𝐒𝐢𝐦𝐮𝐥𝐢𝐳𝐢 𝐭𝐚𝐦𝐮 𝐲𝐚 𝐌𝐚𝐝𝐚𝐦 𝐇𝐑
...𝐇𝐮𝐮 𝐧𝐝𝐢𝐨 𝐦𝐰𝐚𝐧𝐳𝐨 𝐰𝐚 𝐬𝐢𝐦𝐮𝐥𝐢𝐳𝐢 𝐲𝐚 𝐌𝐚𝐝𝐚𝐦 𝐇𝐑...𝐔𝐬𝐢𝐤𝐨𝐬𝐞 𝐤𝐢𝐥𝐚 𝐬𝐞𝐡𝐞𝐦𝐮 𝐡𝐚𝐝𝐢 𝐭𝐚𝐦𝐚𝐭𝐢...𝐮𝐭𝐚𝐢𝐩𝐞𝐧𝐝𝐚

                *****𝐌𝐀𝐃𝐀𝐌 𝐇.𝐑*****
                 ***𝐬𝐞𝐡𝐞𝐦𝐮 𝐲𝐚 1****
𝐌𝐭𝐮𝐧𝐳𝐢:Mike Gonard
𝐖𝐡𝐚𝐭𝐬𝐚𝐩𝐩:+254794012673
𝐅𝐚𝐜𝐞𝐛𝐨𝐨𝐤:Mike Gonard
𝐄-𝐦𝐚𝐢𝐥:𝒎𝒊𝒌𝒆𝒈𝒐𝒏𝒂635@𝒈𝒎𝒂𝒊𝒍.𝒄𝒐𝒎
.....
"Hello,mambo darling?"
Ni sauti ya kike,legevu na ya kuvutia iliyokuwa ikiongea upande wa pili wa simu.
"Poa nambie dear?"
Mike alijibu salamu hizo akiwa kajawa na furaha kweli kweli,ni sauti aliyoizoea,sauti tamu na ya mahaba.
"Niko poa nashukuru,vipi hali yako tangia jana mpenzi,nimekumiss kiroba aisee!"Sauti ya kike iliendelea kuboboja maneno matamu kiana yake.
"Pia mzima,mmh jamani  Madam HR,si ni jana tu tulishinda wote,tukaenjoi siku nzima na tukamalizia siku nzima tukiwa pamoja."
"Woi, Mike hujui vile hunifanyaga mpaka yani nikahisi niko ulimwengu mwengine ndio wasema hivyo,mwenzio natamani tuwe wote kila siku,ni vile hali ya kazi haituruhusu,si wajuwa kazi ya mhindi wewe?"
"Usijali Madam HR"
"Mike sipendi vile unaniita,si nilikwambia usiniite Madam HR."
"Pole basi,hivi nikuite nani labda?"
"Wajua,ni faida tu yenye wataka,"sauti hiyo ilikuwa ya hasira kidogo.
"Sawa beib,"Mike aliongea kiutani kiasi.
"Wow! asante darling uwe na siku njema ,nakupenda sana mpenzi wangu, mmwaaahuh!"
"Nawe pia beib,nakupenda sana pia bye!,mmwaah"

Tu! tu! tu!Simu ilikatwa kutoka upande wa pili baada ya mazungumzo marefu.Yalikuwa mazungumzo baina ya kijana Mike na Boss wake,Madam HR ama Lavinia

....Lavinia ni kati ya wanawake wenye bahati kwenye hii sayari iliyojaa tabu na matatizo tele yasiyokuwa na hesabu sana sana upande wa ajira,aliajiriwa na kampani moja la nguo lililoko Changamwe mtaa mmojawapo jijini Mombasa.Yeye ndio alikuwa meneja ama msimamizi mkuu wa kitengo cha usimamizi wa rasilimali ama Human Resource Management,kwa ufupi yeye ndio alikuwa Rasilimali Watu kwa maana ya HR(Human Resource).

