NGOJA NILEWE 3

Emmanuel Lee
By -
0

NGOJA NILEWE 3


MTUNZI: Mbogo Edgar



ILIPOISHIA 2 : Huyo anaitwa Adellah, ni mtoto wa tatu wa mzee Mwakafwila, anamwezi wapili sasa, toka afike hapa jijini Dar es salaam, akitokea wilaya ya Lungwe mashaliki, ambayo sasa hivi inaitwa busokero, kijiji cha Lufilyo, huko mkoani Mbeya, akiwa amekuja kwa dada yake Sophia, alie olewa na kijana Philipo Mazengo, mwenyeji wa mkoa wa Dodoma. ,…… . ENDELEA……..


Lengo la safari ya Adellah, kuja jijini Dar, ni kuja kutafuta kazi, ambayo ingemsaidia kubadirisha maisha yake, napengine ya familia yao kwa ujumla, yani mzee mwakafwila na mke wake, maana dada yake ambae ni Sophia, ambae anaishi na mume wake hapa kibamba kwa mangi, na kaka yake Rusajo, ambae alikuwa anaishi mbeya mjini na familia yake, licha ya kuwa na nafamilia zao, lakini bado maisha kwa upande wao ayakuwa mazuri, japo hii ilitajwa kama sababu singiziwa, na kwamba kuna sababu kuu ambayo ilimfanya Adellah, alazimishe kuja mjini, licha ya dada yake kumweleza kuwa mjini mambo magumu.


Sofia dada wa Adela na mume wake, wanaishi maisha ya hali ya chini kwenye nyumba ndogo ya kupanda, ya chumba kimoja, ambacho sasa wanalazimika kukata chumba kwa panzia, ili Adellah, alale sebeuleni na watoto wao wawili, kwakutandika mkeka pale chini, maana apakuwa na kochi ata moja, zaidi ya meza nasturi mbili, na kuna wakati katika kujigeuza geuza Adellah, angejikuta kwenye vungu ya kitanda, ni kutokana na ufinyu wa chumba kile.


Malengo Adellah, ya shindikina kutimia, Adellah, anakosa uelekeo, awezi kupata nauri wala awezi kundelea kuishi mjini, maana hali ni ngumu, shemeji yake ambae alikuwa anategemea kipato cha tano moja kwa siku ambayo anapata kibarua cha saidia fundi, katika ujenzi wa nyumba binafsi, kazi ambayo kuna wakati kama ilivyo sasa, inakosekana pia, saa anasiku ya nne ajaipata, kitendo cha mwanamke huyu kupata fedha hii, toka kwa seba, ilikuwa ni kama neema toka juu, akiombea akutane na kijana huyu siku kwa mala nyingine.********


Naaaam dada yake Adellah, yani Sophia, akiwa amekaa pale nyumbani, anwatazama watoto wake wawili, waliokaa kiunyonge, kwa njaa iliyokuwa inawatafuna matumbo yao, huku wakiachia miayo ambayo ungeshindwa kuielewa kama ni ya usingizi au njaa, arufu nzuri ya vyakula toka kwenye vyumba vya jirani, inapenya kwenye matundu ya pua zao, na kwenda kuchokoza njaa iliyokuwa tumboni mwao, hakika ilikuwa ni udhuni kubwa kwa dada huyu, ambae mume wake, bwana Mazengo, au Philipo kama walivyo zowea kumwita vijana wenzake, alikuwa ametoka kidogo, kwenda kunyoosha miguu, ni kweli alishindwa kuwatazama watoto wake, ambao walionekana wameshikwa na njaa kali, Sophia anawaza maisha magumu waliyo nayo, anawaza kuhusu watoto, anawaza kuhusu mdogo wake, ambae ni kama amekuja kuzidisha ugumu wa maisha, ana anatamani kukubariana na mume wake, kuwa Adellah amekuwa mzigo kwao, Sophia anailahumu hakiri mbovu ya mdogo wake Adellah, ambayo ilimtuma kuja Dar, kwaajili ya kumfwata mwanaume ambae ajiwezi katika maisha, na siyo kutafuta kazi kama alivyosema, hakika kama angekuwa na nauri, basi angemrudisha nyumbani haraka huko Lungwe.


