NGOJA NILEWE 1

Emmanuel Lee
By -
0

NGOJA NILEWE KIDOGO


EPISODE 1 


MTUNZI: Mbogo Edgar


WHATSAPP 0743632247


Ilikuwa ni saa sita za usiku, mjini songea, mwaka 1999, mtaa wa mjimwema, giza nene lilikuwa limetanda, baridi kali ilikuwa inapuliza, mitaa ya mji wa songea ilikuwa kimya, ungebahatika kusikia sauti ya mtu, basi ni mikoromo ya usingizi, zaidi ya hapo ni sauti ya ndege wa usiku yani bundi, au mipaka na mijibwa iliyokuwa ina lia kwa sauti kuu, ungesema nibinadamu, huu ndio wakati binadamu ambao atujuwi vilio vile vina tokana na nini kwa wanyama hao, uwa tunasema uchuro, ndio mida ambayo ungesikia mtu anamtukana mbwa au paka, akidai usiniletee uchuro, ila kwakuwa sina taluma nalo, siwezi kulisemea sana.


 Naaam katikati ya usiku huu, wenye baridi la kusuruisha ndoa, usiku ambao kila mmoja uwa anawai nyumbani, na wale ambao wapo wapweke, yani single, yani awaja oa, au kuolewa, uwa wana jaza nyumba za wageni, au kujifungua magetoni mwao na wapenzi wao, na ndio muda ambao mimba nyingi za waschana wakazi kwa watoto wa maboss wao wenye nyumba upatikana, japo kuna watu, ambao ujiita miamba, wao umalizia baridi kwa pombe kali.


lakini leotuna mwona kijana mmoja mwenye umri wa miaka ishilini na tano, akiwa amekaa nje, pembezoni mwa kiambaza cha nyumba moja kubwa sana, iliyo kaa kwa mtindo wa shule, au behewa la treni, kwamaana ilikuwa imelala kama namba moja, huku ikionekana kuwa na milango mingi mingi pamoja na dirisha moja kila mlango, anaoneka kijana mmoja akiwa amekaa, huku amejikunyata kwa baridi iliyokuwa inampuliza, kama friji la bar, "kwanini nimestahili aya yote, kosa langu ni lipi?" alijiuliza kwa sauti ya chini, kijana yule, ambae akuwa na ata kipande cha sueta mwilini mwake, zaidi alikuwa amevaa tishert jepesi na kaptura ya kaki, huku sauti yake, ikionyesha wazi kuwa anamachungu makubwa sana moyoni mwake.


 Hapakuwa na magari, wala dalili ya watu waliokuwa wanatembea katika mtaa ya mji huu, ambao ulikuwa na nyumba zilizo jitenge tenga, kutokana upya wake, maana ukitoka nyumba ile kubwa, ambayo kijana wetu alikuwa amekaa nje, huku vyumba, taa za ndani zikiwa zime zimwa, karibu kila chumba, cha nyumba hii ya kupangisha, pembeni kulikuwa na msitu wa shamba la maindi makavu, la nusu hekari kila upande, yani kulia na kushoto, mbele ikikatiza barabara kubwa ya vumbi, na mita kama mia moja upane wa hamsini upande wa kulia, kulikuwa na nyumba nyingine, ambayo hii ilikuwa nani ya uzio mkubwa sana, wa ukuta tofari, ambao pia ulizungukwa na shamba kubwa la maindi ambayo yalikuwa yanasiburi kuvunwa, upande wa kushoto, mita kama hizo hizo, kulikuwa na banda moja kubwa la kuifadhia mbao za biashara, lililopakana na safu ya vyumba vinne vya biashala maarufu kama flemu, sehemu iliyofahamika kwa jina la kwa mama Eva, japo kati yake, ni vyumba viwili tu ndio vilikuwa vina tumika, kwamaana ya kwamba, kimoja kilikuwa duka la kawaida, huku moja ikiwa ni duka la vinywaji, kwamaana ya grocer.


 Licha ya uchovu wa kutembea kutwa nzima mjini, akiangaika kwenye maofisi ya watu, akisaka kazi, bila mafanikio, lakini akuweza kusinzia ata kidogo pale nje, ni kutokana na baridi kali, iliyokuwa ina nyanyapaa, [apamoja na njaa iliyokuwa inamchonyota, maana toka alipokunywa chai na viazi vitamu asubuhi, akuwai kuweka chochote mdomoni mpaka mida hii, sababu, fedha alikuwa amemaliza leo asubuhi kununulia sukari.


 Mwonekano wa kijana huyu, mgeni toka dar es salaam ungejuwa kuwa, hakuwa hapa nje kwa hiyari yake, ila ilimlazimu kuwa nje ya nyumba mida hii bila kujari baridi iliyokuwa ina puliza usiku huu, na sidhani kama alifuzwa kwao, "jamani mpenzi, hivi lini tutaanza kuishi pamoja" ilisikika sauti ya kike, toka ndani, ikipitia kwenye dirisha la karibu, lililokuwa karibu kabisa na pale alipokuawa amekaa, sauti ambayo aikuwa na dalili ya usingizi ata kidogo, "usijari mpenzi, subiri kwanza Seba, apate sehemu ya kuishi, ni kama week moja tu atakuwa amesha ondoka" ilisikika sauti ya kiume toka kwenye dirisha ilo ilo, ambalo lilikuwa limezimwa taa.