Mbali na kazi,Lavinia ni mwanamke aliyebarikiwa na umbo la kipekee na la kuvutia,kaumbwa kaumbika.Mwanamke anayepata umri wa miaka 35 lakini ilikuwa sio rahisi kutambua hilo labda pesa humsitiri mtu kwa mengi,sawa. 
Lavinia alikuwa na umbo la nane na makalio yaliyo makubwa akianza kutembea utadhani anafanya maksudi vile yalikuwa yakitikisika kwa kupishana,ndio raha ya vijana wa siku hizi,hawataki kuona makalio makubwa yakigongana kwa zamu  na kiwazimu wazimu yakipita mbele yao.Kwako mpenzi msomaji...haiwezekani uupende msambwanda wa Madam Lavinia kuliko Simulizi yenyewe.
 
...Upande wake Mike baada ya kuona kazi yake ya mjengo haimfai tena aliamua kutoka Mishomoroni na kuamua kuenda kutafuta ajira za kampuni.Alikuwa fundi mzuri sana wa vigae vya sakafu kwa maana ya tiles,lakini kuna mambo yaliyomfanya akaachana nayo,sana sana alikuwa anaweza kupata kazi kwa mwezi mmoja na miezi mitatu badae akakosa.Elimu alikuwa nayo ila ajira ndio hakupata,vyeti alikuwa navyo lakini hakuona faida zake kamwe.Kwa wakati huo mgumu alioupitia Mike ndio ulimfanya akaamua liwe liwalo kazi yoyote ile ya kampuni atakayoipata atafanya almradi aweze kupata mkate wa kila siku.

Kabla hata jogoo wa kwanza kutangaza siku mpya,Mike alikuwa kajitayarisha tayari kwa safari ya kuenda kutafuta,akilini mwake akilenga Kingo'rani maeneo ya Changamwe kulikokuwa na kampani ya nguo iliyojulikana kama Hantex EPZ Ltd.Kuvaa kwake kulikuwa kwa kawaida kama mtu aendavyo mahojiano yoyote ya kazi.Mfukoni alikuwa hana hata senti moja yenye itamsaidia angalau upande wa chamcha,kabeba vyeti vyake na simu yake ya mkononi
 
Saa kumi alfajiri alikuwa  tayari katoka,aliingia vichochoroni mdogo mdogo pasipo uoga wowote wa vijana wakorofi wafanyao kazi awamu ya usiku,kupora vya wenzao,kupiga ngeta,tabia mbaya kweli kweli hii.Takriban dakika kumi na tano hivi tayari alikuwa Kisauni,akapita katikati ya vichochoro hivyo mara akajipata Lights kwenye soko kuu la Mji wa Mombasa,tayari watu walikuwa kwenye pilka pilka zao za siku hiyo.Kunao waliosukuma rukwama kupeleka bidhaa na mazao sokoni almradi waingize siku,wengine walibeba mizigo yao kwa vichwa.Mike alinyosha barabara iliyokuwa ikipitia Nyali Bridge moja kwa moja hadi Sabasaba kupitia  Bakstan.

Ilipogonga saa kumi na mbili juu ya alama,Mike alijipata nje ya lango kuu la kampani hilo.Waajiriwa na waajiri walimiminika ndani ya kampani hilo,kunao walioingia kwa miguu,wengine kwa magari.Watafutaji kama Mike walibaki nje ya lango hilo baada ya wakati wa kuingia kwa wafanyikazi kuisha,lango lilifungwa,kilichobaki ni kungojea wakati wa kuchukuliwa kwa wafanyakazi wapya kutoka langoni.Mike alikuwa akifikiria sana kama siku hiyo ilikuwa ya bahati yake au la.

Jinsi alivyokuwa kazama kwenye dimbwi la fikra mnamo saa mbili na nusu hivi lango kuu lilifunguliwa,na mbele yao watafutaji akiwemo Mike kasimama mwanamke mrembo ajabu,lakini akilini mwa Mike hakuuona urembo huo,akili ilijaa kazi na kazi tu!