Lakini ghafla wakati aliekuwa amekaa kwenye ngazi za mlango, akimsubiri Sophia, ambae akuwa na matumaini ya kwamba atarudi na kitu, kutokana na madeni waliyo yalimbikiza, katika sehemu ambazo wanakopa, mala ghafla anawasikia wa toto wake, “mamdogo huyoooo” walipihga kelele huku wanainuka na kukimbilia kule ambako kuna jia ya kutokea pale nyumbani, Sophia anatazama kule ambako watoto wanakimbilia, anamwona mdogo wake yani Sedellah, akiwa anakuja huu abeba mfuko uliojaa vitu vingi sana, Sophia anatoa macho ya mshangao, maana ata kama angefanikiwa kupata viazi fungu mbili kwa Baraka, visingekuwa na uwezo wa kujaa mfuko kama vile.


Sophia anazidi kushangaa, baada ya kumwona mdogo wake, anatoa maandazi kwenye mfuko na kuwapatia watoto, “aya zawadi yenu hii hapa” anasema Adellah, ambae anawapa toto maandazi na kuendelea kutembea kuusogelea mlango anapofika mlangoni, anaingiza tena mkono kwenye mfuko wa Rambo, na kutoa andazi jingine, na kumpatia dada yake, “pooza njaa kidogo, wakati tunapika” anasema Adellah, huku ambae baada ya kumpatia dada yake andazi, anaingia ndani na kuanza kusembua vile vitu alivyo vibeba, huku dada yake nae akiingia ndani, wakifwatiwa na toto, ambao wanazidi kuchangamka, baada ya kuona kuna mchele na samaki wa baharini, nyanya naviungo vingine, tofauti na mama yao ambae alikuwa ametoa macho ya  mshangao, maana akuamini alicho akiona mbele ya macho yake, siyo kwakuwa mdogo wake aliondoka bila ata shilingi moja, yenye mkono ulishika mwenge, ila pia  Sophia kwa miaka wili sasa, akuwai kuona mzigo kama ule ukiingia pale nyumbani, “Adellah, umepata wapi vitu vyote hivi?” aliuliza Sophia kwa sauti yenye mshangao mkubwa, huku anamtazama mdogo wake alie jawa na furaha.


Jibu lilichelewa kidogo, kupisha tabasamu la Adellah lihishe kidogo, “yani uwezi amini, wenzio kuna kaka mmoja ameamua tu kunipatia ela, yani ata simfahamu” aljibu Adella, ambae alimweleza dada yake kilichotokea kule gengeni kwa Baraka, “yani dada nikikusimulia, ata uwezi kuamini” alisema Adellah, wakati wanasaidiana kuchambua vile vitu, wakivitenga kutokana na aina ya vyakula vyenyewe, “kama nikweli nitaamini tu, we nieleze umevipataje vitu hivi, usije ukaende kuongeza deni, mpaka wakaja kuchukuwa kitanda change” alisema Sophia, akitaja kitanda, maana ndiyo mali pekee ya thamani waliyokuwa nayo, “mh! kukopa ndio ngebakia na chenji, kwanza wenye mduka ya mchele ata siwajuwi” alisema Adellah, ambae alimsimulia dada yake kila kitu kilichotokea wakati wanachambua mchele na kukufanya mapishi, “yani mkaka mwenyewe mzuri huyo, alafu ata alingi, yani ajaniuliza ata jina” alisema Adellah, akimwaga sifa kwa kijana wetu Sebastian, “kwahiyo alikusaidia tu, na kuondoka zake?” aliuliza Sophia kwa mshangao, “yani ata akutaka ata kuni juwa jina, ila inaonekana uwa anaendaga kununua ndizi kwa Baraka kila ijumaa” alisema Adellah, akimaanisha jambo, ambalo ata dada yake alilielewa, “lakini anaweza kuwa mume wa mtu” alisema Sophia, na Adellah akapinga vikali, “hapana bado ajaowa, mbona anaenda kujipikia mwenyewe” alisema Adellah, akionyesha kuwa na uhakika na anachokisema, ata dada yake akajikuta anajitabasamulia mwenyewe, “lakini angalia usije kuginga nisha magari” alisema Sophia, japo akufafanua, lakini nikama alikuwa anatoa tahadhari.*********


Naaaam siku zilizofwata maisha yalikuwa mazuri kwao, wakitumia kwa mpangilio mzuri chakula walichokuwa nacho, mpaka siku ya sita, usiku ambapo chakula na chenji yote viliisha, huku shemeji yake Adellah, akiwa ajapata kibarua chochote, huku kasheshe ikija siku ya saba, ambayo ilikuwa ni ijumaa, ambapo waliamka bila chakula chochote.


