa rafiki yake, “kwataalifa yako baba ile ndio sehemu salama kwake, kumbuka kwajinsi habari zilivyo tapakaa, lazima mzee Nyati atakuwa amesha mtambua, na kupanga kummaliza” insp alijikuta akifichua siri ya kuwa mzee Nyati ni mzima, “inamaana uliidanganya serikali kuwa Nyati amekufa?” aliuliza Masinde kwa msnagao mkubwa sana, apo insp akuwa na ujanja, akamweleza jinsi mambo yalivyo kuwa na jinsi alivyo gundua kuwa mzee Nyati ni mzima, baada ya miezi tisa, lakini licha ya kusimuliwa mkasa wote huo, mzee Masinde akaamini kuwa hizi zilikuwa ni janja ya mwanae ili kumtisha yeye aachane na mipango yake, hivyo alikataa kabisa kuachana na mpango wake wa kumtoa rafiki yake mahabusu, pamoja na kumwepusha na kifungo, akiwa anaujanja insp akaondoka zake, na kurudi nyumbani akipanga kuweka ulinzi mkubwa sana wasiri kwa mzee Kaijage, akishatoka mahakamani, **** juma mosi, asubuhi baada ya Denis kuondoka kwenda kazini, Jackline alianza kazi ya kuikagua silaha yake, aina ya mugnum sniper rifle, baada ya kuakikisha hipo vizuri, aka hiifadhi vizuri na kujiandaa kutoka, pamoja na mwanae France, ***** siku hiyo ya jumamosi ilimkuta Busungu akiwa kibamba ccm, ame tulia maeneo ya njia panda ya mloganzila, kalibu kabisa na waendasha pikipiki, kwenye nye kijiwe cha Masafiri cha kununua vyuma chakavu, pia jirani palikuwa na banda la chips la Majani, akiongea na marafiki zake ambao alizoweana nao siku kadhaa zilizo pita baada ya kaa mala kwa mala maali pale, story zilikuwa nyingi sana pale kijiweni, licha ya wakina msafiri na Halfani majani, kuongea na Busungu siku zote lakini awakumtambua kuwa ni polisi, wala lengo la uwepo wake maali pale, ilikuwa saa tano kasoro za asubuhi, Pc busungu akiwepo maalipale mala akasikia sauti za miguno ya watu, “ebwa heee! yani yule demu ni mkari kinyama” aliongea mjani na kuwafanya Msafiri na Busungu, wageuze shingo zao, na kutazama kule alikokuwa anatazama Majani, Busungu kaduwaa, “siamini macho yangu, yani leo kiulaini” alijisemea Busungu kimoyo moyo, huku yeye pamoja na wenzake wakiendelea kumtazama mwanamke alie kubwa amebeba mtoto, “hoya anakaa wapi yule demu” aliuliza Busungu, akiendelea kumtazama Jackline Michael Nyati, ambae alikuwa anatokea kwenye kibanda cha mchoraji, anae julikana kwa jina la #MbogoEdgar, “mh! mimi mwenyewe ndio kwanza namwona leo” alijibu Msafiri, huku wakimtazama Jackline, ambae kwa sasa alikuwa anavuka barabara na elekea upande wapili, “hoya nakuja sasa hivi” alisema Busungu huku anainuka na kuanza kumfwata Jackline kule alikoelekea, “kuwa macho kaka mali zaatu hizo” aliongea Majani akimtahadharisha Busungu, wote wakacheka, wakati huo Busungu alionekana akitembea haraka na kusimama pembeni ya barabara, akisubiri magari yapite iii na yeye aweze kuvuka, wakati huo huo Busungu alichomoa simu yake na kuipiga, **** insp Johnson mda huo alikuwa ametulia nyumbani kwake akiwaza hili na lile, huku mwanae Bite akimsumbua sumbua kwakudai safari ya beach, mala akasikia simu yake ikiita, kuitazama ilikuwa inatoka kwa Busungu, akajuwa kuna jambo jipya, akaipokea haraka na kwa shahuku ya hali ya juu, “niambiae busungu kuna lolote?” aliuliza Johnson, “kaka huku mambo mazuri, atimae nime mwona yule kahaba” alisikika Busungu akiongea kwa mbwembwe, “sikia busungu mfwatilie kwa ukaribu na umakini wa hali yajuu kabisa, mimi nipo njiani nakuja” aliongea Johnson na kukata simu, kisha akapiga kituo kikuu, akiagiza waangaliwe askari kumi haraka sana wakutane kibamba ccm, dakika chache baadae insp alikuwa njiani anaelekea kibamba ccm, **** baada ya kuvuka barabara, pc Busungu alimwona Jackline akielekea upande wa njia panda ya shule, ni kijia kilichopo pembeni kabisa ya barabara kuu iendayo morogoro, akaanza kumfwata kwa mwendo haraka sana, njia hiyo ilikuwa ni yenye ulefu wa mita mia tano, yenye watu wachache waliokuwa wanaenda na kurudi, pc busungu