Mara..."Kijana...yeah..ndio wewe hapo...njoo..,"ilikuwa sauti ya yule mwanamke ikiita,na alikuwa akiashiria Mike ndio aende.Raha iliyoje,aliona kama milango imeanza kufunguka hata kabla ya mwanamke huyo kusema kitu chochote."Mambo..?" kabla Mike hajajibu salamu hiyo kaambiwa nifuate na wao wakaingia ndani na lango likafungwa.Mwanamke huyo alisimama baada ya kutembea hatua chache kutoka langoni.
"Kijana naomba unisubirie hapa kuna kitu nimesahau kidogo,"alimwambia Mike maneno hayo na huyo akarudi langoni.Dakika tano ni nyingi alirudi akiwa kaongozana na wasichana wawili.Wasichana hao pia walikuwa kati ya lile kundi la watafutaji waliokuwa langoni.Walipokaribia alikokuwa Mike,mwanamke huyo alimwambia ajumuike na wenzake na wamfuate.

Walipofika ofisini mwa mwanamke huyo alianza kwa kujitambulisha,,

"Naitwa Madam Lavinia,ninachotaka toka kwenu kuanzia hivi sasa ni ushirikiano wenu katika kazi iliyo mbele yetu,"alipomaliza kuongea maneno hayo alichukua simu iliyokuwa juu ya meza na kupigia mtu fulani.

"Hajji nakuomba ufike ofisini kwangu sasa hivi,"akakata simu hiyo.

Kabla Hajji hajafika, Madam Lavinia aliendelea  na utambulisho,

"Kijana wangu na binti zangu,mimi ndio H.R kwenye kampani hili,ushirikiano wenu utatupeleka mbali pamoja,"alihitimisha maneno yake na punde tu Hajji akadunda ndani ya ofisi.

"Hajji nakuomba uwachukuwe vijana hawa na ukawaonyeshe mazingira ya kufanyia kazi kote kampunini,"Madam Lavinia aliongea hivyo huku akizikusanya stakabadhi za watatu hao na kuzihifadhi kwenye faili.

Hajji alifanya kama alivyoagizwa,kwani pia yeye alikuwa kazini,na kazi yake ilikuwa kuwakaribisha wafanyakazi  wageni na kuwaonyesha majukumu yao.Aliwazungusha  watatu hao kwa takriban nusu saa hivi ndipo akawasimamisha mahali fulani kwenye nguo nyingi zilizohifadhiwa vizuri.

"Sasa kama mlivyosikia mimi ni Hajji,kuanzia leo nyie wote mmechukuliwa kama Wadhibiti Ubora wa nguo Kampuni nzima,majukumu yenu kuanzia sasa ni kudhibiti ubora wa nguo,kwa maana nyenginge nyinyi ndio ma QC yani Quality Controller,nadhani tumeelewana kufikia hapo,"Hajji alimalizia usemi wake.

"Ndio tumeelewana Bwana Hajji,"waliitikia kwa pamoja watatu hao.

Bwana Hajji aliwarudisha watatu hao kwa Madam Lavinia baada ya kutimiza majukumu yake.
"Kila kitu kiko sawa Madam,"Hajji alimwambia Madam Lavinia punde tu walipofika ofisini mwake.
"Pongezi  Hajji kwa kazi yako nzuri,sasa vijana wangu itabidi mrudi nyumbani kujitayarisha kuanza kazi  rasmi hapo kesho,nadhani tumeelewana,"Madam Lavinia aliongea maneno hayo lakini alikuwa akimwangalia sana Mike kwa jicho legevu.

"Tumeelewa Madam,"waljibu kwa pamoja na kuanza kutoka ofisini humo,binti wawili wakitangulia Mike akiwa nyuma yao.Mike ndiye aliyetoka wa mwisho ofisini humo,punde tu alivyogeuka kuukomelea mlango nyuma yake akakutana ana kwa ana na mkonyezo wa jicho la Madam Lavinia kisha na busu la hewani...Madam Lavinia alikuwa kalegeza macho na kushika kifuani mwake na mikono miwili akitikisa  nyonyo zake kumuonyesha kijana Mike.
Kwa wakati huo Mike tayari kazubaa..."Hivi ana nini huyu Madam,ama ni mtego ili niikose nafasi ya kazi tuliyoonyeshwa,"Mike alijisemea moyoni.

"Wewe njoo tuende huku bwana tumekuja wote hatuwezi kutoka pekeyetu",ilikuwa sauti ya binti mmoja kati ya wale wawili waliochukuliwa langoni siku hiyo ndio iliimuita Mike.Alikurupuka toka ulimwengu aliokuwa hajui kafikaje na kuwafuata wenzake.

