JINI SUKUBI

Emmanuel Lee
By -
0

MTUNZI:Mike Gonard
Facebook:Mike Gonard
Facebookpage:simulizi za mike Gonard

kati yetu....kuna jini mwanamke anayebaka wanaume jinamizini...

Kama ilivyokuwa kawaida yake Gonard ilipogonga saa mbili usiku alijipata ndani ya mjengo wa Printing wa Mombasa Apparel ama M.A.3 kama ilivyojulikana na watu wengi hususan wafanyakazi wa Kampani hilo.M.A.3 ni kampani ya nguo iliyoko mjini Mtwapa,katika pwani ya nchi ya Kenya. Gonard ni kijana barobaro,mpole na mchapakazi.Vile vile ni mfupi kama nyundo.Wakati Maasai wakifuga ng'ombe na kufaidika na maziwa na nyama Gonard aliachiwa kufuga nywele na ndevu. Mengineyo hayatuhusu na hayana maana kwa sasa.Muhimu zaidi ni kuwa Gonard alijiunga na M.A.3 Printing kama msaidizi wa msanifu wa lebo za nguo kwa maana ya assistant designer.Hili ni baada ya kusitisha masomo yake ya chuoni KMTC kwa ukosefu wa karo.

Alisitisha masomo yake ya Medical Engineering kwa maana ya uhandisi wa matibabu na kuamua kujitafutia karo mtaani ,hatimaye akaangukia M.A.3.Hajakata tamaa bado,moyoni mwake bado yuko na uhakika na ari kuwa siku moja atapata nafasi ya kujiendeleza kimasomo. ..Aliwakuta wenzake wakisafisha mashine za kuprint.Mara,"Mamba ndio huyo amedunda mjengoni,leo hakuna mtu kusinzia wala kulala ni kazi kwenda mbele", ni sauti iliyotokea pembeni mwa jengo hilo kulikokuwa na mashine za heatseal, Ilikuwa sauti ya mtani wake Gonard pia rafiki yake wa dhati,Haroon Chula ama Benja kama wenzake walivyokuwa wakimtambua. Mamba ni jina la utani walilotumia kumuitia kijana Gonard,asili na chanzo cha jina hilo ndio ni kitendawili.

Gonard aliwaamkua wenzake akiwa amezama kwenye kidimbwi cha furaha riboribo wengine wangesema mpwitompwito yani furaha isiyokuwa na kifani,labda kwa vile aliwaona wenzake wote buheri wa afya.Ama kweli ilikuwa siku njema,wenyewe wanasema huonekana asubuhi lakini yao ilikuwa usiku. Wenzake Gonard ni wakiwemo Benson,Omar,Manu,Bashir,Juma Hassan,Salim(fadha) Bakar Hussein na wengineo.Ilichukuwa takriban nusu saa nzima kutayarisha mashine zote.Omar Zingzing aliziseti screen zote zilizokuwa zitumike kwa kazi ya siku hiyo.

Mnamo saa mbili na nusu kila mmoja alikuwa ametulia kwenye mashine yake.Mashine nambari moja ndio Gonard na wenzake wanne walikuwa wafanyie kazi siku hiyo. Usiku huo ulikuwa mtulivu ajabu,isipokuwa vijisauti vya paka waliokuwa wakikimbizana nje ya jengo hilo,ndio viliharibu utulivu na ukimya huo.Huenda ilikuwa ishara fulani,waswahili wangesema dalili ya mvua siku zote huwa ni mawingu.Haikuwa kawaida paka hao kukaribia maeneo yale.Tuwaache paka hao waendelee kulialia na kujamiiana ili waongeze kizazi chao,tuendelee na stori yetu. Okay Alex alivunja ukimya ule uliokuwa umetanda kila kona ya jengo hili

"Tuone leo kama zawadi ya Vinoth itaenda kwa nani kunapopambauka "Ilikuwa kawaida yake Master Vinoth kutoa vijizawadi vidogo vidogo kwa mashine inayofanya vyema katika suala zima la uzalishaji ama production.Master Vinoth ni mhindi aliyekuwa anajali sana utendakazi wa vijana wake tofauti kabisa na wahindi wenzake waliojawa na kiburi, roho mbaya,chafu kabisa! Sauti ya Alex ilikuwa ya kichokozi kwa sababu mashine yake ndio ilikuwa ikiibuka na ushindi ,walikuwa wakiprint zaidi ya kiwango walichowekewa kama lengo ama target kwa kila lisaa,hivyo basi alikuwa akiwachokoza wenzake tu.