Asubuhi ilipita nyeupe, mchana ukapita mweupe, watoto wakimlilia mama mdogo, ambae aligeuka mkombozi wa muda mfupi, ata dada yake na shemeji yake walifuta lile wazo la kumrudisha mbeya, ata awakumwona tena kuwa ni mzigo kwao, “wala msiwe na wasi wasi, jioni nitaenda kuleta mchele” kauri hii iliwapa nguvu watoto awa wa dada yake Adellah, ambae kichwani alipanga lake, asa mida ya jioni.



Naaam! mida ya saa kumi na mbili za jioni, Adellah akiwa ameoga vizuri na kuvalia gauni lake la kanisani, alitoka nyumbani, na kuelekea magengeni, ambapo alienda kusimama sehemu moja nzuri mbali kidogo na genge la Baraka, alicho akikisha ni kwamba anaona vizuri kila mtu anaingia nakutoka gengeni pale, akutaka kusogelea gengeni kwa Baraka, kwa kuofia kuwa, angebainika kuwa anavizia msaada toka kwa kijana yule, mwenye moyo wa kipekee, japo ata Adellah mwenye akujuwa kama angeanzaje kuweleza kijana huyu, kwamba anaitaji msaada wake, lakini akutaka sana kuumiza kichwa, kwamba cha msingi ni nene la kuanzia kuongea nae, hayo mengine yange jiseti yenyewe juu kwa juu.******


Yap! muda ulienda, sekunde, dakika, mala saa la kwanza likakatika, hiyo ilikuwa ni saa moja, mala saa lapili nalo likakatika, ikiwa ni saa mbili za usiku, japo Adellah akajuwa kuwa, leo aikuwa bahati yake kukutana na kijana yule ambae akujuwa ata mpata wapi, hakike ingekuwa miaka ya sasa, ingekuwa lahisi kwake, maana ukiachilia kuwepo na maboresho ya simu za mkononi, ambazo wakati huo, zilikuwa zikionekana kwenye flamu, na maongezi ya vitu vya kufikilika, pia miaka hii ni lahisi kwa mwanamke kumtafuta mwanaume wazi wazi, ata kwa kumwuliza mtu anae mfahamu kama ilivyo baraka anavyo mfahamu Sebastian, lakini kwa miaka hiyo, ambayo mksa huu ulitokea, ilikuwa ngumu kidogo, hakika Adellah, ambae alilelewa kijijini lufilyo, asingekuwa na uwezo wakufanya hivyo ata kidogo, ata kitendo hiki cha kumsubiri hapa, kilimpa wakati mgumu.


Adellah baada ya kuona kuwa, amesha pitisha masaa mawili bila mafanikio, kionyonge kabisa, huku akiwa amesha poteza matumaini, anaamua kuondoka zake kurudi nyumbani, njaa tumboni ina mchonyota kama vile kuna siafu wana muuma ndani ya tumbo, alimfikilia dada yake na watoto wake, akapata picha ya jinsi watoto wa dada yake watakavyo mlilia, kila mmoja akillamika njaa, tena huku wapua zao zinanusa arufu ya nzuri ya vyakula, vya aina mbali mbali, toka kwenye vyumba vya wapangaji wenzao.


Naam wakati Adellah anamaliza mtaa wamagengeni, mala anamwona yukijana mmoja mbele yake, alie vaa kama yule aliemsaidia ijuma iliyopita, akiwa amebeba, mfuko wa rambo mkononi mwake, alie kuwa anatembea kuelekea kule ambako yeye alikuwa anaelekea, Adellah, alitamani kupaza saut kumwita kijana yulembae akuwa anamfahamu jina, lakini kutokana na kuwepo kwa watu weng maalipale, akashindwa kufanya hivyo, na baada yake akaongeza mwendo ilikumfikia kijana yule, ambae alikuwa na uhakika kuwa bila kujiuliza mala mbili, Adellah akaongeza mwendo kumuwai kijana yule, ambae japo alikuwa mbali kidogo, lakini alikuwa anatembea taratibu.