"Hivi nini kimekuzubaisha pale na tumeambiwa turudi kesho,"waliuliza binti wale.
"Wee bwana acha tu,"Mike alijibu huku akitafakari sana alichokiona kikifanywa na Madam Lavinia.Walitembea aste aste mpaka wakatoka langoni mwa kampani hilo,ilikuwa yapata saa sita na robo hivi.Watafutaji wengi walikuwa bado wako langoni pale wakingojea bahati yao ifike...kila mja na siku yake..ipo siku pia watapata... nawaombea siku njema iwafikie..siku njema kama ya Ken Walibora...itafika tu!....
Watatu hao walitembea barabarani huku wakiwa wamezama kwenye gumzo..

"Samahani dada zangu mimi naitwa Mike,naishi Mishomoroni,sijue wenzangu?"ilibidi Mike aulize.

"Mimi ni Yusra Ahmed,"alijibu binti mmoja kati ya wale wawili,alikuwa na asili ya uswahilini hata kuongea kwake,mtoto mweupe,sura yenye tabasamu ilizidisha urembo wake.

"Mie ni Zahra Shaaban,Yusra ni rafiki yangu tunayependana sana,mtaa wetu ni Mwembetayari karibu na Msikitini pale,"binti huyu aliongea kwa sauti tamu,vile vile alikuwa mrembo kiaina yake,alihitimisha utambulisho mzima.

"Jamani mko na majina mazuri dada zangu,"Mike alisema maneno hayo lakini sana sana alikuwa akimuangalia sana Yusra.

"Asante kaka,mbona pia lako zuri,"walinena binti wale.

"Shukran pia,"Mike alisema kwa ufupi.

Walizama kwenye ulimwengu wa gumzo wasijue ni vipi walifika Sabasaba.Waliachana,mabinti wakaelekea Mwembetayari naye Mike akafululiza na safari yake ya Mishomoroni.Kusema kweli ni mwendo mrefu kutoka Sabasaba mpaka Mishomoroni,Mike alipiga mguu ..saa kumi juu ya alama alikuwa kashadunda mtaani.

Aliingia chumbani mwake,kabla hajapumzika alichukuwa mkate uliokuwa ndani ya kabati na kikombe,alimimina chai aliyokuwa kaihifadhi kwenye chupa ombwe,na kuanza kunywa...njaa ilikuwa imemuweza.Akiendelea kunywa chai yake simu yake ya mkononi iliita...kuangalia hivi alikuwa kahifadhi jina la mpigaji kam..love of my life..kipenzi cha maisha yangu...aliipokea

"Mike mambo...,"sauti ya kike ilisikika ikiongea upande wa pili.

"Niko poa Melvina vipi hali yako,"Mikenalijibu salamu hiyo.

"Pia mzima beib,ila nimekumiss sana mpenzi,ninavyoongea nipo kwenye dala dala naja kwako,nimefika hapa Bamburi Junction,hope nitakukuta Mike,"Melvina aliongea kwa sauti iliyolegea na yenye mahaba ndani yake hali iliyofanya Mike asitishe unywaji wa chai yake.

"Utanikuta beib niko hapa,nikuulize kwani leo huendi kwa mama,"Mike alimuuliza Melvina kwa sababu ilikuwa kawaida yake Melvina kumtembelea mamake aliyekuwa akiishi mtaa wa Nyali,hii ni baada ya Melvina kutoka kazini kwake.

Melvina alikuwa akifanya kazi kama Nesi katika hospitali moja ya kibinafsi kule mjini Mtwapa,vile vile alikuwa akimtembelea mpenzi  Mike wake mara kwa mara.

"Usitoke basi mpenzi pls,"Melvina alisisitiza.
"Sawa beib nakungoja isitoshe kuna jambo nataka nitakwambia ukifika huku,"

"Jambo gani tena hilo Mike?"sauti ya Melvina ilibadilika ghafla kuskia hivyo.
"Wala usijali ni jambo jema tu ata sio baya,"Mike alimtuliza mwenzake.

"mmmh, sawa Mike",Melvina aliguna kisha akashusha pumzi,"kuashiria mihemko ilipungua kidogo.

