DADA MDUNGUAJI EPISODE 7

Emmanuel Lee
By -
0
DADA MDUNGUWAJI EPISODE 7 STORY NA Mbogo Edgar ILIPOISHIA EPISODE 6 : kijana mmoja kati ya wale watatu alimwona Jackline, akajaribu kuvuta kumbu kumbu ya kuwa amemwona wapi huyu mwanamke mrembo, lakini kijana huyu, kwa kuwa alikuwa kazini, akapotezea akijiambia kuwa ule aukuwa mda wakutamani wanawake, japo aliendelea kumtazama mpaka alipo ingia kwenye jengo la MH Production, endelea ....... Ndani ya ofisi ya mkuu wa kitengo cha upelelezi, insp Johnson David Masinde, alikuwa amesimama mbele ya meza kubwa yenye vikolombwezo vingi sana, ukiachilia ma file mengi yaliyo pangwa vizuri, pia ulikuwa na vibendela vidogo viwili kimoja cha taifa na kingine cha jeshi, diary peni za kla rangi, vitabu vya sharia na simu tatu za mkononi, bla kusahau simu ya mezani, huku mbele kabisa ya meza hiyo kikionekana kibao kidogo, chenye maadishi, cssc J J Kishiko “jambo afande” alisalimia insp Johnson, kwa kupiga saruti, “jambo inspector, kuna swala moja nyeti nime kuitia,” aliongea afande Kishiko, “ndo afande nakusikiliza,” alijibu Johnson ambae alikuwa amesimama imara mbele ya mkubwa wake, “imegundulika kuwa gari la bwana Mathayo, lili ripotiwa kuibiwa siku tano kabala ya tukio, hivyo bwana Mathayo ausiki na mauwaji ya wale watu wawili waliotoroshwa” hapo Kishiko alitulia kidogo na kutoa lost riport na kumwonyesha Johnson, ambae wakati huo alisha anza kuhisi kuna jambo lime tendeka, juu ya swala hilo, “lakini afande, huyu mzee ni mtu muhimu sana katika kesi ninayo ifwatilia” aliongea Johnson baada ya kuiangalia ile lost riport, “ok! utafwatilia baada ya yeye kuondoka hapa kituoni, maana juu ya swala la mbezi lipo kwenye kitengo changu, kwahiyo leo usi mhoji lolote” alongea bwana Kishiko, na Johnson alipotaka kuongea jambo, mzee Kishio alimdaka juu kwa juu, “hiyo ni amri, unaweza kwenda sasa” hapo Johnson hakuwa na neno, akapiga saruti na kuondoka zake, akiwa amejawa na hofu kubwa sana juu ya kesi hii, ambayo kuto kuifanikisha ni sawa na kuruhusu kifo cha baba yake, wakati anatoka nje, ndipo alipo mwona baba yake, akiwa ameongo zana na mzee Mathayo, wanatoka nje ya jengo la ofisi za kituo hicho, “samahani nyie wazee wawili” mzee Masinde na Mathayo, ambao walikuwa wamesha fika mlangoni, wakageuka na kumwona Johnson, akija usawa wao, wakasimama kumsubiri, huku wameachia tabasamu kwenye nyuso zao, “hooo! insp habari za asubuhi?” aliongea mzee Masinde, “safi mzee wangu, shikamoni” aliwa salimia kwa pamoja, nao wakaitikia kwa pamoja, “hongereni kwa ushindi wa kupapatua kesi hii” aliongea Johnson na yeye akionyesha tabasamu, “kama wewe unashindwa kuni saidia mimi rafiki wa baba yako, unazani tuta fanyaje?” alijibu mzee Mathayo, kwa sauti ya chini sana, akimlahumu mtoto wa rafiki yake, Johnson akawasogelea zaidi wa zee awa wawili na kuwanog’oneza “baba ilimlilolifanya siyo kwamba mnatatua tatizo, ila mna zidisha tatizo” hapo wazee awa waliachia kicheko huku wakipeana ishara ya kuondoka zao, **** Jackline Michael Nyati, alikuwa juu kabisa ya jengo la MH Production, lenye gholofa sita tayari amesha iseti silaha yake aina ya mugnum siper rifle, aliyo ielekeza kwenye jengo la kituo kikuu chapolisi ambacho kilikuwepo umbari wa mita kama mia tatu toka alipo kuwa yeye, jicho lake la kulia lilkuwa kwenye kilengeo, ambacho kilikuwa kina uwezo mkubwa wa kuona mbali bila matatizo yoyote, Jackline alikagua jengo la kituo kile kwa kupitia madirishani, lakini hakuona kitu, alikagua sana bila mafanikio, lengo lake likiwa ni kumwona mzee Mathayo na kumtandika risasi, mwisho Jackline akategeshakileneo kwenye diridha la chumba cha mahojiano, akiwa na uakika kwa siku hiyo ya jumatatu, lazima mzee Mathayo ahojiwe hivyo lazima amuwai kabla ya kurudi mahabusu, alikuwa tayari kushinda utwa nzima, akimsubilia mzee Mathayo aingie kwenye chumba hicho ili aseme nae, japo kuna wakati alitembeza silaha yake kuangalia maeneo mengine ya jengo lile, sasa basi, wakati anapitisha kwenye mlango ndipo alipo mwona mzee Mathayo akiwa na mzee Masinde, wakitoa ndani yay a kituo hicho na kuelekea kwenye mahegesho ya magari, “yes! nime wapata washenzi, kumbe mpo wote wawili” alijisemea Jacklini huku akikoki silaha yake na kuingiza risasi kwenye chemba, hapo sasa Jackline akawa ana lenga kwa umakini, akitafuta uswa wa watu wale wawili ili atumie risasi moja kuwa maliza wote wawili, wadunguaji wanaita moja kwa mbili, **** insp Johnson David Masinde alisimama mlangoni akiwa tazama baba yake na rafiki yake wakitembea taratibu huku wakiongea na kucheka kwa furaha, kiukweli insp Johnson aliumia sana kwa swala la kuachiwa kwa mzee Mathayo, kwani ange msaidia sana kumaliza swala hili, “sasa wao wana jifanya wajanja, awajuwi kuwa kifo kina wawinda” alosema Johnson, huku akitikisa kichwa kwa masikitiko, wakati anafanya hivyo mala akahisi ame mlikwa na mwanga wa kioo, toka kwenye jengo moja refu, lililopo umbali wa mita mia tatu toka pale kituoni, akatazama tena vizuri, safari hii alikiona vizuri kitu kinachong’aa kilicho tazama upande wa kituoni, hapo akijiuliza mala mbili insp Johnso alitoka mbio kumwafwata wale wawee wawili, huku akipiga kelele, “lala chiniiiiiiiii” kamailivyo kawaida ya waswahili ndio kwanza wakamsangaa kamanda hyu wapolisi, ambae ali powafikia waina mzee Masinde ali mrukia baba yake na kumpiga kikumbo, kilicho wapeleka chini wote wawili, huku wakirukikwa na damu nyingi sana zilizo changanyika na uji uji mweupe, kisha wakamtazama mzee Mathayo aliekuwa bado amesimama, kama anasubiri bendera ipandishwe, kisha sekunde chache akaanguka ‘chini puu!’ huku kichwa chake kikionekana kimevurugika kwa kupasuliwa upande mmoja, na mwengine ikionekana arama ndogo tu! kama kama alie jichoma na msumari, “lala chiniiiiiiii” aliongea Insp Johnson, huku akiwa bado ame mzuwia baba yake pale chini, “baba najuwa bado uja saau mambo ya kivita, jitaidi utambae mpaka kwenye yale magari,” Johnson alimwambia mwambia baba yake, ambae alikuwa anatetemeka kwa uoga, “sawa usiniache mwanangu” aliongea mzee Masinde kwa sauti ya uoga ulio pitiliza, tupo pamoja baba, usogope” aliongea Johnson nakuanza kutambaa, kuelekea kwenye gari lakalribu yao, huku akimvuta baba yake ambae nae alijitaidi kujivuta, sambamba na mwanae, **** huku nako wale vijana watu walishuhudia tukio la mmoja wa bosi wao akipigwa risasi, “yule demu” aliongea mmoja kati ya wale vijana, wa aliekuja pale kwaajili ya ulinzi wa mzee Masinde na Mathayo ambae kwa sasa tayari yupo chini, “demu gani wewe” aliuliza kijana mwingine ambae alikuwa akitazama jinsi mtafaruku ulivyo kuwa mkubwa pale kituo cha polisi, ambapo, olisi wote walikuwa wame lala chin kwenye maficho ya kichwa, (wapiganaji wanaita, over head cover), na wanchi wakiwa wana kimbia huku na huku, “alipita hapa, ameelekea kwenye jengo lileeee” aliongea tena yule kijana huku anafungua mlango wa gari na kuchukuwa bastora ambayo ilikuwa imeifadhiwa chini ya seat, “jamani tunachelewa, tumuwai” aliongea yule jamaa kwa msisitizo, hapo nikitendo cha haraka sana, wale wenzake waka chukuwa bastora zao kama alivyo fanya mwenzo, kisha wakaanza kukimbilia kwenye jengo lile alilo onyesha wenzao, jenge la MH Production, wakiwa waeficha vizuri bastora zao, **** “baba tulia hapa hapa” baada ya kumfikisha baba yake kwenye maficho, ambayo aliamini yanaweza kuwa salama kwa baba yake, kisha akatoka mbio kuelekea ndani jaengo nakueleea moja kwa moja kwenye ghala la silaha, akiamrisha askari ambao walikuwa wame jificha mlendani wachukuwe silaha na kuelekea kwenye kwenye gholofa la