"Alex wacha masihara,leo usishangae Mamba akikutangulia kwa sababu, mashine yake inasukumwa utadhani lile fani la jehanamu linalozunguka kwa kasi ya ajabu kupunguza joto la huko,"Bashir alidakia kauli ya Alex. Gonard naye akaongezea kauli yake,"Mwambie ukweli Bashir ,tutavikusanya vijizawadi vyote vya Vinoth kutakapo pambazuka sababu Mamba yu'tayari kuishi ndani ya dimbwi la maji moto kuanzia hivi sasa,"

Kauli yake Gonard iliwafanya wenzake wapasue anga ile tulivu kwa kicheko kilichowafanya hata wale waliokuwa wakisinzia wachangamke. Muda wa mapumziko ulikuwa ukikaribia aste aste,saa saba na robo ilikuwa imetinga .Ilikuwa bado takriban robo saa hivi wafanyikazi wote waende kwa kipindi cha mapumziko mafupi kabla ya kuendelea na kazi yao mpaka alfajiri.

Gonard aliwaomba wenzake ruhusa na nafasi kidogo ili aweze kuenda msalani kujisaidia.Sehemu iliyotengwa kwa ajili ya kujisaidia ilikuwa hatua kidogo kutoka lilikokuwa jengo la Printing.Wenzake walimkubalia na kumruhusu aende.Aliwashukuru wenzake kwa hali yao ya uelewa wa haraka na huyo akatoka pole pole.Punde tu alivyorusha hatua mbili nje ya lile jengo alianza kuhisi vitu vya maajabu mwilini mwake.Upepo ulianza kuvuma hali isiyokuwa ya kawaida,nwyele na malaika ya mwilini mwake yalisimama tisti .

Uoga ulimvamia asijue nini cha kufanya.Alijikaza kiume na akapiga moyo konde,liwe liwalo.Isije nikajisaidia na kujitabawalia kwenye nguo ikawa aibu kwangu,kidogo ajichekeshe mwenyewe.Moyo wake uliendelea kumdunda du! du! du! kama wasemavyo waswahili na viswahili vyao.Alipiga ishara ya msalaba na kutamka maneno haya "Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu,Amina"kuashiria dua kidogo. Aliendelea kutambaa polepole,alinyatanyata mdogo mdogo tena kwa makini.Kimya kilichotanda kwenye kampani hilo usiku huo ilikuwa rahisi kuskia miondoko na hatua zake Gonard,ungeskia hata moyo wake ulivyokuwa ukimdundadunda ovyo kuashiria uoga.

Kadri alivyokuwa akikaribia vyoo hivyo alianza kusikia milio ya maajabu ikitokea ndani humo.Milio hiyo ilififia alipokaribia zaidi na alianza kuskia sauti za watu wakinong'ona tu.Kusema kweli Gonard alichanganyikiwa sana.Mara kwa mbali alisikia sauti za watu wakiongea ndani ya choo kimoja,alikaribia choo hicho kwa kunyatanyata ili aweze kuskia kilichokuwa kikiendelea . Gonard alikuwa na hamu hamumu kujuwa ni kina nani waliokuwa wakiongea na walichokiongelea,ukitia ndani kuwa wenzake wote walikuwa ndani wakiendelea na kazi hakuna hata mmoja aliyetoka wakati huo isipokuwa yeye ndio alikuwa wa kwanza kuenda msalani ,je wanaweza kuwa kina nani?

Hakuweza kubaini wala kutambua sauti hata ya mtu mmoja ya waliokuwa wakiongea chooni humo,ila kilichomshtua na kumtia baridi zaidi ni chenye kilikuwa kikiongelewa ndani humo,hali iliyomfanya azidi kuingiwa na uoga vilevile wasiwasi. "Leo Sukubi kapata rijali,kijana barobaro,atakidhi haja zake na kutoa hamu zake zote" ni sauti mojawapo ya waliokuwa wakiongea,ilipita na kupenya vizuri masikioni mwake Gonard."Hawa watu wanafanya nini humu ndani"Gonard alijiuliza maswali yaliyoishia bila majibu,asijue kijana aliyekuwa akiongelewa alikuwa yeye mwenyewe!Gonard alizubaa asijue nini cha kufanya,alishtukia kitasa cha mlango kikitikisika kuashiria kulikuwa na mtu akitoka,aligutuka na kujaribu kukimbia,Gonard alikuwa kunguru mwoga kutaka kukimbiza mbawa zake lakini juhudi zake ziliambulia patupu. Kabla hajaruka hata hatua moja alihisi mkono laini umemkamata ikifuatiwa na sauti nyororo na legevu,"usitoroke mpenzi,uko katika mikono salama,bora ufanye chenye nataka"Gonard alimuangalia aliyekuwa akiongea maneno hayo kutoka utosini ila hakufika chini,macho yaliishia kifuani mwa mtu huyo.