Baada ya kutembea kwa kwa hatua kama kumi hivi, na kuona kwamba wezi kumfia kwa haraka kutoka na umbali waliokuwepo, Adellah, ambae asingeweza kukimbia, kwenye lile kundi la watu, akaamua kusubiri aliache ene la magengeni, na kuanza kupaza sauti, “we! Kaka, We! Kakaaaa” aliita Adellah, huku anajitaidi kutembea, akamwona yule kijana anageuka nakutazama nyuma, yani anamtazama yeye, ukweli ni kijana yule yule, wa sikuile pale gengeni kwa baraka, lakini kijana yule kama vile akuamini anaitwa yeye, akageuka nakuendelea na safari, hapo Adellah akaona isiwe kesi, akaanza kukimbia, tena nizile mbio za mwanafunzi anae wai shuleni, katika zamu ya mwalimu mnoko, huku macho yake yameelekea kwa kijana yule, akutaka ampotee ata kidogo.


Kona ya kwanza, kona ya pili, akamwona kijana yule mita chache mbele yake, anakata kona kulia kuingia kwenye nyumba moja kubwa yenye gari nje, ambayo mala zote Adellah, uwa anapita hapo kwenda nyumbani, ni nyumba ambayo uwa, ajawai kukuta tu, zaidi siku moja moja, uwa akipita anasikiaga arufu ya nyama choma, na sauti kubwa ya music, Adellah akaongeza mwendo, pasipo kujali kuwa mbio zile zingemtoa jasho ambalo linge msababishia arufu.


Mbio za Adellah, ziliza matunda, maana wakati kijaana yule ambae sasa alikuwa amesimama mlango, anatoa funguo ili fungue mlango tu, Adellah huyu hapa, yule kijana anasikia vishindo vya Adellah, anageuka haraka, anamwona Adellaha anaingia pale nyumbani mbio mbio, “shikamoo kaka” alisalimia Adella huku anahema juu juu, Kijana anamtazama Adellah kwa mshangao, maana anaona wazi kuwa kama siyo Adellah akamzidi angalau mwaka mmoja au miwili, basi wanalingana, sasa shikamoo imetokea wapi, au mwanamke ayupo sawa, anamtazama toka chini mpaka juu, anamwona ni mwanadada mzuri sana, mwenye kufaa kwa matumizi ya ndani, asa akipata ving’alisho ndiyo baraha zaidi, “zatoka siku ile kaka, nilikuona kwambali, nikasema nije kushukuru kwa msaada wasiku ile” alisema tena Adellah, akiwa bado anahema juu juu, na kumfanya kijana azidi kushangaa, lakini akimtazama mwanamke huyu, anamwona yupo sawa tu, anasura nzuri tena ya kumananisha, umbo zuri la kawaida, ambalo licha ya kuwa ndani ya gauni pana pana, lakini bado lilivutia, “samahani dada, utakuwa umenifananisha” alisema yule kijana, japo kiukweli aliuona uzuri wa mwanamke huyu, lakini isingekuwa vyema kusema ndie yeye, wakati anaanimi kuwa amefananishwa.


Ilimshangaza sana Adellah, ambae alikuwa na uhakika kuwa ni kijana huyu huyu ndie alie msaidia sikuile, “we kaka kwani unikumbuki, ulipa ela, siku ile pale gengeni kwa baraka” alisema Adellah, huku anasogeza uso wake, karibu na kijana huyu, ambae tuna mfahamu kuwa ni Sebastian, “hooooo! Nimekumbuka, habari za toka siku ile?” alisalimia sebastian, kwa sauti yenye uchangamfu, “salama tu, yani ningejuwa unakaa hapa nisinge angaika kukutafuta, maana sikuile uliondoka ata sijasema asante” alisema Adellah, kwa sauti yenye furaha ya kukumbukwa, na kijana huyu, “aukuwa na aja ya kufanya hivi dada yangu, mbona ni kawaida tu” alisema Sebastian, huku anaanza kufungua tena mlango wa nyumba yake, “unasema ilikuwa kawaida, wakati mwenzio nyumbani wamekushukuru sana, vitu nilivyo nunua tume vimaliza jana” alisema Adellah, kwa sauti yenye uchangamfu.