MH Productin, dakika chache baadae askari kumi na tatu, walikuwa na wakiwa na silaha aina ya smg mikononi mwao walikuwa wakielekea kweye jengo la MH Production, **** Jackline Michael Nyati, alifungua silaha yake, akitenganisha kifaha kimoja baada ya kingine, na kuweka kwenye begi lake, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana, alipo maliza akaliweka begi lake begani, nakuanza kushuka ngazi kwa haraka sana, lakini hakufika mbali akawaona vijana watatu wakipandisha ngazi mbio mbio, akajuwa kuwa ni wageni wake, hapo akajuwa uwa anatakiwa kufanya jambo kabla awaja mchelewesha, maana alisha juwa kuwa kuna polisi alishaona uwepo wake kule gholofani Jackline Michael Nyati akaachia tabasamu lake la kuogofya, huku akitoa begi lake begani na kutoa kibati kimoja kinachotumika kuzuwia mitambo ya silaha yake, (resever cover) akakishika kono wa kulia na begi mkono wa kushoto, kisha akaanza kukimbia kwa kasi ya hajabu kushuka chini, ambako wale vijana watatu walikuwa wana tokea, nao awakuwa mabwege kwani walisha juwa kuwa huyu mwanamke siyo wa mchezo mchezo, wakasimama na kutoa bastora zao, toka mafichoni, na kuanza kuzikoki, tayari kumshambulia mwanamke huyu ambae alikuwa ana washukia kwa speed ya hajabu, lakini walichelewa, maana wakati wana jiandaa kumshambulia, tayari walimwona yule mwanamke ambae kimtazamo ni mrembo na mzuri sana, akiwa ameruka juu kama mwana sarakasi, akiwapita nakutua karibu na mwenzao ambae alikuwa nyuma kabisa kisha akamshindilia kile kibati shingoni, na kusababisha damu zimwagike kwa fujo, kama kuna bomba la maji lime pasuka, huku Jackline akiushika mkono wa yule jamaa ulioshikilia bastora na kugeuka nae kuwa tazama wenzake, kama afanyavyo mwalimu wa shabaha, anae mfundisha mwanafunzi kulenga kwa mala ya kwanza, hapo vijana wawili waliobakia, wakajuwa kuwa wakizubaa wa tapotea maisha, hivyo kitendo bila kuchelewa, waka ekelekeza bastola zao kwa Jackline na kumimina risasi kwa fujo, ambazo zilimwingia yule mwwenzao ambae tayari alikuwa amesha kata roho, ilisikika milindimo ya risasi mfurulizo, zilizo sikika mpaka kwenye gholofa ya pili, ambako wanchi waikuwa wengi wakifanya manunuzi kwenye maduka yaliyopo ndani ya jengo lile, na kusababisha mtafaluku ndani ya jengo lile, watu walikiambia hovyo huku na uku, wakitafuta mlango na ngazi za kutokea mahali pale, wale vijana wawii waliendelea kumwaga risasi bila kukoma, mpaka walipo sikia ‘kacha kacha’ tayari walisha ishiwa risasi, waka mwona Jackline akiwa bado amesimama nyuma ya mwenzao, ambae alikuwa anavuja damu, kama maji kwenye mfuko wa Rambo, ulio dondokea kwenye mti wa miba, na ndipo walipo juwa kuwa zile risasi zilikuwa zina mchakaza mwenzao, na siyo mwanamke walie mkusudia, hapo Jackline akuwapa nafasi ya kujiuliza, akiwa ame mshikilia yule kijana wa kwanza aka fanya kama ana mfundisha kupiga risasi, akawa tandika wale vijana wawili risasi za vichwa, kisha akamwachia yule kijana ambae kwa sasa alikuwa ametobolewa vibaya sana kwa kwa risasi, akadondoka chini, hapo jackiline ambae alikuwa ame chafuka kwa damu bahadhi ya sehemu za mwili wake, aka shuka ngazi kwa kasi ya ajabu, mpaka kwenye golofa ya pili akiungana na wanachi wengine kukimbia, huku akiangalia hhuku nahuku mpaka alipo liona duka la nguo, akatabasamu kidogo “yes” alijisemea Jackline huku akinyoosha mkono na kufuta nguo moja mfano wa kanga nyepesi, ***** Denis alikuwa sambamba na Mahadhi, ndani ya ofisi yao wakifanya makadilio ya ramani ya jengo moja kubwa la kisasa walilo li sanifu wenyewe, kwa ajili ya wateja wao toka Nigeria, ambao walikuwa wana taka kutengeza hospital hapa nchini, “Denis kumbe unaishi na mke alafu uniambii kaka?” aliuliza Mahadhi, wakati wanaendelea na kazi yao, Denis akatulia kidogo na kushusha pumzi kwa nguvu, kisha akamtazama rafiki yake Mahadhi, “tena nikuambie kitu kaka?, yani ata leo nimekuambia kwa bahati mbaya tu!” aliongea Denis, kwasauti ambayo ilionyesha akuwa anatania, “haah! Denis inamaana tuna bifu?” aliuliza Mhadhi kwa mshangao, “hatuna bifu, ila nikikuona unamvizia mke wangu, itakuwa zaidi ya bifu” maneno hayo ya Denis, yalimfanya Mahadhi aangue kicheko kikubwa sana, “wecheka tu, maana nakuona jinsi unavyo jifanya bingwa la mademu” aliongea Denis kisha akaendelea na kazi ya kuitathmini ile ramani, “usifanye hivyo Denis, kweli wewe wakini fikilia hivyo?” alilalamika Mahadhi, huku bado anamalizia kicheko chake, “ndio maana sikuhizi uwa unanikimbia” alisema tena Mahadhi, Denis hakujibu kitu, zaidi aliendelea na kazi kimya kimya, huku ikimjia kumbukumbu ya miadi yake na yule dada mwenye shepu ya kuvutia kingono, “yule demu asije akawa najilengesha, maana anajifanya kunijuwa sana” aliwaza Denis, ambae alipania kumficha Mahadhi kuhusu miadi hiyo, maana alisha ambiwa na yule dada kuwa aende peke yake iliaweze kumsimulia kilicho msibu, **** wakati Denis anawaza hayo huku nako, yule dada tapeli Sablina aliuwa anapanga yake, maana mda wote alikuwa anachezea simu yake kuandika ujumbe ujumbe kwenda kwa mwanaume wake, ‘zingatia muda, ili tuwai kumkamua’ aliandika Sablina nakuituma, ‘nimeshafika zamani sana, nipo big braza’ alijibu mwanaume wa Sablina, ‘nikitoka nae, nimlete wapi?’ aliandika Sablina, mlete kona ya mabibo, tena aje na gari lake, ili iwe lahisi kuondoka nalo’ alijibu yule mwanaume, ‘akikataa itakuwaje?’ aliuliza tena Sablina, ‘siyo tabu, utanijulisha sehemu mlipo, nitakuja mala moja’ **** polisi walioekana wakipandisha ngazi mbio mbio, wakipisha na wananchi waliokuwa wanakimbia hovyo, kutoka nje ya jengo hilo la MH Production, polisi wakiongozwa insp Johnson, ambae leo alikuwa makini sana, maana alikumbuka siku ile kule buguruni, Johnson aliofika kwenye ngazi za kupandia ghorofa ya sita akasimama ghafla, huku akionyesha ishara ya kusimama kwa askari wake waliokuwa wanamfwata nyuma, nao wakasimama nakujificha kwenye kiambaza, insp Johnson alioneka amekaza macho yake mbele akitazama juu ya ngazi kadhaa, ambapo aliona miili ya watu watatu wakiwa wame lala kwenye madimbwi ya damu, lakini akukuwa na mtu aliesimama, “ameondoka huyu mshenzi” alisema kwa sauti ya kunong’ona, huku akianza kupandisha ngazi kusogea pale walipo lala wale watu watatu, huku akifwatiwa na askari wenzake, ambao nao walishikwa na mshangao, “ok! akuna kushangaa, nyie watano kagueni eneo hili, na msubiri hapa mpaka waje watu wa alama na michoro, sajenti utabakinao, wapigie simu mala moja watu wa mochoro” alisema Johnson, akionyesha kwa vidole askari watakao bakia, kisha akaondoka nao wale walio bakia, akiwapa maelekezo ya kutawanyika kenye mitaa ya pale kaliakoo, pia Johnson akapiga simu kuomba askari zaidi, waongezeke kumsaka muuwaji, maana Johnson aliamini kuwa, alie wauwa wale vijana ndie alie muuwa mzee Mathayo, na pia wale vijana ni kati ya wale vijana walio uliwa pale Matumaini Dispensal, na nikati ya vijana waliotumia gari la bwana Mathayo kuwatorosha wenzao waliokuwa wameuwawa, kwa hiyo wale vijana walio uwawa pale MH Production, walikuwa wame kuja na wakina mzee Masinde, na inaonekana kuwa walianza kumwona muuwaji mapema, na kuamua kumfwatilia, wakati anaendelea kuangaika kwenye mitaa ya kaliakoo, insp Johnson alikuwa akiwaza na kuwzua jinsi mchezo unavyo kwenda, na kufikilia jinsi atakavyo mlinda baba yake, juu ya kumkamata muuwaji siku ile, insp aliona ni ndoto za mchana, kwani alijuwa wazi kuwa, muuwaji awezi kuwepo eneo lile muda huo, **** taalifa za kuuwawa kwa mwanajeshi mstaafu, aliestaafu miaka mingisana nyuma , akiwa na cheo cha sajenti taji Mathayo, mbele ya kituo kikuu