alimwona kwambari Jackline akiwa na mwanae mgongoni, akikaribia kumaliza eneo hili ambalo lina nyasi fupi pasipo nyumba yoyote, hapo Busungu akajuwa kuwa endapo ata mwacha amlize eneo lile atampoteza, na asingeweza kumwona tena, hivyo akuwa na jinsi zaidi ya kuamua kuanza kukimbia, wakati anakimbia macho yake yalikuwa kwa Jackline , ambae alimwona akiingia njia pnd a shule na kujichanganya kwenye kundi la watu, na kuoweka kabisa, Busungu alifika eneo lile la stend na kuanza kuangaza macho huku na huku, pengine ange bahatisha kumwona Jackline lakini wapi akumwona, akazunguka sehemu mbili tatu, lakini akumwona kabisa, kaaza kuulizia kwa watu wawili watatu waliokuwepo pale stend, lakini akuna alimweleza kumwona Jackline, ***** kumbe basi wakati huo Jackline kuwa na hili wala lile baada ya kutoka kwa mchoraji, nakuona itakuwa nikupoteza mda kusubiri gari, akaamua kutembea kwa mguu, sababu nisehemu fupi sana, alivuka barabara na kuelekea njia panda huku akisikia maneno yakuchukiza ya vijana wa mtaani, wakiusifia uzuri wake, pengine walitumia lugha chafu, ambayo aikimpendeza Jackline, “cheki lile demu mwngu ukimpat yule yani unamla kama samaki” lakini akuwa na lakufanya Jackline alijitahidi kujikaza kidogo, asichukuwe atua kwa watu wale, Jackline alipo kuwa anakaribia njiapanda ya shule, akastuka na kuhisi kuwa, kama kunamtu anakuja upande wake kwa kukimbia, Jackline akutaka kugeuka nyuma, maana kama mtu huyu ana mwata yeye, angegundua uwa ameshaonekana, hivyo akajichanganya na watu wa pale njiapanda kisha akaingia kwenye duka moja la dawa, na kujifanya anaulizia dawa flani, huku akitazama yule aliekuwa anakuja kwakimbia ninani, na kweli baada ya mda mfupi akamwona mtu huyo na kumtambua kuwa ni Busungu, akiingia pale njia panda mbio mbio, nakuanza kutazama huku na huku, kama kunamtu anae mtafuta, hapo Jackline akatulia nakuendelea kumtazama Busungu huku akiendelea kuulizia dawa, alifanikiwa kumwona Busungu akianza kuulizia jambo kwa watu wawili watatu, baada ya kuka kwa dakika kadhaa mle dukani, na kumwona Busungu akikosa uelekeo Jackline akaamua kuondoka zake, akijitaidi asionekane kwa Busungu, **** baada ya kufika njia panda ya shule, insp na askari kumi waliokuja ndani ya defender, walikutana na pc Busungu, nakuambiwa kuwa Jakline ametoweka mbele ya mcho yake, wote wakabaki wameduwaa, “naona kuna dalili ya mafanikio, endelea kuchunguza” aliagiza Johnson nakuamrisha askari kuondoka zao, wakimwacha Busungu anaendelea na uchunguzi wa eneo lile, **** siku ile iliisha kiaina huku siku iliyofwata ilikuwa siku ya Jackline kufundishwa kuendesha gari, maeneo ya karibu na nyumbani kwao, kiukweli kwa Denis ilikuwa kazi ngumu sana, kumfundisha Jaackline kuendesha gari, maana alionekana kuwa mbumbu kabisa, katika zoezi hili la uendeshaji wa gari, yani toka saanne mapaka saa nane, Jackline akuweza kunyoosha tearing yagari, “yani mama France natamani nikuzabue ata vibao, yani utaazani unafanya makusudi” aliongea kwa ukari Denis, huku aki shuka kwenye gari na kuzunguka upande wa dereva na kufungua mlango, “shuka kapande kule” alionge Denis ambae licha ya kutumia mbinu zote za ufundishaji, lakini Jackline akuoonyesa dalili yoyote ya kuelewa kuendesha gari, “lakini baba France si nitaelewa taratibu?” aliongea Jackline kwa sauti ya uoga, mbele ya Denis, hapo Denis akapoa kidogo, “usijari mke wangu kilamala tukipata nafasi, nitakufundisha” wote wakacheka kidogo, “lakini baba France leo ulikasirika hen?” aliuliza Jackline kisha wote wakacheka tena, kabla Jackline aja ongea tena, “sasa tukapunguze hasira kwa mvinyo na .......” aliongea Jackline huku akizigusan asehemu zasiri za Denis, wakati huo walikuwa wanaingia nyumbani kwao, ambapo walikuta France akicheza na wenzake, wakichezea vigari na vibaiskeri, ***** vyombo vyote vya habari vilikuwa vina zungumzia juu ya mahakama yatakayo