 Hapo kijana wetu, ambae bila shaka alikuwa anazungumziwa yeye, ana tikisa kichwa, kwa masikitiko, maana kiukweli hiyo ilikuwa ni taarifa kwake, kwamba akatafute sehemu nyingine ya kuishi akuwa na uwezo wa kutafuta chumba haraka hivyo, na akizingatia ni kwamba, siyo tu kutokuwa na fedha ambayo aliimaliza kwaajili ya kula yeye na mwenyeji wake, aliekuwa ndani na mpenzi wake wakike, pia kijana huyu, akuwa na kazi, na alisha zunguka mitaani na vyeti yake kutafuta kazi, akakosa kabisa, sasa kama angekuwa na uwezo wa kuondoka katika nyumba hii, angekubari vipi kuishi kwa tabu kama hii, kukaa nje akisubiri, mwenyeji wake, amalize aja zake na zampenzi wake, kisha ndio na yeye aingie akalale, kwenye kitanda ambacho kimetoka kutumika kwa watu kupeana dudu, “George saa hizi muda umeenda unasikia mambwa yameanza kulia, mi nataka niende nyumbani, alafu mwenzio yupo ponje” ilisikika sauti ya kike, toka mle ndani ya chumba.


 Hapo kidogo kijana wetu, akaanza kupata tabasamu laini, lililoashiria matumaini ya kwamba sasa anaigia ndani kupata chochote na pengine kujipumzusha, kuisubiri kesho, aone nayo itakuja vipi, kwamba itakuja bahati njema au bahati mbaya, “wala usiwe na wasi wasi, ngoja tumalize cha mwisho nita kusindikiza mpaka kwenu” ilisikika sauti ya mwanaume alie itwa George, safari hii ikiwa ya chini, hapo kijana wetu hapa nje, ambae ilionyesha wazi kuwa, toka arudi kwenye miangaiko yake, akuingia ndani, maana alikuwa na bahasha ya kaki yenye vyeti na vielelezo vya taluma aliyo iombea kazi, akaomba kimoyo moyo kwamba mwanamke huyu akatae, ili watoke na yeye aingie.


 Lakini aikuwa hivyo, ndio kwanza akasikia kicheko laini, “jamani George uchoki, aya basi tufanye haraka, sauti yakike ilikuwa ya kunong’ona, ikifwatia na milio ya kiyanda, iliyoashilia, wawii hao walikuwa wanajiweka sawa, kwaajili ya kuanza mchezo, akuna alie mjari huyu aliekuwa nje, awakujari heshima yake, awakujari njaa wala uchovu wake, zaidi ni kwamba, ulitanda ukimya, ambao ulifwatiwa na na kelele za kitanda kwichi kwichi kwich, na baada ya mchezo kuendelea kwa sekunde kadhaa, ikaanza kusikika “mmmmh!! Mmmmh!! Asssh,!!” ungesema kuna mtu alikuwa anakula muwa huko ndani.


 Japo alikuwa katika machungu makubwa sana, lakini hii aikuzuwia kumfanya kijana wetu, asimamishe mnazi, siyo tu kwaajili ya baridi, ila pia kijana huyu, alikuwa na muda wa kama mwaka na miezi mitatu, aja gusa utamu wa kitumbua, muda mfupi wa kitendo kilichokuwa kinaendelea ndani, tayari eneo lote la nguo ya ndani ya kijana huyu, ilikuwa imesha lowa kwa matamanio, mwenyewe akajikuta anasimama na kuanza kutembea taratibu, kuelekea upande wa barabarani, na kabla aja ifkia barabara ambayo ilikuwa mita kama ishiliini toka pale kwenye nyumba, akaona mwanga wa gari, lililokuwa lina kuja upande ule aliokuwepo yeye, akasimama na kutulia kidogo, ili gari lipite kwanza asije akana mtu wa ajabu lutembea tembea usiku kama ule, wenye baridi kali, pasipo kuwa na nguo nzito ya kuzuwia baridi.


