DADA MDUNGUAJI EPISODE 4

Emmanuel Lee
By -
0
DADA MDUNGUWAJI EPISODE 4 STORY NA Mbogo Edgar WHATSAPP 0743632247 ILIPOISHIA SEHEMU YA KUMI TANO : zikiwepo za kawaida na bikini, aina ya chupi ambazo akuwai kuzitumia, katika maisha yake, pia kulikuwepo na tight saba za rangi tifauti, “huyu ananitania ngoja arudi atanitambua” alijisemea Jackline na kuvirudisha vile vitu ndani ya begi, kisha akalifunga na kulipeleka chumbani endelea ...... Wakati huo Kule hospital insp Johnson aliomba vipimo vya alama za vidole vya marehemu Kileo na walinzi wake, akaletewa kopi kimi na moja, “insp tumekuletea na hivi hapa vingine nane, ukiachilia wale vijana vijana walio uwawa, juzi usiku kule Jambo Pub, pia kuna wengine watano wameuwawa jana buguruni ”aliongea doctor wenye cheo cha luten, ambae aliletwa kwaajili ya kazi hiyo ya kupima alama za vidole toka kituo kikuu, “vya nini hivi vyote, wakati naitaji vya awa watatu tu!?” aliuliza Insp Johnson, akichukua kopi ya mchungaji kileo “afande nime gunduwa kuwa alama za vidole zilizo patikana kwa wote kumi na moja, ni zamtu mmoja, kuanzia kisu kilicho tumika na aina ya upigaji” jibu hilo lilimstua insp Johnson, akazichukua zile copy na kuzikaguwa haraka, kweli anagunduwa zina fanana, “inamaana huyu muuwaji ni mwanamke?” kitu ambacho insp Ernest akutaka kuamini, “hapana sasa hawa walio uwawa bar, wanauhusiano gani na hawa askari wastaafu?” aliuliza yule doctor, “juzi usiku tuliambiwa kuwa awavijana wa hapa bar, walikuuwawa ndani ya chmba cha mwanamke, na yule mwanamke alimshambulia mhudumu na kuondoka zake, hapo Insp akatoka haraka na kuamuru magari ya elekee manzese, mapambano bar and guest house, **** ilisha timia saa tano asubuhi Denis na Maadhi baada ya kumaliza kunywa soup kwa mama bupe, wakaelekea Jambo pub wakapata bia mbilimbili za kuanzia, kisha Mahadhi aka lipa deni la Denis la carton moja ya bia, baada ya hapo kila mmoja akashika njia yake, wakati Mahadhi akiwa anaelekea kaliakoo Denis alielekea sinza, alienda moja kwamoja mpaka kwenye duka la urembo, lenye poster card na midori ya urembo alitumia nusu saa kuchagua mdori mzuri mkubwa size ya kati, ambae alivalishwa kinguo kilicho andikwa “only you can show me, what love is … ” japo alijiuliza sana kuhusu uelewa wa mgeni wake juu ya ile lugha ya kigeni, maana aliamini kwa mwanamke mama ntilie, kuwa amesoma na kupata uelewa wa kusoma na kuielewa lugha ya English, lakini Denis akuwa na namana, aliona bora aanze kutumia ujanja ku fikisha ujumbe kwa mwenyeji wake, pengine anaweza kumwelewa, huu ni ujana alioupata toka kwa Mahadhi, anapo taka kumbembeleza mkewake, akafikilia kitu kingine ambacho kita msaidia kwenye kumlainisha yule mwanamke kule nyumbani, maana swala la kutongoza kwake lilikuwa kazi ngumu sana, Denis akiwa bado anaumiza kichwa, aliendesha gari akirudi alikotoka, na kwenda adi njia panda ya mabibo, pasipo kupatajibu, akapuuzia mawazo yake, na kusimamisha gari kwenye soko la mahakama ya ndizi, akashuka kwenye gari nakuanza kununua mazaga muimu ya chakula, zikiwemo ndizi viazi kuku wakienyeji ambao walichinjwa na kunyonyolewa, wawili, kisha akanunua nyanya na vitu vingi sana, ambavyo viliitajika nyumbani, alibeba kwa wingi sana, wasinge weza kumaliza watu wawili ata kwa mwezi mzima, “awa mama ntilie wanapenda sana kujipikilisha,” saa sita na robo akaanza safari ya kurudi nyumbani, njiani akifunua kopo moja baada ya jingine la bia na kulitandika taratibu, huku akiwaza, endapo mwenye jiwake atakuwa aelewi kusoma English ataanzaje kutafsilia, baada ya kuwaza kwa muda kidogo, akapata jibu, akatabasamu, nibaada ya kuiona bar moja kubwa njiani mtaa wa luguruni, akakata kona ya ghfla kulia, akiikosa kuigonga pikipiki iliyokuwa inapita kwa mwendo wakasi, Denis akaingia na kupaki gari lake pale bar, ikiwa ni karibu na kufika mtaani kwake, akaziacha bia zake ndani yagari, ambazo bado zilikuwa nyingi kwenye gari, akafunga gari na kutafuta sehemu nzuri ya kukaa, kwanza akaagiza chakula, nusu saa baadae aakiwa amesha maliza kula, akaanza kunywa bia, “baada ya hapa ata nikianza kuongea nae, tuta enda sawa, yani mtoto mzuri mpaka namwogopa” alijisemea Denis, aimalizia kwa kicheko, ****** huyu ndie Denis mwenyewe kabisa toka akiwa mdogo, nimwoga sana wa wanawake, licha ya kuwa mwoga kukataliwa, pia ilisha waikutokea safari moja, akiwa kidato cha tatu, kuna binti mmoja Johari, alikuwa ni mwanafunzi mwenzake, mtoto wa mzee Mapande, jina alilopewa kutokana na kazi yake ya kuuza bucha la nyama ya ng’ombe, Johari alijilegesha mwenyewe kwa Denis, akitumia mtego wa vizawadi na vi offer vingi vingi, mpaka Denis alipoingia mtego na kuanza nae mausiano, kweli Johari alimteka Denis kwa fedha na zawadi nyingi tofauti kila siku, na yeye akalipa fadhira kwa kumpatia penzi moto moto Johari, kiasi cha kusababisha, habari yao isambae kama moto kwenye nyasi kavu, baada ya mda kidogo likatokea tatizo, kumbe yule binti Johari mtoto wa mzee Mapande, alikuwa anatembe na kijana mmoja muuza mchele huko sokoni, ndie ambae alikuwa akimhudumia Fedha pamoja vitu vingi sana, nandie aliempatia jeuri ya fedha ya kumkamatia Denis, lakini kutokana na kukolea kwa Denis, Johari akajikuta akishindwa kumpatia penzi kijana muuza