Mbele yake Gonard alikuwa kasimama binti mrembo,sema kaumbwa kaumbika,chuchu saa sita.Umbo la binti huyo lilijichora vizuri kwenye kidress alichokuwa amevalia,mwisho mapajani.Kusema kweli binti huyo alikuwa amejazia hadi nakosa maneno ya kuelezea yote kumhusu. Baada ya kitambo kirefu cha bumbuazi,"Hivi wewe ni nani na unataka nini kutoka kwangu?Halafu unafanya nini ndani ya kampani hili usiku wote huu? Mpenzi msomaji nikwambie ukweli haikuwa rahisi na kawaida kupata mwanamke katika kampani hilo wakati wa usiku,maajabu hayo kama si mazingaombwe aliyoyakuta kijana wetu. "Naitwa Sukubi binti Inkubi,si wewe ni Gonard?" "Umesemaje wewe!.

 "Nani kakwambia jina langu na ni mara ya kwanza kukutana na wewe na sijawahi kuona mtu kama wewe! Gonard alishtuka sana na kauli ya binti huyo,macho yalimtoka pima utadhani kaona mabaki ya Adam na Hawa.Alijaribu kufurukuta angalau aweze kujinasua kutoka mikononi mwa binti huyo lakini juhudi zake ziligonga mwamba,hazikufua dafu kamwe! Katika furukuta zake Gonard,ilimjia picha na taswira fulani miongo miwili iliyopita,alikumbuka vizuri sana sio mara ya kwanza kusikia jina Sukubi.

Kuna siku alikuwa amekaa na babu yake Mzee Ngamba kule kijijini kwao Viragoni kata ndogo ya Kaloleni na kusimuliwa simulizi fulani kuhusu Sukubi.Mzee Ngamba alisafisha koo lake,"sikia mjukuu wangu,katika ulimwengu huu majini yapo na yanaishi kati yetu" "Naam"Gonard aliitikia kwa hamu ya kutaka kusikia zaidi. "Mfano"Mzee Ngamba aliendelea "kuna jini mwanamke anayebaka wanaume jinamizini,anajulikana kama Sukubi,vile vile kuna jini mwanaume anayebaka wanawake jinamizini,anaitwa Inkubi.

Taswira hiyo ilimtoka ghafla,alijipata ndani ya choo akiwa na Sukubi tayari akinyonywa denda.Gonard alijikuta akiitikia busu hilo na kulikaribisha.Kusema kweli kwa jinsi alivyokuwa Sukubi hata ingekuwa wewe mpenzi msomaji haungeweza kulikwepa hilo. Sukubi tayari alikuwa ametoa kidress chake na kubaki na kitopu na ile kufuli pekeake.Woi! kitopu kimejazwa, kufuli nayo ndio hatari zaidi,macho ya Gonard yalipita tu juu chini kwa hamu ya kutaka kujua alichobarikiwa binti huyo,alimeza mate ovyo ovyo tu! Alizidiwa ujanja pale Sukubi aliporusha mkono wake laini na kuitoa maikrofoni na kuanza kuichezea kabla ya kuanza kuimba.Naye Gonard hakuwa mchache vile,aliishika kufuli na kuifungua! Maskini! binti ya wenyewe.. Tayari kashalowesha kufuli ile...Sukubi alipoishika maikrofoni hiyo nao mkono wa Gonard ndani ya kilichofichwa na kufuli iliyolowa...wote wawili walijikuta wakigonga chorus ama kiitikio cha nguvu...aaah...aaiissss...aah!! Ama kweli kuimba kutamu!! "Hivi Sukubi anaweza kuwa jini kweli mambo yote haya jamani" mh! aliguna kimoyomoyo na kuendelea kujiambia " haiwezekani kwa binti mrembo kama huyu kuwa jini,haiwezekani kabisa! alijisemea kwa ujasiri.