cha polisi, zilitambaa kwa haraka sana, huku Redio na Tv mbali mbali, zilitangaza kama taarifa ya hivi punde, (brecking news), saa sita na robo, mzee Nyati alikuwa mbele ya Tv yake akitazama habari hiyo nyeti aliyo kuwa anaisubiri kwa hamu, kilicho mshangaza ni kukutwa kwa maiti zaidi za vijana watatu, hapo akampigia simu mwanae, *** mida hiyo ndio mida mbayo Denis alimtoroka mahadhi na kishuka chini ya jengo la Mazao lenye gholofa tatu, na kumpigia simu yule mwana mke mwenye msambwanda wa ajabu, kama waliambizana kumbe yule mwanamke nae alikuwa tayari amesha shuka chini ya jengo lao la Kamanga Plaza, lengo lake likiwa ni moja tu, kama Denis ange ghaili kuongea nae, basi yeye angemvizia wakati anaenda kwenye chakula cha mchana kisha ange jifanya amekutana nae kwa bahati mbaya, dakika chache baadae walikuwa ndani ya gari, tuna elekea wapi, aliuliza Sablina, “labda useme wewe, sehemu unayo iona inafaa kukaa” aliongea Denis akiwa ajuwi kuwa mwenzie anawasiliana na mwanaume wake kwaajili ya kumfanyia kitu roho inapenda, **** “za saa hizi baba” alisalimia Jackline, baada ya kupokea simu toka kwa baba yake, Jackline ambae alikuwa ndani ya dala dala litokalo poster, alilopandia mnazi mmoja kituo cha baridi, na sasa walikuwa wana katiza manzese, kuelekea ubungo, akika usingeweza kumjuwa kama ametoka kufanya tukio mida ile ile, kwa jinsi alyo jitanza ile nguo aliyo ikwiba pale dukani, “naiona kazi yako, vipi hupo salama?” aliuliza mzee Nyati, “nipo salama baba, ni takupigia nikifika nyumbani,” alisema Jackline akiofia kkunaswa maongezi yake na kijana mmoja pembeni yake, alie kuwa anamtaza sana, “samahani dada sijuwi ulijiumiza sehemu, naona kuna madoa ya damu usoni mwako, unge nunua maji unawe kidogo,” aliongea yule kijana, hapo Jackline alistuka na kumtazama yule kijana, “Haaa! kumbe yule muuza bucha alinimwagia damu nyingi sana?” alijifanya kushangaa Jackline, “lakini aijapoteza mwonekano wako mzuri” alioongea yule kijana huku akiachia tabasamu, wakati huo dala dala lilisimama kwenye kituo cha mahakama ya ndizi, hapo Jackline Michael Nyati, akashuka haraka toka kwenye dala dala, kisha akaanza kutembea akitazama huku na huku, akitafuta sehemu ambayo anaweza kujiweka vizuri kwa kuusafisha uso wake, kwanza kabisa akaingia kwenye vibanda vya wauza mitumba na kununua tishert moja, alafu akamuiza yule muuza mitumba, “samahani kaka eti kuna guest house hous maeneo ya karibu na hapa” yule kijana alimtazama kwanza Jacklie huku ameachia tabasamu la kumsuta, akiamini kuwa mwanamke huyu anamiadi na mwanaume flani, “hapo mbele kidogo kuna bar moja kubwa sana, inaguest nzuri sana ina vyumba vizuri sana” hapo Jackline akaaga na kuondoka zake, akielekea upande alioelekezwa na yule muuza mitumba, mpaka alipoona bar moja kubwa sana, ailiyo jaliwa na watu wengi sana, wakipata chakula cha mchana, na wengine wakishushia vinywaji mbali mbali zikiwepo pombe, akachepuka na kuingia ndani ya bar hiyo kisha akaenda moja kwamoja kwenye sehemu ya mapokezi, akaomba apatiwe chumba kimoja chenye bafu ndani yake, kwaa jili ya kujifanyia usafi, **** baada ya kuangaika kwa mda mrefu sana, akiangaika kwenye mitaa ya kaliakoo, sambamba na askari wake, akimtafuta Jackline Nyati, insp Johnson aliamua kurudi kituo kikuu, ambapo alimkuta baba yae akiwa pale anamsubiri, ni kwelimzee huyu akuweza kuinua makalio yake kurudi nyumbani, akiofia usalama wake, Insp Johnson baada ya kukamilisha report yake, aliaga na kuondoka na baba yake wakitumia gari la baba yake huku lie jingine 110 walilokuja nalo wale vijana watatu, liligunduliwa na polisi na kupelekwa kituoni, “baba huu ni wakati wakuweka wazi kila kitu, iliniweze kuokoa maisha yako” aliongea Johnson, baada ya kutoka kituoni pale, “mwanangu kwakweli akuna ukweli wowote uliojificha, sijuwi huyo mtu anatuandama kwanini?” aliongea mzee huyu ambae alioneka bado anania ya kuficha swala hili, “atakama ujuwi chanzo lakini siuna juwa nanani anausika?” aliongea Johnson, “yani muuwaji ndio kitenda wili kikubwa” alongea mzee huyu bila aibu yoyote, “baba sijuwi kwanini una nificha mimi mwanao ambae ndie nawezakukusaidia kuepuka na hili, maana kama msinge mjuwa muuwaji, msinge watuma wale vijana kwenda kumteka yule binti” hapo mzee Masinde akatulia kimya kabisa, akitazamambele ya gari, “kumbuka nilicho kuambia dakika chache kabla ya mwenzio kuuwawa?” aliongea Johnson akionyesha kushikwa na uchungu mkali juu ya baba yake, ambae aliamini kuwa yupo hatarini kupoteza maisha, “Johnson naomba uelewe kama ninavyo kuambia, simjuwi muuwaji na sijuwi anafanya hayo kwa sababu gani?” alisema mzee Masinde kwa hasira, hapo Johnson akakaa kimya kidogo kisha aka ongea kwa sauti ya upole kidogo, “nitajitaidi kuyalinda maisha yako mpaka hapo utakapoona inafaha kunieleza ukweli” **** baada ya kuoga na kubadiri tishert, Jackline alitoka kwenye chumba alicho kodisha, na kutokeza kwenye sehemu ya bar, akitaka kwenda kurudisha funuo a chumba mala akashangaa kuona gari la Denis likipaki kwenye maegesho ya ile bar, “mh! so Denis yule?’ alijiuliza Jackline huku akisogea sehemu nzur ambayo aliamini anaweza kumwona Denis pasipo yeye kumwona, akajisogeza karibu na ukimgo wa ile sehemu iliyo kuwa na watu wengi waendelea kupata chakula na vnywaji, sehemu ambayo ilikuwa karibu kabisa na liliposimama gari la Denis, wakitenganishwa na uzio wa mbao, ulio tengenezwa kwa mtindo wa draft ndogo ndogo, na kufichwa na maua malefu yaliyostawi vyema, akiwa pale amesimama akastuka kumwona akishuka kwenye gari, mwanamke mmoja mwenye shepu ya maana, “ni yule wa juzi, nilijuwa tu huyu mwanamke analake jambo” aliwaza Jackline, huku wivu wa hatari ukiwa ume mkamata, aliona wazi kuwa kuna kila dalili ya kuchomoa roho ya mtu, “karibu dada ni kuhudumie nini?” Jackline alistuliwa na sauti ya muhudumu wakike, hapo Jackline akatazama pembeni yake na kuona kunameza yenye viti vitatu, ambavyo havikuwa vimekaliwa na mtu, “naomba soda” aliongea Jackline huku akitoa fedha na kumpatia yule mhudumu, kisha yeye akaa kwe kiti kimoja kati ya vile vitatu, na kuweka lile begi lake chini karibu kabisa ya miguu yake, huku muda wote macho yake yakiwa kwa Denis na yule mwanamke, ambao aliwaona wakiingia mle ndani nakwenda kukaa meza ya nne toka alipo kaa yeye, mala mhudumu akaleta soda yake, hapo Jackline akiwa amejitanda vizuri ile nguo aliyo iba kule kaliakoo, alikunywa soda yake taratibu akiwa fwatilia Denis na yule mwanamke, ambao walionekana wakiagiza kitu kwa mhudumu, na baada ya mhudumu kuondoka, wakaonekana wakiongea jambo flani, na mwongea ji alikuwa yule mwanamke ambae alikuwa aamsimulia kitu Denis, “samahani dada naweza kukaa hapa” Jackline alistuliwa na sauti nzito ya kiume, akamtazama mwongea alikuwa jamaa moja ambae kimwonekano ni kipande cha mtu kilicho panda hewani, na kutanuka maeneo ya kifua, akionyesha kuwa ni mtu anae jishughulisha na unyanyuwaji wa vitu vizito, Jackline akaona kuwa itakuwa vyema akia na mtu mwingine pale mezani iliasionekane kilahisi, “hapana tatizo kaa tu!” alijibu Jackline , ambae sasa alibadiri mfumo wa utazmaji, maana hakutaka huyu jamaa wa pembeni yake, ajuwe kama kuna watu anawafwatilia, **** baada ya kumfikisha baba yake nyumbani insp Johnson alirudi kituo kikuu kwenda kupata alama za vidole, za muuwaji alie wa uwa wale vijana watatu, ambmae aliamini ndie alie muuwa mzee Mathayo, alipofika pale kituoni alikuta bahadhi ya polisi wakiwa nje ya jengo la kituo wakijadiliana kuhusu tukio lililo tokea leo asubuhi, ni baada ya kuangaika mtaani wakimsaka muuwaji, walieambiwa