mchele, huku akimpiga kalenda ya kumpatia kitumbua kila kukicha, yule muuza mchele aliona mabadiriko, katika penzi lake na Johari mtoto wa mzee Mapande, baadea ya kwaza sana akaona achunguze ni kitu gani kinacho sababisha mapenzi yao yaporomoke, mwishoe aka gundua kuwa, kuna mwanafunzi mwenzake na Johari, ndie anae mzuzua mpenzi wake, hivyo akaamua kuunda mtego wa kumnasa Denis, akipania kumfanyia kitu mbaya, iwapo atamkamta akiwa na binti huyo, wakati huo huo, mzee Mapande nayeye alisha sikia tetesi za kuwa, kuna kijana muuza mchele anatoka na mwanae, kumbe siku ya fumanizi, ndiyo siku ambayo baba wa yule binti, alipanga kufanya fumanizi la mwanae na muuza mchele, na muda alio ambiwa kuwa, mwanae anaye msomesha kwatabu, ameonekana anaingia guest house, muda huo alikuwa buchani, baba wa yule binti akaambatana na njemba zipatazo sita, wote wakiwa na zana za kazi zitumikazo buchani, wakaelekea kule guest house, wakati huo huo kule guest, baada ya Denis kusikia mlango wa chumba cha guest, unagongwa kwa nguvu, ikioyesha ishara kuwa anafumaniwa, haraka sana akapanda juu ya dali, akipitia kwenye seheu mahalumu ya kuingilia dalini endapo mafundi wa umeme wanaitaji kufanya marekebisho, kisha akajibanza kimya kabisa, akawa anachungulia mle chumbani kwa kutumia pale alipo ingilia, aliweza kumwona muuza mchele anaingia mle chumbani, na kuanza kupiga yule Johari, akimlazimisha aseme Denis yupo wapi, yule binti alilia sana maana muuza mchele alikuwa bounce, yani anamwii mkubwa, wakati yule muuza mchele akiendelea kumpiga Johari, kutahamaki baba wa yule binti akaingia na timu yake, hapo ndipo kilipotokea kitu mbacho, tokea siku ile Denis akuwai kijiingiza katika mapenzi wala kutamani kufanya hivyo, mpaka alipo mwona huyu mama ntilie, Maana ndani ya dakika tano, Denis aliweza kumwona yule jamaa muuza mchele, akipatwa na dhahama ya kuchalangwa na visuvikari ambavyo wakina mzee Mapande, uvitumia buchani, na mwisho wake wakimuacha muuza mchele alikuwa amelala kwenye kijito cha damu, mwili wote utazani mbuzi yupo machinjioni, mzee Mapande akamchukuwa mwanae, aikiwa na wale watu wake wakaondoka zao, baada ya kuona hivyo Denis alipita juu kwa juu na kutokea upande wapili, yani chumba kingine, nakuondoka zake, tokea hapo licha ya kuwa Denis ni kijana mtanashati, na mwenye kuvutia mbele ya wanawake wengi, wa nyumbani na kazini, ambao walijilengesha sana, wakiwepo wasichana wadogo na wake za watu, ambao walikuwa wakitamani kuwa naye, lakini Denis aliwa mwaga, akuonyesha kuangaika nao, kuna kipindi wakamkashifu, kuwa dudu yake mbovu aiwezi kula kitumbua, lakini yeye akujari, na mengine akuyasikia sababu hakuwa na mazowea na watu wa pale mtaani, ambapo alikuwa ameamia miezi mitatu nyuma **** Magari ya police ya lisimama nje ya mapambano bar, insp Johnso David alishuka nakuingia ndani ya bar hiyo, akaulizia kuhusu muhudumu wakike alie shuhudia yale mauwaji ya wale vijana watutu, kwenye chumba kilicho pangwa na mwanamke toka kijijini, akaambiwa kuwa, baada ya tukio la mauwaji, ile bar aija funguliwa tena, na wafanya kazi wote wapo makwao, kuhusu yule binti, inasemekana yupo mbezi kwa dada yake, lakini akuna anaye pafahamu, na simu yake, alikuwa ameuza baada ya kukosa fedha za kusafirishia mizigo yake, kwenda mbezi, insp Johnson akuwa na ujanja, akarudi kwenye gari na kutoa uelekeo mpya wa kigamboni kwa mzee Soud, brigedia mstaafu, gari zikaanza kuondoka huku akichukuwa simu yake na kuiweka sikioni, akipiga kwa brg msataafu, Soud, ***** Saa nane mchana, insp Johnson alikuwa nyumbani kwa brg msaafu, Suod Hassan masoud, nje ya jiji la Dar es salaam, kitongoji cha mji mwema wilaya ya temeke (kipindi hicho) jimbo la kigamboni, Insp Jonhson David alikuwa ametulia akimsikiliza mzee Soud, ambae alikuwa akimsimulia juu ya wanajeshi saba ambao walisafiri kwenda nchi Congo, ambapo walirudi, sita mmoja wao akiwa amepote kwenye mission, mzee Soud alienda mbali zaidi na kuelezea wasiwasi wake juu ya kupotea kwa Michael Nyati, ni kwamba, mpaka yeye anastaafu kazi, wazazi na ndugu wakaribu wa mtu huyu, awajawai kuja kumtafuta ndugu yao, na bado anahesabika mtoro kazini, “katika kumbu kumbu zangu, niliwai kupokea simu moja tu, ya mtu akiulizia juu ya Michael Nyati, sasa ndiyo Napata picha kamili, yule alikuwa Michael mwenyewe, sababu aliulizia watu wote walio enda Congo kipindi kile” akaelezea pia mashaka yake juu ya watu sita walio rudi, toka Congo, ni kuhacha kazi mala tu baada ya kumaliza likizo yao ya mwezi mmoja, ambayo walipewa baada ya kurudi toka kwenye kazi nzito, “na baada ya miaka michache mbele tukaanza kuwaona wakiwa na maisha mazuri, wengine wakaanzisha makanisa wengine ni wafanya biashara wakubwa, mpaka sasa” aliongea mzee soud akionyesha umakini juu ya swala hili, kama kuna kitu alianza kukihisi insp Johnson “samahani mzee Soud, unakumbukumbu yoyote ya hao watu walio safari kwenda Congo?” aliuliza insp akimtazama mzee Soud, ambaye aliinuka na kuelekea chumbani kwake, baada ya dakika chache akarudi akiwa na kitabu cha picha mkononi (photo album) kubwa akaiweka mezani, akafunua kurasa chache, kisha akamgeuzia bwana Jonhson akionyesha kwa kidole picha moja, “ni hawa hapa, hii picha nilipiga nao siku wanaondoka