Ilimshangaza kidogo Sebastian kusikia kuwa nyumbani kwao yule mwanamke, walimshukuru kwa elfu nne, aliyo mpatia yule mwanamke, “inamaana siku ile nyumbani akukuwa na kitu chochote?” aliULIZA Sebastian kwa sauti ya mshangao, yenye fadhaa ndani yake, hapo Adellah nae akanyongea kidogo, “yani uwezi kuamini, ata leo nimeondoka pale awana ata unga wa uji” alisema Adellah, kwa sauti iliyo nyongea, “karibu ndani” alikaribisha Sebastian, na bila kusita, Adellah akaingia ndani, ambako alikuta jiko lipo sebuleni, pembeni kuna sinia lenye vinde vya kuku, ambae ukiamua kumuunganisha tena, angekosa utumbo na miguu tu, akiwa anasubilia kupikwa au kuchomwa, pamoja na vitu vingine kama vile chumvi, pili, nyanya vitunguu, pia kulikuwa na ndizi kama ilivyo kawaida, na chupa ya wine na grass kwa pembeni, japo nyama zilikuwa azijapikwa wala kuchomwa, Adellah alihisi mate yana mjaa mdomoni, kwa uchu aliokuwa nao, huku njaa ikiongezeka mala dufu, ila alishangaa kwanini kijana huyu anapikia sebeleni.


Adellah anavutiwa na mwonekano wa pale sebuleni, anashangazwa na utimilifu wa sebule ile, ambayo inavitu vingi vya kisasa ambayo vingi kati yake, Adellah, akuwai kuviona kwa macho, maana kule Lungwe kipindi hicho akukuwa na vitu kama hivyo, labda kwa mkuu wa wilaya, “niliishiwa mkaa, ndio maana nikatokakidogo, kwenda kununua hapo magengeni” alisema Sebastian, huku anaweka mfuko chini, “kwanini usinge mtuma dada yako au mke wako?” aliuliza Adellah, huku anatembeza macho pande zote za sebuleni, kutazama mandhari ya mle ndani, yana zidi kumvutia, kiasi cha kuamini kuwa, kijana huyu humu ndani, anaishi na wazazi wake au mke wake, “naishi peke yangu, bado sija bahatika kuoa” anasema Sebastian, ambae sasa alikuwa anajipapasa mfukoni.


Jibu lile linamanya Adellah, achanueshe tabasamu kimoyo moyo, “ebu nikusaidie kaka yangu” alisema Adellah, huku anamfuko wa mkaa, kwa lengo la kumsaidia Sebastian, kuweka jikoni, huku kichwani mwake akimani sana, kuwa mama mwenye nyumba hii, hakika ikitokea hivyo, safari yake ya Dar isingeenda bule, “hapana dada yangu, nisikusumbue, we ngoja ni kupe ela kidogo, ukanunue chakula, kwaajili ya ndugu zako, maana muda umeenda sana” alisema Sebastian, huku anatoa wallet mfukoni na kutoa noti moja ya shingi elfu moja ya kitanzania, na kumpatia Adellah, “chukuwa hii, ukanunue chakula cha usiku huu, alafu kesho mchana, tutajuwa la kufanya” alisema Sebastian, ambae kama kawaida yake, licha ya kutamani kufanya jambo na dada huyu, lakini akuweza kumweleza, kwa hofu ya kukataliwa, “sawa, lakini naomba nije baadae kuangalia video” alisema Adellah, huku anajichekesha kike, “hoooo karibu, lakini waisha kwanza chakula” alisema Sebastian, ambae alipanga kuwa, endapo huyu dada atakipindua tu, asingeweza kulaza damu.


