DADA MDUNGUAJI EPISODE 13

Emmanuel Lee
By -
0

DADA MDUNGUAJI


EPISODE 13


STORY NA Mbogo Edgar


ILIPOISHIA EPISODE 12 : wakati huo mzee Nyati alikuwa sebuleni kwake ndipo alipo sikia habari ya hivi punde, ikionyesha tukio lililo tokea paradise tower, ya muuwaji wakike kukimbia polisi, “mh! mambo magumu” alisema mzee Nyati kwa kunong’ona, kisha akasema “mama Jack, jiandae na safari ya dar es salaam, leo hii” endelea.......

 Kuli hiyo ya baba Jack, ilimstua sana mama Jack, ambae ambae alikuwa ndani kipindi hicho, “kuna nini baba Jack, au Jack amepatwa na tatizo?” aliuliza mama huyu, huku akiingia pale sebuleni, akitokea jikoni, akamwona mue wake akiwa ameelekeza macho kwenye Tv, huku pad yake ikiwa mezani, “Jack huyo?” aliuliza mke wa bwana Nyati, na yeye akitazama TV, ambayo ilionyesha tuko lililo malizika pale hotelini, na mtangazaji akielezea juwa muuwaji amefanikiwa kukimbia na gari la polisi, japo polisi walikuwa wana mkimbiza kwa magari yao, “masikini mwanangu, safari hii atafanikiwa kuwakimbia kweli?” aliuliza mama Jackline, hukusauti yake ikiingiwa na wasiwasi, mzee Nyati akujibu kitu zaidi alitazama pad na kuona kuwa ile tracking ya Jackline ikielekea tambaa na mandera load, ikielekea upande wa buguruni, hapo akachukuwa simu yake Haraka sana kumpigia Jackline, akionyesha kustuka juu ya jambo flani, “sijuwi kama atapokea..” aliwaza mzee Nyati na wakati huo huo, simu ikapokelewa, “ndio baba” ilisikika sauti ya Jackline sambamba na sauti za magari zilizo zidiwa na ving’ora vya polisi, “sikia Jackline, fwata maelekezo yangu, kama unaendelea kutumia gari basi fwata barabara mliyopita jana, ile ya kinyerezi, ukinyoosha tu umekamtwa,” alieleza mzee Nyati, **** insp Johnson akiwa nyuma kabisa yam bio hizi za magari yapolisi, huku magari ya kiraia yakiwa yame kaa pembeni, pasipo kujuwa lile lambele kabisa ni la mwalifu, insp aliyaona magari ya polisi mita mia mbili mbele yake, huku barabara ikiwa nyeupe magari yapo pembeni, insp huku anaendelea kuwasiliana na makao makuu aliomba askari zaidi, na mbwa maalumu wa polisi, wanao tumika kufwatilia waalifu, wawa fat kule watakapokuwa wanaelekea, wakati huo huo insp kwambali akashuhudia gari la polisi lililo kuwa mbele kabisa na kuyahacha mengine kwa mita kama mia tatu, likichepuka kwa ghafla njia ya tabata, pasipo kusubiri taa zimruhusu, na kusabisha magari yaliyo kuwa yanatokea buguruni, ya pate misukko suko ya kuchuna black za ghfla na yale ya nyuma yaki yagonga yambele, hapo magari ya polisi yakaonekana yaki jipenyeza na kupita sehemu ile, kisha yakaendelea kulifuuza gari analoliendesha Jackline ambalo lilizidi kuwaacha, lakini nao wakiwa wanatembea kwa ukaribu zaidi, magari kumi na saba ya polisi, yalitimua mbio kwa speed ya hajabu kulifukuzia garri hilo linaloendeshwa na Jackline Michael Nyati, huku askari wakionekana kujaa kwenye magari hayo, na silaha zao, wananchi wali shangilia kila walipokuwa wanapita, lakini mpaka wana maliza barabara ya lami, yani kinyerzi mwisho, awakuweza kumwona Jackline wala gari, walipo ulizia kwa wananchi wakaambiwa kuwa ame endelea na barabara ya malamba mawili, inayotokea mbezi, hapo mala moja wakapiga simu kituo cha polisi mbezi, wazuwie barabara hiyo, na wao wakaanza kutimua mbio kufwata barabara hiyo, lakini walipo fika malamba mawili, wakaambiwa kuwa gari lapolisi limeiacha barabara ya mbezi na kuelekea barabara ya mashambani ambayo uelekea mkoa wapwani, maeneo ya kisopwa juu, nao bila kuchelewa waka fwata njia hiyo ambayo ilikuwa baya sana, kutokana na mashimo mengi sana katika njia hiyo, bahati ikawa upande wao, ni baada yay a kutembea kidogo, walianza kuona vumbi kwa mbali, na walipo tazama vizuri waka gundua ni gari lao alilo liiba mwanamke muuwaji lilikuwa lina zidi kuchochora, Johnson akaamlisha madereva waongeze speed, na sasa walikuwa wamesha ziacha nyumba za wananchi, na kuingia kwenye mapoli na vichaka, kagiza kalikuwa kamesha anza, magari yakawasha taa, lakini gari la mbele ambalo lilkuwa na Jckline awakuliona wala wanga wake, mala ghafla wakakuta gari la polisi, lililo chukuliwa na yule mwanamke, likiwa lime simama barabara, nakuziba kabisa ile njia, hapo waka simama kwa umbari wa mita kama hamthini hivi, haraka saba askari wakashuka mala moja, wakiwa na silaha zao mikononi, wengine waka kaa kiulinzi waki tazama pande zote za barabara, huku askari kama kumi hivi wakianza kulisogelea lile gari, kwa mwendo wa taadhari, wakionyeshana ishara ya kuwa waangalifu, walitembea taratibu wakiritazama lie gari kwa umakini sana, wakiakikisha kama kunamtu ndani ya gari hili, lakini mpaka wanafika pale awakuona mtu wala kitu chochote kinachiashilia kuwepo mtu, “akuna mtu afande” alisema mmoja kati ya askari wale, walio enda kulikagua lile gari, lakini wakati anayaongea hayo waka ona kitu kama flash (mwanga mkali) ukipasua giza lililo tanda na kuishia kwenye uawa wa tank la mafuta, hapo ikafwatia mlipuko mkubwa sana, wakina Johnson wali shuhudia lile gari liki rushwa juu likiwa lina waka moto mkubwa sana, ulio sababisha kusambaa kwa vipande vya vyuma vyenye moto, vilivyo warukia wale askari kumi na kuwa potezea maisha yao, katika maumivu makubwa sana, maana ukiachilia wengine walio chomwa na vyuma na kufa mala moja, kuna wale ambao moto ulio cha nganyika na mafuta, uliwarukia na kushika kwenye miili yao, hivyo wakaanza kuungua huku waipiga kelele, wakina Johnson awakuwa na uwezo wa kuwasaidia wenzao, ambao wali poteza maisha mbele yao, zaidi Johnson ali towa amri ya askari kufwata uelekeo ulio tokea risasi, yani ule mwanga ulio toboa tank lamafuta, hapo askari wakazagaa poli lote, huku insp Johnson akipiga simu kituo cha polisi mbezi, pamoja na kikosi cha askari wa mbwa wazungukie upande wa kibamba na kuanza kusaka pori lote kuanzia ruguluni na kibamba ccm, wakija upande walipo wao, yani kisopwa, ili wakutane kati kati, wakiamini kuwa watamweka kati Jackline, na wao wakina insp waka amrisha magari ya zungukie upande wa mbezi na kutokea kibamba, iliwao wakakutane nayo kwenye barabara ya kisopwa, kwenye barabara inayo tokea kibamba, magari yakaondoka huku gari moja likiwabeba askari walio lipukiwa na gari, ambao sasa walikuwa wamesha poteza maisha,  wakati huo huo, insp akapokea simu, toka kwa koplo Mashiba, simu ambayo ilimpa matumaini insp Johnson, taalifa iliyo mjulisha kuwa baba yake mzee Masinde licha ya kujeruhiwa vibaya sana, lakini bado mzima, na madoctor wanaendelea kumpatia matibabu, japo kwa sasa likuwa bado amepoteza fahamu, insp akaagiza ulinzi imara hospitalini hapo, asa chumba alicho lazwa mzee Masinde, ambae polisi bado awakufahamu kuwa ni baba mzazi wa insp Johnson, ***** kibamba njia panda ya shule Denis alikuwa nyumbani kwake na mwanae France wanamsubiri mama Fance, ambae alitoka mchana akielekea saloon kusuka nywele, lakini mpaka saa mbili kasoro, akumwona mke wake, kiukweli mke wake akuwa na tabia ya kutoka nje ya penzi lao, na wala akuwai kuonyesha dariri ya kufanya hivyo, “sasa inakuwaje?” aliwaza Denis ambae aliamua kuweka filamu yakivita kwenye TV, nakuanza kutazama akisaidiana na mwanae France, huku akichukuwa pombe na kuanza kuifakamia, maana kiukweli akuelewa hii tabia