uwa ni mwanamke, , bila mafanikio yoyote, insp Johnson akiwa na mawazo mengi sana, alipitiliza ndani moja kwa moja, akiwaacha askari wkiwa makundi makundi wakipiga porojo, Johnson akaingia ofisini kwake, na kukuta report ya mtambuzi wa alama ikiwa mezani kwake, akaitazama kwa umakini sana, akagundua kuwa report ile ni tofauti na report za siku za nyuma, hii ilionyeshakuwa marehemu wame uwana wenyewe kwa wenywe, kwa kutumia bastola zilizo kutwa eneo la tukio, “itawezekana vipi?” alijiuliza insp Johnson, “huyu mtu anaonekana, anamafunzo makubwa sana ya kijeshi” alendelea kuwaza Johnson, wakati huo akakumuka jambo, akachukuwa simu yake, na kupiga kwa pc Busungu, aikuchukuwa mda mrefu akapokea, insp Johnson akamwelekeza wakutane nyumbani kwake jioni, akidai kunajambo anataka kumweleza, **** akiwa ajuwi lolote Denis pale coner bar, akinywa bia pamoja na Sablina, ni baada ya kumaliza kula, huku anamsikiliza yule mwanamke tapeli, ambae alikuwa anamsimulia story ya uongo, akidai kuwa, kuna mwanaume ambae alipanga kuoana nae, hivyo kwa kujuwa ndie mmewake mtarajiwa yeye Sablina akauza nyumba yake ya urithi, aliyo achiwa na marehemu mama yake, na fedha akamlkabidhi yule mwanaume, ili afanyie biashara itakayo wasaidia katika maisha yao, sablina alidai kuwa yule jamaa yake alitoroka na zile fedha, na mpaka leo haja mwona tena, “dah! pole sana” alisema Denis, ambae alionekana kuanza kukolea kilevi, huku anaweka chupa tupu ya bia mezani na kufungua nyingine, “sante mbona nilisha sahau maumivu” alisema yule mwanamke, huku akiandika ujumbe kwenye simu yake, ‘naona pombe imesha anza kumlegeza’ akaituma kwa mwanaume wake, ambae alikuwa amekaa meza ya nne toka walipo kaa wao, aikuchuuwa mda mrefu jibu likarudi, ‘poa endelea kumpigisha story, mpaka alegee kisha tumwamishe maana naona hapa kazi itakuwa ngumu’ Sablina alipo maliza kuisoma ile sms akaiweka simu yake mezani, “yani nili hapa kuwa sitopenda tena tena, lakini nashangaa nilipokuona kwa mala ya kwanza nikajikuta natokea kukupenda sana” aliongea Sablina tapeli, huku akijichekesha chekesha, ni kauli iliyo mstua Denis, “mh! ume nipenda, ki vipi?” aliuliza Denis kwa mshangao, “yani ata mimi sielewi, nime tokea kukupenda tu!, unaonekana mstaarabu, mpole, unamoyo wa huruma, na jisikia raha kukaa karibu na wewe, yani natamani kama unge kuwa mume wangu” aliongea Sablina kwa sauti ya uzuni, huku akijidai kujizuwia kulia, kiasi cha kumfanya Denis aingiwe na huruma, lakini moyoni mwake akakili kuwa leo amekutana na kituko cha mwaka,mala Denis akahisi kuwa kuna ujumbe umeingia kwenye simu yake, akachomoa simu yake na kusoma ujumbe toka kwa Jackline, ‘hupo wapi?’ Denis akajibu, ‘nipo coner ya mabibo na pata bia kdogo nirudi nyumbani, vipi ume nimiss?’ kisha akaitumwa kwa mama kijacho, “usijari mungu atakupatia mume mzuri zaidi” aliongea Denis wakati anasubiri jibu toka kwa Jackline, ‘sidhani kama nita mpata kama wewe, kwani unachati na nani?” aliuliza sablina ambae alianza kutilia mashaka juu ya uchezeaji wa simu wa Denis, aikuchukuwa mda mrefu jibu lika rudi, ‘yani nahisi kama naibiwa, maana hapa nilipo chini kunatekenya sana?’ “hahahahaha! nachati na mke wangu” Denis alimjibu Sablina, huku anaandika sms, kurudisha jibu kwa mpenzi wake Jackline, ‘usijari uwezi kuibiwa, nakuja kukuletea dudu, maana najuwa inabidi tumkuze mtoto’ kisha akaituma, maongezi yaliendelea huku vinywaji vina endelea, walitumia mda mrefu sana, wakiongea na kunywa pombe, Denis alioneka kunywa pombe nyingi sana, lakini akuoneka kulewa mpaka, kupitiliza, ndipo Sablina akaomba ushauri kwa bwana wake, kupitia sms, ‘huyu jamaa anaoneka nimzoefu wa pombe sasa tufanyaje?’ jamaa yake akajibu, ‘tutumi plani B, akiinuka wenda chooni tu! nifwate, hapa nilipo kaa’ sablina akajibu ‘sawa’ atimae saa kumi na mbili na nusu, ndipo Denis alipo inuka na kuelekea chooni, akidai kuwa, akitoka chooni wamalizie bia zao waondoke, ile Denis anapotea kwenye mlengo wa choo, Sablina akainuka haraka na kumfwata jamaa yake, ambae alikuwa ame kaa meza ya nne, toka alipo kaa yeye na Denis, alimfikia mwaume wake ambae alikuwa ame kaa pamoja na mwanamke mmoja alie jitanda nguo kichwani na kushindwa kumtambua vizuri, kutokana na ile nguo na giza lililoanza kutanda, “amesema akitoka chooni anamalizia bia tunaondoka, kwa hiyo tunafanyaje?, amaana namwona kama hajalewa vizuri” aliuliza Sablina akiwa ame simama mbele ya meza hile aliyo kalia mwanaume wake, ambae aliingiza mkono kwenye mfuko wake wa suluali na kutoa kichupa kidogo hivi, akamtazama yule mwanamke wa pembeni yake, ambae muda wote alikuwa akichezea simu huku anakunywa soda, akamwona yupo busy na mambo yake, akamgeukia Sablina, nenda ka mwekee hii kwenye bia yake, akinywa kidogo tu! msisitize kuondoka maana akichelewa kuingia kwenye gari ata lala pale pale, itakuwa msala kumbeba” aliongea yule jamaa huku anampa Sablina kile kichupa, sablina akakipokea na kurudi haraka kwenye meza yake akakifungua kile kichupa na kumiminia tonye la maji kwenye chupa ya bia ya Denis, alafu akakifunga ile kichupa na kukiweka kwenye mkoba wake, Denis akiwa ajuwi kinacho tokea, alitoka chooni na kurudi pale alipo mwacha Sablina, ile anakaa tu akapokea ujumbe kwenye simu yake, akaitoa simu yake mfukoni, huku akiinua bia yake na kupiga mafundo mfululizo mpaka ilipo kuwa imekwisha, akaiweka chupa tupu mezani na kuufungua ujumbe kwenye simu yake ‘usinywe hiyo bia’ hap Denis aliduwaa, akajaitazama ile chupa mezani, akaiona ikiwa na wenzake kama watatu huku zikicheza cheza kama zipo kwenye bembea, na kuanza kufifi kwa mwanga usoni kwake, kabla aja mwona yule dada akisimama na kumshika mkono kisha kuanza kumpeleka kwenye gari, lakini Dens anahisi miguu yake ina kuwa mizito, kiasi cha kutaka kudoka, mala anaongezeka mwanume mmoja mwenye nguvu, ambae ana mskika kwanguvu na kuzidi kumsogeza kwenye gari lake, hapo Denis anaona giza nene likitanda usoni mwake, macho yake yana shindwa kufumbuka, kina fwata kimya kizito, mala anaanza kisikia sauti ya mvumo wa feni, inayotembea taratibu, akasikia sauti ya music wa taratibu, na sauti za watu wakiongea karibu yake, “kwahiyo shemeji ujajuwa alifikaje hapa?” ilikuwa sauti ya Mahadhi, “yani tena nashukuru aliiweza kufika mpaka hapa, maana ange zidiwa huko mbali sijuwi ingekuwaje” iilikuwa sauti ya Jackline, “daaa! ila shemeji una moyo sana, umeweza kukaa na mtu ambae ajitambui kwa siku tatu” sasa ilikuwa ni sauti ya boss wake, hapo Denis akapata picha kwamba yupo nyumbani kwake na hao ni wakina Mahadhi, akajaribu kufumbua macho, yaka fumbuka, akajikkuta yupo ndani ya chumba chake nyumbani kwake kibamba njia panda ya shule, ameamka jamani, wakwanza kumwona alikuwa Mahadhi, “we mshenz... umefikaje huku bila kuniambia nawakati nilikucha ofisi, au... unampango na mke wangu” aliongea Denis kwa sauti ya uchovu, huku akijaribu kuinuka toka kitandani, kumfwata Mahadhi, ambae akutaka kumwonywsha kabisa mpenzi, Wote mle ndani walicheka sana, kasolo Denis mwenyewe ambae aliduwaa akiwatazama wenzie wakimcheka, “Denis siwezi kufanya kitu kamahicho rafiki yangu, kuwa na amani” alongea Mahadhi wakati huo Jackline alikuwa amemuwai Denis asiinuka, akamshika na kumrudisha kitandani, “tulia mume wangu, bado auna nguvu” aliongea Jackline, ambae mda huu wote alionekana mwenye tabasamu la furaha, kwa sauti ya upole na unyenyekevu, kiasi cha kuwasisimua wakina Mahadhi, “hivi ilikuwaje kuwaje, maana nakumbuka nilikuwa naongea na dada mmoja hivi….. yuleeee tulie mpa lifti juzi, mala… nikazidiwa na pombe” aliongea Denis, kwa