Naam kusikia hivyo Adellaha akatoka mbio, “sawa nakuja sasa hivi, usinifungie mlango” alisema Adellah, huku anatoka nje, sauti yake ikionyesha wazi kuwa, alikuwa katika furaha kubwa, Sebastian nae pasipo kujuwa kuwa, Adellah alikuwa akatika mikakati ikubwa ya kumnasa, akajikuta anaanza kupanga namna ya kumpata huyu dada mwenye mwonekano wa kufaa kuwa mke, “kwaribu muda wowote  utagonga mlango, siwezi kulala saa hizi” alisema Sebastian, huku anasimama mlangoni na kumsindikiza kwa macho mwanadada huyu.*******


Sophia, akiwa katika hali ya kukata tamaa, amejifungia ndani anatokwa michozi kimya kimya, kwa kuwahurumia watoto wake, ambao kiukweli akujuwa wangewezaje kulala najaa usiku huu, hii nikikutokana na kukata tamaa ya kuona mdogo wake Adellah, anarudi na kitu, sababu tayari yalisha pita masaa karibia matatu, bila mdogo wake huyo kurudi, na nikitu alicho amini nikwamba, bahati aliyo ipata mdogo wake siku ile isingeweza kujirudia mala mbili, maana yeye toka amefika dar, akuwai kuona mtu anatoa kitu cha bule kama msaada, tena kwa mtu asie mfahamu.


Sophia ambae alikuwa bado yupo ndani watoto wacheza nje, anatamani kusikia sauti ya jilani yake ikiwaita watoto waende kula, lakini asikii wakikaribishwa ata kwa ile karibu ya uongo, uchungu zaidi unakuja baada ya kusikia watoto wengine, wanaitwa na wazazi wao kwenda kula, anategemea muda wowote kuona watoto wakiingia ndani, na kudai chakula walichoa mbiwa watakila usiku, Sophia anaumia moyoni, anafikia hatua ya kujilahumu kuolewa na mwanaume alie nae, na kuzaa nae haraka haraka watoto wawili, pengine watoto wasinge zaliwa katika dhiki kama hii.

Lakini wakati Sophia anendelea kuwaza, huku watoto wake wanaendelea kucheza huko nje, mala anasikia watoto wanamshangilia mama mdogo, hapo angalau kidogo Sophia akaanza kutabasamu, lakini je amefanikiwa, na kama amefanikiwa huyo mtu anamalengo gani na mdogo wake mpaka amsaidie, wakati akuna ata mmoja anae mfahamu mwenzie, na akichukulia ni kwamba, mdogo wake ni mgeni hapa jijini, lakini hiyo yote, aikuwa kitu bora aje na chochote kitu, sasa vipi kama ata kuwa amekosa kabisa.


Wakati anawaza hayo mala akasikia sauti ya mdogo wake toka nje, “aya chukueni hii mgawane” hapo kidogo Sophia anajiwa na matumaini, kwamba mdogo wake amekuja kitu, tabasamu linakuja usoni, anafuta machozi haraka, anajiweka sawa, na dakika hiyo hiyo mlango unafunguliwa, anaingia mdogo wake, watoto akiwa amewaacha nje, “vipi umekutana nae tena?” aliuliza Sophia, huku anapokea mfuko toka kwa Adellah, na uchungulia ndani, anaona kuna mazaga kama yote, “yani karibia nikate tamaa, mala namwona huyu hapa” alisema Adellah, na kusimulia ilivyo kuwa, mpaka yule kijana alipo mpatia elfu moja, na kumweleza kuwa kesho watajuwa lakifanya, “nimemwacha anatazama video, akaniambie niende nikamsaidie kupika wali yeye awezi, mimi nimemwambia siwe kwenda” alisema Adellah, akiwa amegeuza kidogo maneno, “mh! jamani siumesema anakaa hapo juu tu, nenda kamsaidie, we uoni kaka wawatu anavyo kusaidia” alisema Sophia, huku anaanza kusembua vitu vilivyopo kwenye mfuko, aliokuja nao Adellah.


Adellah akajichekesha kidogo, “lakini dada je akitaka tulale, unazani nitafanyaje?” alisema Adellah, kwa sauti ambayo ungeshindwa kuielewa kama anataka au ataki, “hapo sasa hakiri kichwani, kama unamwona anakufaa na anamalengo na wewe, sawa, kama unamwona akufai sawa, mimi siwezi kukukatalia, ata kama ukilala nae na baadae ukagundua akufai, pia sawa, kwaniumesha tembea na wangi na umeachana nao” alisema dada Sophia, huku akiwa busy na kutoa mazaga kwenye mfuko, “basi mimi nitaenda, sasa nikichelewa kurudi shemeji utamwambiaje?” aliuliza Adellah, kwa sauti ya kujifanya kama anaogopa, “kwani shemeji yako anakuzuwia kuwa na mchumba, mbona yule mbabaishaji anakuja mpaka hapa” alisema Sophia, na wote wakacheka kicheko cha chini chini, “lakini kabla ujaondoka uoge ubadiri nguo ndio uende, maana nasikia kajasho kwa mbali” alisisitiza Sophia, nikama alikuwa anatengeneza mazingira ya mdogo wake kwenda kuliwa bumunda.