 Sekunde chache baadae, lilionekana gari aina ya Nissan patrol lililokuwa lina kuja kwa mwendo wa taratibu, na kupita usawa ule, mpaka lilipoenda kusimama mbele ya geti la jumba lile kubwa, lililopo karibu na nyumba ile ambayo kijana wetu alifikia, dereva wa gari ili anapiga honi mbili mfululizo, kisha anatulia, dakika mbili baadae, geti lina funguliwa, na gari linaingia ndani, inamkumbusha jambo kijana wetu, ambae leo asubuhi, ilikuwa ni mala ya pili, anamwona dereva wa gari lile, ambae siyo tu mwake mwenye mwonekano wa kuwa na uwezo, wa kifedha na kimaisha, pia alikuwa ni mzuri na wenye kujipenda, kimavazi na kiurembo, ni wazi mwanamke yule alikuwa amemzidi kati ya mwaka mmoja au miwili, japo akuna uhakika, siku za nyuma angekuwa ameshapata ata ujasiri wa kumsalimia, lakini kwa sasa, asingepata ujasiri wa ata kumtazama kwa sekunde kumi, maana angeisiwa mwizi, kutokana na mwonekano wake wakipindi, lakini sura ya mwana mke huyu mzuri wa sura na umbo la kiafrika, aikuwa ngeni machoni pake, lakini angeanzaje kumwuliza alimwona wapi, ata hivyo alichukulia ni wenge lake tu, maana hapa songea mjini akuwa mwenyeji kabisa.


 Kijana wetu anamwona mwanamke mmoja, ambae bila shaka ni dada wakazi anafunga geti, na kupotelea ndani ya uzio ule mkubwa wa jumba la kifahari, Ukweli machungu ya kijana huyu, yana mambo mengi sana, kazi mfamilia aliyo poteza, yani mwanamke alie mpenda kuliko wanawake wote aliowai kutembea nao, mwanamke alie mpa ufalme wake wote, na baadae kuja kusaliti, na kuwa na mwanaume mwingine ambae kiukweli, kila kijana huyu anapokumbuka, anatamani kulia kwa sauti, lakini anakumbuka kuwa aito saidia, maana toka alipoanza kulia, aikumpunguia machungu ata kidogo, zaidi ilizidi kumuumiza, yani licha ya kumsaidia na kumpatia kazi, mwisho siyo tu kumfukuzisha kazi, ila pia kumwibia mke, na pia kumfanya sindwe kumlea mtoto wake wake mpendwa na wapekee, na kumpatia huduma zamsingi kama baba, ni vyema kama tukitumia muda huu, wakati kijana wetu anasubiri George ale bumunda, kukusimulia kilicho mtokea kijana wetu.*********

 

 Huyu anaitwa Sebastian samweli, ni kijana alie kulia kijijini Namabengo, akiwa anaishi na mama yake tu, kwakifupi nikwamba akuwai kumfahamu baba yake, ata mama yake akuwai kumweleza baba yake ni nani, ilo alituhusu, chamsingi ni kwamba mama Seba alihakikisha anamlea mwanae kwanguvu zake, pasipo kujari masimango toka kwa dada yake, ambae alikuwa anaishi na mume wake waliojaliwa kupata watoto watatu, mmoja wa kume alie mzidi Seba miaka miwili, na wakike wadogo, kwa seba, yani mkubwa alizidiwa miaka sita na Seba, na mwingine alikuwa amezidiwa miaka mitatu na dada yake.


 Seba akumwangusha mama yake, na akalipa thamani jasho la mama huyu, mwenye haki, kwa kufauru mtihani wa darasa la saba, na kujiunga na shule ya sekondari ya wavurana ya bweni ya songea, maarufu kama box 2, kumbuka kuwa miaka tisini mpaka 2000 mwanzoni, ufuru wa darasa la saba, ulikuwa mgumu sana, tena ufauru wa hali ya juu, wakati huo binamu yake George, alie mtangulia Seba madara mawili, akiwa ameandikishwa katika shule ya sekondari ya kutwa ya Namabego, iliyomilikiwa na jumuhiya ya wazazi, Elimu ambayo iliishia kidato cha nne, kwa kuondoka na alama sifuri nukta sifuri.


 Miaka miwili baadae Sebastian, ambae alikuwa katika hali ya kujipenda na kujitanashatisha, anamaliza kidato cha nne, nakufauru kwa alama ya division 2 ambayo inamfanya aendelee kusoma pale pale songea wavulana, upande wa bweni, hii inaleta mzozo mkubwa sana, katikati familia mbili hizi, yani familia ya mama Sebastia, na ile ya mama yake mkubwa Sebastian, yani mama George, ambae mume wake alikuwa ni mwalimu wa shule ya msingi Namabengo, ni kama iliwachukiza sana baba na mama George, siyo kwamba walichukia kwamba mtoto wao ameanguka mitihani, hapana, ila walichukia sababu Sebastian alifauru mitihani yake.


 Licha ya kwamba, Sebastian aliendelea na masomo yake katika wakati mgumu, lakini mama yake alikuwa na wakati mgumu zaidi huko kijijini, maana akutakiwa kukosa kitu chochote cha matumizi yake binafsi, iwe chakula, chumvi au dawa za dharula, maana kila alipoenda kwa dada yake kuomba kitu chochote, angeambiwa kuwa “siunajifanya ela yako unajuwa kusomeshea, subiri mwanao apate kazi akununulie chumvi” ilimuuma sana mama Sebastian, ambae mwisho wa siku, aliamua kukomaa yeye kama yeye, huku akisaidiana na majirani wengine.