sauti ya kichovu, huku anajaribu kuvuta kumbu kumbu, “mimi mwenyewe na shangaa umekuja na gari ukasimama hapo nje kisha uka lala humo humo, na siyo leo ni juzi” aliongea Jackline, na kumfanya Denis ashikwe na mshangao mkubwa kama ameonanyoka mwenye miguu, “toka juzi, inamaana leo lini?” aliuliza Denis akitazama dirishani, akaona mwanga mkali wa jua, ikionyesha ni kama saa tano za asubuhi, akakumbuka alipo kuwa pale bar ilisha timia saa kumi na mbili na dakika zake, akajuwa kuwa inawezekana akawa kweli amezima gari kwa siku tatu, “punguza pombe Denis, utaibiwa mke” aliongea Mahadhi, ambae toka alipo mwona mke wa rafiki yake, alikilikuwa kimya cha rafiki yake kilikuwa na maana kubwa sana, “nita kunywa supu ya mtu siku nikijuwa naibiwa” aliongea Denis ambae bado alikuwa kitandani akionyesha kuwa akuwa na nguvu za kutosha, Jackline akatoka kwenye kile chumba chawageni alicho lazwa Denis, na kuelekea jikoni ambako dakika chache akaja na uji wenye mchanganyiko wa nafaka mbali mbali, kama karanga ulezi ngano soya, mahindi na vitu vingine vingi sana, ukiwa uanfuka moshi kwenye bakuri kubwa sana, “kunywa kwanza huu uji, kiisha nikuletee, supu ya kuku, aliongea Jackline akiweka mezani, lile bakuli la supu na kumsaidia mume wake kukaa pale kitandani, ilianywe uji, “ungekuwa ujapata mke, sijuwi kama tusingekukuta umsha kauka” aliongea boss wao wakina Mahadhi, ambae alioneka na kuwa ni mcheshi sana, wote mle ndani wakacheka,kasolo Denis ambae alikosa nguvu yakucheka, “lakini boss mwambie Mahadhi ni malufuku kuja kwangu kama mimi mwenyewe sipo nyumbani” aliongea Denis wote wakacheka tena, kasolo Denis mwenyewe, ambae alikuwa ana nyweshwa uji na Jackline mpenzi wake, baaa ya kushindwa kukimiliki kijiko kutokana na mkono wake kutetemeka sana baada kujaribu kukamata kijiko, wakina Mahadhi walikuwawepo pale kwa mda mrefu, waliongea sana mpaka saa kumi za jioni, walipo amua kuondoka, wakimtaka Jackline aendelee kumtazama Denis, nakwamba akiwa anaitaji msaada wowote awajulishe mala moja, ka kutumia simu ya mumewake, yalishapita masaa saba, toka Denis azinduke toka kwenye usingizi wa siku tatu kasolo, “samahani Jack, nime kutesa sana mpenzi wangu” aliongea Denis ambae alisha anza kulejewa na nguvu zake, na sasa walikuwa wame kaa sebuleni wakitazama Tv, “wala ujanikosea, ni bahati mbaya tu inatokea, ila usinywe tena pombe kwenye bar ukiwa peke yako, au na mtu usie mfahamu vizuri” alijibu Jackline akimlaza Denis kwenye mapaja yake, licha ya kuwa ni mapenzi makubwa aliyo nayo kwa mwanaume huyu, lakini pia Jackline alifanya hivyo, kwaajili ya kumzuwia Deinis asitazame picha zilizo kuwa zikionyeshwa kwenye Tv, zinazo husu habari iliyo kuwa inaendelea, “watu hao wanao tajwa kuwa ni mume na mke waliowai kufanya matukio kadhaa ya utapeli, wakutwa wame uwawa kwenye poli la hifadhi la kisopwa, sikuchache zilizo pitwa, kisi cha miili yao kuliwa na wanyama wa polini, “kama ni matapeli wacha tu wauwawe” alisema Denis pasipo kutazama kwenye Tv, “alafu yule mwanamke sijuwi aliniwekea nini kwenye pombe yangu?” aliuliza Denis huku akivuta kumbu kumbu flani, “yani kama unamachale hivi, umenitumia ile sms, kwamba nisinywe tena pombe, ndio yakanikuta majanga” aliongea Denis akionekana kujilahumu sana, “ila mimi ni noma yani nimeendesha gari bila kujitambua mpaka hapa, duuh!” ilo lilimshangaza ata Denis mwenyewe, ambae alimfanya Jackline aangue kicheko, “ila yule mwanamke nita mtafuta nijuwe alikuwa na maana gani, si amesema anauza duka la simu pale Kamanga,” aliongea Denis safari hii akionyesha kupania, “wala aina haja, mume wangu kana alikuwa nania mbaya anaweza kukudhuru” aliongea Jackline akijifanya kuwa na wasiwasi, “weeee! aniwezi, mimi mwenyewe mtoto wa mjini” alijitapa Denis na kumfanya Jackline acheke tena, “vipi mtoto anasemaje alinimissi” aliongea Denis akiwa analipapasa tumbo la Jackline, wote wakacheka kidogo, **** ilikuwa hivi, Jackline akiwa bado amekaa pale kwenye meza na yule jamaa, akaona kama kuna mawasilano yanaendelea kati yake na mtu mwingine aliopo maeneo ya karibu, na yeye akazidi kuwa makini, asa alipohisi kuwa, yule jamaa karibu yake anawasiliana na mwanamke alie kaa na Denis, hapo akaona kuwa hilo siyo fumanizi tena, kinachofwata ni kumwokoa mpenzi wake, ambae alisha jaribu kumpima kwa kumtumia ujumbe kuwa yupo wapi, ili aone kama atamdanganya au atamweleza ukweli, Denis nae akiwa na mapenzi ya kweli kwa Jackline akamweleza ukweli, hapo ndipo Jackline akajuwa kuwa hapakuwa na usaliti, lakini kuna jambo linataka kutokea, wakati akiwa amesha choka kusubili, na amesha mwona mpenzi wake amekunywa pombe nyingi, akataka kwenda kumchukuwa na kuondoka nae, lakini akamwona anainuka nakuelekea chooni, akajuwa kuwa akitoka ndio utakuwa wakati mzuri wa kuondoka nae, lakini akasngaa kuona yule mwanamke aliekuwa amekaa na Denis akiinuka na kuja pale alipo kaa yeye na yule mwanaume, alicho fanya yeye nikujiziba vizui na ile nguo aliyo iba kaliakoo, akiofia kugunduliwa na yule mwanamke, ambae walishawai kukutana nae, siku tatu zilizopita walivyo mpatia lifti pale kibamba, kweli akamwona yule mwanamke akija mpaka kwenyeile meza yao na kuongea na yule mwanaume, akimwambia kuwa anawasi wasi ya kushindwa kufanikisha mpango wao, sababu Denis anaonekana bado ajalewa, ndipo yule jamaa alipo mpa kile kichupa cha dawa, akisisitiza kumwinua mala tu baada ya Denis kunywa pombe yenye dawa hiyo, kwanza kabisa Jackline alitaka kuanza kazi pale pale, lakini akajuwa itakuwa ni hatari sana kwake sababu Denis ata usishwa kwenye tukio na kusababisha yeye kupatikana kilahisi,akatulia huku akichekecha kitu cha kufanya, wakati huo alimwona yule mwanamke akichanganya ile dawa aliyopewa kwenye bia ya Denis, ambayo aliambiwa kuwa ni ya usingizi, hapo Jackline akapata wazo la kumwai Denis kule chooni, akachukuwa begi lake jeusi chini ya miguu yake kisha akainuka na kuanza kuifwata njia ya kuelekea chooni, lakini akuwai kwani Denis alisha toka na kuelekea kwenyemeza yake ndipo yeye alipo ghaili kuelekea chooni na kuelekea nje, huku akiandika ujumbe na kuutuma kwa Denis “usinywe hiyo bia” licha ya kumwona Denis akiitoa simu yake toka mfukoni, lakini akashangaa kumwona akianza kuimalizia bia yake kisha akausoma ule ujumbe, “amechelewa” alijisemea Jackline huku aki tembesa haraka na kwenda kusimama kwenye maegesho ya magari, yapale coner bar, Jacklne Michael Nyati akiwa amesimama ubavuni mwa gari la pili, toka kwenye gari la Denis, aliwaona yule mwanamke na mwanaume wakimkokota Denis wakija usawa wa gari la Denis, ambae alionekana kuzidwa na ulevi, akuna mtu alie wajari, maana mambo ya klewa mpaka kuzima garo, uwa yanatokea sana kwenye mabar mengi, Jackline aliwaona wale watu wawili wakimfikisha Denis kwenye gari lake, alafu yule mwanamke anaingiza mkono mfukoni mwa Denis na kutoa funguo ya gari kisha akafungua mlango mkubwa nyuma wa lile gari, alafu wote kwapamoja waanza kusaidiana kumwingiza Denis ndani ya gari, mpaka walipo fanikiwa, wakaufunga ule mlango wa nyuma na wote wakaamia seat za mbele wakipitia ndani kwa ndani, yule mwanamke akampatia funguo yule mwanaume ambae alikuwa amekaa kwenye seat ya dereva, mala moja bila kuchelewa yule jamaa akaliwasha gari, “yes linamafuta yakutosha” alisikika yule jamaa akiongea huku akiingiza gia tayari kuondoa gari, ndipo kwa haraka sana Jacklin Michael Nyati alio chomoka toka mafichoni na kuwai mlango wa wa nyuma wa gari na kuufungua kisha akaingia ndani ya gari kwa haraka sana na kuufunga mlango, “nani wewe”aliuliza yule jamaa kwa sauti ya uoga na