Naaam! Sebastian mida hii alikuwa sebuleni kwake, amekaa chini kabisa, kama kawaida yake, kochi lake la kisasa, likiwa ndiyo kiegemeo chake, akisaidiwa na mto mmoja mkubwa sana, ambao ni mmoja kati ya mito minne, iliyokaa kwenye kila kochi moja kubwa, huku tayari minofu ya kuku hipo juu ya waya ulio tandikwa juu ya jiko, ikiiva vizuri taratibu, sambamba na ndizi zilizokuwa zinachomwa vizuri kwa mafuta ya kuku huyu wakienyeji, yeye kijana wetu anakata kachumbali taratibu, macho kwenye TV, huku mkono mmoja wa kushoto mala moja moja ukiwa unanyakuwa grass yenye wine, na kuiweka mdomoni, anapiga funfa moja kisha anairudisha chini, harufu nzuri ya mchomo wa minofu ya kuku ilitawara mle ndani, pengine ilikuwa inasikika ata kule barabarani kama iliyo kawaida yake.


Sebastian anawaza jinsi mwanamke mzuri kama yule, anavyoweza kuwa na maisha magumu namna ile, kiasi cha kushinda kutwa nzima ajapata chochote tumboni, tena siyo yeye peke yake, ni pamoja na watoto, ambao kiukweli wanaishi wakiwatazama wanao walea, zaidi ya hapo awakuwa na uwezo wakujitafutia, “mh! inatia huruma kwakweli, yani ndio napata watoto alafu nawaacha wanaangaika namna hii” aliwaza Sebastian huku anahisi moyo wake unasisimka kwa maumivu.


Yap wakati Sebastian anaendelea kuwaza huku anageuza minofu na ndizi, bila kuacha kukata kachumbari, ambayo sasa ilikuwa inaelekea kumalizika, mala anagutushwa na sauti ya kugongwa kwa mlango, “hodiii!!!” inasikika sauti ya kike toka nje ya nyumba ile kubwa, Sebastian anatulia sekunde kadhaa, akiitafakari hodi hii, ya saa tatu usiku, “hodiiiiii” inasikika tena sauti ya kike, sambamba na kugongwa kwa mlango, “hoooo! niyule dada, yani ameamua kuja saa hizi?” najiwazia Sebastian, huku anainuka na kwenda kufungua mlango, nikweli anamwona Adella, mschana ambae amjuwi ata jina, ambae safari hii alikuwa tofauti na alivyokuwa muda ule, “hooo kumbe ni wewe, karibu ndani, nilijuwa huto rudi, maana muda umeenda” alisema Sebastian huku anamtazama sasa wawatu ambae licha ya kujifunika kanga nyepesi, lakini ndani alivaa gauni jepesi na fupi, ambalo licha ya kuonyesha vyema hips zilizo chomoza kidogo za Adella, na makalio yake yenye ukubwa wa wastani, lakini gauni ili, lilishindwa kufunika kuanzia mapajani mpaka miguuni, “we acha tu, nilikuwa navizia kumtoroka dada, najuwa angenikataza kutoka” alisema Adellah, huku anaingia ndani, ambae safari hii siyo siri, alifanikisha kuishtua dudu ya Sebastian, sijuwi kwanini alivutika na midomo ya mwanamke huyu, ambayo ilikuwa ime pakwa rangi yenyekundu.


Sebastian anamsidikiza Adella kwa macho, akitazama jinsi maeneo ya paja yake yaliyoonekana kidogo maeneo ya magoti kwa juu, ambae anaenda moja kwa moja na kukaa kwenye kochi dogo, linalotazama kule aliko kuwa amekaa Sebastian mala ya kwanza, “sasa ukirudi siatakusema sana?” aliuliza Sebastian, huku anafunga mlango na kurudi pale alipokaa na kuendelea kukata kachumbari yake, “nita mwomba msamaha” alisema Adellah, huku anainuka na kwenda kusogelea pale alipokuwa amekaa Sebastian, “ngoja nikusaidie” anasema Adellah, huku anachuchumaa kuchukuwa bakuri na vitu vya kutengenezea kaachumbali, pasipo kujari kuwa gauni lake fupi limeachia uvungu, na kwabahati mbaya, macho ya kijana wetu Sebastian, yanaelekea kwenye ile vungu ya mwanamke, ambae yupo upande wake wa kulia, anachokiona anashindwa kuelewa kama ni nguo ya aina gani, lakini hakili yake inakataa kwamba mwaname huyu ajamaa nguo ya ndani.