ya mke wake imeanza lini, “unajuwa kama mwanake ujamlamba ata makofi machache, awezi kukuheshimu” aliwaza Denis akiendelea kugugumia pombe yake, Farance, akimshangaa baba yake,***** kumbe wakati huo Jackline ndio kwanza alikuwa katikati ya msitu akitafuta njia ya kutokea kwenye barabara ambayo anaifahamu,ni barabara ya kisopwa, barabara aliyowai kufanyia mauwaji mala mbili, akiamini kuwa endapo ataipata barabara hiyo, basi atakuwa ameshafika nyumbani kwake, simu yake alikuwa ameshaizima, kutokana na kwamba akutaka polisi waone mwanga wasimu hiyo, pindi atakapo pigiwa, pia akutaka kupokea simu ya mume wake Denis, sababu akuwa na jibu la kumpa mume wake, endapo angempigia na kumwuliza yupo wapi mida hiyo, Jackline Nyati baada ya kulilipua gari kwa kutumia bunduki yake ya kudungulia, ambayo aliifungua na kuiweka kwenye begi, ikiwa vipande vipande, akaendelea na safari yake huku akikimbia kwa speed kari sana, huku smg yake aliyo ichukuwa pale hitelini, baada ya kuuwa polisi, Jackline alikimbia kwamwendo wa lisaa lizima, huku kwambali akisikia kelele za polisi, zikija nyuma yake, wakati Jackline akitokea bara bara ya kisopwa, Ghafla aka liona kundi la polisi kumi na tano wenye tochi mikononi mwao, na mbwa wakubwa wanao bweka kiukari sana, “mama yangu, kwanini sikufikilia mapema juu ya hili” alijiuliza Jackine, huku akiwasimama na kuwa tazama wale polisi wakiwaachia mbwa wao, nakuanza kumfwata kwaspeed, Jckline akapachika SMG yake begani, na kuchomoa bastola yake, aliyo ikamata mkono wa kushoto, na mkoni wa kulia akashika kisu, **** plisi wakikosi cha mbwa mbao waliokuwa na tochi mkononi mwao, wakiamini kuwa wamesha mtia nguvuni, waliwatazama mbwa wao, wakimfikia yule mwanamke, na kuanza kumshambulia, lakini kilicho tokea, awakuwai kuelezwa katika mafunzo yao, kama inaweza kutokea jambo kama hili wanalo liona kwamacho yao mida hii, kwani walimwona yule mwanamke akitummia kisu chake na bastola yake kupambana na mbwa kumi natano , na ndani ya dakika moja, mbwa wote walikuwa wame lala chini, huku wakiwa na majelaha makubwa yakisu, au matundu ya risasi, polisi wakiwa na tahamaki kwakilicho tokea, wakastuka mwanamke yule, ambae walizani kuwa ni jini au mzimu, akiingeuza SMG yake toka begani na kuanza kuwa miminia huku aki sort kurudi kichakani, mpaka anasimama yari askari kumi natano walikuwa wamepoteza maisha, “huuuu! poleni mashujaa!” alisema Jackline huku akikatiza miili ya Askari wale na kuondoka zake, atuwa chache mbele akaona taa za magari mengi sana, yakija mbele yake, akazama polini, maana muungurumo wa magari hayo ulimjulisha kuwa ni wa magari ya polisi, ni kweli, Jackline akiwa amejificha kwenye kichaka, pembeni ya barabara, dakika mbili baadae akayaona magari kumi na tani ya polisi, yaki katiza mbele yake, likiwa limepungua moja, lililo wapeleka wale marehemu hospital ya muhimbili, hapo Jackline akayatazama mpaka alipo akikisha yame potea akaanza kutimua mbio kuelekea kibamba chama, akitumia pori kwa pori, ***** insp Johnson akiwa na askari wake zaidi ya mia na arobaini, walisikia sauti za mbwa wakibweka kwanguvu, wakionyesha kuona kitu na kutaka kushambulia, lakini sekunde chache, wakaanza kusikia milio ya mbwa hao ikibadirika, na kuwa ile ya maumivu na kushambbuliwa, huku kwambali wakiona tochi nyingi sana, mala sauti za mbwa zika koma, na ikafwatia milio mfululizo ya risasi, kwa sekunde chache, kisha kimya, tuukio hili waliliona na kilisikia likitokea mbleyao kwa umbari wakama kilomita moja, toka pale walipo “munguwangu, ebu tuwai jamani, anawamaliza askari huyu shetani” alipiga kelele insp Johnson, na askari wakaanza kukimbia kuelekea kule waliko iona mianga yatochi, walitumia dakika kumi kufika eneo latukio, wakakuta magari yao yameshafika kwenye eneo lile, huku taa za magari yao, zikimulika miili ya mbwa wa kipolisi na askari wao, hapo insp Johnson akachuchumaa chini, huku akionekana kuchoka, na kwa askari waliokuwa jirani yake, walimwona akifuta machozi machoni mwake, “haaaa! sijuwi kwanini wazee awa walimchokoza huyu shetani?” ilisikika sauti ya insp, iliyo ambatana na simanzi ya kilio cha uchungu, insp akiwa amechuchumaa pale chini, akitulia kwa dakika kadhaa, kichwani mwake akijaribu kuwaza namna ya kumpata Jackline Nyati, akakumbuka kuwa eneo lile mwanamke huyu, alisha wai kufanyanyia matukio kadhaa, hapo likamjia wazo, “ kibamba njia panda, kupitia luguruni” allikurupuka insp Johnson ambae alikumbuka maelezo ya marehemu Busungu, kuwa mwanamke huyu anatokea njiapanda ya shule, na pia yalisha tokea matukio jadhaa eneo hilo la kibamba njia panda, “pandeni kwenye magari haraka sana mimi nitaongoza” alisema insp huku anakimbilia kwenye gari la nyuma kabisa, akaingia kwenye gari huku askari wakigawana magari na kuingia harakasana, kisha magari yaka yakageuka alikotoka nakuanza safari, huku gari alilopanda insi Johnson likiwa mbele, **** wakati huo Jackline Nyati, aliekuwa anakimbia pembeni ya barabara, kwenye vichaka, alikuwa anapita usawa wa bwawa la kisopwa, wakati anapanda mwinuko wa eneo hilo, akaona mianga ya magari yapolisi, ikija tokea nyuma yake, hapo Jackline akajificha na kusubiri yapite, lakini akayaona yaki katisha kulia na kuelekea upande wa barabara inayo elekea luguruni, hapo Jackline akatabasamu, “wamepotea” aliwaza Jackline na kuendelea na safari yake, akijitaidi kukimbia ili kumwai mume wake akipanga endapo atawai maduka ya kibamba anunue nguo yoyote ili kumzuga mume wake, sababu wakati anaondoka pale numbani, alikuwa amevaa gauni jekundu, na viatu vyeupe vya mchuchumio, ***** saa tatu usiku, kituo kikuu cha jeshi la polisi, ndani ya ofisi ya mkuu wa jeshi hilo, walionekana makanda wanadhimu wa jeshi hilo, wakiwa wame kaa wakiizunguka meza kubwa, wakiwa wametulia kwenye viti vyao, redio call ikiwa kati kati ya meza hiyo, wakiendelea kusikiliza taalifa za kimawasiliano ya kikundi kizima kilicho kwenda kumsaka muuwaji anesemekana ni wakike, Jcklne Michael Nyati, makamanda awa waliokuwa wanaongozwa na CGP, yani Chief General polisi, mwenyewe, walikuwa wamekutana toka saa kumi, baada ya kuona tukio la Pradise Tower, sasa wote walikuwa kimya wameinamisha vichwa chini, mioyo yaom ikiwa ime jawa na wasi wasi na hofu kubwa, maana walisikia jinsi vifo vingi vya askari vilivyokuwa vina endelea kutokea, wakiwemo mbwa wao waliokuwa wanategemea kwa kufwatilia nyayo za waalifu, chumba kili kuwa kimya, ni redio peke yake ndiyo iliyo sikika, na sasa waliwasikia askari wao waliokuwa wakilizunguka eneo la kibamba, na kupanga kuwa tukio la sasa liwe la kuvizia sana, **** Jackline Michael Nyati sasa alikuwa ameshafika kibamba chama, tayari alikukuwa amesha itupa hile smg, aliyoipora kwa polisi, akachukuwa mkebe mwingine wa risasi, na kuupachika kwenye bastora yake, moder 88 5.5 mm, na kuirudisha nyuma ya kiuno chake, usawa wa mfereji, ulio yagawa makalio yake, kisha akaingia ndani ya duka moja kubwa languo na viatu, na kununua gauni moja jekundu na viatu vyeupe vya mchuchumio, kwanza alitaka abadirishie hapo hapo, lakini nikama roho yake ilisita, ni baada ya kumwona kijana muuza duka, akimshangaa sana kwa jinsi alivyo kuwa amechafuka damu sehemu kubwa ya nguo zake, mpaka