mstuko, “islael mtoa roho” alijibu Jackline kwa sauti kavu yakike, na kitendo bila kuchelewa, yule jamaa akahisi kitu kizito kikitua shingoni mwake karibu na kisogo, na kumlegeza pale pale, “he! wifi nanii dada, nili kuwa nanii, shemeji amelewa sana…” alisema yule mwanamke huku akijaribu kufungua mlango ambao ulikuwa bado kwenye lock, lakini alistukia nay eye akipigwa kama yule mwanaume wake na kulegea pale pale kisha kutulia, hapokamamwizi Jackline aka laza seat zote za mbele walizo kalia wale mtu na mke wake ambao walikuwa wamezimia,akawa vutia kwenye seat za nyuma, kisha akakaa kwenye seat ya dereva, kitu ambacho Denis alikuwa akijuwi ni kuwa mke wake anajuwa kuendesha gari, tena amejifunzia kwenye gari ngumu sana land lover one ten, manu transmision gear, na nyumbani kwao songea anamiliki gari, toyota harrier, ambayo alinunuliwa sikuchache kabla ya kuja dar es salaam kwa kazi maalumu, hivyo kwa hili toyota noah kwa ke aikumpa shida, dakika chache nusu saa baadae alikuwa ndani ya msitu wa kisopwa, akiwa shusha abilia wake ambao baada ya kuwashusha, aliwa sachi mifukoni akiwakuta na visu, simu ile chupa ya dawa camera ndogo na kamba nyembamba kama ya kuvulia samaki, alicho kifanya aliwa vutia kwenye kichaka na kuwa wakata shingo zao kwa kutumia kile kisu alicho wakuta nacho, maana chakwake akuweza kutembea nacho siku hiyo, kutokana na nguo alizo vaa, Jackline akuweza kuwaacha watu awa kutokana na kuwa yule mwanamke alisha mtambua kuwa yeye ninani, hivyo ingekuwa lahisi wao kumtaja endapo polisi wange tangaza juu ya kutafutwa kwa mwanamke muuwaji, alipo akikisha ame maliza kuwa kata shingo zao pasipo kuzitenganisha na kiwili wili, Jackline Michael Nyati aliingia kwenye gari na kuelekeanyumbani kwao kibamba njiapanda ya shule, ambako ali mshusha mume wake, kisha akaoga na kuzisafisha nguo zake alizo fanyia kazi mwisho akaelekeasebuleni akawasha tivi na kusikilizia matukio aliyo yafanya kaliakoo, huku akiendelea na mapishi, akiamini mume wake ataamka asubuhi baada ya pombe na dawa aliyowekewa kuisha nguvu, ****wakati huo insp Johnson alikuwa amekutana na PC Busungu, kumweleza kuwa anaitaji amfwatilie mzee Masinde yani baba yake huku akimficha kuwa ni baba yake, “akikisha unakuwa nae makini sana kufwatilia nyendo zake, maana naishi uwenda na yeye ni mmoja kati ya watu wanao takiwa kuuwawa, kwa hiyo jitaidi, sana kuwa nae karibu, na akikisha apatwi na jambo lolote baya, sababu ni shahidi muhimu katika kesi hii” huo ndio ujanja alio utumia Johnson kumlinda baba yake, alipo toa maelezo hayo, wakaagana na kuelekea nyumbani kwake mbezi beach,ambako alipokelewa na mke wake, ambae kwakipindi hiki alijawa na wasi wasi mwingi juuya kazi za hatari za mume wake, ***** usiku waleo bwana Masinde Alex na Kaijage akuna alie weza kwenda kwenye msiba, kila mmoja akiofia kuuwawa, maana waliona kuna kila dalili ya adui yao kuwa shinda nguvu, walibaki wakitumiana meseji, wakijadiliana juu ya mabo yanayo tokea, ‘kama vipi twendeni songea tuka mtafute Nyati’ lilikuwa wazo la Alex, ‘alafu tukifika tutamwambia atuelewe?” aliuliza mzee Masinde, “akun swala jingine zaidi ya kuomba samaha, na kumpatia kiasi cha pesa’alishauri tena Alex, ‘nazani tukifanya hivyo,atuta pata atanafasi ya kuwekewa matanga, atatuuwa kimya kimya nakutufukia huko huko’ lilikuwa wazo la Kaijage’ mzee Masinde akaunga mkono, wakidai kuwa huyu jamaa lazima atakuwa na hasira kali sana juu yao, ‘kwahiyo hapa tusubili zamu yetu?’ lilikuwa swali toka kwa Alex, ambae aliamini kuwa suluhisho ni kumfwata Michael Nyati na kumwomba msamaha, huku wakimpatia kiasi kikubwa cha fedha, ‘mimi naona tuame mji’ alishauri Kaijage, ‘unazani nisehemu gani hapa tanzania, atashindwa kutufikia?’alihoji mzee Masinde, kwakweli mjadala huu ulikosa mwafaka, *** siku yapili Jackline aliamka saakumi nambili nanusu, akamtazama mume wake akamwona bado amelala, akajaribu kumwamsha, lakini hakustuka kabisa, akatoka kitandani na kuelekea sebuleni, na kuanza kufanya mazoezi, alitumia lisaa lizima kisha akafanya kazi zake za kila siku, mpaka alipo stuliwa na simu, ya Denis ambayo ilikuwa ina ita, akaifwata na kuitazama, mpigaji alikuwa ni Mahadhi, akaipokea, “hallow, habari” alisalimia Jackline, “hooo! shemeji hongera sana” aliongea Mahadhi kwa sauti ya uchangamfu utazani wamesha wai kuonana, “hongera ya nini?” aliuliza Jackline kwa sauti ambayo aikuwa ya uchanga mfu wala ya hasira, huku akionyesha kushangaa, “au Denis ametudanganya, amesema una ujauzito” hapo Jackline akajikuta akitabasamu na kumtazama Denis pale kitandani, “nikweli shemeji, asante” alijibu Jackline, “tuta kuletea zawadi zako, ok! huyu bwana vipi, mbona ajaja kazini?” aliuliza Mahadhi, “anajisikia vibaya kidogo bado amelala” alijibu Jackline ambae aliamini kuwa, mda wowote Denis anaamka, “ok! kumbe unajuwa tulipatwa na wasi wasi, maana jana alinitoroka mchana, nashangaa mpaka leo kimya, nasi utatujulisha anavyo endelea” waliagana na kukata simu, Jackline akamtazama tena Denis, “amka mume wangu, tayari wabaya wako wamesha pata malipo yao” alinong’ona Jackline, kiisha akarudi jikoni kuendelea na kazi zake, mpaka saa nne ina ingia bado Denis alikuwa amelala ajitambui,ndipo Jackline akaamua kumpigia baba yake, iliapate ushauri, bahati nzuri akapokea mama yake, “hongera mwanagu, naona umebakiza watatu, ndani ya miezi mitatu” alisema mama yake baada ya kumaliza kusalimiana, Jackline alimweleza mama yake kilichotokea jana juu ya Denis, hapo mama yake akamwambia, asubiri baada ya mda mfupi atapewa maelezo kwanjia ya sms, na kweli baada ya mda mfupi akapokea sms, iliyo mwelekeza kitu cha kufanya, akashauliwa aende kwenye duka la dawa za hasiri (wengine wanaita dawa za kisuni) huku wakiholozesha dawa za kwenda kununua, kisha awapigie wampe maelekezo hapo mala moja Jackline aka jiandaa na kuanza safari ya kuelekea barabarani madukani, akiwa amevalia nguo za kiheshima ya kimama, licha ya kuvaa gauni lakini alijiziba kwa vitenge mwili mzima akiachia uso peke yake, lakini uvaaji huu aukuzuwia bahadhi ya vitu kuonekana, asa msambwanda, pale kibamba apakuwa na duka la dawa za hasiri, alielekezwa aende mbezi, ilikuwa bahati yake, maana baada ya mda fupi kufika mbezi alipata kila kitu alicho kiitaji, akaingia kwenye dala dala na kuanza kurudi kibamba, ***** pc Kessy ni askari polisi wa kituo kikuu, waliopo chini ya insp Jonhson, ni mmoja kati ya askari walio kuwepo kwenye tukio la kumkimbiza Jackline, kule buguruni, miezi mitatu iliyo pita kwenye jengo la baraka shopers, leo akwenda kazinin baada ya kupatwa na udhuru, akiwapigia simu kazini kwake kuwa anakwenda kumwona mgonjwa, tumbi hosptali, huko kibaha, kaini ilikuwa ni mbinu ya kwenda kula starehe nanyumba ndogo yake inayo kaa kiluvya kwa komba, PC Kessy akiwa amevalia mavazi nadhifu ya kiraia, alipanda magari yaendayo mbezi mwisho, akitokea nyumbani kwake magomeni kagera na kushilia mbezi mwisho, kisha akapanda gari la mkata kwa minajili ya kushukia kiluvya kwa komba, lakini akiwa ndani ya daladala linalo subiri habilia wajae, mala akamwona mwanamke mmoja alie jitanda vitenge akiingia kwenye gari hilo na kukaa siti moja karibu kabisa na mlango, licha ya PC Kessy kuvutiwa na uzuri wa huyu mwanamke pia alijaribu kuvuta kumbu kumbu kwamba aliwai kumwona wapi, maana sula yake aikuwa ngeni kwake, licha ya kujaribu kuvuta sana kumbukumbu lakini akufanikiwa, akawa ana mtazama kwa umakini uzuri wa yule mwanamke, ambae alikuwa amekaa mbele yake, baada ya mda gari likaondoka, huku kondakta mwenye mbwewe akianza kukusanya nauli, akianza