......Urafiki ama uhusiano baina ya Mike na Melvina ulianza kitambo kidogo,tangia wakiwa shule ya upili mwaka wa 2014 wakiwa kidato cha nne.
Mike alikuwa kidato cha nne katika shule ya upili ya St Georges na Melvina alikuwa kidato cha nne katika shule ya upili ya St Johns almaarufu Vipusa wa mtakatifu Yohana.Shule zote mbili zinapatikana Kaloleni Giriama pwani ya nchi ya  Kenya.

Kuna kongamano la kisayansi ama science congress lililofanyika shule ya upili ya Mariseco iliyoko  mjini Mariakani,hilo ndilo liliwaunganisha wawili hawa.
Mike alikua akiwakilisha shule yake na mradi wa Reverse Osmosis kwenye somo la Biolojia naye Melvina vile vile  alikuwa na Project hiyo hiyo.

Siku hiyo kulikuwa na shule tofauti tofauti zikiwa na miradi tofauti tofauti.Mike aliweza kuwaona pia rafiki zake kutoka shule zengine,wakiwemo Jacob Andau aliyekuwa akiwakilisha shule ya upili ya Ngalla Memorial,Frank Gaunga  akiwakilisha 
Ribe boys na wengine wengi.

Waliwasilisha miradi yao kwa majaji wa kongamano hilo kisha wakaambiwa wasubirie majibu kama mradi gani utachaguliwa kuenda mbele.Zoezi hilo lilichukuwa karibu siku nzima.Ilikuwa yakaribia kufika  saa kumi ndipo Mike alimuona binti mmoja aliyekuwa kakaa pekeyake kwenye baraza ya kidato cha pili cha shule hiyo.

Mike alimnyemelea binti huyo,akaenda kukaa karibu naye.Alikuwa binti mzuri kweli kweli,sare yake ilikuwa imemkaa vizuri,kwa juu kifuani t-shirt yake iliinuliwa juu hiyo yote ni kazi ya Brookside company..aya sawa,mwanafunzi lakini kajazia kiukweli.

"Dada mambo naitwa Mike sijui  mwenzangu?,"Mike alianza kuhoji
.
"Safi vipi,mimi ni Melvina,"alijibu binti huyo kwa sauti nyororo.

"Wow! Uko na jina zuri kama wewe mwenyewe vile,Melvina.. smooth brow!...gentle lady!....chieftain!...zuri sana aisee!" Mike alimimina sifa kwake Melvina..

"Mmmh uko na vituko wewe,asante!"Melvina aliguna kidogo.

"Samahani dadangu kuna jambo nataka kukwambia,iwapo litakuudhi utaniwia radhi,"Mike alivaa ujasiri na kuamua kusema yaliyokuwa moyoni mwake.

"Sema tu wala usitie baridi,"Melvina aliongea akiashiria kuwa na hamu ya kutaka kujua.jambo hilo.
Waliongea mengi hatimaye Mike akampa Melvina nambari ya simu.

"Wakati wowoti ukiipata simu utanitafuta,"Mike alihitimisha mazungumzo hayo huku Melvina akiagana na Mike kuelekea kwenye basi lao la shule tayari kurudi shuleni mwao.

"Nitakutafuta Mike tukienda kwa mapumziko mafupi ya muhula huu,"Melvina aliongea maneno hayo kuashiria alikuwa amekubali ombi la kuwa na Mike.Alitikomea na kupanda kwenye basi lao naye Mike vile vile.Wakarudi shuleni mwao.Hivyo ndivyo urafiki wa Melvina na Mike ulianza.....

......Mike alikuwa kapitiwa na usingizi kidogo ilikuwa yapata saa moja na nusu jioni ndipo alisikia kwa mbali mlango ukigongwa


Mike alikurupuka na kujifurukuta na kuenda kuufungua mlango,kuufungua tu mlango alikutana na sura ya kike aliyoizoea,sura ya kupendeza..

"Wow kumbe ni wewe Melvina,karibu ndani beib,"Mike alisema maneno hayo huku akiwa nyuma ya Melvina.Alizungusha mikono yake kiunoni mwa Melvina kichwa chake kikiwa begani karibu na sikio la kushoto la Melvina.
Walishikana hivyo kuelekea kwenye sofa na kukaa huko.