 Naam mwaka 1997 ndio mwaka ambao Sebastian alimaliza elimu yake ya kidato cha sita, na kupata kazi kwenye kampuni ya FSC, ni kampuni binafsi ya kutengeneza na kuuza kandambili aina ya Faru, yani Faru Sanders company, kilichopo mji mwema kigamboni, ilikuwa bahati yake kijana wetu, maana siyo tu kuanza kazi dar es salaam kama ndito za watu wengi zilivyokuwa kipindi hicho, pia alianza na mshahara mkubwa wa elfu hamsini, na pia alipangiwa nyumba nizima, maeneo ya karibu na kivukoni, mtaa ambao watu wengi walikuwa wampanga, kiasi kwamba wenyeji walikuwa wachache sana.


 Miezi miwili baada ya kuanza kazi, kutokana na malupu lupu aliyo kuwa anayapata kijana wetu, licha ya kununua kila kilicho itajika ndani ya nyumba yake, pia aliamua kumjengea mama yake nyumba, huko kijijini namabengo, ikiwa pamoja na kumsaidia kukodi watu katika swala zima la kilimo, akuishia hapo Sebastian ambae siku zile alikuwa amegundua kuwa wine na bia zina utamu wake, aliwasaidia ndugu zake wengine, asa watoto wa mama mkubwa, ni wale wadogo wakike, ambao sasa walikuwa wanasoma sekindari, mmoja kidato cha nne, mmoja kidato cha kwanza, ambao mala kwa mala walikuwa wanaandika barua kuomba fedha kwa binamu yao huyu, nae akuwanyima, kama wazazi wao walivyo fanya kwa mama yake


kuna wakati ata Geroge, ambaea aliandika barua kwa Sebastiaan akiomba msaada wa kiasi flani cha fedha kwaajili ya kwenda mjini kuanza maisha mapya, nae alitumia mala mbilli yake, na ndiyo fedha ambayo Geroge alipangia hiki chumba ambacho anaishi mpaka sasa, na kununua vitu ambacvyo vipo ndani ya chumba hicho.********


 Naam! Licha kumhudumia mama yake na kumfanya ajione kama malikia na kujivunia uzazi wake, kijana wetu pia alikuwa na ratiba zake zenye kufurahisha kama siyo kuchekesha, ratiba ambayo ilianzia siku ya jumatatu, ambapo ange amka mapema na kujiandaa, kisha ange tembea umbali wa mita kama mia nne hivi, mpaka kivukoni, kisha angepanda dara dara, na za mji mwema, ambako kuna kiwanda, nae angekaa ofisini kwake, ikiwa ni ofisi ya makusanyo ya fedha za mauzo, kabla ajapeleka kwa mhasibu wa kiwa masoko, ambae angepeleka kwa mhasimu mkuu wa kampuni, nae angefanya mahesabu yake kabla ya kuwapa motisha kidogo, kutokana na fedha za ujanja ujanja zilimpa jeuri bwana Sebastian, ambae siku ya ijumaa, uenda buchani na kununua kilo tano za nyama ya ng’ombe au kuku wawili, na ndizi chana kadhaa, na box moja la wine, au sanduku (kreti) la bia na kujifungia ndani mwake, akichoma nyama na ndizi huku akinywa pombe, na kutazama filam au music kwenye TV, nasiyo kwenda bichi kuogelea kama alivyokuwa anafanyaga mwanzo.


 Tabia hii ili msaidia sana kukwepa vishawishi vya watoto wa kike, ambao wengi wao walikuwa ni wanafunzi wa vyuo mbali mbali, walikuwepo wanafunzi wa CBE, IFM vilivyopo maeneo ya posta, na wale wa Chuo cha mwalimu pale pale kigamboni, zaidi ya starehe yake ile ya pombe na nyama choma na music, akuwa na starehe nyingine, siyo kwamba akutamani wanawake.

Hapana, ukweli ni kwamba kijana wetu alisha ingia kwenye vishawishi mala kadhaa, asa ukichukulia kwamba, mtaa huu aliokuwa anaishi, ulikuwa unawapangaji wengi ambao ni wanafunzi wavyuo, ambao ungesema walijichagua kutokana na uzuri wa sura zao, na mbaya zaidi, ungesema kuwa walikuwa wanashindana kwa mavazi, na kujipodoa.


Ata hivyo bwana Sebastian, siyo kwamba alitamani kila mwanamke, au mschana alie mwona hapa mtaani, ila macho yake yalituwa kwa maschana mmoja ambae siyo tu kushindwakumsogelea kutokana na uzuri na mwonekano wa mwanamke huyo, ambae kama usingehisi ni nyumba ndogo ya waziri au kiongozi flani, kama siyo tajiri mubwa, basi ungeuhisi anatoka kenye moja ya familia za watu kama hao, maana ukiachilia uzuri wa sura wa mschana huyo mwenye mkadirio wa miaka ishilini na tatu hivi, pia alijaliwa umbo moja matata sana, umbo la kusahaulisha kudai chenji dukani, mwanamke siyo tu alivutia kutkana na mwonekano wake wakuvutia, ila pia alivutia lutokana na upole wake, kiasi kwamba, ilimuwia vigumu Sebastian ata kumsogelea na kumweleza lolote, japo siku moja moja, alipokutana nae alimsalimia kwa heshima kubwa.*********