"Mbona umejamu ghafla mpenzi na nikama wafikiria sana,hebu njoo darling!" Baada ya matayarisho ya takriban dakika ishirini hivi,Sukubi alichukuwa maikrifoni na kuiweka mahali pake na wote wakaanza kuimba na kucheza...jamani chorus ndio ilichukuwa sehemu kubwa ya wimbo huo,Ungemsika Gonard akiimba...aaah...mmmh...oooh.. Naye Sukubi aliachiwa hizo ..aaiiiss...mmh..aaahh! Show ilikuwa kali ajabu,kwa sababu wasanii wote walijumuika kwa pamoja. Baada ya kama nusu saa hivi,show ilianza kuwavutia wazungu kutoka pande zote.Jamani! kumbe wazungu hupenda nyimbo nzuri na mitindo tofauti ya kucheza...Sukubi alikuwa anataka kumtangulia mwenzake,alisikika akisema...oooh.. aaah...beiiib naku...! Kabla ata kauli hiyo kumalizika,kuna kitu fulani kilimshtua Gonard na kufanya apige kamsa,hiyo ni baada ya kuona miguu ya Sukubi.Haikuwa miguu ya mwanadamu wa kawaida.Amini usiamini ilikuwa miguu ya punda na kwato zake! Mfarakano na hali ya kuchanganyikiwa kwa Gonard ilifanya wazungu warudi kwao uingereza baada ya mchezo huo wa kuimba na kucheza kusitishwa ghafla.. Gonard alipiga nduru kwa mara ya pili tena kwa sauti kidogo! "Gonard! we Gonard! mbona unapiga nduru kakangu kuna nini? Hebu njoo tuprint huku muda wa mapumziko umekwisha" Kijana wetu alikurupuka ghafla toka alipokuwa baada ya kuisikia sauti ya Bashir akimwamsha toka kwa jinamizi! "Mmh jamani" Gonard aliguna na kujiambia kumbe ilikuwa jinamizi tu! Siamini macho yangu,ila Sukubi kafanya mambo yake tayari,amekidhi haja zake! JINI SUKUBI KANIBAKA. Bashir alijaribu kumrai Gonard amwambie alichokiona lakini alidinda.

Hali ya kuchanganyikiwa kwa Gonard imsababishia kutoona jinsi Sukubi binti Inkubi kutoka Ujinini alivyoyeyuka ndani ya hewa nyembamba. Anachokumbuka ni maneno ya mwisho aliyosema Sukubi,"Nitakuwa nikikutembelea mara kwa mara" Maskini kijana wetu Gonard! Ndio matatizo yanaanza na tayari yamekuwa tipitipi..... Kusema kweli usiku ulikuwa mrefu kwa Gonard,ukichanganya kazi pamoja na ndoto aliyoota kipindi cha mapumziko ilimfanya ajawe na fikra nyingi na mawazo mchafukoge pamoja na wasiwasi. Baada ya usiku uliokuwa mrefu na kazi nyingi hatimaye kulikucha. Eric aliyekuwa mwakilishi wa wafanyikazi wenzake alichukuwa karatasi za uzalishaji na kuziwasilisha kwa Master Vinoth.Vijana wote walikuwa wamechoka tiki! Walitoka nje ya jengo hilo la Printing walipokuwa wamehakikisha kila kitu kilikuwa sawa.Tayari jua lilikwisha chomoza,lilimwaya miale yake angavu likiashiria siku njema.Kuchoka ni kwa kawaida baada ya kazi lakini kwa Gonard ilikuwa zaidi ya kawaida. Gari ya kampuni ilikuwa tayari kwa ajili ya kuwabeba vijana hao makwao.

Ilivyokuwa kawaida kwa Gonard,alishukia msikitini kwa Abuu,kwa vile alikuwa akiishi mtaa wa kati kutoka kwa kampani hilo.Alipiga kona ya kwanza na ya pili na kuingia kwake alikokuwa akiishi.Hakuwa na hamu ya kula chochote wakati huo alipoingia chumbani mwake,fikra zote kwa lile tukio la usiku aliloliona jinamizini.Alichemsha chai rangi na mahamri mawili,hicho ndicho kilikuwa kiamsha kinywa chake asubuhi hiyo. Baada ya kiamsha kinywa hicho,Gonard aliamua kuchukuwa kidaftari chake alichokuwa akiandika simulizi zake na kuendeleza Simulizi aliyoipa kichwa cha Jini Sukubi.Mtiririko wa mawazo katika uandishi wa simulizi hiyo ilimfanya asahau kidogo kichotokea usiku,alitiririka nayo kwa kitambo kirefu,takriban lisaa lizima hivi. Mara kwa mbali aliona mtu akimkaribia. Gonard aliingiwa na kijibaridi na wasiwasi wa ghafla baada ya kung'amua mtu huyo hakuwa mwengine bali Sukubi. Gonard alijikuta akiropoka kwa mshangao na hasira kidogo,"Ni wewe tena! Unachonitafuta mimi kitu gani lakini?" kwa kuibia ibia alikuwa akiongea hivo uku akiangalia miguu ya Sukubi.Kinyume na alivyokuwa akitarajia,aliona miguu ya mwanadamu wa kawaida kinyume na chenye alikiona usiku uliokuwa umepita. "Ndio ni mimi Sukubi binti Inkubi,halafu mbona unaniongelesha kwa ukali hivo?"Sukubi aliongea kwa sauti iliyolegea zaidi na yenye mahaba ndani yake."Sasa hivi tuko pekeyetu ndani ya chumba hiki,nataka unifanye,unitoe nyege zote".