usoni, maana kazi ya mwisho ya mbwa ilikuwa siyo mchezo, Jackline akaondoka haraka sehemu hiyo, na kuelekea njia panda ya shule, ambako alipanga akatafute chochoro moja nakubadiri nguo zake, baada ya kuipita stendi ya daladala na pikipiki, nakutembea atuwa kama miambili, akaanza kuingia sehemu yenyenyumba chache na kufanya eneo hilo kuwa lenye giza kidogo, hapo Jackline akaanza kuangalia sehemu ambayo inge maidia kubadiri nguo zake, akaona sehemu moja iliyoonyesha kuwa inatumika kama kiwanda cha mbao, hapo akaona kuwa ndio sehemu anayoweza kubadiriisha nguo, aka piga atuwa kadhaa kuifwata ile sehemu yenye giza, iliyo tapakaa mizigo ya mbao, lakini Jackline aliyekuwa ameshika mfuko wa plastic, akasimama ghafla, na kutazama kwa umakini mahali pale, huku anapeleka mkono wake kwenye kiuno  chake, usawa wa mferji uliogawa makalio yake makubwa, na kuikamata bastora yake aina ya Mic galilry moder 88, 5.5 mm, “tulia hivyo hivyo Jackline Nyati,” ilisikika sauti ya insp Johnson toka nyuma ya Jackline Nyati, hapo Jackline akatulia vile vile, akitazama kule aliko kuwa anatazama mwanzo, yani kwenye mbao, akawaona askari wawili wapolisi wakichomoka toka mafichoni, nyuma ya mbao zilizo kuwa zime pangwa mafungu mafungu, wakiwa na silaha zao mikononi, “geuka nyuma mshenzi wewe” ilikuwa ni sauti ya insp Johnson iliyo tawaliwa na ukari na hasira ya hali yajuu, Jackline akageuka, naam hapo akajikuta akitabasamu, alikuwa amesimama mbele ya kundi kubwa la askari, qaliokuwa wamemwelekezea silaha zao za kivita, huku wengine wakiongea na redio call kutoa taalifa kwa wakuu wa vituo vyao, wakidai kuwa wamesha kamata Jackline Nyati, ***** mpaka hapo ndani ya chumba cha kuongea na mahabusu, Denis alimtazama mke wake, huku akishusha pumzi ndefu, ya kuchoshwa na mzigo, “kwahiyo ulifikaje nyumbani, wakati pale njiani walikuwa wamesha kuzunguka?” aliuliza Denis akimtazama mke wake alie kuwa anatazamana nae, “mh! nazani umesha sikia mengi ya kutisha, juu yangu, sina shaka kuwa auta ogopa nikikusimulia kilicho tokea,


 Denis akaitikia kwakichwa huku akiachia tabasamu lililo onyesha wazi kuwa alikuwa katika wakati mgumu, ambao Jackline akujuwa ni wanini, hapo Jackline Michael Nyati akaendelea kumsimulia mume wake, juu ya kilichotokea usiku wa jana yake, pale kwenye sehemu ya kuuzia mbao, “nilikuwa nilijuwa nimesha fiia mwisho, sababu nilihisi polisi wanapajuwa nyumbani, ndio maana waliweza kuja na kujificha maeneo yale” alisema Jackline wakati anaanza kumsimulia Denis kilicho tokea, “hivyo sikutaka kukuingiza kwenye matatizo, wewe na mtoto,” Jackline akaweka kituo kidogo, akimtazama Denis usoni, baada ya insp Johnson kuongea maneno yake, na mimi kuwa nimesha wageukia, wale polisi wengi nikiwaacha wawili nyuma yangu, nikawaona pia polisi wengine wakitokea kwenye chochoro zenye giza, hapo nikapaza sauti kumwambia insp Johnson, ***** “hongera insp kwakuni kamata, lakini naombi moja, familia yangu aiusiki, wala kujuwa chochote, kama wewe usivyo usika, wala kujuwa aliyo yatenda baba yako” baadhi ya polisi walikuwa wanayasikia maneno haya kwa mala yapili, yani wakimsikia mwanamke huyu akionyesha kuwa anamfahamu mkubwa wao, washangaa sana, huku polisi wote wakigeuza shingo zao na kumtazama insp Johnson, wakitafakari maneno ya mwanamke muuwaji alie simama mbele yao, “inamaana insp anausika nahili?” ndvyo kila mmoja alivyo jiuliza, insp aliliona hilo, akakumbuka kosa alilo lifanya kule paradise Hotel wakati Jackline alipo kuwa amemshikilia Pc Ngaga, kabla ya kutokea kwenye kioo, hapo insp akainua bastora yake akimwonyeshea Jackline, ambae alihisi mda wowote atafanya ujanja, “kimya we Malaya, weka chini kla ulichonacho” aliongea kwa hasira insp, hapo Jackline akatabasamu, huku akiinuwa juu mfuko wa Rambo wenye nguo mpya na viatu, huku mkono wake wa kulia ukiwa bado umshika bastora nyuma ya kiuno chake, begi jeusi likuwa bado begani, “unamaanisha ilibomu” aliongea Jackline huku akiurusha mbele ule mfuko wa Rambo, mbele ya askari, nikama alivyo tarajia, askari walitawanyika kwa uoga, akiwepo insp mwenyewe, ambae seunde chache baadae akakumbuka kuwa alisikia akipewa report kuwa Jackline alikuwa dukani ananunua nguo, insp akagunduwa kosa, akainua uso wake na kumtazama Jackline, ambae alikuwa anageuka kwa speed ya haraka sana, huku akichomoa bastora yake, na kuji rusha pembeni upande wa sehemu ya kuuzia mbao, akijivilingisha kwa sarakasi, huku miali ya moto, pasipo sauti yoyote ikisikika, ili penya kwenye vichwa vya askari wawili walio kuwa nyuma ya mwanamke huyu harari, kisha kudondoka kama mizigo, “shambuliaaaaaa” alipiga kelele insp Johnson huku yeye akianza kupiga risasi kuelekea pale kibandani, ikifwatia milipuko mingi sana ya risasi za SMG bastora na uzi gun, huku mili mikali ya moto ikipiga kwenye ile sehemu ya kuuzia mbao, na kupasua pasua mbao za mwanachi, zinazo msaidia kama kitega uchumi, shambulizi hilo lilitumia dakika nzima, lakini akukuwa na dalili ya uwepo wa mtu eneo lile, “simamisha mapigooooo” alisema insp Johnson akirudia rudia, huku akisaidiwa na masajenti na makoplo aliokuwa nao, wakafanikiwa kusimamisha mapigo, hapo insp akajuwa akichelewa amesha mpoteza mwanamke huyu, kaamua bola askari watawanyike na kuanza kumfwata lia yule mwanamke, nikweli kwa msaada wa tochi zao, walizo zichukuwa kwa maremu askari wa mbwa, wakaanza kufwatilia nyayo za buti za mwanamke huyu, huku magari yakipita barabarani ***** wanadhimu wakuu wajeshi lapolisi, waliokuwa pamoja na mkuu wajesho hilo, ndani ya ofisi yake, pale kituo kikuu cha polisi, walisismuliwa na jinsi tukio lilivyo kuwa linatokea huko kibamba njia panda ya shule, “hapana huyo awezi kuwa mwanamke, lazima apatikane akiwa mzima” aliongea CGP, hapo hapo msaidizi wake akaichukuwa ile redio call iliyo kuwa mezani wakiitumia kupata habari, akaanza kuita, huku akibonyeza kitufe flani pembeni ya simu, “hallow sierra bravo, kutoka charle Gorf kunaujumbe, over” hapo mala moja upande wapili ukajibu, “charle Gorf, tuma over” kisha maongezi yaka endelea, yakimtaka insp Johnson kuakikisha huyo mwanamke hatari anakamatwa na kufikishwa makao makuu, akiwa mzima kabisa, ni kweli kila mmoja mle ndani ya ofisi, alipata hamu ya kumwona huyo mwanamke hatari, mwenye uwezo wakimapigano, mfano wa askari commando, aliefuzu vyema mafunzo ya kijeshi, katika ngazi ya juu sana, (master level) tena kwenye chuo hatari na kikubwa cha kijeshi, chenye wakufunzi wenye uwezo mkubwa sana, maana awakuamini kuwa ni mwanamke kweli, ***** insp alipo ipokea taarifa ya kuto muuwa mschana huyo hatari, aliona wanazidi kumwongezea mzigo, wakazi maana kumuuwa tu ilikuwa ni kazi ngumu, itakuwaje kumkata akiwa mzima, lakini chi ya kuwaza hayo insp aliendelea kuongoza askari wake kumkimbiza Jackline Nyati wakifwata nyayo za buti zake, ambazo kuna wakati walizi poteza na kuzipata tena, kitu kingine ambacho insp alianza kukiona kuwa ni kigumu, ni kwamba endapo Jackline Nyati atakamatwa, akiwa hai, basi kama baba yake alifanya uovu, kwa mzee Nyati wakiwa congo, unge bainika na kusababisha matatizo mengine kwa mzee huyo, ambae kupona kwake, ni kwa huruma ya mungu, kutokana na hari aliyo kuwa nayo, polisi waliendelea ufwatilia