 Naaaam!!! Ijumaa moja ya mwisho wa mwezi wa saba, mida ya saa kumi na mbili za jioni, Sebastian akiwa anatoka kazini, amesha pitia kwenye manunuzi yake, na kununua nyama, ndizi, na katoni lake la wine lenye chupa sita, alipofika mtaani kwao akakuta mtaa ukiwa umechangamka sana, wale vijana wenzie ambao vijana wanafunzi, wakike kwa wakiume, ambao wengi wao walikuwa na umri sawa na Sebastian mwenyewe, walio valia nguo zenye kushawi, kwa wale wakike, walionekana nje ya nyumba zao walizopanga, wakiwa wamekaa kihasara hasara, usingeuliza kuwa ni wapenzi, au ni watu wenye makubariano ya kingono, wakiongea na kucheka kwa furaha, wengine wakinywa pombe, au kutumia urahibu wa aina flani flani, huku wengine sauti za redio zao zikiwa juu kabisa, na music ulio sikika ni kutoka kwa wamamusic maarufu wa ulaya na marekani, kama vile SPICE GIRLS, SWV, Boys two Man, KC and jojo, destiny’s Child, na wanamusic wengine wengi, ilionyesha wazi kuwa awanafunzi awa walikuwa na furaha iliyopitiliza.


 Japo wanafunzi awa walikuwa katika mavazi ya kutamanisha, kiasi cha kutamani ange mpata mmoja wa kumsindikiza usiku ule, lakini Sebastian akuwa na uwezo wa kumwita ata mmoja na kumpatia lile pendekezo lake, hivyo akaachana nawazo ilo, ambalo akutaka ata kujaribu, siyo kwamba akuwa na fedha au mwonekano mzuri, ila ni uoga wa kutamka ndio ulio mfunga mdomo.


 Sebastian aliingia ndani mwake na kuweka kila alicho kujanacho, sehemu iliyo usika, na kisha akabadiri nguo akivalia kaptura ya jinsi, na tishert, iliaanze kufanya yake, lakini anagundua kuwa mkaa iliuwa umeisga, hivyo ana chukuwa noti ya tashilingi mia mbili, na kuelelekea kwenye magenge ya jilani, ni kama mita hamsini toka pale kwake, ambapo ananunua mkaa na kuanza kutembea kurudi nyumbani, mala anasikia sauti ya kike toka nyuma yake, “habari kaka”, hapo Sebastian akageuka mala moja kutazama nyuma, ilikotokea sauti ile.


 Siyo kwamba Sebastian, aligeuka kwakujuwa alikuwa anasalimiwa yeye, ila aligeuka kumtazama mwanamke anaemiliki ile sauti nzuri yenye kutibu ugonjwa wa moyo, lakini ile kijana wetu anageuka tu, macho yake yakatua kwenye uso wa mwanadada mrembo wa rangi ya chungwa, umbo lenye upana wa wastani kifua kilichobeba matiti mazuri yaliyosimama vyema na kuonyesha alama ya mchongoko wa chuchu, kwenye shati jepesi alilokuwa amevaa, huko chini usiseme, japo alivalia skirt ndefu na pana, lakini akuweza kufisha hips na makalio makubwa aliyo jaliwa, mwana dada huyu, ambae alikuwa anamtazama kwa macho ya liyo jaa tabasamu, lilizo sababisha vijisima mashavuni mwake, nakufanya uzuri wake wa hasiri uongezeke mala mbili, ni yule ambae Sebastian anamtamani kila siku zote.


 Japo Sebastian alihisi kuwa aliesalimiwa ni yeye, lakini bado alikuwa na kigugumizi kuitikia, akabakia anamtazama dada wa watu, kwa macho ya yenye kujiuliza, huku wote wakiendelea kupiga hatua, kuelekea upande mmoja, “naona unaenda kujipikia” alisema yule mwanamke, kwa sauti ile ile tamu, yenye kusisimua, ambae alionekana kuwa, alikuwa amechoka kidogo, kutokana na matembezi aliyokuwa ametoka kuyafanya.


Safari hii Seba alifunga mdomo wake, “kupika chezo dada yangu, ninaenda kuchoma nyama na ndizi tu” alisema Sebastian, ambae bado akuwa anaamini kama kweli huyu dada, leo kamsemesha, “uchoyo huo, siunikaribishe tuchome wote, au wifi yangu atakufumania” alisema yule dada kwa sauti iliyo jaa utani, “wifi yako atoke wapi dada yangu, ndio kwanza naamza maisha, we karibia tu kama auto jari” Sebastian alijikuta amesha jibu, na wakati huo, walikuwa wamesha karibia kwenye nyumba kubwa, aliyokuwa amepangishiwa Sebastian na FSC, “mhhh! Karibu hiyo yaukweli ukweli, weshauri yako, mi nakuja, ngoja nika oge kwanza” alisema yule mwanamke ambae Sebastian, alimtambua kuwa ni mwanafunzi, japo akujuwa alikuwa anasoma chuo gani, wala kujuwa alikuwa anachukuwa kozi gani, “wala usijari we karibu tu” alisema Sebastian, ambae licha ya yule mwanamke kusema mwenyewe atakuja lakini yeye aliona kuwa ni utani, na kwamba singekuja, “sawa maana najuwa leo watu watakuwa na ujinga mwingi sana, sito weza kukaa nika ushuhudia” alisema yule mwanamke mrembo, na kila mmoja akaelekea upande wake.********