fanyika kesho juu ya bwana Kaijage, ambae gari lake licha ya kukutwa na nyara nyingi za serikali, pia gari lake lilisababisiha vifo vingi sana, kwa uzembe wa dereva wa gari hilo, ambae mpaka sasa ina semekana kuwa dereva huyu amesha fariki dunia, maoni yawatu wengi walio hojiwa juu ya tkio hilo, walionekana kushauri hadhabu kari kwa mmiliki wa gari hilo, **** siku yapili ilikuwa jumatatu, siku ambayo iliannza kwa shamla  shamla toka asubuhi, ukiachilia watu wengi kumiminika mahakama kuu, pia waandishi wa habari na vyombo vyao vya habari, walianza kujiandaa kuelekea mahali hapo, siku hiyo ilianza vibaya sana kwa Denis, maana baada ya kuwatayari amesha jiandaa kwenda kazini, alitoka na kuelekea kwenye gari lake, lakini kalipo jaribu kuliwasha gari alikuwaka, kila alipo jaribu kuliwasha ikashindikana, hapo akashuka na kumkabidhi mke wake funguo za gari, “vipi baba France, mbona unaacha gari?” aliuliza Jackline kwa mshangao, huku akipokea fungu za gari, “sijuwi gari lina matatizo gani, wacha niende kwa mguu, nitapata pikipiki njiani” aisema Denis huku akiondoka na kushika njia kuelekea barabarani, ***** saa moja na robo za asubuhi busngu alikuwa ndio anaingia, kibamba ccm kwenye kijwe cha wakina Msafiri, japo story zilikuwa ni nyingi sana pale kijiweni, watu wakizungumzia juu ya mahakama itakayo endeshwa leo, na kila mmoja alkuwa na hamu ya kujuwa kitakacho tokea, “wewe ujuwi mambo ya polisi, mwenye fedha afungwi” aliongea Majani na Msafiri akadakia, “ila naamini kuwa huyu lazima afungwe, tena amekamatwa na ushaidi wawazi kabisa, atakwepaje,?” aliongea Msafiri, wakati huo Busungu alikuwa anakaa na kujiunga nawenzie, “wewe unakuwa mgeni na mahakama zetu bwana” aliongea Majani, wakati huo Busungu alikuwa analitazama gari ainia ya Toyota Noah, ambalo lilikuwa linatokea pale kwa mchoraji, akaona tazama ndani, akitumia dirisha la upande wadereva ambao yeye ndio alikuwa nao sambamba, akamwona dereva wa gari lile kuwa ni Jackline Michael Nyati, akiwa amejitnda nguo aina ya vitenge, nasasa alikuwa anapandisha vioo vya gari lile, hku gari hiilo likiingia barabara kuu na kushika uelekeo wa mjini, “nimekufuma mshenzi wewe” alioea Busungu na kuinuka hara sana kukimbilia sehemu zilipo egeshwa boda boda, “ingia barabara kuu elekea mjini?” alisema Busungu baada ya kukodi moja ya boda boda, bila kuzubaa yle boda boda akawasha pikipiki na kushika njia ya kuelekea mjini, wakati huo Busungu alikuwa anapiga simu kwa insp Johnson, na wakati huo hoo alikuwa anasoma namba zagari zilizo kuwa zina someka vizuri, kutokana na ung’aavu wa kibao cha namba za gari lile, 


 Ambalo kwasasa alikuwa analitazama kwambele, simu ya insp iliita kwa mda mrefu pasipo kupokelewa kabisa, “insp unanini wewe? tutampoteza huyu, kahaba, pokea simu” aliongea Busungu kwa sauti ya chini huku, kiasi cha yule dereva wa boda boda kuto sikia vizuri, “usi jari braza si yule demu mkali alie tokea pale kwa Artist,?” aliongea dereva wa boda boda huku akijitaidi kuyakwepa magari na kuyapita, kwa fujo kulikaribia gari la Jackline Michael Nyati, lakini Busungu aka mzuwia boda boda yule asi likaribie lile gari maana ingekuwa lahisi kwa Jackline kustuka na kujuwa kuwa anafwatiliwa, licha ya boda boda ku punguza mwendo, lakini alikuwa amesha chelewa, maana walikutana na askari polisi wa usalama barabarani, waliosimama maeneo ya mbezi kwa Yusuph, “awa nao weseng... kweli, sijuwi wanataka nini?” aliongea Busungu kwa sauti ya chini, wakati piki piki inasimama na yeye akaruka haraka sana na kumfwata yule polisi alio wasimamisha, huku anatoa kitamburisho chake mfukoni na kumwonyesha yule polisi, “samahani afande, kuna dharula naomba niwai nitampoteza mtuhumiwa ninae mfwatilia” hapo yule polisi akachukuwa kile kitambulisho na kukitazama kidogo, kisha akamtazama Busungu kuakikisha kama kweli picha ya kwenye ID ni yakwake, alafu aka