nyayo za Jackline Michael Nyati, zilizo kuwa zina zidi kuchochora kuelekea upande wajuu, wa mtaa huu wa kibamba njia panda ya shule, ikivuka shule ya msingi na kuzidi kuelekea ndani zaidi ya mtaa, ***** ilikuwa saa nne kasoro, mida mbayo Jackline akiwa anasikia ving’ora vya mgari ya polisi, na michakato ya vishindo vya polisi waliokuwa wanamfwata kwa kasi, aliifikia nyumba yake hapo akaongeza speed kuufwata mlango, wa nyumba yake, akasikilizia kidogo, kama angasikia sauti yay a mtu yoyote kutoka ndani, akasikia sauti ya Tv pekee, Jackline akiwa na wasi wasi wa kuwa pengine mume wake amelewa na kuzima gari, akanyonga kitasa cha mlango, mlango aukufunguka, hapo akagonga mlango kwa tahadhari, “baba France! baba france” aliita Jackline, akijuwa fika kuwa lazima mume wake ambae alikuwa anamsubiri kwa hamu, kama ajazima gari, basi atafungua mlango haraka sana, nadivyo ilivyo kuwa, akasikia michakato ya miguu ya mume wake akikimbilia mlangoni na kufunguwa mlango, na yeye akuchelewa akazamandani haraka sana, akamwona mume wake akifunga mlango, kisha akaganda kumshangaa, yeye akumjari, kwanza kabisa akaona bola afiche ushaidi, akapitiliza mlango wa jikoni, uku anasikia ving’ora vya magari ya polisi, vikizidi kusogea karibu na nyumba hiyo, Jackline akapitiliza mpaka nje na kuingia kwenyesehemu ya kuegesha gari akainua bati moja chakavu chini kulikuwa na kama shimo flani, akaweka begi lake lenye zana zake zote za kivita, sasa sauti za ving’ora namuungurumo wa magari ya polisi vilikuwa vinasikika nje ya nyumba yao, Jackline akarudi ndani ya nyumba na kuelekea sebuleni, akamkuta mume wake Denis, na mwanae France, wakiwa wameganda kama masanamu wakimshangaa, Jackline akawatazama kwa macho ya huruma, huku ana waza mambo mawili, moja akiofia kuwaingiza katika matatizo, pili aliona uenda ukawa mwisho wa penzi lao na mwanaume anae mpenda kuliko wote, baada ya mwanamume huyu kubaini ukweli juu yake, mala wote kwa pamoja wakasikia sauti toka kwenye kipaza sauti, ikisikika toka nje ya nyumba, ni kama ile ya kuuzia sumu yapanya, “Jackline Michael Nyati, ilinijeshi la polisi, tupo nje ya yumba yako na silaha zenye risasi za moto, fungua mlango, utoke nje ukiwa mikono juu, vinginevyo tuta tumia nguvu zaidi kukutoa humo ndani” Denis na mke wake wote kwa pamoja, waliuangalia mlango, ile sauti ya kwenye kipaza sauti ikarudia tena maneno kama yale yamwanzo, Denis akiwa aelewi, kinacho endelea, au mkewake amefanya nini, Jackline yeye aliwatazama mume wake na mwanae, akamwambia mume wake “Denis kesho njoo tuonane, popote watakapo nipeleka, utafahamu kila kitu” hapo Jackline akaitoa simu yake mfukoni, na kumkabidhi mume wake, naomba piga simu kwa baba, mjulishe baba mwambie nimekamtwa, lakini kazi nimesha maliza, usi saau pia kesho kuja mahabusu yoyote nitakayo wekwa” Denis aliitikia kwa kichwa, kuonyesha aemkubariana na mke wake, huku akionyesha kujawa na wasiwasi, na pombe aliyo kuwa ameinywa ikimtoka kichwani, kiasi kwamba akaanza kumwogopa mkewe, alie tapakaa damu mwilini, hapo Denis akamwona mke wake mama France au Jackline, alie ishi nae kwa miaka miwili na miezi kadhaa, inayo karibia kufika nanusu, akifungua mlango taratibu, na kujitokeza nje, **** insp ambae alisha toa amri ya kuto kupiga risasi, akiwa na kundi kubwa la polisi wenye silaha, za kivita, walimwona Jackline akijitokeza nje ya nyumba hiyo, huku kijana mmoja akiwa nyuma yake amebeba mtoto, kijana yule alionyesha kushangaa, kwanini polisi wengi vile tena wenye silaha, wana kuja kumkamata mke wake, “simama hapo hapo ulipo, kisha piga makogoti, weka mikono nyuma yako kisogo” kile kipaza sauti kikapaza sauti yake, na Jackline akafanya kama alivyo amriwa, na hapo haraka sana, askari polisi sita, wakiwa na silaha aina ya SMG, sub machine gun kwenye mikono yao, pia wame valia mavazi maalum yakuzuwia risasi (bullet proof), walimzingira Jackline, huku wakimwelekezea mitutu ya bunduki zao, kitendo kile kilimshangaza sana Denis, mke wake amefanya kitu gani mpaka awekwe chini ya ulinzi namana ile, wakati huo Denis alishuhudia kundi kubwa la askari wengine, wakiwa wamevaa kama wenzao, pia mikononi walikuwa na siraha tofauti tofauti, kama bastora, SMG na uzi gun, walikuwa wamezunguka nyumba nzima, kiukweli ungezani wanapambana na kundi kubwa la majambazi, au magaidi waliojaribu kuiba ikulu, wakati wale askari sita wakiwa wame msogelea Jackline nakumlaza chini, kifudi fudi, wakimfunga pingu mikono kwa nyuma, (mgongoni) hapo insp Johnson akatabasamu kidogo, nakuanza kumsogelea Jackline aliekuwa amekandamizwa pale chini, alipofika pale huku bado tabasamu pana, likiwa usoni mwake, akachuchumaa chini, karibu na pale Jackline, alipo kandamizwa na askari sita, ungesema wana mdhibiti simba au #mbogo, insp Johnson akasogeza mdomo wake, sikioni kwa Jackline, kisha akamwambia, “hupo chini ya ulinzi mshenzi we! Utalipia vifo vyote” Jackline alikuwa anamtazama huyu inspector kwa hasira na ghazab, kisha kwa shida sana, kutokana na kukandamizwa na goti la askari sita, alimwambia yule insp Johnson “nitakuja kuongea na wewe, sizani kama unajuwa unachokifanya” hapo yule polisi mwenye nyota tatu, insp Johnson, akatabasamu tena tabasamu lililo chanyika na hasira kari sana, “ulishindwa kuongea na mimi kabla ujafanya upuuzi wako, utaongelea mahakamani” alisema yule inspector, huku akimtazama mama France kwa zarau kubwa sana, lakini kitu cha hajabu Jackline akatabasamu, tabasamu lililo changanyika na maumivu ya kuminywa na wale askari, “mahakamani?, sijajuwa ataenda nani, kati yako na yangu, ila ukweli nitakuja kwako kesho jioni” maneno hayo, yalionekana kumchukiza sana yule inspector, ila alijidhibiti asije kufanya makosa kama aliyo wai kuyafanya malakadhaa, nakusababisha Jackline amponyoke, “pelekeni ndani ya gari hii takataka” aliongea Johnson kwa hasira kali, Wakati huo Denis akiwa amembeba mwanae France, alikuwa amesimama mlangoni akimtazama mkewe akiwekwa chini ya ulinzi, na kundi kubwa la polisi ambalo lipo kamili na silaha za kimapambano mikononi, na sasa alishuhudia mke wake akipelekwa kwenye gari, lakini Jackline kabla ajaingizwa kwenye gari, aligeuza kichwa na kuwatazama, mume wake na mwanae France, macho yao yaka gongana, Jackline akaachia tabasamu, lililoongeza machungu moyoni kwa Denis, huku mwanae France akianza kuangua kilio, akimlilia mama yake, yule jamaa mwenye nyota tatu, inspector Johnson, alimfuata Denis pale mlangoni aliposimama namwanae, huku akiwapa ishara polisi wenzake, kuipekua ile nyumba yote, “nazani wewe ndie mume wa Jackline Michael Nyati” aliuliza insp Johnson, Dennis akaitikia kwa kichwa, akikubariana na maneno ya insp kuwa yeye ndie mume wa Jackline, “mkeo anashikiliwa na polisi, kwa kuhusishwa na mauwaji mfurulizo ya watu zaidi ya ishirini, wakiwepo viongozi wadini na wafanyabiashara wakubwa, polisi na wanchi wakawaida, maelezo zaidi utayapata kesho, fika kituo kikuu cha polisi, ambako mkeo atakuwepo pale akisubiri kushtakiwa” aliongea insp Johnson, kisha kama asiye taka swali lolote, akageuka na kuelekea kwenye moja ya gari, “tuma repot kazi imefanikiwa” aliongea insp kwa majigambo, huku akiendelea kutembea kwa madaha, akifwatiwa na askari