Naam!! dakika kuishilini baadae, tayari Sebastian, alie ambae akuwa anaamini kama, ni kweli mschana yule atakuja pale nyumbani kwake, alikuwa amesha washajiko, na kuweka nyama na ndizi juu yake, na kuliweka jiko ameliweka sebuleni, hiyo ni kawaida yake, anapoamua kunywa mvinyo au bia, kisha akakaa na chini kabisa, yani sakafu, kama vile yupo kwenye mkeka, wine kwenye grass, na chupa moja pembeni, “akija ndio nitaenda kumnunulia soda” alijisemea Sebastian, huku macho yake ameyaelekeza kwenye TV, ambayo ilikuwa inaonyesha filamu nzuri ya #BIBI_HARUSI_MTARAJIWA.


Dakika zilisogea, sauti kubwa na kelele za watu, zilisikika toka nje, zilikuwa ni za wale wanafunzi wa chuo, aikujulikana wanashangilia nini, Sebastian aliendelea kuchoma nyama huku anakuywa wine yake taratibu, mala zote akiwa ametega sikio, kusikiliza hodi au vishindo vinavyo sogelea mlango, lakini hapa kuwa na chochote kati ya hivyo kilicho sikika, ata vilipo sikika vishindo, Sebastian alichechetwa kwa mshawasha, lakini baadae vishindo hivyo kutokweka hewani, Sebastian anatazama saa yake mkononi, ni saa mbili kasoro, chupa ya kwanza hipo nusu, ndizi na nyama zinaendelea kuiva, huku zikitoa harufu nzuri yenye kuongeza njaa, “au alikuwa anatania?” anajiuliza sebastian ambae alisha kata tamaa ya ujio wa mwanamke yule mwenye kuvutia, pale nyumbani kwake.


Yaaaap!!, dakika tano baadae, seba stian akiwa anaendelea kunywa wine yake na kugeuza ndizi na nyama jikoni, mala akasikia mlango ukigongwa, mwanzo alizania ni wenge lake tu, hivyo akatulia na kuendelea kutazama filamu yake, “ngo ngo!!! Hodiiii” safari hii, ilisikika sauti ya kike, ni ile sauti tamu ya kuvutia, hapo Sebastian kwa haraka sana aliinuka, “karibu karibu pita ndani” wakati anayasema hayo seba stian, tayari alikuwa ameshafika mlangoni, na pua zake, zikinusa harudfu nzuri ya manukato ya gharama.


Naaam!!! Ile Sebastian anafungua mlango, anakutana uso kwa uso na tabasamu mwanana, toka mrembo matata, alie valia tisheti moja laini, na chini akiwa amejifunga kitenge, kilicho kaa vyema kiunoni mwamschana huyu, na kufanya hips na makalio yake yaonekane vyema yalivyo jaa, “jamani nyama inanukia vizuri” alisema yule mwanamke mrembo, huku anaivua viatu na kuingia ndani, Sebastian anamsindikiza kwa macho mwanamke huyu, ambae analifwata jiko moja kwa moja, na kuanza kugeuza vilivyopo juu yake, Sebastian anainama kuchukuwa viatu vya yule mwanamke, na kuviingiza ndani, kisha anafunga mlango, “yani nilizania umeshalala, nikasema huyu kaka mchoyo ameninyima nyama” alisema yule mwanamke, ambae licha ya mwonekano wake wa heshima na upole, lakini leo alionekana kuchangamka kidogo kwa ucheshi, “nilale sasa hivi, wakati ndio kuna kucha, yani hapa kulala saa sabaaaa za usiku” alisema Sebastian, huku anarudi pale alipokaa, na kukaa, lakini safari hii. Alisimama, “hafadhari, maana awa wapuuzi na ujinga wao, wangenifanya nikishe” alisema yule mwanamke huku anakaa kwenye kochi.


Mwonekano wa mwanamke huyu, juu kochi ulivutia zaidi, na kumduwaza zaidi Sebastian, “ok! utatumia soda gani nikufwatie dukani?” aliuliza Sebastian, huku anamtazama yule mdada, ambae sasa alliinuka tena na kulifwata jiko, “wala usisumbuke, nilipenda ninywe hiyo wine, ila naona hipo kidogo, nita kumalizia” alisema yule mwanamke, huku anainama nakugeuza nyama na ndizi,pale jikoni, akiacha msambwana ukining’inia nyuma yake, nakama ujuwavyo wamacho ayanaga panzia, asa kwenye vitu kama hivi, Sebastian akajikuta anatazama sehemu ile ya kukalia, ya mwanadada huyu mrembo.