"Beib ulivyokata simu nilipitiwa na usingizi  ata nilikuwa nikiota mapema kabisa,"Mike alianzisha gumzo.

"Pole mpenzi ndio maana nimegonga mlango karibia mara tatu hukushtuka,nikadhani uko na binti humu ndani,"Melvina aliongea maneno hayo kwa sauti legevu.

"Woii  hapa ndani hakuingii binti mwengine isipokuwa wewe Melvina...Melvina Mike tu!,Ama umesahau ninachokwambia kila siku?".Mike akamkumbusha maneno haya...

                              '𝐌𝐢 𝐰𝐚𝐤𝐨 𝐣𝐞𝐧𝐞𝐫𝐚𝐥𝐢,
                              '𝐖𝐞 𝐥𝐮𝐭𝐞𝐧𝐢-𝐤𝐚𝐧𝐚𝐥𝐢,          ©️ᵐⁱᵏᵉᵍᵒⁿᵃʳᵈˢᵃᵘᵗⁱᶜʰᵃⁿᵍᵃ
                               𝐖𝐞𝐧𝐠𝐢𝐧𝐞 𝐚𝐭𝐢𝐟𝐚𝐥𝐢,
                         
"Wow ndio maana nakupenda Mike,na nakuahidi kitu kimoja,"Melvina akaangusha ahadi kiaina yake....
                              
                               𝐓𝐚𝐤𝐮𝐩𝐚 𝐩𝐞𝐧𝐳𝐢 𝐤𝐚𝐥𝐢,
                               𝐊𝐮𝐬𝐡𝐢𝐧𝐝𝐚 𝐤𝐞𝐦𝐢𝐤𝐚𝐥𝐢,       ©️ᵐⁱᵏᵉᵍᵒⁿᵃʳᵈˢᵃᵘᵗⁱᶜʰᵃⁿᵍᵃ
                               𝐓𝐚𝐦𝐮 𝐤𝐚𝐦𝐚 𝐚𝐬𝐚𝐥𝐢,
                               
                              
"Hongera sana mpenzi wangu,halafu umekuwa malenga siku hizi,umetema uswahili beib,"Mike alikuwa kachangamka ajabu kwa uwepo wa Melvina.

"Hahaaa! beib haya yote kanifunza wewe,alafu mbona iwe sauti changa na tayari iko na uwezo mkubwa wa utunzi?"Melvina alihoji kidogo.

"Mmh beib kusema kweli zipo sauti zilizonguruma kwenye tasnia au ulingo wa ushairi kwa vipindi vinne,kwenye kipindi cha urasmi mkongwe,kipindi cha utasa,kipindi cha urasmi mpya na kipindi cha sasa...zipo sauti zingurumazo katika kipindi cha sasa,sauti nzito zilizobobea,mimi ni sauti changa tu ya kipindi cha sasa...acha nibaki kuwa sauti changa hadi kipindi cha sasa kitakapo tolewa na kipindi chengine kijacho,"Mike alihitimisha falsafa zake zilizokuwa hazihusiani na ujio wa Melvina.

"Haipaswi kujidharau hivyo Mike,wewe unaweza na ipo siku..."Melvina alimpa moyo mpenzi wake.

"Asante Melvina,yote tisa kumi...,
              
      
                           𝐓𝐮𝐦𝐮𝐨𝐦𝐛𝐞 𝐉𝐚𝐥𝐚𝐥𝐢,
                           𝐏𝐞𝐧𝐝𝐨 𝐥𝐞𝐭𝐮 𝐭𝐚𝐰𝐢𝐥𝐢,              ©️ᵐⁱᵏᵉᵍᵒⁿᵃʳᵈˢᵃᵘᵗⁱᶜʰᵃⁿᵍᵃ
                           '𝐒𝐢𝐰𝐞 𝐧𝐚 𝐟𝐚𝐢𝐧𝐚𝐥𝐢,

"I love you Mike,tangia siku ya kwanza kukutana na wewe Mariseco sikutarajia kabisa tutafika mbali kiasi hiki,"Melvina aliongea maneno hayo huku kashika kichwa cha Mike kwa mikono yake miwili na kusogeza lips zake na kuzigusanisha na za Mike...kimya kikatawala chumbani humo kwa takribani robo saa...denda ndio aliongea...walikulana denda...mwaaah!..mwaaah!...mwaaah!..mmmmwaaaaahuh!..