na yule mwanamke aliekuwa amekaa karibu na mlangoni, akamwona akitoa shilingi miambili amsini, “kwani ukusikia wakati tuna tangaza” aliongea yule kondakta akikataa kupokea ile ela toka kwa yule mwanamke mzuri wakutamanisha, “kwani nauli ya kibamba ni ngapi?” aliuliza yule dada kwa mshangao, “kwani umeambiwa ili gari ni la kibamba? lipia mia sita nauli ya maili moja” aliongea yule konda, huku akichukuwa nauli kwa mtu mwingine, “kama ni uzuri kwa mume wako, sisi tume tumwa elea mjini” PC Kessy alimwona yule dada akifungua pochi yake na kutoa noti ya elfu kumi, akamkabidhi yule konda, “hivi we demu mbona una nyege hivyo, yani mia sita nikate kwenye huu msimbazi” yule Kondakta alisema hayo huku akiipokea hile fedha, Kessy alimeona yule dada akiwa anamtazama yule kondakta huku amekunja hasira, “angekuwa na uwezo amnge mmeza mzima mzima” aliwaza Kessy, huku akiwatazama kondakta na yule mwanamke, wakati huo bahazi ya watu walionekana kushundwa kuvumilia maneno ya yule kondakta, nakumwonya aache kauli zake chafu, lakini ndio kwanza yule kondakta akazidisha, weunazani nitatoa wapi, chenj ya buku kumi, ela zenywe mna ongwa, alafu unakuja kutusumbua tu!, sasa utashukia nitakapo pata chenji” abiria wote mle ndani walizani kuwa maneno ya konda ni ya hasira tu! ange mshusha yule dada kibamba, “nishushe kibamba” lakini wakaamini baada ya kuona gari lina pita kibamba kwa speed kali, licha ya mschana huyu kupiga kelele za kuomba kuwa ashushwe, hapo kila mmoja akiwa anamtazama kwa huruma yule dada mkimya, walimsikia kondakta akiendelea kuongea, maneno yake ya hajabu, “siku nyingine utakuwa umejifunza, utamwambia mteja wako awe anakupa buku buku, ilikuondoa usumbufu, simama hapo gogoni tumwache huyu changu” aliongea yule Kondakta huku akisogea mlangoni na kugonga ubavu wa gari kwanguvu, pc Kessy akiwa kama mtu wa usalama wa raia alikuwa ametulia kimya akitazama yule mwanamke anazalilishwa, garilikapunguza mwendo na kusimama, hapo kikatokea kitu mambacho hakuna aliamini macho yake, kitu ambacho kilimfanya pc Kessy amkumbuke huyu mwanamke, maana baada ya gari kusimama yule kondakta akatangulia kushuka chini akampatia yule dada noti yake ya elfu kumi kama ilivyo, “naoba ela ya texi” ilisikika sauti ya yule dada, ikionyesha akuwa na utani, “mwe malaya una kichaa nini, ela yanini wakati ela yako sija…” mpaka hapo watu wote awakusikia manemno ya mwisho ya yule kondakta, zaidi walishuhudia kipokea ngumi nzito ya mdomo, iliyo sababisha damu nyingi ziruke toka kwenye mdomo wa konda, zikiambatana na meno matatu, “mama nakufaaaaa!” alipiga kelele yule kondakita huku akipepesuka nakwenda kujibamiza kwenye ubavu wa gari, na kuanguka chini, na kuziachia fedha alizokuwa nazo mkononi, hapo yule mwanamke akaziokota, na kuhesabu ambazo zinge tosha kupandia taxi, wakati huo yule kondakta alikuwa anajiinua toka alipo anguka na kumfwata yule dada, kwa nia ya kupambana, maana akuamini kama amepigwa na mwanamke kama yule, konda akarushangumi ambayo ilidakwa na huyu mwanamke, kisha akaonekana kiuminya kwanguvu sana, “sijisikii kuuwa naomba usinifwate” alonong’ona yule mwanamke, kisha akampatia yule konda fedha zilizo bakia, dereva kuona kuwa mwenzie amezidiwa na mwanamke akaona labda mwenzie alizidisha dose ya ulevi anao tumia, bola akamsaidie kumwadabisa yule mwanamke, wakati huo abilia wote walikuwa wana shangilia, wakimtazama dereva akijiingiza kwenye mikono hatari,hapo sasa kilicho fwata kilimfanya pc Kess ashuke haraka kwenye gari, Dereva alipo mfikia yule dada, akajaribu kurusha ngumi, lakini akashangaa mkono wake ukidakwa na kubanwa kwanguvu, kama umebanwa na ile spana ya kutengenezea mabomba, huku konda kita akiwa ameachiwa, ana jikagua mdomo wake uliokuwa unavuja damu kwa kukosa meneo, Dereva alijaribu kufurukuta, lakini wapi, alibanwa kwanguvu sana kiasi cha kuhjisimkono wake una waka moto, wakati anasikilizia maumivu ya mkono, alistuka akipigwa ngumi moja mzito sana ya shavu, huku akiachomoka kwenye mkono wa yule mwanamke ambae sasa, aligunduwa kuwa, sio wa mchezo mchezo, kondakota na yeye akaona wakati huu mwenzie anatandikwa na yeye ndio wakati wa kulipiza kipigo kwa huyu mwanamke, akamzungukia kwa nyuma na kurusha teke kwenda kwa yule mwanamke, lakini bahati aikuwa upande wake, maana mguu hule ulikutana na mguu wa mwanamke huyu wa hajabu, ikasikika “paaaa!” kama sauti ya kuvunjika kwa mti mkavu, akiwa ajatambua killicho mkuta mwenzie, Dereva na yeye akarusha ngumi kumpiga mdada wa hatari, lakini ilikuwa siku mbaya kwake, maana mkono wake ulidakwa, na kukutana na ngumi mfululizo za usoni, zilizo sababisha yule Dereva aone giza usoni, na kujibwa ga chini kama kiloba, huku damu nyingi zikimchuruzka sehemu mbali mbali za uso wake, ***** insp Johnson alikuwa ofisini kwake akijiandaa kwenda kwa mzee Soud ili kupata ushauri, mala akasikia simu yake ya mkononi ikiita, akaitoa na kuitazama ‘Pc Kessy’ akaipokea, vipi Kessy mgonjwa wako anasemaje?” aliuliza insp Johson mala tu baada ya kupokea simu toka kwa askari huyu, alie omba kwenda kumtama mgonjwa wake hospital ya tumbi uko kibaha, “afande bado sija fika hospital nipohapa kiluvya gogoni” aliongea pc Kessy, kwa sauti ya chini kidogo, “ebu! ongeza sauti kidogo maana kuna kelele sana hapo ulipo” alishauri insp Johnson, “afande hapa nilipo kuna fujo zina tokea, namwona yule mwanamke wasikuile buguruni akiwapiga kondakta na Dereva wake” ahapo Insp Johnson alistuka na kusimama toka kwenye kiti alicho kalia, “una uakkika pc?” aliluza huku anauendea mlango wa ofisi nakutoka nje, nauwakika ni yeye, na mambo anayo yafanya hapa kwakweli kla mtu anashgaa, maana anawapiga awa jamaa, utazani yeye ni askari sita wajeshi la ulinzi” alisisitiza pc Kessy, “ok! nachukuwa askari tunakuja wewe mfwatilie mpaka anapo elekea, tutakuwa tua wasiliana” **** “ndiyo afande fanyeni haraka, mimi sina la kufanya, maana sina silaha yoyote” aliongea Kessy, huku anamtazama yule dada ambae baada ya kumaliza kuwaadhibu wale watukutu wawili, kisha akavuka barabara na kuelekea kwenye kituo cha daladala zinazo rudi kibamba, hapo pc Kessy na yeye akavuka barabara halaka sana na kuwa kwenye kituo hicho cha daladala zinazorudi kibamba, akamkuta yule dada akiwa pale kituoni, alipo litazama lile basi upande wapili wa barabara bado lilikuwa lipo pale pale, lime zungukwa na watu waki washangaa wale watukutu wawili, aikuchukuwa mda mrefu, likaja daladala likitokea kibaha likasimama pale kituoni Kessy akategemea umwona yule mwanamke akipanda haraka, ilinayeye apande lakini aikuwa hivyo alishangaa kumwona yule dada akiliacha lile gari likishusha abilia na kupakiza kisha likaondoka, mala simu yake ikaita Kessy alipoitazama alikuwa ni insp Johnson, “bado hupo nae” lilikuwa swali toka kwa insp Johnson, “ndio” Kessy alijibu kwa kifupi, “swa sisi tupo njiani tuna kuja wewe endelea kumfwatilian na kutupa report,” hapo wakakata simu, pc Kessy akatulia pale kituoni akimfwatilia yule mwanamke, ambae sekunde chache baadae akamwona akipokea simu, “kisha akayanasa maongezi yake, “ndio nimesha pata, ..... ndio nilipitilizwa na gari... ndio nasubiri gari la kurudi” sawa nitakujulisha” yule mwanamke alimaliza kuongea na simu, na muda mchache baadae likaja daladala lingine, hapo Kessy akamwona yule dada akipanda haraka ndani ya gari hilo, na yeye akuzubaa akapanda haraka, mala simu yake ikaita,akaipokea, “samahni nitakupigia nikishukakwenye daladala aliongea Kessy, huku gari likiondoka, kuekea kibamba njia panda ya shule, kutoka gogoni mpaka njiapanda ya shule nimweno wa