Aliongea maneno hayo huku macho yakiwa ameyalegeza na akiwa akimaanisha alichokisema. Sukubi aliendelea kuongea ila Gonard alikimya tu kumwangalia binti huyo."Nataka turudie mchezo wetu kwa sababu uliniacha katika hali mbaya sana," Sukubi aliongezea huku akilegeza macho zaidi na kuumauma midomo yake hali iliyomfanya Gonard kubaki hoi bin taaban. Kusema kweli Sukubi alikuwa na uzuri wa ajabu sana,mzuri kwelikweli,alikuwa amekamilika kila idara .Umbo lake lilimaliza Gonard kabisa. Kidogo kidogo hivi Sukubi alimsogelea Gonard na kuchutama mbele yake.Kumbuka kwa wakati huo Gonard alikua amekaa kwenye sofa lake.Sukubi alimkumbatia Gonard na kumbusu shavuni,maskini alifanya kijana wetu akasisimka.Gonard alibaki hoi na hakuongea kitu kwa kitambo kirefu.Mara Sukubi alivamia midomo ya Gonard na kuanza kula denda,midomo yake laini na iliyokuwa na joto joto kwa mbali ilimfanya Gonard kuanza kugunaguna,raha hiyo aliyoipata kijana wetu. Mara Sukubi akaeka mkono ilikokuwa maikrofoni,"Mmmh"Sukubi aliguna,"Tayari imetuna,alafu likubwa vizuri,nalipenda hili,"Sukubi aliongea hivo huku akiiminyaminya maikrofoni kama mtu aminyavyo embe lililoiva.Kwa mara ya kwanza Gonard hakusita kama ilivyotokea usiku,alikubali na kutii amri,alimuachia Sukubi afanye mambo yake.Aliachia maikrofini ichezewe vilivyo,naye Sukubi aliichezea alivyotaka.Aliigugumia kinywani,mara ndani mara nje.Hali ya jotojoto lililokuwa kinywani mwa Sukubi ilifanya Gonard agune zaidi kwa raha alizokuwa akizipata.Sukubi alisukuma ndani nje na kuonyesha ufundi wake."Oooh..aaah...mmmh..aaah! "baada ya kama takriban dakika kumi na tano,wazungu walikuwa wanakaribia,Gonard alimsukuma Sukubi,alikuwa hataki wazungu wake waende mahali pasipostahili.

Gonard alimsimamisha binti huyo aliyekuwa amepandwa na mashetani ya mahaba,akamsukuma kwa kitanda.Ndani ya dakika mbili Gonard alitolewa bukta aliyokuwa kavaa wakati huo na kubaki alivyozaliwa.Sukubi alikuwa kajitoa kimini chake pamoja na kufuli yake mwenyewe kweli lilikuwa na hamu janajike hilo.Sukubi alijilaza chali huku akiwa amepanua mapaja yake,hali iliyofanya kitumbua chake kilichonona na kulowa kijitokeze wazi kabisa.Kijana wetu alijikuta akisukuma ulimi ndani ya kitumbua hicho,alipitisha ulimi wake hali ya kuchora namba nane juu ya kiarage kilichotuna kwa wakati huo. Maskini! Sukubi aliguna kwa mautamu aliyokuwa akipata,"aaaisss..aah!..aahh!..asante beiiib!...apooo .yeees! Alibana kichwa cha Gonard ndani ya mapaja yake,kumbe mtoto wa wenyewe alikuwa akimwaga hata kabla ya maikrofoni kutumika kwenye uimbaji huo. Punde tu kuona hivo,Gonard alichukuwa maikrofoni na kuiweka pole pole mahali pake,ilizama yote kwenye kitumbua cha Sukubi kilichobana vizuri na kubakiza mia mbili tu zikiwa nje.Walianza kuimba,Sukubi alikatika mauno ajabu,uku mwenzake akitia na kutoa maikrofoni.Kwa takriban nusu saa hivi ya chomeka chomoa,Gonard alipiga chorus ya nguvu ..."uuuwah.." Alimalizia wimbo wake na wazungu wote wakapenya ndani hali iyofanya Sukubi agugumie kwa raha kwa sababu wazungu walikuwa wengi,sijui kwa vile kuna joto jingi huko pwani ndio ilifanya wajitokeze kwa wingi,sijui! huku Sukubi akiachiwa hizo.."asante darling".."i love you beib" Walipokuwa wako kwenye harakati ya kuwakaribisha wazungu kwa safari ya tatu.... 