kuelekea Congo, na huyo alie chuchumaa kushoto ni Michael Nyati,” aliongea mzee Soud, huku insp Johnson akiwa ana itazama ile picha kwa umakini mkubwa ulio changanyika na mshangao, ni kama akuamini alichokiona, “unataka kuniambia, kuwa hawa wote walienda congo?” aliuliza insp Johnson, akionyesha kuwa kama kuna kitu aja kiamini katika ile picha “hapo kasoro mimi tu! sikwenda, lakini hao wote unao waona walienda, na huyo bwana mdogo alie chuchumaa hakufanikiwa kurudi” alijibu mzee Soud akijiamini kuwa anachoeleza ndicho kilichopo, “kwani kuna maelezo zaidi waliyatoa juu ya kilicho mtokea mwenzao?” aliuliza insp akiwa ameikazia macho ile picha, “mpaka sasa hakuna anaye ujuwa kweli, zaidi ya hapo wanne waliobakia” alijib mzee Soud Hassan, akimtazama Johnson kwa umakini, “mzee naona nikuache, wacha nika endelee kulishugulikia swala hili” aliongea insp Johnson huku akiinuka toka kenye kochi alilo kalia, akionyesha wazi kuvurugwa na kitu katika ile picha, “kijana mbona imekuwa ghafla hivyo?” mzee Soud alisha gundua mabadiliko ya usoni kwa insp Johnson, na alitegemea kutokea kwa kitu kama hicho “mzee wangu majukumu yamenibana sana, wacha niwai nika pambane” aliongea Johnson, nakuanza kutoka nje, akisaau kuwaaga wengine waliompokea, na sasa walikuwa jikoni wakiandaa chakula, mzee Soud alimtazama sana insp Johnson, adi alipo fika mlangoni aka mwita,”Johnson kuna kitu ni muhimu kuzingatia , unapo mtafuta Michael Nyati, lazima uwe makini sana, maana nimtu hatari sana, husi jaribu kuladhimisha hisia zako, ukikwama nitafute” Johnson alisikiliza kisha akakubariana na mzee Soud, lakini kiukweli mawazo yake hayakuwepo mahali pale, kunakitu kili mvuruga, **** saa kumi jioni mzee Masinde alikuwa msibani kwa mchungaji Kileo, ni baada ya kutoka kwenye msiba nyumbani kwa mchungaji Chilumba, ndipo alipo pokea simu yake ya mkononi, iliyo kuw ikitoa mlio ikiashiria kuna simu ilikuwa ina ingia, “hallow…. Ndiyo…” aliongea mzee Masinde huku anainuka nakusogea pembeni kidogo, nasasa alionekana akiongea na simu pasipo kusika upande wapili, “vipi mbona akuna ata salamu ….. ok! nipo msibani …. njoo nyumbani saa mbili usiku … usijari tutaongea vizuri” alimaliza mzee Masinde nakukata simu, akarudi alipo kaa mwanzo, akachukuwa simu yake na kuandika messeji kisha akisend kwa kudi ( yani kwa namba zaidi ya moja) kisha akairudisha simu mfukoni, huku uso wake ukianza kuonyesha mashaka na wasiwasi **** mida ilikuwa imesogea giza la saa moja lilishaanza kutanda, Michael Nyati alikuwa ametulia na mke wake Anitha juu ya kochi moja la watu wawili, wakikata mvinyo taratibu, macho kwenye TV, walifanyiana michezo ya kimapenzi, nikawaida yao siku zote, walisha zowea siku zote za maisha yao, ata mbele ya Jackline, wao walicheza kama watoto, “vipi umesha wasiliana na jambazi wako?” aliuliza Anitha au mama Jackline, “nilikuwa nasubiri anipigie, lakini naona kimya” alijibu baba Jackline, huku akiinua simu yake toka mezani akacheki muda, ilikuwa saa mojaza usiku, inakaribia na nusu, “wacha nimpigie bwana, kama yupo na huyo mlevi, shauri zake atajuwa cha kufanya” alisema baba Jack na kuanza kupiga simu, mwanae Jackline “hahahah mlevi anamcheka mwenzie” alicheka sana mama Jackline, **** Saa mbili na dakika tano, mzee Masinde alikuwa ametulia nyumbani kwake akamsubiri mwanae ambae alimwambia aje hapo nyumbani mida hii ilionyesha alikuwa ana kitu muhimu anataka waongee, mala mlango uka gongwa “fungua tu! hupo wazi” mlango ukafunguliwa akaingia Insp Johnson akiwa amevalia mavazi ya kiraia, tofauti na aliivyokuwa mchana, Akamwona mwenyeji wake, akivuwa viatu na Suluwali, akibakia na boxer, dudu yake bado ime simama sana, hapo Jackline akajiweka tayari kumtandika Denis, kama angemsogelea, lakini ikawa tofauti akamwona anasogelea kabati, kisha akamwona akivuta shuka, alafu akaja nalo mpaka kitandani, na kumfunika, toka miguuni mpaka maeneo ya shingoni, alafu na yeye Denis akaelekea bafuni, mle mle chumbani, kisha ikasikika sauti ya kumwagika kwa mkojo mrefu sana, ulio tumia dakika nzima, alafu akatoka na kurejea chumbani, akajilaza pembeni ya Jackline, pasipo kujifunika shuka, baada ya dakika chache, Jackline akamsikia Denis akianza kukoroma, kiukweli kitendo kile kilimkumbusha mbali sana Jackline, kipindi akiwa mdogo, siku ambazo alikuwa na choka sana, kwa ajili ya michezo ya kitoto au mazoezi, baba yake au mama yake walikuwa makini sana, kuakikisha Jackline analala salama, mala kwa mala waliigia chumbani kwake na kumfunika vizuri, **** saa kumi na moja za alfajili, vijana nane walikuwa ndani ya gari moja aina ya land lover 110, wakitokea morogoro kuelekea Dar es salaam, ambako waliitwa kwa ajiri ya kazi muhimu, na kwamba huko Dar es salaam, wangeungana na wenzao wanne, gari lilienda moja kwamoja mpaka mbezi msakuzi, na kusimama mbele ya jumba moja kubwa la kifahari, ambalo lilionyesha kuto kukaliwa na watu, pembeni waliliona gari nyingine kama walilo kuja nalo wao, lilikuwa lime park maali pale, na vijana watano wakiwa wamesimama pembeni yake, walikuwa wanawafahamu, ni vijana wa mzee Masinde, mala nyingi uwa wanakutana kwenye matukio ya uvushaji wa meno ya tembo, na ngozi za wanyama mbalimbali, wakaungana nao baa da ya