Licha ya kuto kujuwa kama ni nguo au ni yenyewe, lakini Sebastian anapatwa na msisimko wa ajabu, kiasi cha mwiko wakekuzidi kusimama, anainua uso kumtazama Adellah, anamwona anatabasamu, pasipokuwa na wasi wasi, kwamba ile vungu hipo wazi, “haaa!! pumzika tu dada, nimesha maliza, leo wewe ni mgeni wangu wacha nikuandalie vitu” alisema Sebastian huku anaikuka pale aliposimama na kunyayuwa bakuri analiweka mezani, macho ya Adellah yanatuwa kwenye kaptulah ya kijana wetu, usawa wa zip, anaona jinsi mtu wa mwiko ulivyo jaa vyema, anakosa uhakika, kwamba kuna kitu aliweka ndani kijana huyu, au ni ile ile ya mwanaume, anajikuta akisisikwa, huku akifurahi kimoyo moyo kwamba, anafanikiwa kumtoa nyoka pangoni, “ndani nina soda za cola tu, uwa natumiaga asubuhi, kukata uchovu wa wine, unaweza kutumia?” aliuza Sebastian, huku anamgeukia yule mwanamke mgeni, ambae sasa alikuwa amerudi na kukaa alipokuwa amekaa mwanzo, anagundua kuwa macho ya mwanamke yule, yapo kwenye usawa wa zip yake, kwa hiyo ameona jinsi dudu ilivyo jitutumua, anatamani kuiweka sawa, lakini anashindwa kufanya hivyo mbele ya mwanamke yule, hivyo anageuka, na kujifanya anaweka sawa vitu mezani.


Ukweli Adellah, kwa sababu alizo zijuwa mwenyewe, anatamani sana kufanya chochote na mwanaume huyu, na kuwa tayari kusingizia kitu chochote, ili kieleweke usiku huu huu, “mmmh! Kwani hiyo unayokunywa ni chungu sana?” aliuliza Adellah, huku anatazama chupa ya wine, “siyo chungu, lakini nipombe” alijibu Sebastian, huku anaelekea upande wa jikoni, “lakini nikinywa kidogo sitoweza kulewa sana, maana nisipokunywa nitashindwa kukaa hapa vizuri, muda wote nitaona aibu” alisema Adellah, na hapo bila kujiuliza chochote, au kutilia mshaka, Sebastian anakubariana na mgeni wake, ambae anamletea grass, huku amebeba sahani mbili, ambazo waliweka nyama na ndizi kachumbali pembeni, kisha wakaanza kula taratibu, huku wakishushia wine.


Naaam! nusu saa baadae, tayari walikuwa wamemaliza kula, sasa wanaendelea kunywa wine, huku wanaongea ili na lile, macho kwenye TV, wakitazama filam, lakini kuna jambo lilianza kwenda tofauti kidogo, maana kila muda ulivyo zidi kusonga, Adellah, alianza ujiachia katika ukaaji, siyo tu kuegemea kochi, ila pia kutanua miguu, na kuacha duka la mzungu wazi, na kumfanya Sebastian atambue kuwa, mwanamke huyu ambae sasa walisha tambuana majina, kuwa ajavaa nguo ya ndani, “kwanini aujaowa mpaka sasa, wakati unamaisha mazuri?” aliuliza Adellah, ambae sasa alikuwa amepandisha mguu mmoja kwenye kochi, na kuachia kutumbua wazi, yani kama avile akuwa na taarifa ya uwazi huo, uvunguni kwake, ata alipo mtazama usoni, alimwona akimtazama kwa macho legevu ya kutamanisha kumnyandua, “nitaoa tu” alisema Sebastian huku anacheka kama bwege. .

Itaendelea

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)