"mmmhh "Melvina aliguna na kujitoa kwenye lips za Mike,"Mike naomba tule kwanza pls,kuna chakula kidogo nimebeba kwenye ule mfuko,"Melvina aliashiria kwa kidole ulipokuwa mfuko wenyewe.Mfuko ulikuwa umeangushwa mlangoni nusu saa iliyopita Melvina alipoingia ndani mle,hakuna aliyejali...yanaitwa mapenzi...ndio ni mapenzi.Mike aliuchukuwa mfuko huo na kutoa kila kitu kilichokuwa ndani na kukiweka juu ya meza,Melvina alikuwa kabeba pilau,kuku choma na chips kidogo.Wakati huo wote Melvina alikuwa kakaa kwa sofa akimtumbulia Mike macho yake yaliyokuwa yamelegea na kukoleza wekundu,kaachiwa kutabasamu tu.

Mara Melvina alinyanyuka na kuenda mahali kulikokuwa na beseni la kuogea na kulijaza maji,alichukuwa kibegi chake na kutoa kanga..Wakati huo Mike naye alikuwa akiangalia tu..kisha...

"Mike funga macho,"Melvina aliongea huku akichekacheka..."Beib funga macho plss nataka kutoa nguo.
"Mmh beib hamna haja nifunge macho ingia kwa hilo pazia la kitanda utoe hizo nguo,"Mike alimwambia.Dakika mbili  ni nyingi Melvina alitoka nyuma ya pazia hilo kajifunga kanga...

"Mike tuoge kwanza halafu tule,"Melvina alimkaribia Mike na kumshika mkono.
"Sawa beib,"Mike alikubali na kuenda kutoa nguo na kujifunga taulo.
Melvina alilibeba beseni la maji na kuingia nalo bafuni Mike akiwa nyuma yake.Waliufunga mlango wa bafu hilo kisha wakaanza kamchezo ka kurushiana maji ndani mle utadhani watoto wadogo vile na kila mmoja mtu mzima na kamsitu kake ka Amazon  kule Amerika...ndiyo kamsitu ka Amazon...miti imeota huko.

Muda mfupi tu wa rusha nikurushie  maji,kanga na taulo zililowa,Melvina ndani ya kanga iliyolowa maji,kanga na utovu wa nidhamu ikaamua kugandamana  na  mwili mwake.Kwa nyuma Everest yote ilionekana wazi vile ilipanda na kuteremka,Melvina alikuwa kajazia kwa nyuma,kifuani ndio usiseme,Brookside kampani lile,kajaziajazia
kifuani binti huyo..kwa chini karibu na kitovu..kidogo kanga ituonyeshe jungu kuu...jungu la asali...

Wakiwa wamelowa,walikatisha zoezi hilo na kuzubaa,waliangaliana kwa macho,mara Melvina akaitoa kanga iliyolowa maji na kuiweka kwenye kamba iliyokuwa bafuni mle,Melvina alisimama mbele ya Mike kama alivyozaliwa.

Macho yote ya Mike kwenye kitumbua cha Melvina kilichonona,kilikuwa kimefura kama kimezidi hamira vile,kaanza kudondokwa na mate ya hamu ya kukionja kitumbua hicho alichokila miezi mitatu iliyopita...kilikuwa kama hajawahi kukiona vile,msitu wa Amazon ulikuwa umefyekwa kama wiki moja hivi..miti ilianza kuota tena...Amazon iliweza kupendeza zaidi kwa miti mipya iliyoanza kuchipuka...

Melvina aliinama mbele ya Mike na kumtoa taulo iliyolowa pia,dudu lilikuwa limeanza kusisimka...alilishika kwa mkono wake laini...

"Waaaah beib...nimelimiss hili limaikrofoni langu kiukweli,sijaimba nalo miezi mitatu sasa,"Melvina alichangamka ajabu!...

ITAENDELEA...