kusalimiana, wakatulia kama dakika tano ndipo yakaja magari mawili mengine likiwepo land lover 110 na Nissan patrol, yakasimama na kwenye land lover alibakia madereva peke yake, na ndani ya Nissan alikuwepo mzee Mathayo peke yake, akashuka na kuwapatia ufunguo wa nyumba, “ingieni mpumzike, mkijuwa kuanzia sasa mpo kazini kumsaka muuwaji, alie wauwa wakina Chilumba, tutawasiliana kujuwa mtaanzia wapi kazi yenu” wale vijana pamoja na madereva wa yale magari matatu, waliingia ndani huku mzee Mathayo, akiondowa gari lake na kupotea zake, **** Saa kumi na mbili na robo nyumbani kwa Denis, Jackline alikuwa amesha amka, na sasa alikuwa sebuleni akifanya mazoezi baada yakuona mwenyeji wake akuwa na dalili ya kuamka, Jackline akiwa amevaa kile kigauni chake kifupi alicho lalia usiku, ndani akiwa na kikaptula kifupi, lakini bila kisu wala bastora, alifanya mzoezi kwa nguvu sana, lengo likiwa kutumia muda mfupi, kabla mwenyeji wake haja amka, chumbani nako Denis aliamka nakujikuta yupo peke yake lakini anakumbuka kuwa usiku alikuwa amelala na mgeni wake, akainuka na kubadiri nguo alizovaa, na kuvaa bukta, kisha akaingia chooni mlemle chumbani kwake, baada ya kumaliza kujisaidia alitoka chooni, akasimama chumbani kwake, alipepesa macho huku na huku, ndani ya chumba wakati huo alijaribu kuvuta kumbukumbu, ya matukio yake ya jana usiku toka alipo rudi, “mh! siku sija haribu kweli?, maana mh! nilikuwa tungi” aliwaza Denis akiendelea kuangalia huku na huko kama anatafuta kitu, akaliona begi kubwa alilo m’bebea mgeni wake juzi, likiwa chini pembeni karibu na ukuta, juu yake kuna begi jingine, analikumbuka ni la mgeni wake, anayachukuwa na kuya weka kwenye kabati, la nguo lililo jengewa humo ndani, kisha akachukuwa mswaki akaweka dawa nakuingia tena bafuni, baada ya dakika kumi Denis alikuwa amesha maliza kupiga mswaki, alitoka na kuingia sebuleni akumwona mgeni wake , akafunguwa friji na kutowa kopo la soda, na kuanza kuinywa, huku akielekea jikoni, akamkuta mgeni wake, dada mama ntilie akiwa amelowa maji kwenye kigauni kifupi alichomletea kwa ajiri ya kulalia, (ayakuwa maji ni jasho) alikuwa ameinama anamalizia kudeki jikoni, kiukweli kule kuinama kulisababisha kigauni kishindwe kuhifadhi baadhi ya sehemu ya maumbile ya nyuma ya mwili wa Jackline, kosa kile kipens cha jinsi, tungeongea mengine, ilimfanya Denis aduwae, maana mapaja mazuri ya Jackline yalionekana kwa uwazi kabisa na ule mkao wakuinama ndio kabisaaaa, maana Jackline alijariwa makalio mazuri ya duwara yaliyo jaa vyema, Denis akajikuta mapigo ya moyo yanaenda mbio, damu ikachemka nakukimbilia chini, na kujaa kwenye dudu, nayo ikasimama, akajikuta anapaliwa na soda, aliyokuwa akiinywa, Jackline akastuka nakugeuka kumtazama mwenyeji wake, macho ya Jackline yalituwa kwenye bukta ya Denis, Jackline akashuhudia dudu ya mwenyeji wake ikiwa ime simama, kama ameficha ndizi kwenye bukta, “ho! Umeamka niliona nisi kuamshe maana ulirudi ume choka” aliongea Jackline akikwepesha macho kutaza ma dudu ya Denis, kitendo ambacho denis alikiona, “hapana tatizo niliamua kulala, sababu leo juma mosi siendi kazini” alijibu Denis akigeuka kuficha dudu ambayo ilikuwa ina mzalilisha, “hoo kwahiyo leo tupo wote hapa nyumbani?”aliongea Jackline akitabasamu, kauli ya Denis ilionekana kum furahisha, “yaa lakini tutatoka wote jioni, tuka tembee kidogo, maana umekaa sana ndani” Denis alimjaribu mwenye jiwake, kuona kama atakubari, “mh! kwani tutanaenda wapi?” aliuliza Jackline kwa shahuku, bado akionyesha furaha, “tunaenda mbezi, au wewe unaonaje?” aliuliza Denis, “hakuna tatizo, ila husinywe sana pombe mpaka tunalala kwenye kochi” wote waka cheka huku Denis akielekea sebuleni, “ngoja nika shushe mizigo kwenye gari” alisema Denis akiondoka na kumwacha Jackline akimalizia kudeki, “sawa nakuja kukusaidia” Denis alielekea nje kabisa ya nyumba, huku akiendelea kuigugumia soda ya baridi, Jackline alikuwa ameona jinsi, dudu ya Denis ilivyo shikwa na hasira, akawaza kidogo kuwa anampa shida mwenyeji wake, maana alilijuwa ilo kutokana na kufafahamu jinsi umbo lake lilivyo, na usumbufu anaoupata kila siku, toka akiwa na umri wa kischana mpaka leo mdada, kutabasamu kidogo huku anamaliza kudeki, akamfwata Denis nje namkumkuta anashusha mizigo aliyo inunua jana sokoni mabibo, akaanza kumsaidia, “hivi kaka unaitwa nani? maana ata jina sikujuwi” aliuliza Jackline, Denis naye akakumbuka, “ ni kweli ata mimi sikujuwi jina” wote waka cheka, kisha waka tambulishana majina, Siku hiyo Denis na Jackline, walishinda pamoja siku ile, huku kila mmoja akimtazama mwenzake vizuri, maana awakuwai kukaa pamoja kama hivi mchana toka wamefahamiana, Denis alikubari kuwa Jackline siyo mtoto wakawaida, alishangaa mschana mzuri kama vile akawa anazurula mtaani, akifanya kazi za mama ntilie, kiukweli Jackline akufanana na kazi hizo, wakati Denis akiwaza hayo, Jackline naye alikuwa anawaza yake, baada ya kumtaazama Denis, aligunduwa kitu juu ya kijana huyu, licha ya kuwa mtanashati pia alikuwa mcheshi, na mwenye moyo wa upendo sana, kuna vitu alivihisi ndani yake, japo alijaribu kuvipuuza, maana hakuwai kumpenda mwanamume ata siku moja, kwani alijisikia raha sana kukaa karibu na huyu kijana, “sasa Jack