mruhusu aende, akiwa amesha mchelewesha, lakini baada ya hapo Busungu akiwa na dereva wa boda boda, wali chapa mwendo bila afanikio, huku busungu akijaribu kupiga simu kwa insp mala kwa mala lakini simu aikupokelewa, kwa kuwa Pc Busungu alikuwa amesha zikalili namba za gari la Jackline, akaziandika kwenye meddeji na kuzituma kwa insp, akiandika hivi ‘Jackline anakuja mjini anatumia gari aina ya Toyota Noah, lenye namba T 182C..P’ mpaka wawili awa wanafika ubungo mataa, na kuzuiliwa na taa za kuongozea magari, walikuwa awajaliona gari la Jackline, “huyu atakuwa ameenda mahakamani anataka kufanya tukio kama la sikuile kituoni” alichekecha akili, nakupata jibu hilo, “twende posta” Busungu ali mweleza yule mwendesha pikipiki, baaada ya taa kuwa ruhusu, dereva boda boda akafwata maelekezo akitarajia kutimiza hesasbu ya bisi wake mapema sana, **** huyu alikuwa Jackline Michael Nyati, ambae tokea asubuhi mumewake ajaribu kuwasha gari na kushindwa, na kuondoka kwa miguu akielekea barabarani, kutafuta usafiri mwingine, Jackline baada ya kusubiri kwa mda flani, nakuakikisha Denis amesha ondoka,  yeye akaingia chumbani na kunza kujipanga, akivalia kikaptulah kifupi cha jinsi, na tishet jeusi, kisha akaelekea kwenye banda la kuifadhia gari, ambako alichukuwa begi lake jeusi na kuingia nalo ndani, ndani ya dakika kummi na tano, Jackline alikuwa amesha weka tayari silaha zake kiunoni kwenye mkanda wa kiuno wa kikaptulah chake, ikiwa ni bastorah yake yenye risasi kumi, na kiwamb sauti, kisu chake cha kijeshi, kamba yake ndefu kihasi iliyo fungwa vizuri na kuonekana ndogo, alipo maliza akavaa gauni lake kwa juu, kiasi cha mtu yoyote kuto kutambua kilicho fichwa ndani ya gauni hilo, baada ya hapo Jackline akamchukuwa mwane France ambae alisha mwanda, wakaingia kwenye gari na kuanza safari, kituo cha kwanza kibamba ccm, kwa mchoraji, akachukuwa plate namba alizoacha kwa mchoraji amchoree kibao hicho, akimkabizi namba nyingine kabisa ambazo alikuwa anazitoa kwenye simu zake, akwa msaada wa mchoraji huyo Jackline akabadirisha namba za gari, kisha safari ikaanza, wakati anatoka kibamba ccm, na kuikamata barabara kuu iendayo morogoro, na kutembea kama mita mia hivi, akaiona piki piki ikiingia barabaran, na kuja upande aliko yeye, mwanzo akujuwa kama ina mfwata, kilicho mtua ni fujo za ile pikipiki, ambayo ilipo mkaribia ilipunguza mwendo, nayeye akaiacha, na hapo ndipo Jackline alipo pata nafasi ya kumtambua abiria wa ile bodaboda, alikuwa ni Busungu, wakati anapanga kuwakimbia, bahati nzuri akaiona ile pikipiki ikisimamishwa na polisi, wa usalama barabarani, hapo alicho kifanya Jackline au mama France kuchapa mwendo wa ambulance, mpaka anafika posta akuwaona kabisa wakina Busungu, kwa kujiachia kabisa Jackline akaenda kuegesha gari lake nyuma ya mtaa wa mahakama kuu ambayo hipo jirani na kanisa kuu, yeye akaendesha gari taratibu, kisha akaliegesha pembeni ya jengo la Wajasiliamari, jengo kubwa la ghorofa nne, ambalo lipo umbali wa mita mia tano toka mahakama kuu, alicho kifanya Jackline alimwachia mwanae vifaha vya kuchezea, pipi na choclate za kutosha, “Franceeee nakuja sasa hivi naenda kuleta pipi nyingine, sawa babaaaaa” alisema Jackline huku akimchezea France shavuni, na yeye akaitiki kwa kichwa, hapo Jackline akachukuwa begi lake na kutoka nalo kwenye gari kisha akaelekea ndani ya jeng ilo la ghorofa nne, lenye ofiso kadhaa zakibiashara, huku Jackline akiwa amejitanda kanga kichwani, akapotelea ndani ya jengo lile, ambalo mda huo lilikuwa na pirika pilika za watu wengi sana, ***** ndani ya ofisi ya wasanifu wa majengo, wakina Denis walikuwa wamejikusanya  mapokezi, pale kwa Janeth, wakitazama kwa bashasha trevishen ambayo ilikuwa ina rusha moja kwa moja matangazo yake toka kwenye viwanja vya mahakama kuu, ambapo kwa kupitia tv wakina Denis, Mahadhi Janeth na boss wao, waliweza