 "Hodiii..! Gonard...! Ngongongo...fungua mlango kidogo uchukuwe chaja yako nimekuletea.Gonard alishtuka kutoka kwenye lindi zito la usingizi baada ya kusikia mlango ukibishwa...kitabu alichokuwa akiandika Simulizi yake ya Jini Sukubi kilikuwa kimelowa mate ajabu!.. Chini ya bukta aliyokuwa kavaa alihisi mzizimo fulani wa kiana yake,alipogusa tu hivi alihisi kuna kitu kilichoteleza teleza,jamani tayari alikuwa amechafua bukta hiyo,ililowa hasa."Maskini Sukubi kanibaka tena" alijisemea Aliivua bukta haraka haraka na kujifutafuta na kuirusha bukta hiyo chini ya mvungu wa kitanda.Alijifunga taulo na kuenda kufungua mlango...kumbe alikuwa Jimmy Mrima jirani yake,alikuwa karudisha chaja aliyoomba pindi tu Gonard alivyoingia kutoka kazini. "Vidze nambira Gonard?" "Mambo gasawa Jimmy nambira haliyo? "Nashukuru Mulungu pia nimzima,nmekurudishia chaja yako,pole kwa kukusumbua" "Usijali Jimmy,karibu," Baada ya salamu hizo Jimmy alienda zake naye Gonard kurudi ndani.Alitafakari sana kuhusu jinamizi hilo,mara ya pili sasa,alikosa usingizi siku hiyo ukitupilia mbali na kuwa alikuwa kakesha kazini.

Gonard aliishi siku zote hizo hakuwahi kuambia mtu yaliyokuwa yakimtokea.Naye Sukubi hakukoma kumtembelea mara kwa mara alivyoahidi awali. Iliendelea hivyo kwa muda wa miaka miwili Gonard akiendelea kulala na Jini ambaye ni Sukubi.

Hatimaye siku moja Sukubi alijitokeza mbele ya Gonard akiwa kabeba mtoto."Leo umeamua kuja na mtoto na umefanana naye kweli,ni wa nani!"Gonard aliuliza kwa mshangao. "Huyu mtoto ni wako,hukumbuki mara ya pili ulivyolala na mimi ulinipea ujauzito?"Sukubi alisema. "Haiwezekani mimi kuwa na mtoto na jini!"Gonard alihoji kwa hasira na mshtuko kidogo. Kauli hiyo ilifanya mambo yakabadilika ghafla,Sukubi alibadilika haraka sana kuanzia macho yake,yalitokwa na michirizi ya machozi ya damu yakidondokea midomoni mwake kulikokuwa kumetokelezea meno mawili marefu upande wa juu! Miguu nayo ikawa ile ya punda kama awali.Sukubi akabaki dude dude tu lisiloeleweka na la kuogofya.Hali iliyomfanya Gonard akakemea,"Ushindwe na ulegee katika jina la Yesu kristo aliye hai!"Gonard aliona cheche zikimwagika kuashiria kutoweka kwa Sukubi. Aligutuka kutoka usingizini mnamo saa tisa usiku akiwa amelowa jasho huku akitetemeka kwa uoga.Aliwaza sana kuhusu suluhisho la kumaliza uhusiano wake na jini,hatimaye likamjilia wazo la kuenda kwa mchungaji. Akakumbuka kuwa kuna mchungaji fulani maeneo ya Shanzu Mjini Mombasa aitwaye Ezekiel Karisa,alikuwa hajamuona tangia azaliwe alimuona tu kwenye kituo chake cha runinga cha New Life Ministries.Kwa kweli Ezekiel alikuwa akitenda miujiza na kuponya watu waliokuwa na matatizo aina yoyote ile.