hizi siku mbili huja fanya kazi, sasa uta watumia nini wazazi wako?” aliongea Denis akimuondoa Jackline katika mawazo yake, “hoo! tena wameniambia mama nimgonjwa, nika mwambia mimi sijafanya kibarua chochote, hivyo hapa sijuwi ata nifanyaje” aliongopa Jackline, ili kumfanya Denis amwamini kuwa wazazi wake wapo kijijini, na awajiwezi, “ok! usijari, utanikumbusha baadae, nikupatie kiasi cha fedha, ili ukawatumie, kwani unawatumiaga kwa njia gani” aliongea Denis akionyesha kuguswa na swala lile, Jackline akaongopa kuwa, anatuma fedha kenye bus, waliendelea kuongea, wakati huo walikuwa wanakula chakula cha mchana, **** mbezi msakuzi vijana wakazi walikuwa wana panga mikakati ya kazi yao waianze vipi, baada ya kutafakari kwa muda mrefu, waliafikiana kuwa waanze kwa kuwatafuta ndugu wa Michael Nyati, ambae inasemekana kwao ni Songea, hapo mala moja wakaanza kufanya mawasiliano na watu wao waliopo Songea, baada ya kuulizia sana kwa watu wao waliopo Songea, kwa msaada wa mzee Masinde, waliweza kugunduwa kuwa Michael, ana mtoto mmoja tu!, binti yake ambae amesafiri kuja Dar, ambae awakujuwa amekuja kufanya nini, hapo wakaona wamesha pata njia ya kumnasa Michael Nyati, mala moja waka fanya juhudi za kutumiwa picha ya binti huyo, kwa njia ya fax, japo aikuwa na rangi, lakini ilionekana vizuri, wakapanga kumtafuta na kumteka, ili wamshinikize bwana Michael Nyati, aje sehemu watakayo mwelekeza ili wamtie miikononi mwao na kumpotezea maisha, yeye na mwanae Jackline, wali waza hayo, pasipo kujuwa uwezo wa Jackline, kwa kifupi mawazo yao yalikuwa tofauti na ukweli, waliamini kuwa Michael, amekodi muuwaji wakike, ambaye amuwauwa wakina Kileo, awakuwenza kujuwa kuwa muuwaji ni Jackline mtoto wa damu wa mzee Michael Nyati, ambae wanapanga kumkamata, pia mpango wao mwingine ulikuwa ni kwamba, leo jioni wamtafute kwanza Dada mfanyakazi wa mapambano guest house, ambae aliwai kumwona muuwaji huyo wakike, pengine wangepata mwanzo mzuri wakumpata ata muuwaji wanae mtafuta, maana baada ya kufatilia, waliambiwa kuwa mwanamke huyo, yupo mbezi, anapatikana sana kwenye bar moja maarufu ya Full dose, ambapo ujifanya anamtembelea dada yake anaye fanya kazi hapo, huku lengo lake likiwa ni kuvizia wanaume wapenda vitumbua, ili ajipaie pesa za kujikimu, wakapanga jioni hiyo wajige watatu waende Full dose na wengine waende mjini, ambako waliamini wange bahatisha kumpata Jackline, kila mmoja wao alikuwa na kopi ya picha ya Jackline, huku kila mmoja akijisemea kimyo moyo kwamba Jackline mschana mrembo na mzuri sana, hivyo akimpata, lazima kwanza ale kitumbua, **** saa moja usiku, Jackline na Denis walikuwa mbezi kwenye Pub moja nzuri sana ambayo watu wengi upenda kuja kustarehe mida ya jioni, Full dose pub, walikuwa wamekaa kwenye kona moja ya kujificha wakipata kinywaji, ambapo Denis alikuwa anakunywa bia na Jackline alikuwa anakunywa soda, muda wote wakiongea kwa furaha huku wakifanyiana masihara, kama ungewaona unge sema ni wapenzi, tena wa muda mrefu, walikuwepo hapo Pub toka saa kumi jioni, Denis alisha kuwa amekunywa bia nyingi sana, alikuwa ameshaondowa ahibu, kuna muda Denis alimtazama Jackline, ambapo walikuwa wamekaa kwa kutazamana, wakitenganishwa na meza, Denis alimkazia macho Jackline kwa muda mrefu, alimtazama mpaka Jackline akaanza kuona ahibu, akakwepesha macho, na kutazama chini, Denis akashika mikono ya Jackline, ambayo ilikuwa mezani, Jack akainua uso wake na kumtazama tena Denis, macho yao yakakutana, kuna hali flani ilimjia jackline, mwili ukamsisimka, “Jack” aliita Denis “abee” kiukweli Jackline akumbuki mala ya mwisho aliitikia lini kwa mtindo huo, ilikuwa sauti nyembamba ya chini na nyororo, iliyo jaa ahibu, sauti ambayo iliamsha hisia za mbali sana za Denis, macho ya Jackline yalikuwa yamesha anza kulegea, hakuwai kutokewa na hali kama hiyo ata siku moja, “unajuwa kama wewe nimzuri sana,” Sali la Denis lilikuwa gumu kwa Jackline, alijibu kwa kutabasamu, nitabasmu ambalo akuwai kutabasamu akiwa na umri mkubwa kama huu, nitabasamu ambalo Denis akuwai kuliona ata kwenye TV, tabasamu lililo sababisha kuonekana kwa vijishimo (dimples) mashavuni kwa Jackline, nakusababisha uzuri wake uzidi mala dufu, Denis akaduwaa tena ni mshangao wawazi kabisa, mpaka Jackline akagunduwa, ni mshangao ambao ulimfanya Jack astuke kutoka kwenye hali aliyokuwa nayo, ya hisia za mapenzi mbele ya huyu mwenyeji wake mlevi, akaitoa mikono yake kwa Denis haraka sana, akajikuta ana pandwa na hasira za ghafla, akakunja sura akimtazama Denis, lakini sura yake ilizidi kupendeza “vipi Jack nimekuhudhi?” aliuliza Denis akiwa ame udhunika, kwa hali aliyo ionyesha Jackline, Japo sura yake ilizidi kuwa nzuri, “hapa, ilaaa!.. naitaitaji kwenda chooni” aliongea Jackline akijitaidi kuondoa ile hali ya chuki zidi ya wanaume iliyo ingilia ghafla, “hooo! ok! ok! ebu nikupeleke” aliongea Denis huku akijiandaa kusimama, Jackline alibaki amegana kwenye kiti akimtazama Denis kwa hasira, kwani akupenda jinsi anavyo onyesha kumjari, kwaupendo mkubwa, Jackline alimtazama Denis, akiinuka na kuzunguka pale alipokaa kisha aka mshika mkono, Jackline alishangaa moyo wa huyu kaka, akajikuta anatabasamu, huku hasira zikiyeyuka, Jackline aka inuka