dakika tatumpaka nne kwa gari la habilia, kwa hiyo aikuwachukuwa mda mlefu kufika na gari kusimama, hapo Kesy akamwona yule mwanamke akishuka toka kwenye gari, pamoja na abilia wengine, hapo na yeye akuzubaa akashuka mala moja, na kumtazama yule mwanamke, akamwona akivuka barabara na kuelekea upande wa pili, hapo Kessy akchomoa simu yake huku aksubiri magari matatu yaliyo kuwa yana pita barabarani yapite ili na yeye avuke kumfwata huyu mwanamke, kama alivya agizwa kufanya, Kessy alitumia muda huo kupiga simu kwa insp Johnson, “tumeshkuka kimba njiapanda ya shule mkono wa kushoto kama unaenda kibaha,” aliongea haraka haraka, huku akianza kuvuka bara bara, “sawa tunakuja tupo mbezi, endelea kumfwatilia kwa umakini” alisistiza Johnson, na kukata simu, baada ya kuvuka barabara Kessy alimwona yule mwanamke hatari akii toka kwenye duka moja, ambalo alionekana kama alikuwa ananunu kitu flani, kisha akaingia kwenye moja ya chochoro ya maduka yale, hapo Kessy akatembea haraka na kuifwata ile chochoro, lakini hakuona mtu mbele yake, akatembea mbele kama atuwa hamsini mpalka sitini akizipita nyumba kadhaa, mpaka akatokea kwenye makutano ya chochoro nne, zilizo tenganisha nyumba nne, akashidwa aftwate njia hipi kati ya zile, akakosa ata mtu wa kumwuliza, maana chochoro ilikuwa kimya sana, akachomoa simu yake na kunnza kuongea na isp Johnson, ***** “tupo kibamba kwa mangi, vipi bado hupo nae” aliuliza insp Johnson mala tu alipo ipokea simu toka kwa askari wake, afande kwakweli amenipote, katika mazingila ya kutatanisha” kauli hiyo ilimstua sana insp Johnson, sababu alijuwa kuwa muuwaji alisha gunduwa kuwa anafwatiliwa hivyo kinachofwata, “bado ujanipoteza, nipo hapa” kupitia kwenye simu ya askari wake, insp Johnson aliweza kusikia sauti ya mwanamke, ikimdhiaki askari wake, “ “mungu wangu nmekwisha” likuwa nisauti ya kunong’ona iliyo jaa uoga ya askari wake iliyo mfikia masikioni mwake, kupitia kwenye siimu ya pc Kessy ambayo ilikuwa bado aijakatwa, “ongeza mwendo, mwenzetu yupo kwenhatari” alipiga kelele insp Jonson akimwamlisha askari wake aliekaa kwenye kiti cha dereva akitembea speed ya mia themanini, ambayo alitembea nayo toka walivyo toka mjini kituo kikuu, huku askari sita wakiwa wana ning’inia nyuma ya gari hilo aina ya land lover 110, huku wameshikilia vyema silaha zao, zilizo jaa risasi, na sasa gari alikuwa na uwezo wakukimbia zaidi ya hapa, insp Johnson akiwa bado ameiweka simu sikioni, alijaribu kumwita Kessy, “hallow hallow, kessy unanisikia, ebu kimbia mahali hapo haraka” aliongea insp Johnson bila kujibiwa kitu, zaidi alisikia kishido cha kitu kizito kikidondoka chini, kikifwatiwa na mikoromo ya mtu alie kwenye mauivu makali, na arakati za kukata roho, hapo insp akajuwa kuwa amesha poteza askari mwingine, mwili ulimwisha nguvu, akabaki ameganda na simu bado hipo sikioni, “hallow insp wafundishe askari wako namna ya kufwatilia mtu! alafu nakuomba kaambali na hii kesi, wacha nimalizane na watu wangu pasipo kuongeza wasio usika” iinsp aliweza kuisikia sauti ya mwanamke ikisikika kwenye simu yake, ilizihilishakuwa Kessy hayupo duniani, “hallow, ebu tuambie unataka..” insp Jonson akuweza kumalizia maneno yake kwani simu ilikatika, dakika chache baadae waliingia kibamba njia panda na kusimamisha gari lao mbele ya maduka yaliyopo pembeni ya barabara, kisha ikatlwa amri askari wote wasambae kwenye chochoro za yale maduka, kumtafuta mwenzao, ambae hawakutumia mda mrefu kumpatana, wakikuta kisu na simu ya Kessy , waka mchukuwa mwenzao, na kuondoka nae haraka sana, wakiwaacha raia wanashangaa wasijuwe kinacho endelea, ***** Jackline Michael Nyati, ambae alikuwa amekosa amani, kutokana na afya ya Denis, baada ya kumaliza kutoa roho ya askari polisi aliekuwa anamfwatilia alirudi barabarani na kujibanza sehemu akiwa tazama polisi wakizunguka eneo alilo fanyia tukio, mda mfupi uliopita, aliwaona wakichukuwa mwili wa mwenzao na kuondoka zao, ndipo yeye alipo panda boda boda na kueleka nyumbani, baada ya kufika akapiga simu kwa baba ake na kumsimulia, kilicho tokea kuanzia makondakta wa daradara na yule askari polisi, baba yake alimsisitiza kuwa makinisana kwa sasa ikiwezekana apumzike kufanya mauwaji ya aina yoyote, ili kuwa sahaulisha polisi, pia baba yake alimwelekeza namna ya kutengeneza, dawa ya kumnywesha Denis, huku akimtahadharisha kuwa ajiandae kwa matokea ya mikojo, atakayo ikojoa huyu jamaa, ***** saa tisa jioni insp Jonson alikuwa yupo kituo kuu cha polisi, akiwa amesimama nje akiwasikia polisi wenzakewapale kituoni wakijadiliana juu ya mauwaji yanayo endela, “unajuwa mimi siamini kama huyo muuwaji ni mwanamke kweli” aliongea askari mmoja alie kuwa zamu ya ulinzi pale kituoni, “sikia kijana kuna mfungwa mmoja hivi, yupo ukonga, anaitwa Majaliwa, uwa anaendaga wizalani kufyeka, yule jamaa ukitazama usowake unaweza kusema alikatwa na mapanga, yani atamdomoi amepoteza bahadhi yameno, uliza sasa kilicho mkuta” aliongea askari polisi mmoja mwenye cheo cha sajenti ambae sikuhiyo alikuwa mkuu wa zamu pale kituo kikuu, “alifanywa nini” aliuliza yule askari, huku wenzie wanne waliokuwa pamoja, wakitega masikio, sambamba na insp Johnson ambae akili yake ilikuwa imeganda, “yule mfungwa alisimulia kuwa, wakati yupo kidato cha pili walijaribu kumbaka binti mmoja, unaambiwa huyo binti ni mzuri sana, yani kwa kipindi hicho huko Songea, akuna mwanamke angeweza kumfikia kwa uzuri, lakini kilicho watokea ni balaha, maana licha ya kuwa watatu lakini walitembezewa kichapo mpaka wakaelewa somo, yani siku yapili walienda kuripot wenyewe kitu cha polisi” alisimulia yule askari ambae ata kwa umri alionekana kuwa ni mtu mzima kidogo, ile story ili mvutia Johnson, “huyo mfungwa anaweza kuwa na umri gani?” aliuliza insp Johnson, huku akisogea eneo la tukio, “mh! ni miaka ishilini na nne au natano hivi, maana usoni amepondeka sana, uwezi kukadiria umri wake” alijibu yule askari sajenti, “ok! ilikuwa Songea, unasema huyo mfungwa anaitwa nani?” aliuliza Johnson, kwa umakini sana, **** saa tatu usiku Jackline alishapokea simu toka kwa Mahadhi akiulizia hali ya Denis,akamjib kuwa bado ajisikii vizuri, Jackline aliwaficha hali halisi, ili wasije kutemblea pale nyumbani na kumkuta mwenzao yupo vile, wakati huo Jacline Michael Nyati, alikuwa amesha nadaa ile dawa, aliyo elekezwa na baba yake, alicho kifanya ni kumwamishia Denis chumba cha wagenikisha akatafutakipisi kifupi cha mpra wa kupitishia maji, akamvwesha Denis kwenye dudu yake, kisha ule mpira akauweka kwenye dumu la lita tano, kisha aka mnywesha ile dawa, alafu akaenda kutulia sebleni na kusubiri kwa muda wa lisaa lizima akaenda kutazama lile dumu la lita tano, lilikuwa limejaa mikojo nusu, aka lichukuwa na kwenda kumwaga kisha akarudi na kuliweka tena, kisha akarudi sebuleni, nakumpigia simu mama yake, ilikumweleza matokeo ya dawa inavyoanza kufanya kazi, “endelea kumwangalia, ila akiamka akikisha unampa uji wamoto, na supu” aliongea mama Jackline, lakini wakati wanaagana kunakitu mama Jackline akaonekana kutilia shaka jambo flani, “hivi Jack hupo salama kweli” aliuliza mama Jaackline, “zaidi ya salama, siunajuwa mimi zaidi ya kikosi cha makomadoo” alijibu Jackline kwa kujiamini, “hacha utani mwanangu, atakama ni komadoo sijuwi kitu gani, lakini kumbuka, ukali wote wakiu lakini mbele ya maji uonekana mjinga, namaanisha umeziona sikuzako, maana sielewi jinsi unavyo hema sielewi elewi” hapo Jackline akatulia kidogo na kushusha pumzi kwa nguvu, ITAENDELEA...

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)