wake, wakiwepo wale walio ingia kufwanya ukaguzi, kila mmoja, akipiga kelele, “hakuna kitu” “hakuna kitu” “hakuna kitu” wote wakaingia kwenye magari yao, magari yakaondolewa kwa kasi ya hajabu, huku gari alilopakizwa Jackline au mama France, lilikuwa katikati ya magari mengine, likilindwa na askari wenye silaha, waliokuwa wamening’nia kwenye magari ya wazi (defender), baadhi ya raia ambao walishaanza kutoka majumbani kwao, walishangazwa na tukio lile, na kuanza kuongea kila mmoja la kwake, ilimladi wanafiki awakosekani, ***** ndani ya chumba cha CGP, wanadhimu wakuu wali piga kelele za shangwe, huku wakipongezana na kupeana mikono, “dah! yani kesho saa nne, tuna mtangaza mbele ya vyombo vya habari, na sasa hivi msemaji mkuu atoe taalifa kwenye TV ya taifa” aliagiza CGP, huku akiongoza wanadhimu wake kutoka nje ya ofisi, wakienda kusimama kwenye viwanja vya kituo kikuu, kumsubiri, muuwaji alie ikisa nchi kwamuda wa miaka miwili na nusu, “tena afande kitu cha kuflahisha, yule mzee Masinde bado mzima ila, ni kwamba hali yake siyo ya kilizisha japo madoctor wana sema wamejaribu kuokoa maisha ya mzee huyu, na wamesema kuwa paka kesho asubuhi, atakuwa vizuri, japo kuwa amepoteza sehemu zake zasiri” hiyo ilikuwa ni taalifa ya mnadhimu wa kitengo cha afya na tiba, akimweleza mkuu wake CGP, “huyo binti sijuwi amelele vipi, yani pamoja na ukatili nilio wai kuushuhudia katika matukio mengi sana, lakini huyu mwanamke ni kiboko yao” alisema CGP, kwasauti ya mshangao, **** wakati huo mzee Nyati, baada ya kuona mwane Jackline apatikani, kwenye simu yake, na ile alama ya tracking kwenyepad yke ikiwa imeptea, akahisi pengine mwanae amepatwa na matatizo, hivyo akaamua bola ajiandae mazima, kwa safari ya kwenda dar es salaam, kuakikisha anampata mwanae akiwa mahabusu, hospital au mutual, akiwa anapakiza mizigo kwenye Toyota V8, akisaidiana na mke wake, mala Michael France Nyati, aka sikia simu yake ikiita, akaitoa mfuko kwa pupa, na kutazama mpigaji, alikuwa ni mwane Jackline Nyati, akapokea malamoja, “ndiyo Jackline nipe report” aliongea mzee Nyati, akizani anaongea na mwanae wapekee, “hapana mzee ni mimi” hapo ndipo Michael Nyati askari wa zamani, alipo gundua kuwa kunatatizo kwa Jack, ni baada ya kupigiwa simu na Denis mume wa binti yake, lakini taalifa ya Denis ili mpa matumaini Nyati, na kuaidi kukutana na Deni siku yapili ili kushughulikia swala hili, Japo aliona wazi kabisa kuwa mkwe wake huyo alkuwa katika mshangao na kuchanganyikiwa, lakini mzee Nyati alielewa ni kwanini, sababu sikuzote Denis alikuwa anajuwa kuwa yeye mzee Nyati ni kikongwe kinacho ishi kwenye nyumba ya udongo, huko porini, ***** saatano na nusu usiku, Jackline Michael Nyati alifikishwa mbele ya mkuu wa jeshi la polisi, na wanadhimu wakuu wa jeshi hilo, ambao walionyesha mshangao wa wazi kabisa, kwani walitarajia kumwona mshana mwenye umbo la hajabu mweusi, aliekomaa, kama mpika sumu, “haaaa! insp mnauakika kuwa ndiyo huyo?” aliuliza kwa mshangao mkuu wa polisi, “ndiyo afande, anaitwa Jackline Michael Nyati, mtoto wa mwanajeshi mtaafu wajeshi la ulinzi” alisema insp Johnson kwakujiamini, huku akiwa akipiga saluti, kwa mkubwa wake huyo, “ndio maana, aliweza kumnasa mzee wawatu na kumkata sehemu za siri, siyo kwa uzuri huu” alisema CGP, kwa mshangao, na wenzake wakacheka na kumuhunga mkono, wakati huo Jackline alikuwa amepigishwa magoti mbele ya wanadhimu hao, waliokuwa wakiusanifu mwili na uzuri wake, “yani ni binti mzuri sana sijuwi kwanini asinge olewa, na kutulia kwa mume wake” alisema mkuu wa upelelezi, Jackline alikuwa ametulia kimya akiwaza juu ya mskabari wa maisha yake, akiombea Deins japo awashe simu, maana alijuwa nnivigumu kupiga simu pengine angehofia kuwa stua wazazi wake ambao siku zote alikuwa anatambua kuwa, ni wazee wasio jiweza, “ona sasa ame mtia kilema cha maisha mzee wawatu” maneno hayo ya mkuuwa kitengo cha tiba, yalimstua Jackline, akizani labda aja yaelewa, “hivi akuna uwezekano wa kumrudishia u uume wake yule mzee?” aliuliza CGP, akimtazama mkuu wa kitengo cha tiba, “inawezekana ila ni operation kubwa sana, ambayo nchi yetu aiwezi kufanya, la kikubwa ni kwamba yupo hai” alijibu mkuu huyo wa tiba, hapo Jackline alipata uakika kuwa mzee Masinde bado mzima, akamtazama insp Johnson alikuwa amesimama na wale wanadhimu, akamwona kijana huyu akionyesha mstuko kidogo, akijitaidi wale makamanda wake, wasijuwe kuwa amestushwa na taarifa, ya kukatwa sehemu za siri kwa mzee wake, “haya insp, huyu aingie mahabusu kama gaidi, na adibitiwe sana, kesho saa nne tuna itaji kuongea na waandishi wa habari” hapo Jackline akainuliwa na kwa fujo na kungizwa ndani ya jengo la kituo kikuu, akipitishwa mapokezi na kuvuliwa viatu vyake, kisha akapelekwa kwenye mahabusu iliyopo chini ya jengo hilo, under ground, insp Johnson mwenyewe akiongoza, “nivyema kwakipindi hiki, unge sema nikuletee chakula gani, ambacho ujawai kula, usije ukanyongwa kabla ujakionja” alisema insp kwa dhiaka, wakati ana mfunga minyololo kwenye miguu na kuiunga nisha na mikononi, utani wa insp ukaonyesha kumpendeza Jackline, maana alitabasamu kidogo, kisha akamtazama insp aliekuwa anamalizia kunga minyololo, na kulifunga gate lenye nondo kubwa za mm 20, “asante asana, insp Johnson, kwakuni karibisha chakula, naomba kiwe cha kesho jioni, nyumbani kwako” 



kiukweli ata kama ungekuwa wewe, ungezani kuwa Jackline ni taahila, kwa maneno aliyo yaongea mbele ya insp, ambae aliona kuwa mwanamke huyu amesha changanyikiwa, hivyo akaondoka zake, mpaka mapokezi, “maagizo hakuna mtu yoyote kumwona huyu shetani zaidi, kuna mtu mmoja tu! mume wake, ambae nae atarhuhusiwakumwona malamoja tu!” aliongea Johnson, kisha akatoka nje ya kituo hicho, akachukuwa gari moja la polisi na kueleka Hospital, wakati huo wakubwa wake walikuwa wamesha ondoka zao, ***** usiku ule insp alienda mpaka hospital kuu ya muhimbili, akaelekea kwenye chumba maalumu cha wagonjwa VIP wadharula, ambako aba yake alikuwa amelazwa, nje alikuta walinzi wa polisi, wakiwa na silaha zao, na mavazi maalumu ya kuzuwia risasi, wakamsalimia kijeshi kwa kumpigia saluti kisha yeye akaingia ndani ya chumba hicho alicho lazwa baba yake, ambae alimkuta akiwa amesha patiwa matibabu na ikiwepo kufanyiwa operation ya kuziba sehemu alizo chomwa na visu, na kushonwa sehemu ilipo katwa dudu yake wakiakikisha tundu la mkojo likiwa wazi, na sasa alikuwa amelala kimya, huku amefunikwa shuka mpaka kifuani, kwamacho tu! alionekana kupua, kama mtu alie lala, usingizi wa kawaida, “bado kaputi aija isha, mpaka asubuhi atakuwa amesha rudiwa na fahamu” ilikuwa nisauti ya mhuguzi mmoja wakike, aliekuwa mle ndani ya chumba kile, pasipo kusema kitu insp akamtazama baba yake, kwa dakika kadhaa, kisha akaongea kwa kunong’ona, nimejitaidi kadiri ya uwezo wangu, lakini amekupata, ila baba taalifa njema nikwamba, nimesha mkamata, ato kusumbua tena” yule muhuguzi alikuwa amesimama oembeni akimtazama insp kwa macho ya huruma, “samahani kaka polisi, huyu mzee umesema ni baba yako” hapo insp aka geuka na kumtazama yule mhuguzi, akaitikia kwa kichwa, akijitaidi kuzuwia machungu na hasira ya wazi, aliyokuwa nayo, “ok! dada nita kuja kesho