akimfwata Denis, na kuanza kutembea wakiwapiti watu mbalimbali, walio kaa kwenye meza zao, wanaume waliomwona Jackline akipita na Denis, walikodowa macho ya matamanio bila kificho, kwani alipendeza sana, kwa nguo alizo vaa na hips zilichomoza vizuri sana kwenye suluali ya jinsi aliyokuwa ameivaa, na pia maziwa yake mazuri yalionekana kusimama vyema, yakiinua kishati alicho kiva, unaweza kusema chuchu zake, zinaweza kutoboa ile nguo, wanaume wangine walinaswa vibao na wenza wao wakike, kwaajili ya kukodoa mimacho, kumshangaa Jackline, mmoja kati ya watu walio kuwa wakimkodolea macho Jackline, ni yule mdada muhudumu wa vyumba, wa mapambano guest house, alimwona Jackline na kumtambua mala moja, Moja kwamoja Denis alimpeleka Jackline kwenye mlango wa choo, Jackline akainia chooni akimwacha Denis anamsubiri mlangoni kwa nje, Jackline ambae akiwa amemwona yule mwanamake wa Mapambano bar, mle chooni akiwa peke yake, aliwaza kidogo juu ya hisia zinazo mnyemelea juu ya Denis, akajilazimisha kukojoa, japo akubanwa na haja hiyo, mwisho wasiku akapotezea mawazo yake na kutoka nje, akimkuta Denis bado ana msubiri, ambae alimshika tena mkono, nakuanza kurudi walipokuwa wamekaa mwanzo, kiukweli kitendo cha kushikwa mkono, kiliusisimua mwili wa Jackline, ambae toka amejitambua, wanaume anawaona akama maadui, kutokana na kauli za baba yake, lakini usiku huu wa leo atamapigo yake ya moyo, yalimwenda kasi, Huku nako dada muhudumu wa vyumba, alikuwa anamtazama kwa umakini sana Jackline, alijiuliza kama anamfananisha au ndiye mwenye, kilicho mchanganya, leo anaonekana tofauti na siku ile alivyomwona kule mapambano, maana siku ile alionekana kuwa ni mwanamke mwenye uwezo duni kimaisha, kutokana na mavazi aliyokuwa ame vaa siku ile, lakini leo anaonekana zaidi ya mwanamke mrembo mwenye maisha mazuri, yule dada aliwaangalia Denis na Jackline, mpaka walipokaa kwenye meza yao, akawaza anamna ya kwenda kumtazama vizuri, ili kumtambua kama ndiye au siye, alisubiri kama dakika tano kisha akainuka alipo kuwa amekaa na kuanza kutembea kuelekea usawa wa walipokaa wakina Denis, wakati huo Jackline alikuwa ameshikwa mikono yote miwili na Denis, “vipi Jackline, maisha unayaonaje pale kwang?” aliuliza Denis, akimtazama Jackline usoni, wakati huo alikuwa ana suguwa sugua viganja vya mikono ya Jackline kwa kutumia vidole gumba, kitendo kilicho zidi kuusisimua mwili wa Jackline na kumfanya ashindwe kumtazama Denis machoni, “mazuri tu,” alijibu Jackline kwa sauti nyororo, yenye kulegea sana, huku muda wote tabasamu mwororo likiwa alibanduki usoni kwa Jackline, wakati Jackline anakwepesha macho yake yasitazamane na yale ya Denis aligeukia nusu ya upende wake wakulia, yani nyuma upande wa kushoto wa Denis, macho yake yaka muona mtu, mwanamke akisogelea pale walipo, akamtambua mala moja, ni yule muhudumu wa vyumba, pale mapambano bar, moyo wa Jackline ukastuka, asa alipomwona anakuja upande wake, japo alikuwa gizani kidogo lakini aliweza kumshuudia yule dada akikazia macho upande wake, Jackline akajuwa alishaonekana muda mrefu, ila huyu dada anachotaka ni kusibitisha tu!, sa kwa namana alivyo mwona, Jackline akatulia kama ajamwona, akajifanya yupo busy na Denis, kwa macho ya ujanja sana, Jackline alimwona yule dada akipita karibu yao huku macho ameyaelekeza kwake, akamshuhudia yule dada akitoa macho ya mshangao na mstuko, kisha ghafla akageuka alikotoka, jackline alimtazama yule mwanamke mhudumu akitembea moja kwa moja, na kutoka nje, alionekana wazi kustuka baada ya kumwona Jackline, hapo Jackline alitabasamu “ho! Denis ngoja kwanza kidogo, naona kama tumbo linaanza kuuma, wacha niende chooni mala moja nikirudi tuondoke zetu” alisema Jacklie akiinuka huku akishika tumbo, Denis naye akainuka iliamsindikize chooni, lakini Jackline akamzuwia “pumzika wala usijari” Denis akatulia, Jackline akatoka na kuelekea upande wa vyoo, lakini akufika mbali, akageuka nakuelekea nje ya bar, kilikuwa kitendo cha haraka sana, kiasi kwamba Denis akuona, ukizingatia na mtungi ulisha kamata sehemu kubwa ya kichwa cha Denis, baada ya kutoka nje ya ile bar, Jackline alivuta atuwa za haraka kuelekea kwenye maegesho ya magari, ambayo ndiyo njia yakutokea mahali hapo, mala atuwa chache mbele yake, akamwona dada mhudumu, akitembea haraka kuelekea bara bara kuu, lakini kabla haja amua la kufanya akamwona yule dada akimsimamisha mwanaume mmoja aliekuwa anaingia pale bar, Jackline akajibanza ubavuni mwa gari oja wapo lililokuwepo karibu yake, ***** dada mhudumu wa vyumba wa mapambano, akiwa anaamini kuwa yule dada muuwaji ajamuona kabisa, alitoka nje bar lengo ni kukimbilia kituo cha polisi, kutoa taharifa ya uwepo wa mwanamke muuwaji, alianza kutembea kwa mwendo wa haraka sana kufwata barabara kuu iendayo morogoro, ni mita kama mia tano mpaka kilipo kituo cha polisi cha mbezi, lakini wakati anaendelea kutembea, atuwa chache toka Full dose pub, eneo la maegosho ya magari, akamwona jamaa moja ambae ni mteja mkubwa sana wa ile bar, ambae anamfahamu kuwa ni Polisi, akaona bora amwambie yule polisi anaye julikana kwa jina la Masoud, alikuwa amevalia kiraia, alimweleza jinsi alivyo mwona yule dada, na kuwa anauakika ni yeye kabisa, Masud akatoa simu