Gonard hakujuwa kanisa lilipokuwa,aliamua kuwa lazima aulizie ilimradi afike na kumuona mchungaji. Asubuhi ilipofika,baada ya Gonard kufanya kila kitu na kumaliza,alianza safari ya kuenda kwa Mchungaji.Guu mosi guu pili hadi kituo cha magari cha Majengo Kanamani hicho ndicho kilikuwa karibu na alikoishi Gonard.Aliabiri daladala kutoka hapo mpaka kituoni Shanzu,alishuka na kuingia vichochoroni huku akiulizia lilipokuwa kanisa la New Life.Alitembea hadi alipofika mtaa wa Karisa Maitha street alipatana na binti mmoja aliyekuwa kavalia vizuri. "Samahani dada,mambo?",Gonard alimuamkua dada yule kwa heshima. 
"Poa sana kaka,nambie?" 
"Nashukuru mzima,naulizaje kanisa la Pastor Ezekiel liko maeneo gani?" 
"Kwani unaenda huko"aliuliza binti huyo. 
"Ndio naenda huko lakini ndio mara ya kwanza sijui mahali liko",Gonard aliongea kwa hali ya upole sana. 
"Usijali kakangu pia mimi naenda huko huko tu,"aliongeza dada huyo. Gonard alimshukuru sana binti huyo na wakaandamana.Kwa wakati huo Gonard alijawa na fikra tele kumhusu Sukubi,"Kumbe yule ni jini kweli jamani"alijisemea kimoyomoyo."Uzuri wote ule ama kweli uzuri wa mkakasi..."alikuwa anaendelea kutafakari mara,"Tumefika ndio lile pale kanisa lenyewe",ilikuwa sauti ya yule binti aliyempata njiani kama muelekezi wake.
 "Nakushukuru dada kwa msaada wako ubarikiwe"Gonard alijibu. "Wala usijali kaka,"aliongeza dada huyo.

Kusema kweli lilikuwa kanisa kubwa kweli na kulikuwa kumejaa sisisi,na bado watu walikuwa wakifurika.Ibada ilikuwa ikiendelea .Punde tu ilipoisha,Gonard alienda hadi alikokuwa mchungaji,alisukumana na watu hadi akamfikia. Gonard alipiga magoti mbele ya madhabahu,kabla hajaeleza kitu chochote mchungaji alimwekea mkono kichwani mwake na kumwambia,"Kijana umeandamwa na jini,shetani mchafu wa ngono,mubakaji,hadi sasa wakosa amani maishani mwako",Mchungaji aliendelea,"Jini huyo anasema ana mtoto wako" "Ndio mchungaji huo ni ukweli,"Gonard aliongea kwa ujasiri akiona ukombozi kwa mbali. "Ulipokuwa waja huku yeye ndio kakuelekeza hadi umefika hapa,"mchungaji aliendelea kutoa tabiri zake. "Whaaat! impossible...!"Gonard alitokwa na uzungu wa ghafla kwa mshtuko,"Kwa hiyo mchungaji unamaanisha binti mwenye nimekuja naye alikuwa Sukubi binti Inkubi?" "Ndio ni yeye,na madhumuni yake alikuwa aje kuniangamiza mimi kwanza halafu baadaye akupeleke baharini akaishi na wewe na haungeonekana tena asilan,lakini Mungu ni mkubwa hakuna lisilowezekana kwake,"mchungaji aliendelea..."Binti huyo hakuweza kukanyaga ndani ya kanisa hili ameishia huko nje." Kwa kweli Gonard hakumuona alikokwenda binti huyo. "Tutaomba kwa pamoja na baada ya maombi nitakukabidhi kitambaa na mafuta,utajipaka mafuta na kurusharusha chumbani mwako wakati wa kulala na pia wakati uko safarini usisahau kuyabeba"mchungaji alisema. "Tumsifu Yesu Kristo,milele na milele,Amen! Mchungaji alihitimisha maombi hayo na kumkabidhi Gonard alivyomuahidi.