mapema sana” alisema insp Johnson huku akitoka nje na kuacha maagizo kwa walinzi wadumise ulinzi, nakwamba watapokelewa na wenzao, kesho mapema, kisha akaondoka zake kuelekea nyumbani kwake mbezi beach, ***** siku yapili saa kumi na mbili kamili, lisaa limoja kabla Denis ajafika pale kituoni, kukutana na Jackline mkewake, insp Johnson aliingia  kwenye kituo cha polisi, na kupitiliza moja kwamoja kwenye chumba cha mahabusu, cha magaidi, ambacho leo hii alkuwemo Jackline Nyati, akamkuta mschana huyu akifanya zoezi ya push up, licha ya kuwa alikuwa amefungwa mivyololo mizito lakini dada huyu mrembo alionekana kipiga push up kwa speed kari sana ata baadhi ya askari wake wasingeweza, “karibu insp tupate chai” aliongea Jackline, huku akiendelea kupiga push up, mfululizo, akionyesha kuwa alikuwa amenza muda mrefu, maana mwili wake, ulikuwa ume lowa jasho sana, na majasho mwengine kudondoka chini na kulowesha sakafu, utazani pame mwagiwa maji, kitendi kile kili shangaza insp Johnson, ambae akutaka Jackline ajuwe, kuwa ameshangazwa na kitendo kile, “naona unajiandaa kwenda kupambana na wakina chilumba, huko kuzimu” aliongea insp kwakejeli, “insp kazi ya kuni liwaza kwa maneno kama hayo, ni ya mumewangu, siyo wewe” aliongea Jackline kwa lengo la kumwondoa hapo insp Johnson, ili kusiwepo na kikwazo chochote endapo Denis atakapokuja, na kuitajai kuingia, insi akacheka kidogo, “hahahaha, Jack bwana, umesahau kuwa wewe ni mwanafunzi mwenzangu?, yakwamba tullisoma wote” aliongea Johnson akimkumbusha Jackline sikulile aliyo mkuta nyumbani kwake, yupo na mke wake, hapo Jackline aka jifyetua kwa wepesi sana, akasimama, na pinguzake mkononi, aka kumsogelea insp, kisha wakasimama wakitenganishwa na gate la nondo, “insp mimi siyo muhimu kwako, achana na mimi, muwai baba yako hospital, pengine akakueleza machache ambayo akuwai kukueleza, pia msaidie kuficha ushaidi wa yule mwanamke kahaba, wa hotelini, waliotaka kumchinja” hapo insp akaduwaa, kama ameuona mzimu, kisha Jackline akarudi pale alipo kuwa anafanya mazoezi, kisha akasimama kidogo na kumtazama insp, “mengine tutaongea kwenye chakula cha jioni nyumbani kwako” hapo insp akaona Jackline bado amechanganyikiwa, akaondoka na kuelekea mapokezi, “sitaki mtu yoyote akutane na huyu gaidi, zaidi wale walioandikwa kwenye horodha tu” alisema insp kwa ukari, na kuondoka zake kuelekea hospital ya muhimbili, kumwona mgonjwa, **** baada ya Deins kukutana na baba yake Jackline, ambae alimtambua kuwa ni mzee alie mwona malambili, siku ambayo Jackline alisukuma meza yao kwa bahati mbaya, na siku yapli yake, ambayo Jackline alikuwa ameshikwa na uchungu wa ghafla, wa kujifungua mtoto wao wapekee, akapewa vile vitu viwili yani unga mweusi, na kishikizo kilicho viligiwa kitambaa, kisha wakaachana maeneo ya fire,  yeye akaelekea kaliakoo, kilipo kituo kikuu, na gari aina ya Toyota v 8, likakata jushoto na kulekea upanga, **** Denis alimtazama mke wake, kwa macho ya mshangao mkubwa sana, kama vile anasema ‘watakunyonga mke wangu’ “Denis, nazani mpaka hapo, nazani umenielewa, mimi ni ninani, na kwa nini nilifanya hayo yote” alisema Jackline huku akiifadhi vizuri zile vitu alivyo pewa na Denis, Denis akaitikia kwakichwa, huku akitazama kushoto na kulia, kuwatazama watu wngine waliokuwa wanaongea na mahabusu, “Denis mpenzi wangu, ulisema unampenda dada mdunguaji siyo?” aliuliza Jackline akimtzama Denis usoni, huku ameachia tabasamu, Denis nae aliekuwa analngwa lengwa na machozi, akatabasamu huku anaikia kwa kichwa, “kwa hiyo unazidi kuni penda mume wangu sindiyo?” aliuliza tena Jackline huku akimkazia macho mume wake, “Jackline, unafahamu kuwa sina mwanamke mwingine ninae mpenda zaidi yako, sasa unazani nitaishije bila wewe, siwata ....” alishindwa kumalizia Denis akaanza kuachia kilio cha kwikwi, “Denis mume wangu si umkuja kuni toa mahabusu, sasa kwanini unalia, awawezi kuninyonga” aliongea Jackline kwa sauti ya chini sana, hapo Denis akakata tamaa yamaisha kabisa, ni baada ya kusikia maneno hayo ya mke wake, akahisi mke wake amesha changanyikiwa kwa kuhofia kunyongwa, Denis akazidi kuangua kilio cha chini chini, “Denis mume wangu unawasi wasi gani?, ebu nyamaza bwana, leo tutakuwa wote usiku” Denis alimsikia Jackline akiongea maneno kama chizi, kwa sauti ya chini, akionyesha msisitizo, sasa baada ya kulia Denis akaangua kicheko kilichoambatana na uchungu, mkubwa sana, uchungu ambao ulimfanya Jackline ayahisi mapenzi makuwa aliyo nayo mume wake, juu yake, “usijari mama kweli, leo tutakuwa wote” alisema Denis akiendelea kucheka kwa uchungu kubwa sana, uku akimtazama mke wake, ambae alimtazama kwa tabasamu, huku akipeleka mikoni yake, mdomoni mwake na kuwa maka ana ficha tabasamu lake, kisha akaitoa mdomoni ile mikono yake iliyo fungwa kwa pingu, na kuisiogeza kichwani kwake, akajikuna kidogo kwenye nywele zake alizo zisuka jana, hapo ndipo Denis alipo elewa kinachoendelea, ni baada ya kuona mke wake akipachika kile kishikizo kwenye nywele zake, hapo Denis akamtazama Jackline usoni, Jackline akamkonyeza kimahaba, kwa jicho la upande, “jiandae leo unipe kama juzi” aliongea Jackline kwa sauti ya kunong’ona, akiachia tabasamu huku midomo yake ikicheza cheza, akionyesha kuwa anatafuna kitu flani, “haya kijana muda wa umekwisha, Jackline Michael Nyati, anaitajika kwa mahojiano na wakuu, ikiwa ni kuonyeshwa kwa waandishi wa habari” ilikuwa ni sauti toka pembeni yao, wote wakaangalia upande uliookea sauti hiyo, wakawaona polisi saba, wakiwa wamesimama pembeni yao sita wenye siraha wakiwa wamesimama atuwa tano, toka walipo kaa wao, alafu mmoja asiyekuwa na bunduki, alikuwa karibu yao kabisa, akionekana kuwa navyeo vikubwa mabegani kwake tofauti na yule aliye kuja kumkamata jana, huku akitikisa fimbo yake ya kipolisi mkononi mwake, hapo Denis akamtazama Jackline kwa macho ya kweheri, akamwona akimalizia kumeza kile alichokuwa anatafuna, Jackline kama limwelewa mpenzi wake, “nenda kaandae mvinyo mume wangu, usiku wetu utakuwa mzuri sana” aliongea Jackilene kwa sauti yachini, huku akiiweka mikono yake juu ya magoti ya Denis, ambae alikuwa anainuka taratibu, na kwa unyonge wa hali ya juu sana, “askari mchukueni,” Denis alisikia amri ikitoka kwa yule asfisa wapolisi alie simama karibu yao, hapo nikitendo bila kuchelewa, haraka sana wale polisi sita wali msogelea Jackline, na wawili wakamshika huku na huku na kumnyanyuwa toka kwenye kiti alicho kwa amekalia, kisha wakaanza kutembea nae kutoka nje ya kile chumba wawili wakiwa mbele, na wawili nyuma, huku wakiwa wamekata silaha zao vyema kabisa, wakiwalinda wale wawili walio mshikilia Jackline, aliekuwa anatembea kwa shida, Denis akatoka nje ya chumba kile na kuelekea mapokezi, akiwa na mawazo mengi sana kichwani mwake, akiamini kuwa, swala la Jackline kuchomoka kwenye mikono ya polisi lilikuwa ni ndoto, “weee kijana ebu njoo hapa?” ilisikika sauti kari ya polisi wakike toka nyuma yake, Denis akajuwa na yeye anaendwa kuunganishwa na mkewake, akasimama malamoja, huku mwili una mtetetmeka utazani ame simama mbele ya simba mnyama shabbat I