kuona jinsi watu wengi sana kwenye, waliojaa nje ya uzio wa mahakama hii kuu, mtangazaji wa terevision hii biafsi, alionekana akiwahoji bahadhi ya watu waliokuwepo eneo lile, ambao walikuwa wana hamu ya kusikia matokeo ya Mahakam hii, inayo muhusu mmiliki wa gari ambalo licha ya kukutwa na nyara za serekali, pia gari hilo lilisababisha hajari kubwa sana, iliyo ondoka na roho nyingi za watu, “yani huyu jamaa ataondoka na mvua zakutosha sana” aliongea Mahadhi, “wewee ujuwi kitu kabisa, yani mtu anacheza diri kama hizo alafu afungwe kilahisi” aliongea Denis akionyesha kutokuwa naimani na vyombo vya sheria, “ila Denis bwana, kumbe ni mlevi, lakini una waza mbali sana” aliongea boss wao huku wakiendelea kutazama tukio lile kwenye TV LIVE, **** Ndani ya mahakama kuu watu walikuwa wengi wakisikiliza kesi mbali mbali, huku lengo ni kusikiliza hii ya ambayo kwa sasa ndio ilikuwa inatolewa maamuzi, ni kesi ya bwana Kaijage, ambae kwa sasa alikuwa amesimama kwenye kizimba cha mahakama, huku pingu zikiwa mkononi mwake, usoni kwa mzee huyu akuonyesha wasi wasi wowote, kwa watu wanao juwa kudadisi walijuwa juwa kuwa mzee huyu Anaya fahamu maamuzi ya mahakama yanayo tarajiwa kutolewa, insp Johnson akiwa ameondoa sauti ya mlio katoka simu yake, kutokana na sheria za kimahakama, kwamba akukutakiwa kelele za aina yoyote, wakati mahakama ikiendelea, Johnson alikuwa ametulia akisikiliza maamuzi ya Mahakama, “baada ya mahakama kulizika na uchunguzi, na taalifa ya jeshi la polisi, ambao ume thibitisha kuwa gari la mtuhumiwa, nyara za serikali, bwana Charles Kijage, ambapo imegundulika kuwa gari la bwana Kaijage liliibiwa week moja iliyopita, na taalifa ya upotevu ilitolewa, AMBAYO NI PF 3 No 000...1, katika kituo kikuu, na shauri lapilli la gari kusababisha hajari hiyo imefanywa na mwizi wa gari hilo ambae alikuwa ni mwajiliwa wa bwana Kaijage, na sasa ni marehemu ambae amkutwa na umahuti uliosababishwa na majelah ya hajari hiyo, kwa hiyo mahaka aijampata bwana Charle Kijage, na hatia yoyote, hivyo basi mahaka inamwacha huru bwana Kijage kuanzia sasa,” kauri hiyo ilimaliziwa kwa chundo kugongwa mezani, na askari mmoja kusema “koooort” watu wote waka simama kisha yule Jaji akasimama na kuondoka zake, baada ya jaji kutoweka zikaripuka sauti mbali mbali za maongezi, ikiwa ni furaha na malalamiko, akaonekana bwana Kijage akichukuliwa na rafiki zake, nakuanza kutoka nje, huku wakimpongeza kwa kuchomoka kwenye ile kesi, mmoja wa rafi wa Kijage , alikuwepo mzee Masinde,  hapo ndipo insp Johnson alipozinduka na kunyanyuka toka kwenye kiti alicho kalia, na kuelekea nje, ambako mpaka dakika hii, watu walikuwa wamechachamaa, wakipiga kelele, kuonyesha kuwa awakulizika na maamuzi ya mahakama, kelele zilikuwa ni nyingi sana, zikifawatiwa na wanchi kuanza kurusha mawe kuelekeza kwa bwana Kaijage, huku rafiki zake bwana Kijge wakijitaidi kumkinga na kumkimbiza kwenye gari, napolisi nao wakijaribu kuwazuwia mwanachi wasirushe mawe, **** “umeona umeona, sinilikuambia, kikowapi sasa?” aliongea Denis kwa hamaki, “kaka umeona mbali sana, du! nimekubari” alisema Mahadhi huku wiendelea kutazama TV, “cheki wananchi wanavyo chachamaa” aliongea boss, huku wakiendelea kutazama jinsi wananchi walivyokuwa wanarusha mawe, “aitasaidia chochote, yani pale kinachofwata, watapigwatu!” aliongea tena Denis, **** insp alikuwa amesimama kkwenye mlngo wa mahakama, akitazama jinsi wananchi, walivyo kuwa wana rusha mawe, huku rafiki zake Kaijage, wakijitaidi kumkinga na kumsogeza Kijage kwenye magari, pasipo kujuwa kuwa wanausogeza ugomvi kwenye vioo vya magari sababu dakika chae baadae wakaanza kuona mawe yakituwa kwenye vioo vya magari, yaliy kuwepo ndani ya eneo la mahaka, na kupasua vioo hivyo, moja ya gari lilikuwa ni gari la insp Johnson, “pumbavu gari langu” aliongea insp huku anatoa simu yake mfukoni, kwaajili ya kuomba