yake toka mfukoni na kupiga kituoni, akiagiza waje askari wakutosha kwa ajili ya kumkamata muuwaji, akiamini ndiye anayetafutwa na insp Johnson David, toka kituo kikuu cha polisi, baada ya kupiga simu walibaki wakijadirina namna ya kwenda kumwonyesha huyo muuwaji, ili ibakie kumkamata tu!, mala polisi wengine wakija eneo lile, kiukweli Jackline alikuwa atuwa chache sana toka waliposimama Masud na yule dada, aliwasikiliza wakipanga mikakati yao, hapo Jackline akajuwa kuwa endepo ata chelewa, lazima mambo yatazidi kuaribika, maana huyu mwanamke ndie pekee aliewai kumwona uso kwa uso, hapo Jackline Michael Nyati aka jipapasa kiunoni tayari kutoa zana za kazi, lakini akakumbuka kuwa siku ile akutembea na silaha, sababu akuwai kufikilia laka kuna kitu kama hiki kitatokea, Jackline akainama kidogo na kupapasa kisigino cha kiatu chake, akakuta kisigiono hicho chini kipo bapa (flat), akikuchongoka vile anavyo taka, hivyo kisingefaha kwenye kazi yake, muda una zidi kwenda, Jackline aka zidi kutazama chini sehemu inayo mzunguka, akaona kuna chupa ya bia iliyo vunjika, aka inama na kuchagua kipande cha chupa ambacho kingemfaha, wakati huo Masud na yule dada mhudumu, walisha afikia makubaliano ya kurudi ndani, ili akamwonyeshe alipo kaa muuwaji, lakini basi ilewana geuka tu! ghafla kama upepo, yule polisi alimshuhudia mwanamke mmoja mrembo, aliye pendeza kweli kweli, akiwa amewatokea mbele yao na kuupeleka mkono wake shingoni kwa yule dada muhudumu wa vyumba, hapo alimshuhudia yule muhudumu akishikilia shingo sehemu ya koo, huku akiyumba yumba kama mrevi, na damu zina churuzika nakupenya kwenye vidole vya yule dada, na kumwagika kama maji kwenye bomba lililo toboka, polisi Masud kuona hivyo akajuwa kumbe muuwaji yupo mbele yake, Masoud akarusha ngumi kali sana kumlenga yule mrembo muuwaji, ambayo ilipita bule, na kumfanya Masoud ayumbe kidogo kutokana na nguvu aliyoitumia kurusha ngumi ile, kuwa kubwa sana, ile anataka kukaa sawa alikutana na kitu chenye ncha kali, kikizama shingoni kwake na kwenda kukita kwenye koo lake, na yeye akashikiria shingoni, na kuanza kuyumba yumba, kabla ya kujibwaga chini kama mwenzake, kisha kuaza kukukuluka kama kuku alie ponyoka kwa mchinjaji, **** Huku ndani ya bar Denis pombe ilisha mkolea kichwani, mawazo yake sasa yalikuwa ni juu ya Jackline, atamaliziaje kumlainisha mdada huyu, ili awe demu wake, maana aliona kuna dalili kubwa ya mgeni wake kuelewa somo, wakati anawaza hayo, mala akamwona Jackline anarudi toka chooni, mikono yake ina dalili ya kulowa maji, lakini Jackine safari hii hakukaa kwenye kiti chake, “vipi hukai nimelizie bia” aliuliza Denis huku akiinua chupa yake ya bia nakuiweka mdomoni, Jackline akiwa bado amesimama akamwambia Denis, kuwa tumbo bado lina msumbua, hivyo anaomba amrudishe nyumbani haraka sana, Ilikuwa saa tatu kasoro za usiku ndipo Denis na Jackline walipo ondoka Full dose pub, baada ya kununua bia za kopo na soda za cola, kisha waka elekea nje ya pub, wakati wanatoka wakapishana na vijana watatu wakiingia ndani ya pub, mmoja kati ya wale vijana watatu, alisimama na kumwangalia sana Jackline, adi alipo ingia kwenye gari, hakujuwa ni kwanini, lakini kuna kitu kilimvuta juu ya Jackline, ambacho kilimpelekea kujaribu kuzishika namba za lile gari, Jackline hakuwa makini na yule jamaa, mawazo yake yalikuwa ni kuondoka haraka mahali pale, kabla polisi waliopigiwa simu awaja fika, Denis akaondowa gari taratibu akiifwata barabara kuu ya morogoro, wakati wanaingia barabara kuu waka shuhudia gari la polisi, defender likiingia kwa mwendo wa zima moto, huku polisi wengi wakiwa wananing’inia juu yake, huku mikononi wakiwa silaha zao aina ya smg, wa mwela wanaita sub machine gun, Jackline kwa kutumia side mirror aliweza kuliona defender liki simama nje ya full dose pub, na wao waka shika njia na kuondoka eneo lile, ***** huku ndani ya Full dose Pub, wale vijana watatu walipo ingia ndani ya bar, wakachagua meza moja nakukaa, walikaa sehemu waliyo toka wakina Denis, maana ata baadhi ya vinywaji vyao viikuwa bado mezani, yule kijana mmoja alionekana bado anamawazo juu ya alichho kiona wakati wanaingia, kama aliekumbuka jambo flani, akatowa karatasi mfukoni mwake, lenye picha ya Jackline na kuitazama, akasibitisha kuwa, yule aliemuona wakati anaingia, ni yeye mwenyewe, akawaambia wenzake, “jamani huyu demu tumepishana nae mlangoni,” kwanza wenzake walishangaa kidogo, kisha wakamcheka sana, wakiamini kuwa, mwenzao anamawenge, japo kijana yule alisisitiza sana juu ya alicho kisema, lakini walizidi kumcheka, wakati huo huo waka shangaa polisi wanaingia mle ndani na kutowa amri kwamba hakuna mtu kutoka nje ya bar, wala kunyanyuka pale alipokaa, waka ambiwa sababu kuwa hapo nje kuna mauwaji yametokea, polisi mmoja na raia mwema wameuwawa, wote waka duwaa, ata wale vijana watatu nao waka shangaa, walizid kushangaa zaidi baada ya muda mfupi, walipo gunduwa kuwa, yule waliokuja kumtafuta, naye ameuwawa, ***** Denis na Jackline walifika nyumbani salama, wakaingia ndani, Jackline akajifanya kupitiliza chooni na Denis akabaki sebleni anakunywa bia, Jackline kule chooni (choo cha chumbani, alikolala jana na mwenyeji wake) akukaa sana, akatoka na kurudi