  “wekaka mbona unapitiliza, umeshau kama umemwacha mwanao hapa?” ilisikia tena ile sautiya kike, hapo Denis akashusha pumzi nzito, akarudi haraka sana pale mapokezi, “asante sana dada tangu” aliongea Denis akimchukuwa mwanae, ambae alikuwa anashangaa shangaa, asijuwe kinacho endelea, “we! jifanye umechanganyikiwa tu!, tena shukuru na wewe ujausishwa kwa kukaa na gaidi” aliongea yule polisi, wakati huo Denis akusikiliza lolote, “mama ileeee” alisikika France aliekuwa amebebwa na baba yake akitazama Yuma, yani wanakotoka, Denis akageuza shingo na kutazama nyuma, hapo yeye mwanae wakakutana uso kwa uso na Jackline, aliekuwa anapitishwa kwenye kolido, na kuingizwa kwenye ukumbi wa mikutano, huku tabasamu likiwa lime chanua usoni mwake, France akapunga mkono kwa mama yake, ambae ali endelea kutabasmu, mpaka alipopotea, akisindikizwa na polisi sita, wenye silaha, ile Denis ana tokeanje ya jengo la polisi, akakutana na waandishi wengi wa habari, waliokuwa wana subiri kuingia ndani baada ya mahojiano ya kwanza yanayo mhusu mwanamke huyu gaidi, kuisha, ndipo wao waliokuwa wanatamani kupata picha ya mwanamke huyo hatari, wata ingia ndani kwenda kuiga picha, bahati nzuri wanahabari awakumtambua Denis kuwa ni mume wa Jackline Nyati, hivyo Denis akatiza kwenye kundi la wanahabari, walio kuwa na vyombo mbali mbali vya kuchukulia tukio hilo, na kuelekea kwenye gari lake, aina ya Toyota noah, akafungua milango na kuingia ndani, akampigia simu mzee Nyati,  “ndiyo baba tayari nimesha toka,” aliongea Denis kwa sauti ya knyinge sana, iliyo ambatana na simanzi, “ok! sikiliza sasa, tafuta sehemu nzuri, maeneo ya karibu na muhimbili, ukae na mtoto apate chai, usizime simu nitakupigia, kama ukiweza kunywa bia uzembe ukutoke” aliongea mzee Nyati kisha wakakata simu, Denis akaondoa gari, wakiifwata barabara ya kuelekea muhimbili, sasa France alikuwa macho, “mama kowapi?” aliuliza France, aliekuwa amekaa kwenye seat ya mbele, “atakuja baadae” alijibu Denis, huku akihisi kama kitu flani kikimkaa kwenye koo na kutamani kuachia kilio, “baba! baba! polishi” alisema France ambae alionekana kutaka kujuwa mengi zaidi, ***** leo mitaa ya jiji la dar salaam watu wote walikuwa wanazungumzia kukatwa kwa chana hatari sana, alie nyofoa roho za watu wengi sana, na habari kubwa ilikuwa ni tukio la jana, na jinsi alivyo poteza maisha ya polisi wengi sana, huku kivutio kikubwa ikiwa ni habari ya mzee alie katwa sehemu zake siri, na kuchomwa visu vingi sana, “lakini bado  mzima huyu shetani, uta kuwakazi ya kwanza ya Jack” aliwaza alisema mzee Nyati, ambae alikuwa amekaa seat ya pembeni ya mke wake alie kuwa anaendesha gari, huu mzee uyu akisoma gazeti, sijuwi Michael Nyati na mke wake, walikuwa wanafwata nini hapa hospital ya muhimbili, maana waliingia nagari lao taratibu, wakatiza kwenye gate kubwa la kuingilia magari, ambapo pasipo kukaguliwa, walipewa card ya maegesho ya magari, ambapo walipitiliza, na kwenda kusimama nje ya jengo kubwa lililo andikwa emergence, wakalipita kidogo na kwenda kusimama kwenye maegesho ya magari ya madoctor, mda wote mzee Nyati alionekana kuwa makini sana, akifwatilia sauti iliyo kuwa inasikika toka kwenye kispeeker kidogo alicho kifaa kwenye sikio lake la kushoto, (hear phone), mama Jack naomba uwe makini sana, kwani kosa moja tu! tuta mpoteza Jack” alisema mzee Nyati, akimtazama mke wake, “ondoa shaka mume wangu, sipo tayari kumpoteza Jack” alisema mama Jack, huku akiuvua mfuko mmoja mkubwa toka seat ya nyuma ya gari hilo, na kutoa koti moja jeupe, la kidoctor, akalivaa, “vipi nime pendeza hen?”aliuliza mama Jack, huku aki jitikisa kidogo, “bado uja pendeza, ukiwa na hii ndio utapendeza sana” aliongea mzee Nyati akimkabidhi mke wake kibeji flani cha plastiki cha kona nne chenye kamba ya kuvalia shingoni, maandishi ya utambulisho pamoja na picha yake, mama Jack, au Anitha, aka kipokea na kukivaa shingoni, kisha akafungua mkebe wa kwenye dash board, akatoa kichuma flani kinacho fanana na funguo lakini akikuwa na meno, ila kilikuwa na kitufe chekundu, kwenye mshikio wake, akakiweka kwenye mfuko wa lile koti, pia akachukuwa bastora na kuiviligia kwenye kitambaa cheupe, akiwa amesha ikagua na kuakikisha kuwa ina risasi, mwisho aka chukuwa maji yaliyopo kwenye kifuko cheupe cha plastic, (drip) akakiweka kwenye mfuko wapili wakoti lake, mzee Nyati allafungua mke uliopo mbele yake, kwenye dash bord na kutoa Bp Machine, akampa mke wake, ambae iitundika shingoni, kama wafanyavyo madoctor wenyewe, hapo sasa umependeza, alisema mzee Nyati, “ok! baba kazi kwako, mlinde mkeo na mwanao” alisema mama Jackline, kisha akafungua mlango na kutoka nje ya gari nakufunga mlango, akimwacha mzee Nyati peke yake, ambae ali shuka toka kwenye gari na kuamia seat ya nyuma ya gari, akapeleka mkono kwenye sakafu ya gari na kuibuka na begi dogo jeusi, lile lile alilokuwa anatumia Jackline, akaanza kutoa kifaa kimoja baada ya kingine cha mugnum sniper rifle, na kuiunganisha, kumbe basi, mzee Nyati na mke wake, waliingia Dar es salaam, mapema sana, saa kumi na moja kasoro, wakitokea Songea, kwakuwa alikuwa anapajuwa nyumbani kwa Denis wakaenda moja kwa moja na kusimamisha gari mita mia toka kwenye nyumba hiyo, wakichunguza kama kuna mtu alikuwa ana ichunguza na kuifwatilia nyumba hiyo, lakini aikuwa hivyo, wakatulia ndani ya gari lao mpaka walipo mwona Denis anatoka na gari lake akiwa na France, ndipo  mzee Nyati, mbae alisha wai kuja maali hapa na kujuwa ifadhi ya Jackline ya silaha, akaingia kwenye sehemu ya kuegeshea gari, na kuchukuwa begi dogo Jeusi, ambali polisi walifanya kosa kubwa sana kuto kuli ng’amua lilipo, nandipo walipo anza kumfwatilia Denis, kwakutumia simu tracking, kupitia simu ya Jackline ambayo kwa sasa alikuwa nayo Denis, wakiwa tayari wamesha panga jinsi mchezo utakavyo kuwa, mzee huyu aliendela kufunga silaha hiyo huku macho yake yakiwa kwenye mlango wa jengo la hospital, na msikio yake kwenye hear phone, ***** ndani ya chumba cha mikutano Jackline  Nyati alikuwa amesimamishwa mbele ya wanadhimu wakuu wa jeshi la polisi, walioongozwa na mkuu wajeshi hilo, CGP, ambae kabla ajaongea lolote akatazama huku na huku ni kama aliona kuna mtu muhimu amepungua, akamnongoneza kamanda mkuu msaidizi, “mbona yule insp simuoni tena” hapo makamu aka mnong’oneza mkuu wa upelelezi, akimwulizia kuhusu Johnson, ndipo zilipo anza kupigwa simu kumwulizia mtu huyu, muhimu alie fanikisha zoezi hili na kulipatia heshima na sifa jeshi la polisi, licha ya kupigiwa simu lama kdhaa, lakini akupokea simu, wanadhimu wakaingiwa nawasiwasi, akatumwa mtu kuulizia mapokezi kama kuna taalifa yoyote, wakati huo Jackline alikuwa amesimama kati kati ya ukumbi hule, akiwatazama makamanda wakuu wajeshi la polisi, lakini kichwa chake alikitazamishia chini, pande zote polisi sita wenye silaha kali, walikuwa wanamlinda, mala yule alie tumwa mapokezi akarudi, akaenda kumnong’oneza kamanda mmoja wapolisi, nao makamanda wakanong’onezana, kisha ujumbe ukamfikia CGP, “anaenda kufanya nini Hospital, wakati kazi yake imesha kwisha, ebu fanyeni kilalinalo wezekana, kwenye kikao na waandishi awepo” aliongea CGP, kwa sauti ya ukari sana, hapo mkuu wa kitengoo cha upelelezi akainujka na kutoka, akaagiza pale mapokezi itafutwe namba ya simu ya askari aliepo kule muhimbili, kati ya wale wanao fanya ulinzi kule, kisha waongee na insp Johnson wamwambie aripot haraka sana pale kituo kikuu, baada ya kukamilika hayo ndipo wanadhimu walipo kumbuka uwepo wa Jackline Nyati pale mbele yao, wote wakamtazama yule mwanamke alie tikisa nchi, kitu cha kushangaza wakamwona mwanamke huyo akitokwa na jasho jingi sana, mwilini mwake, wote wakashangaa, “jamani nini kinamtokea huyu mwanamke?” aliuliza CGP, kwamshangao mkubwa sana, akuna alie jibu, zaidi walimkodolea macho na kumwona binti huyu akianza kuishiwa nguvu, na kuregea kabisa, kishaa kubwaga chini kama kiroba, huku akijitaidi kuinuka tena na kushindwa, “ebu waini haraka mkamtazame huyo mwanamke, isije kuwa amekula sumu” alipiga kelele CGP, akimaanisha kuwa isije kuwa Jackline ametumia mbinu za kijasusi, za kujiuwa kwa sumu, akikwepa kutaja wausika wenzake, 