msaada wa polisi wengine kutoka kituo kikuu, lakini ile kuitazama smu akakuta misee call zaidi ya ishilini, toka kwa Pc Busungu, na messeji kadhaa, “mh! kuna nini huko?” alijiuliza insp huku akianza ufngua zile missed call iliapige kwa Busungu, lajini kbla ajapiga akaona simu ikianza kuita tena, mpigaji alikuwa Busungu, insp akaipokea haraka, “afande naombamsaada wa askari hapa wajasiliamri, Jackline Nyati amingia hapa mfupi ulio pita nimeliona gari lake hapa nje” alisikika Busungu akiongea kwa pupa huku akionekana anapanda ngazi, hapo Johnson akajuwa tayari kuna kosa limesha tokea, akawaangalia wakina mzee Masinde wakiwa na wenzake, wanamkinga mzee Kaijage, ambapo sasa walikuwa wamegeuka, na kuanza kurudi walikotoka, yani ndani ya jengo la mahakama, baada ya mvua ya mawe kuzidi, “hallow afande unanisikia?” ilisikika sauti ya Busungu, lakini insp alikuwa amekaza macho kuwatazama wakina mzee Masinde, akamwona baba yake akiwa amemshika mkono mzee Kijage uku wenzake wakiwa wame wazunguka, insp akijaribu kutazama upande wa kushoto kwenye jengo la wajasiliamari, alikoelekezwa na busngu ambae bado alikuwa hajakata simu, naam kwenye gorofa la mwisho kabisa la jego ilo, akaona kitu kama flashi ya radi ndogo ikiambatana kunguru kuruka kwa fujo, kisha ikafwatiwa kelele kutoka kwenye kundi la kina mzee Masinde na wenzake ambao walikuwa wana msadida bwana kaijage, insp akageuza shingo kumtazama baba yake, akamwona mzee Kaijage kichomoka mikononi mwa mzee Masinde, kama ambae alisukumwa na kitu kizito, na kutupwa pembeni, huku kichwa chake kikipasuliwa, na ubongo ulio changanyika na damu kutawanyika, ukiwarukia rafiki zake, na watu walio mzunguka, akiwepo mzee Masinde, 


 “mungu wangu tayari” aliilopoka insp Johnson ambae bado alikuwa ameshikilia smu ambayo bado hipo hewani, ikiwa imepigwa na Polisi Consteble Busungu,  insp aliwaona wakina mzee masinde na wenzake wakiangaika kutafuta sehemu ya usalama, ambayo ilikuwa ni ndani ya mahakama pekee, wakati huo wanchi nao walikuwa wakishangaa tukio walilolishuhudia, kwamacho yao, wakiona mzee Kijage akiwa amelala chini, huku kichwa chake kikiwa akieleweki, pua api sikio wapi macho yalikuwa yamesha hachia kichwa na kuzagaa kama gololi za kuchezea watoto, “vipi tena afande kuna usalama huko?” ilisikika sauti ya busungu ambae bado alikuwa ana endelea kupanda ngazi kwafujo, hapo insp akagutuka toka kwenye mawenge, na kukumbuka kuwa alikuwa naongea na simu, “Busungu, hupo nyumba moja na huyo shetani, na ameshatoa roho ya mtu mmoja” aliongea insp Johnson huku akionyesha ishara kwa askari polisi wachache, ambao walikuwa wame jificha ndani ya mahakama kuogopa risasi ya mdunguaji, akitaka wamfwate yeye ambae alianza kutembea kuelekea upande wa nyuma wa mahaka, upande ambao ni uelekeo wa jengo la wajasiliamali, ambalo inasemekana Jackline Nyati yupo huko, wale askari ambao walikuwa watano huku wenye silaha wakiwa ni wawili tu, awakushangaa walimfwata insp ambae alikuwa na bastora tu!, “insp unasema tayari amesha uwa?” ilisikika sauti ya pc Busungu akiuliza kwa mshangao mkubwa sana, “sikia busungu, mzee Kaijaje tayari yupo chini, unatakiwa uwe makini sana, si unamjuwa huyo mwanamke ni hatari sana?” aliongea insp Johnson, wakati akimaliza kutoka nje ya jengo la mahakama, nyuma yake askari watano wakimfwata, “mama yangu nimechelwa” sauti ya Pc Busungu ilipenya masikioni kwa insp Johnson, kupitia simu yake yamkononi, na kumfanya asisimkwe na nywele zake akiziona zina simama, kama zile waya za kuosafishia sufuria, “hallow busungu” kimya “busungu unanisikia busungu?” aliongea insp kwa sauti yajuu sana, lakini akujibiwa kitu zaidi akasikia ya busunu kama anaongea na mtu mwingine mbele yake, “leo Jack, naomba unieleze sababu ya kufanya mauwaji” insp aliisikia sauti ya Busungu, ambayo ilionyesha kuwa ni yaupole sana, insp akaendelea kuwa sikiliza, kwa