Seba akushangaa sana, kusikia mwanamke huyu mrembo anakunywa wine, maana toka ameingia dar es salaam, alisha shuhudia wanawake warembo wakinywa pombe kali, tena ile ambayo kuimeza kwake, lazima koo liwe na ganzi, “hapana dada, uwezi kunimalizia, kuna chupa tano nyingine” alisema Sebastian huku anaelekea jikoni, ambako akutumia ata dakika mbili, akarudi na grass mkono wa kulia na chupa ya wine mkono wa kushoto, “unapenda sana wine, yani unakaanazo ndani?” aliuliza kwa utani mwana dada mrembo, ambae ata Sebastian mwenyewe alikuwa ajamjuwa jina, huku anapokea grass na tabasamu limechanua mdomoni, “yah! zinanipotezea muda, asa siku za week end” alisema Sebastian huku anaweka chupa mezani na kuchukuwa ile ya mwanzo, ambayo ilikuwa na wine nusu, akaifungua na kumimina kwenye grass, aliyoishika huyu mwanamke.


Naam ile Seba anamaliza tu kumimina, yule mwanamke akakaa kwenye kochi, kisha akaiweka grass mdomoni, na kupiga funda moja, kisha akaweka grass mezani, “samahani kaka, hivi wewe unasoma chuo gani, na kwanini umeamua kupanga nyumba nzima, huoni kama ni hasara, unapoteza fedha nyingi?” aliuliza yule mwanamke, huku anazungusha macho yake kutazama kila kona ya sebule, “hapana mimi siyo mwanafunzi, na hii nyumba nime pangiwa na kampuni, ila nipo mbioni kujenga nyumba yangu, kimara temboni” alijibu Sebastian, huku anakaa chini kama kawaida yake, akiwa tayari amesha funga chupa na kuweka chini, “hoooo! Kumbe mimi nilizania ni mwanafunzi, hongera sana, unaonekana mdogo, lakini tayari umesha ajiriwa” alisema yule mwanamke mrembo, aliewakimbia wenzie, “asante, lakini sina muda mrefu sana, toka nimeajiriwa” alisema Sebastian ambae mpaka sasa, akuamini kama yupo ndani na mwanamke yule mimi


Naaam,  saa moja na robo za asubuhi, ndio muda ambao yule mwana dada, alishtuka toka usingizini, anajitazama mwilini na kuona kitenge alicho jifunga kikiwa pembeni kabisa ya kitanda, na kumwacha wazi eneo la chini, akibakia na nguo ndogo ya ndani, anamtazama kijana alie lala pembeni yake ambae akuwa anamjuwa ata jina lake, anamwona amelala fofofo, anakoroma, aonyeshi dalili ya kuamka hivi karibuni, “mama yangu, niposalama kweli, alijiuliza mwanamke huyu, huku anapeleka mkono wake, kwenye sehemu yake ya kike, na kujipapasa, “afadhari” anajisemea mwanadada huku anamtazama yule kijana, tabasamu likiwa mdomoni mwake,


Mwanadada anajitoa kitandani na kuchukuwa kile kitenge chake, na kujifunga kiunoni, alafu anamsogelea yule kijana, kwa nia ya kumwamsha ili amuage, lakini anaona kuwa itakuwa usumbufu kwake, maana yupo kwenye usingizi mzito sana, hivyo anatoka nje na kuelekea katika nyumba aliyopanga nawenzake, anakuta wenzake wengi wamesha ondoka, ata wanafunzi anaokaa nao chumba kimoja, tayari wamesha ondoka, ana ongea na mwanafunzi wa chumba chapili, “hivi wakina stellah wamewaachia fungua za chumba chetu” aliuliza mwana mke huyu, ambae kiukweli alikuwa na uhakika wakuwa, licha ya kuwa wenzake watakuwa wamesha ondoka, lakini mizigo yake itakuwa salama, maana likuwa ameifunga vizuri, na sanduku alifunga kwa namba maalumu za siri, “dada Vanessa, mbona mlango wenu hupo wazi” alijibu mmoja kati ya waschana wale, wa chumba cha pili, ambao wao walikuwa bado wanaendelea na masomo yao.


Mwana dada huyu ambae uzuri wake uliwatamanisha ata wanafunzi wenzake wakike wakitamani kuwa kama mrembo huyu, alie tajwa kwa jina la Vanessa, anatembea taratibu kwa kuhesabu atua zake, kama ilivyo kawaida yake, akielekea chumbani kwake, alikokuwa anakaan kwa kushirikiana na wakina stellah, huku wenzake wakimtazama kwa mshangao, maana mawazo yao yali amini kuwa, alikuwa amelala kwa mwanaume, na kama ni hivyo, basi usiku ulikuwa ni mwendo wa kunyanduana, ukizingatia binti huyu Vanessa, toka amekuja hapa miaka mitatu iliyopita, akuwai kuonekana na bwana wala buzi.