Mkuu watiba aka kimbilia mbele huku akuagizwa bahadhi ya madoctor waitwe haraka, huku yeye akiendelea kutumia vipimo vya kawaidda vya kienyeji, “afande huyu mwanamke anakila dalili ya kuwa anamalalia kalisana, nashauri akimbizwe hospital ya muhimbili, akapate matibabu haraka sana” alisema mnadhimu mkuu, wa kitengo cha tiba, “haya ufanyike utaratibu haraka sana, ila atibiwe chini ya ulinzi mkubwa sana wa askari” aliagiza CGP, **** Pale nje ya ituo kikuu cha polisi, wana habari waliokuwa wana subiri kuingia kwenye ukumbi wamikutano walishangaa wakianza kuondolewa eneo la mlango, kisha wakaona hambulance ya polisi, ikisogezwa mlangoni na kushuhwa majela, ambayo iliingizwa ndani, ambapo dakika chake ikarudiswa ikiwa imebebwa na askari wanne, safari hii, ikiwa na mtu juu yake, akionekana ni mgonjwa aututi, akaingizwa kwenye gari akiwa juu ya machela, na gari hilo likaondolewa kwa mwendo wa kasi sasna, likifwatiwa na gari tatu za polisi zilizo beba askari wengi nyuma yake, walio beba silaha za kivita, wakiwaacha waandishi wa habari wakishangaa, “sikiliza toka kwangu”ilisikika sauti ya msemaji mkuu wa jeshi la polisi, wana habari wote waka geuka na kumtazama msemaji huyo, aliekuwa amesimama kwenye mlango wa kuingilia kwenye jengo hilo la makao makuu ya polisi, “kuna zarula imetokea, hivyo mnaombwa mtawanyike, mtajulishwa muda wa kuja kupata habari” alimaliza afisa habari wa polisin na kurudi ndani, ya jengo hilo, akiacha polis wanaanza kuwaondoa wana habari, ambao walikuwa na mawili matatu ya kuhoji, ****** “ndivyo ilivyo kuwa, na tulijuwa askari Nyati ameshapoteza maisha, na pia atakama angekuwa mzima tuliamini ataishia mikononi mwahasi, wa ndani ya misitu minene ya congo, sasa sijuwi aliponaje, mpaka akarudi Tanzania” aliongea David Masinde, akimaliza kusiumulia mkasa mrefu ulio tokea congo, 1988, wakati huo insp Johnson alikuwa amekaa pembeni ya baba yake, aliekuwa amelala kwenye kitanda cha hospital, ndani ya chumba cha wagonjwa maalumu wa zalula, akisikiliza story hiyo toka saa moja asubuhi, insp akatabasamu kidogo, “kwa hiyo ndio maana mkatoa taalifa kuwa amepotea?” aliongea insp Johnson na kumfanya baba yake akohoe kidogo, baada ya kushindwa kucheka, kutokana na maumivu makali sana, Johnson akamsaidia baba yake kumweka sawa, maana humo ndani walikuwa wilitu, “usijari baba yame kwisha”, mala insp akasikia mlango wa chumba kile ukifunguliwa, akamwona askari wake mmoja akichungulia, ambae ni koplo Mashiba, “samahani afande, Chef CID anasema pokea simu yako” hapo Johnson akasimama haraka sana, na kuchomoa simu yake toka mfukoni, aliyo iondoa sauti wakati anaingia kwenye jengo hili, lisilo itaji kelele ya aina yoyote, akakuta kuna miseed call zaidi ya hamsini, zikitoka kwa wakuu mbali mbali wa ngazi za juu wa jeshi la polisi, “vipi umetafutwa sana?” aliuliza mzee Masinde, ambae kiukweli zaidi ya kuchezesha domo kuongea, akuwa na uwezo wa kukutikisaa ata kidole chake, “baba naomba upumzike kidogo, nazani naitajika kwenye kikao kilicho pangwa kufanyika saa nne hii na wandishi wa habari” alisema insp huku anatazama saa yake ilikuwa saa, nne kasoro dakika tano, insp akatoka nje ya chumba kile haraka sana, na kumsisitiza Koplo Mashiba, asimamie walinzi, kuakikisha kuwa wapomakini muda wote, kisha yeye aka toka nje kabisa ya jengo lile, na kuingia kwenye gari la polisi alilo kuja nalo, na kuondoka zake, ile insp anaondoka kupitia gate la kutokeana, wakati huo huo kwenye gate la kuingilia, ambulance la polisi kisindikizwa na magari matatu yapolisi likaingia, mzee Nyati akiwa ndani ya gari lake aliona jinsi polisi walivyo kuwa makini kumlida Jackline, aliekuwa amebebwa kwenye machela hajiwezi kabisa, lakini kwa namna walivyo mlinda, utazani wana linda sanduku lafedha, mzee Nyati akacheka baada ya kumwona Anitha akiwa pamoja na bahadhi ya wauguzi wakimbadiri Jackline toka kwenye machela ya polisi, na kumlaza kwenye kitanda chenye mtaili, cha hospital, huku minyololo ikionekana kwenye miguu na mikono ya Jackline, mzee Nyati akuwa na wasi wasi kwani alishamwona insp Johnson akitoka maeneo yale, hivyo akuna wa kumtambua mke wake kilahisi, akawaona manesi walio ongozwa na doctor fake, wakisindikizwa na polisi, kuingia ndani, ambapo manesi waliokuwa wana sukuma kitanda waliongoza moja kwa moja kwenye chumba cha VIP, ambacho kita saidia kwenye ulinzi, kama ilivyo amriwa na kiongozi wa polisi, aliekuwepo eneo lile, huku wakizuiliwa kuingia ndani kwenye chumba, “kama mmekuja na askari wakike aje, ila atuta ruhusu askari wa kiume kuingia ndani, wakati matibabu yanaendelea” alisema doctor mmoja wakike aliekuwa anawasimamia wale manesi, ambao ata awa manesi awakujuwa uwa doctor huyu ni fake, “ok! tutafanya utaratibu wa kumleta askari wakike” alisema afisa wa polisi, huku anarudi nyuma na mlango ukafungwa, wakabaki manesi wawili na yule doctor wakike, “wee nenda kamwandikishe mgonjwa, waulize hao askari majina yake, na wewe nenda kalete drip inaonyesha mgonjwa aepoteza maji mengi, sana akiongea Anitha ambae alijuwa kuwa endapo ata chelewaa kidogo, atabainikia kuwa yeye siyo doctor, na kuharibu mpango mzima, wale manesi wakatoka mbio mbio mbio wakimwacha Anitha peke yake, hapo Jacklline ambae muda wote alioonekana, kuwa kazidiwa, akafumbua mcho na kumtazama mama yake, wakachekea chini, “haya chukuwa mizigo yako haraka” alisema mama Jackline, huku akitoa bastora iliyo viligiwa kitambaa cheupe Jackline akajiinua kidogo, na mama yake akaiweka chini ya godoro, usawa wakichwa, kisha mama huyu aka chukuwa kile kifunguo na kumwekea kwenye nywele, mwisho aka mkamkabidhi ile drip, wakati huo huo mlango ukafunguliwa, akaingia doctor mmoja wakiume, akiongozana na yule kamnda wapolisi alie mzuwia asiingie mlendani, muda mfupi uliopita, “ni huyu hapa doctor mwenyewe” alisema yule polisi mwenye cheo kikubwa begani, akimwonyesha kidole mama Jackline, ackline vizuri, wakati huo Jackline alikuwa ameshaitoboa ile drip, nakuanza kuinywa, kiukweli yalikuwa ni maji flani yaliyo andaliwa kwaajili ya kumpa nguvu, baada ya kumeza ule unga mweusi, mama Jackline alistuka kidogo baada ya kumwona yule doctor akimtazama kwa tahadhari, wakati huo Jackline aliwatazama kwa macha cho ya kuibia, huku akijifanya kuwa, bado amezidiwa,   


Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)