umakini sana, huku akizidi kutimua mbio na wale askari wake kuelekea kwenye lile jengo ambali kwa njia waliyo itumia lazima wangetumia dakiika kumi adi kumi natano, maana kuna sehemu ambaz lazima zinge walazimu kuzunguka, sababu zilikuwa zimezibwa na uzio wa ukuta, huku insp akijuwa kuwa Bungu maisha yake yapo hatarini, japo alikuwa anatumia mbinu flani flani kumchelewesha Jackline iliwao wawai eneo la tukio, ***** kama vile alikuwa amesaau uwezo wa mwili na hakili wa Jackline, busungu ambae baada ya kumpoteza Jackline, mbezi kwa yusuph, akaja kuliona gari la Jackline, nje ya jengo la wajasiliamari, kwa msaada waboda boda aliyekuwa wakwanza kuliona Toyota Noah lenye namba T182 C..P, hapo haraka sana busungu aka mpatia sshilingi elfu tatu boda boda, ambae alikuwa nauakika wa kupata zaidi ya elfu kumi, “lakini braza.....” alitaka kulalamka yule yule dereva wa pikipiki, lakini akashuhudia mteja wake akizi tupa elfu tatu chini “ kwani ujawai kutoa msaada wewe?” aliongea bsungu na kuondoka zake kuingia ndani ya jengo, pc Busungu akiwa anasilaha yoyote, alipandisha ngazi za gholofa hili akiwa anachomoa simu yake ili ajaribu kwa mala nyingine kumpigia insp Johnson, kwa bahati nzuri akapokea, nakuanza kumweleza juu ya uwepo wa Jackline ndani ya jengoo lile la wajasiliamari, nandipo alipoambiwa na insp kuwa tayari Kaijage amesha dunguliwa, muda wote Busungu aliongea na insp huku anaendelea kupanda ngazi mbio mbio, wakati aiingia kwenye safu ya nne na ya mwisho ya jengo ili, ambayo ikiwa tulivu ilyo kosa misongamano ya watu, huku bado akiendelea kuongea na insp Johnson, pc Busungu akastuka akikutana uso kwa uso na mschana mzuri sana mwenye umbo matata, lililoonekana vyema ndani ya gauni lililo shonwa kwa kanga, akiwa amebeba begi dogo jeusi begani kwake, licha ya kugundua kuwa yupo hatarini, lakini Busungu ambae alikuwa anafahamu kuwa insp yupo njiani, anakuja maali pale, tna alikuwa anafwatilia mazungumzo yao sababu, simu yake ilikuwa hewani, akaamua kumzuga Jackline, kwa maswali ili waweze kumtia nguvuni, ndipo alipo mwuliza swali, lile ambalo ata insp alilisikia, lakini Jackline akujibu chochote, zaidi alizidi kutembea kuelekea kule aliko simama Busungu, huku ameachoa tabasamu, kwamaana njia ndiko iliko, mpaka hapo busungu akajuwa kuwa kifo chake kime karibia, akaona bora apambane, hapo Pc Busungu akamsogelea Jackline kwa kasi sana, nakuruka juu akiachia ngumi kwanguvu zake zote, lakini akashangaa kuona mwanamke huyu akimkwepa kidogo sana, ungesema kuwa anapisha na mtu ambae alikuwa anapita njia, na busungu akapitiliza, na kwenda kutuwa nyuma ya Jackline, lakini ile Busungu ana tua chini, akastuka kumwona jackline, akimjia kwa kasi ya umeme, apo busugu ak rusha ngumi nyingime kiulenga uso wa Jackline, lakini ali sha ngaa wepesi wa dada huyu, maana alimwona akiyumba kidogo kisha kwa kasi ileile ya umeme, alizisikia ngumi nne kali zenye uzani mkubwa, zikitua kwenye mbavu zake, nakumfanya ahisi kama amepigwa na kitu kama nyundo au kipande cha nondo, simu yake ika dndoka pembeni, huku ikisikika sauti ua insp ikiita hallow! hallow! busungu“  Busungu  akuwa na uwezo wa kuongea na simu yake, akajishika kwenye mbavu huku akitoa mguno wa maumivu, huku akiinama sura kaikunja kwa maumivu, macho ameyaelekeza kwa  Jackline, akiitaji huruma ya Jackline, lakini ndiyo kama alikuwa anamchochea dada huyu, amtangulize kuzimu, maana alimsongelea pale alipo, na kumwongezea ngumi nzito ya kichwani, karibu na shingoni busngu akajibwaga chini huku akipiga ukelele wa maumivu, hapo Jacklne akakamata kichwa cha Busungu kwa mikono miwili na kukizungusha, na kufwatiwa na sauti ya kha! iliyo ashilia kuvunjika kwa shingo ya Busungu, ata alipo mwacha, Busungu alionekana kutulia pale chini bila uhai, hapo Jackline aka iendea simu ya busungu ambayo bado ilikuwa hewani, akaiwka sikioni huku anatembea