sebleni, ambako alimkuta mwenyeji wake ana piga mtungi taratibu, akakaa kwenye kochi sambamba na Denis, “vipi tumbo limepoa?” aliuliza Denis, sasa kwa sauti ya kilevi zaidi, “ndiyo limepoa” alijibu Jackline kisha akaongezea swali “hivi Denis mbona hujaoa?” Denis akastuka kama ametajiwa kitu cha ajabu, kiasi cha kusababisha Jackline aanze kucheka, “weeee! tena wewe sijuwi umenipa dawa ya wapi, mpaka najikuta nakupenda hivi,” alisema Denis akimalizia kwa kuutetemesha mwili wake, kama mtu alie sisimukwa kwa kuona kitu cha kusisimua, au kumwagiwa maji ya baridi, au kunywa juice ya ndimu, “kwa nini, au unawachukia wanawake?” aliuliza Jackline, na Denis akamsimulia ile story yake ya binti wa mzee Mapande muuza bucha, mpaka anamaliza Jackline alikuwa amecheka sana, ghafla Denis akainuka na kuelekea chumbani, akimwacha Jackline sebuleni, dakika zika pita pasipo Denis kurudi Jackline kajiwazia pengine mwenyeji wake tayari ameshaenda kulala, akainuka nakuingia chumbani, akumwona kitandani mwenyeji wake, Jackline akaangalia upande wabafuni, ambako alikuwa anasikia maji yana mwagika kutoka kwenye bomba la juu, akajkuta anashikwa na mshangao wa mwaka, akaduwaa, macho yakamtoka, akajaribu kukwepesha macho yake, na kutazama pembeni, lakini moyo wake ukamshawishi kutazama tena, akaangalia tena kule bafuni, kweli aliweza kumwona mwenyeji wake akiwa bafuni, alikuwa uchi kabisaaaaaa!, anaoga, Jackline aliweza kuona kila kitu kwa uwazi kabisa, aliweza kuona dudu ya Denis ikiwa ime simeme vyema, ikidondokewa maji ya bomba la mvua, kiukweli katika maisha yake Jackline, akuwai kushuhudia dudu live, ikiwa katika hali kama hiyo, aliangalia kwa sekunde kadhaa huu akiona mabadiliko flani kwenye mwili wake, ghafla akainuka na kurudi sebleni, pasipo Denis kumwona, Jackline alikaa sana pale sebleni baada ya dakika kumi, akamwona Denis akiingia pale sebleni akiwa amevalia bukata nyepesi, licha ya kuoga lakini alionekana wazi kuwa bado pombe ime mzidia, muda wote macho ya Jackline yali tazama sehemu ya mbele ya bukta ya Denis, lakini sasa hivi aliona dudu ikiwa imejichora kwa mlalo, ndani ya bukta, ikionyesha aija simama, kama ilivyo kuwa bafuni, lakini ilionekana kutuna kwenye bukta nyepesi ya Denis, ambaye akuwa anajuwa lolote, linalo wazwa na mgeni wake, na sasa alikuwa amekamata kopo la bia na kuanza kuigugumia, kabla ya kulishisha na kumtazama mgeni wake “lete story Jack, unasema baba na mama wapo songea?” Jackline alistuliwa na sauti ya Denis, akiondoa macho yake kwenye usawa wa dudu ya Denis, “ndiyo! tena si’umesema kesho utapatia ela nikawatumie?” aliongea Jackline akijuwa fika kuwa, wazazi wake awaitaji fedha yoyote, tena wanauwezo mkubwa kifedha, “tena umenikumbusha, dah! nilisha sahau,” waliongea mengi sana huku Denis akiendelea kunywa pombe, na Jackline aliendelea kuwaza juu ya mwanamume huyu, na jinsi alivyo mchungulia kule bafuni, alianza kuhisi kutamani kitu flani, **** kule Full dose baada ya polisi kushindwa kupata chochote walitowa taharifa kituo kikuu, moja kwa moja ikamfikia insp Johnson David Masinde, naye akaamrisha vijana wake kumi, kuingia kwenye magari na kuelekea mbezi, **** saa tano za usiku, Denis alikuwa amelala fofofo kitandani, kazidiwa na pombe, anakorma ajitambui kabisa, “ngoja kesho nita muuliza kwanini anapenda sana pombe” aliwaza Jackline ambae alikuwa amesimama pembeni ya kitanda, akimtazama Denis pale kitandani, akaona jonjisi alivyo lala, bila kujifunka shuka, huku dudu ikionekana kusimama sana, na kukinyanyuwa kile kibukta chepesi, Jackline alitazama kwa sekunde kadhaa kisha akatoka nje ya chumba nakuelekea seuleni, huku simu yake ikiwa mkononi, alipofika sebuleni akampigia simu baba yake, ambae alimweleza kilicho mtokea kule mbezi Full dese pub, na kulazimika kupoteza maisha ya watu wawili, “ok! umefanya vizuri, maana unge ondoka bila kufanya hivyo, huo mwanamke angekuwa tatizo kwako, sasa jitahidi kuwa mkini, na kubadiri mwonekano wako mala kwa mala unapo kuwa umetoka nje ya nyumba hiyo, pia uwe makini na huyo mnweji wako, asijuwe lolote juu ya mambo yetu” alisisitiza mzee Nyati, kabla ya kumaliza maongezi na kukata simu, hapo Jackline akarudi chumbani na kusimama tena pale ale alipo kuwa amesimama mwanzo, akamtazama tena Denis ambae alikuwa amezidi kutopea kwenye usingizi, akaitazama dudu, akaiona bado ime simama vile vile, hapo akatabasamu kidogo, huku ana peleka mkono wake kwenye usawa wa kitumbua chake, ambacho kilikuwa ndani ya suluwali yake ya jinsi, Jackline alipanga kujaribu kufanya jambo flani, kwa kumtumia mwenyeji wake Denis, Jackline akausogeza mkono wake kwenye shavu la Denis, kisha akajaribu kumfinya, akaona ametulia anaendelea kukoroma, huku mapigo yake ya moyo yakimwenda kasi, Jackline akaulaza mkono wake juu ya dudu ya Denis, ikiwa bado ndani ya nguo, akauchezesha kidogo mkono wake, akaiona inazidi kusimama, akautoa mkono wake haraka, akamtazama Denis usoni akamwona bado amelala fofofo, Jackline akatabasamu huku anajilamba midomo, Jackline huku akimtazama Denis usoni akaikamata bukta ya Denis na kuishusha taratibu, adi alipoiona dudu ya mwenyeji wake, ipo nje kabisa ya kibukta, ITAENDELEA...

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)