Naam!! Vanessa anaufikia mlango wa chumbani, ni kweli anakuta mlango hupo wazi, Vanessa anahisi kuwa, pengine wenzake awajaondoka, hivyo anaingia chumbani bila wasi wasi wowote, lakini anacho kikuta kina mshangaza kidogo, maana anakuta dalili zote za kwamba wenzake awakuwepo, maana anakuta kila kitu kimeondolewa, mpaka godoro alilokuwa amenunua yeye mwenyewe, kitandachake, na ata mashuka aliyo kuwa ametandika juu ya kitanda, kasoro sanduku lake na begi lake dogo, ambavyo navyo, kiukweli mwonekano wake, unamshangaza Vanessa, maana avikuwa kama alivyo viacha jana usiku.


Mwanadada anatoa macho kwa mshangao, na mshtuko mkubwa, maana anaona wazi kuwa kifunguo cha sanduku lake, kime vunjwa, haraka anawazia fedha yake ya nauri na matumizi zilizokuwa ndani ya sanduku lile, hivyo anafungua haraka na kuona nguo zake zime furugwa tofauti na alivyo acha yeye, ata fedha alizo ifadhi ndani ya sanduku azipo, “jamani nimeibiwaaaaa” alipiga kelele za kilio cha machungu, nakuwafanya wenzake wajae kwenye chumba kile, “jamani kimetokea nini, dada Vanessa?” Waliuliza mwenzake, nay eye akiwa analia, akasimulia kilicho tokea, “jamani wakina Stellah kwanini wamefanya hivi” kila mmoja aliudhunika.


Vannesa, alie akuwa anaitaji fedha ya nauri, fedha ya kufika stendi au airport, akakumbuka kuwa anaweza kumpigia simu baba yake, na kutumiwa fedha nyingine, aweze kusafiri, ikiwezekana leo hii, lakini kikwazo ni kwamba, walio iba awakumwachia ata shilingi moja,a mbayo angeweza kupigia simu, “nime kumbuka” alisema dada Vanessa na kuanza kukusanya mizigo yake, kwa haraka, na kuelekea nyumbani kwa yule kijana, asie mfahamu ata jina, kijana mwenye ustaarabu na moyo wa kipekee, kijana ambae licha ya ulewaji ule alio lewa jana usiku lakini akumfanya chochote, ambako aliamini kuwa msaada unaweza kupatikana, yani japo elfu moja tu, ya kununua card ya unity, (card maalumu ya kupigia simu, kwenye box la kupigia simu, miaka hiyo lilimilikiwa na kampuni ya simu ya serikali) kwaajili ya kuwasilina na nyumbani kwao, wamtumie nauri nyingine.


Nyumbani kwa kijana yule, anakuta mlango hupo wazi, kama alivyo acha yeye, maana yeye ndie alie ufungua, “bado amelala” anajisemea Vanessa, huku anaingia ndani, na kuweka mizigo yake sebuleni, kisha anaelekea chumbani akipanga kwenda kumwamsha, ili amsaidie fedha ya kununulia card ya kupigia simu.


Akiwa na machungu ya kuibiwa fedha zake, Vanessa anaenda moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha kijana yule, na kufungua mlango, kisha anaingia ndani, ambako kwa macho yake anakutana na kitu ambachi akukitegemea kukiona asubihi ile, maana alimwona Sebastian akiwa amesimama mbele yake mtupu kama alivyo zaliwa, akiwa anajifuta maji mwilini, kwa kutumia tauro, ni wazi alikuwa ametoka kuoga muda mfupi uliopita.


Naaam! Vanesa nasimama kwa sekunde tano akitoa macho kutazama sehemu ya kiume ya kijana huyu, ambayo kama ingekuwa ni utajiri, basi kijana wetu angekuwa anakaribia, wakina mzee James Kalvine, wa #mbogo_land, (#NYUMA_YA_MLANGO_WA_ADUI) mpaka kijana huyu alipowai kujiziba na tauro alilokuwa ameshika mkononi, “hoooo! samahani ! samahani sana, nilizania bado umelala” alisema Vanesa huku anageuka nakutoka mle chumbani, na kwenda moja kwa moja sebuleni, ambako anakaa kwenye kochi, “jamani, huyu kaka anahatari” alijisemea Venesa kimoyo moyo, “angenibaka usiku sijuwi kama ninge umia” aliwaza Vanesa huku anatabasamu peke yake, “sema tu nashukuru ni mstaarab” alijisema Vanesa huku anageuka kutazama upande wa vyumbani, ambako sasa palisikika vishindo vikija sebuleni, “samahani dada yangu, sikufunga mlango, yani sikuwa na wazo kama bado hupo hapa, nilijuwa umesha ondoka” alisema Sebastian, ambae sasa alikuwa amevaa truck na tishert, chini alivaa viatu vya wazi, yani sendo, “nilienda nyumbani, lakini nimekuta wameniibia, ela yangu ya nauri” alisema Vanesa kwa sauti ambayo ilikuwa inakaribia kuangua kilio.


ITAENDELEA 

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)