kushuka chini,  “insp kazi imeanza, najuwa unajuwakuwa bado mmoja nae ni baba yako, ukiendelea kujichanganya, na wewe utaongezeka na kuwa wasaba” alimaliza kuongea Jackline, akadakia Johnso kwa sauti ilio jaa jasira, “hallow we mwana.....” jackline akutaka kusikia Johnson anaongea nini, ndio kwanza akaitupa chini ile simu nakuzidi kushuka chini, ghorofa ya pili na jengo lachini watu walikuwa wengi sana lakini walikuwa wana tazama television kuangalia tukio la mauwaji lililo kuwa lina rushwa live toka mahakama kuu sekunde chache alikuwa amesha fika chini kabisa, lakini akamwaona  insp Johnson akiingia pale mjengoni kwafujo , na kuagiza milango yakutokea ifungwe, na akuna mtu kutoka hakuna mtu kuingia huku akiacha polisi wawili wasimame kwenye ule mlango, Jackline ambae alitumia nguo yakemoja, (kanga) kujiziba nusu ya uso wake, alimwona insp Johnson akiwaacha polisi wawili pale mlangoni, mmoja akiwa na silaha aina ya smg, na mwingine akuwa na silaha, kisha insp na askari watatu wakaendelea kupandishangazi kuelekea juu, kule ambako insp aliona ishara ya kutokea risasi, huku akisikika akiongea na simu akiomba askari zaidi kutoka kituo kikuu,  huku wananchi wakishikwa na taaruki, na kuanza malalamiko ya kila aina, hapo Jackline aka tazama kusho na kulia akabahatika kuona kibao kinacho elekeza vyoo vilipo, akaelekea upande huo, kisha aingia ndani ya choo kimoja wapo na kutazama kwenye dirisha, dogo lililopo juu sana, lilikuwa ni dirisha dogo la vioo lisilo na nondo, Jacklile akatabasamu, kisha aka pandisha gauni lake na kutoa kamba kwenye kapturah yake yajinsi, akaikunjuwa na kuiweka vizuri tayari kwa kazi aliyokusudia, ilikuwa ni kamba ndefu kiasi, ***** wakina Denis, bado walikuwa wanatazama television ambayo ilionyesha tukio wananchi walio kuwa wanafuria kifo cha bwana Kijage alie jaribu kugeuza sheria, na kuzarau vifo vya abiria wengi walio fariki kwenye hajari, japo mtu kubwa wa serekalini aliepewa zamana ya upelelezi, ame isariti serikali iliyo mpandisha vyeo na kumpa zamana kubwa sana, ikimlipa mshahara mkubwa na malupu lupu kibao ikiwemo usafiri na nyumba nzuri ya kuishi, alisahau yote na ku geuza ushahidi, “hiyo ndyo zawadi ya mjanja” alisema Janeth, na kuungwa kono na wenzake, ***** tukio hilo pia lilionyeshwa katika television nachi nzima, na mmoj wa watu waliokuwa wakitazama tukio hilo alikuwa ni mzee Michael Nyati, ambvae alikuwa ametulia sebuleni kwake mbele ya TV yake kubwa, akifwatilia tukio hilo, huku mda wote tabasamu likonekana kuchanua usoni mwake, *** nje ya jengo la wajasiliamari, watu walikuwa wamejaa wakishangaa uvamizi wa jeshi la polisi kwenye jengo lile, tayri waaandishi wa habari walikuwa wamesha fika kwenye eneo lile na kuanza kurusha matangazo, na wakati huo vilisikika ving’ola vya magari ya polisi vikija mbio eneo lile, na wakati huo lilionekana gari moja aina ya Toyota Noah likiondoka, na kupishana na magari matano yapolisi, yaliyo kuja na askari wengi sana, wenye silaha, **** “naona mambo yamekuwa mazito sasa” aliongea boss wao wakina Denis baada ya kuona taalifa imeamia kwenye jengo ambalo inasadikiwa kuna muuwaji, tena ni wakike, wakati huo kamera za wanahabari zilikuwa zinaonyesha magari ya polisi yaliyo kuwa yanaingia kwenye eneo la tukio, “Denis kumbe wewe ni muongo hen! si umesema gari lako bovu, sasa kile nini?” aliuliza Mahadhi huku akisongea kwenye TV nakuonyesha gari aina ya Toyota Noah lililo kuwa linapisha na na magari ya polisi, yaliyo kuwa yanaingia eneo la tukio, hapo wote mle ndani waka toa macho kulitazama lile gari, “kweli bwana” alisema Boss wa Denis huku wakilikazia macho gari lile, ambalo lilionekana wazi kuwa ni gari la Denis, asa kutokana na stiker moja kwenye kioo cha nyuma iliyo tangaza pombe flani, iliyotengenezwa na kiwanda kimoja cha humu nchini, 


Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)