Gonard alianza kuona mwanzo wa ukombozi wake baada ya kutoka kanisani. ....Saa nane na robo hivi usiku wa kwanza baada ya Gonard kuenda kwa Mchungaji Ezekiel Karisa,Sukubi alijitokeza akiwa na huzuni,majonzi na akiwa akilia. "Gonard nifuate"Sukubi hakuwa na maneno mengi na sauti yake ilikuwa imejawa na huruma."Njoo please,kuna kitu nataka kukuonyesha." "Kunionyesha...!"Gonard alijiuliza kimoyomoyo tena kwa mshangao,alitii amri. Mara tu alipokubali kumfuata Sukubi,Gonard alijipata yuko ufuoni mwa bahari."Kanamai beach"Gonard ailjisemea moyoni baada ya kugundua bahari hiyo. "Hakuna siku umeniudhi kama leo,ulienda kufuata nini kwa mchungaji na unajuwa fika kuwa ni kinyume na mila na tamaduni zetu za Ujinini...?" Gonard alibaki kimya na kungoja kitakachofuata kwa sababu wakati huo Sukubi alikuwa kapandisha mori kweli kweli. Katika bumbuazi hilo la Gonard,hali ya anga ilianza kubadilika ghafla,baridi kali na upepo uliovuma kwa kasi ya ajabu iliongeza ukubwa wa mawimbi ya bahari hiyo.Ngurumo za radi zilisikika kote. Sukubi alibadilika hali ya kutisha,ghafla kulitokea viumbe vya maajabu kutoka bahari hiyo,majitu yasiyoeleweka,mashetani mashetani tu! Viumbe hivyo vilizidi kukaribia,"Mungu wangu nisaidie,ama kweli leo ndio mwisho wangu,"Gonard alijisemea kimoyomoyo huku akitetemeka tu asijue nini cha kufanya. "Sukubi mwanangu kijana anayekutesa ni huyu...?"ilisikika sauti kali ikiboboja na maneno yakijirudiarudia."Ndio baba ni huyu..!"sauti ya Sukubi ilijaa kitetemeshi na hasira ndani yake. Kwa wakati huo Gonard alikuwa kabeba kile kitambaa na mafuta aliyopewa na mchungaji.Mara lile jitu liloongea na Sukubi ndilo lilikuwa Inkubi babake,lilijongelea alikokuwa Gonard na nyuma akifuatiwa na yale mengine.Jini Inkubi babake Sukubi alikuwa na maumbile kama ya mwanawe wengine pia vilevile.Jini Inkubi alikaribia zaidi na kuinua kono lake juu,ghafla kulichomoza upanga wa kukata kuwili uliokuwa ukiwaka moto.Jini Inkubi alikimbia kwa kasi ya ajabu kumuelekea Gonard. Gonard alichukuwa kitambaa na kukilowanisha na mafuta aliyokuwa kapewa na mchungaji na kusimama kwa ujasiri kulisubiria jini hilo lililojawa na ghadhabu.Hiyo ndio ilikuwa ngao yake aliyoitegemea na hakuwa na uhakika kama itafanya kazi kweli,lakini alikuwa na Imani kubwa nayo. Yalipojongelea zaidi,Gonard alichukuwa kitambaa kilicholowa mafuta na kwa ujasiri na imani aliyokuwa nayo moyoni mwake alikung'uta kitambaa hicho na kuyarushia majitu hayo...!Amini usiamini mashetani hayo yaliyeyuka katika hewa nyembamba kama donge la barafu liyeyukavyo lipatapo joto. Wakati huo wote Sukubi alikuwa kando akipumua kifua juu juu kwa hasira.
Aliposhuhudia yote hayo yaliyotendeka aliamua kuomba msamaha,"Gonard nihurumie mwenzio,kumbuka niko na mtoto wako."Wakati huo karudisha hasira chini.Mara kilitokea kitoto hicho kikiwa kama mamake vile,kilikuwa kikilia. "Mtoto wangu..! na ushindwe."Gonard alisema maneno hayo kwa hasira na ujasiri wa ajabu na kujikuta amemrushia Sukubi mafuta takatifu. "Maskini Gonard umetumaliza...umetuua..!"Sukubi alitamka maneno hayo huku cheche ya mwisho ya mwili wake na mwanawe ikizimika .Jini Sukubi aliishia hivyo,hakuonekana tena. Gonard aligutuka kutoka kwenye lepe zito la usingizi inapata saa kumi na nusu alfajiri.Alipiga ishara ya msalaba na kujikuta akitamka maneno haya kwa sauti kubwa kuashiria ushindi na ukombozi....KILA MWENYE PUMZI NA AMSIFU BWANA.HALELUYA...zaburi,150:6. 𝐌𝐖𝐈𝐒𝐇𝐎.

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)