NGOJA NILEWE 8

Emmanuel Lee
By -
0

 NGOJA NILEWE 8


MTUNZI: Mbogo Edgar

WHATSAPP 0743632247 

ILIPOISHIA 7 : Hapo Seba akacheka kidogo, maana alijuwa fika kuwa akuwa na ndugu yoyote dar, ila yeye ndie ndugu pekee wa ndugu zake, alie wai kuishi dar, tatizo akujuwa kwanini ameulizwa swali ilo, “hapana dada yangu, akuna ndugu yangu anaeishi dar, labda kama mama ajawai kunieleza” alisema Sebastian ambae alikuwa anasubiri huyu dada amalize ili na yeye amuulize alisomaga sekondari gani, ili uwe mwanzo wa kuelekeza shida yake ya kuomba msaada wakupata kazi, “kweli una uhakika, kaka yangu?” aliuliza yule dada, huku akionyesha kuto kumwamini Sebastian, kwa jibu alilompatia. ,…… . ENDELEA……..


Sebastian mwenyewe akatoa macho ya sijuwi ajibu nini, “kweli dada, kwa mama nimezaliwa peke yangu, na kaka yangu kwa mama yangu mkubwa, anaishi nyumba hii hapa, nimefikia kwake, labda upande wa baba, maana sijawai kuwaona wala kujuwa wako wapi” alisema Sebastian, ambae moyoni alikuwa anawaza jinsi ya kuanza pilika zake, “mh! kama ni hivyo sawa, maana unafanana na kaka mmoja hivi, mwanzo alikuwa anakaa dar es salaam kigamboni, siwezi kumsahau, yani mnafanana sana, kuanzia sura rangi ata uongeaji wenu, jinsi unavyocheka na….” mpaka hapo Sebastian alisha kumbuka kitu, akajikuta anashindwa kusubiri mwanamke huyu amalize kuongea.


Hapo hapo akamkatiza, “weeee! Usiniambie kama wewe ni yule mwanafunzi wa chuo, nilie msindikiza kivuni siku ile mlipo maliza chuo?” aliuliza Sebastian, huku ametoa macho kwa mashangao, huku moyo wake ukijawa na furaha kubwa sana, kwakuona kuwa, sasa anaenda kusadiwa kupata kazi ya maana, “mh! wewe ndie yule kaka wa kigamboni?” aliuliza yule mwanamke akijiziilisha kuwa ndie Vanesa, huku akimtazama Sebastian kwa macho ya kutilia mashaka, kitendo ambacho Sebastian alikitambua ni kwanini, utambuzi ambao ulimfanya Sebastian anyongee, ukweli ni kwamba Vanesa, alishangazwa kwa mwonekano wa Sebastian, ambae ambae mala ya mwisho alimwona kama kijana mtanashati, mwenye uwezo mzuri kifedha, tofauti na anavyoonekana sasa hivi mbele yake.


Kwakulijuwa ilo, Sebasyian akajuwa kuwa sasa anaenda kukosa ata ule msaada ambao alikuwa anautarajia, “ni mimi dada yangu, nazani umeshtushwa na mwonekano wangu, ni hadithi ndefu sana” alisema Sebastian kwa sauti yakinyonge yenye kukata tamaa, “hadithi ndefu, hipi kaka yangu, au ulizidisha ulevi ukafukuzwa kazi?” aliuliza Vanesa kwa sauti ya kusimanga, huku lile tabasamu likiwa limeondoka kabisa usoni mwake, “hapana dada yangu, ila wema wangu ndio umeniponza, kuna watu niliwasaidia wakaamua kuchukuwa kila kilichokuwa changu, na kuniacha kama hivi nilivyo” aliongea Sebastian kwa sauti ya kinyonge, huku anapiga hatua moja nyuma toka kwenye gari, akimwachia nafasi yule mwanamke, aondoke zake, nae akaondoa gari kwa speed kali sana, tofauti na vile ambavyo tumezowea kumwona akiendesha.


Sebastian alisimama akilitazama lile gari, huku moyoni mwake akizidi kuthibitisha kuwa, tenda wema nenda zako, usingoje kuambiwa shukrani, maana kama dada huyu, ambae alimsaidia kusafiri tena kwa ndege, leo hii na yeye anaondoka kwa kumzalau kama hivi, lakini akuwa na lolote la kufanya, zaidi ya kutimiza mpango wake wa kurudi kwa mama yake, japo ni wazi anaenda kumtoa machozi mama yake huyo.


Sebastian akiwa anawaza juu ya mstakabari wa maisha yake, alienda kununua maandazi na kisha akarudi na kuwasha jiko kwaajili ya kuchemsha chai, huku akiona wazi jinsi wapangaji wenzake na George walivyo kuwa wanamtazama kwa macho ya kumsuta, inaonekana waliona wakati anaongea na Vanesa, japo awakusikia walichokuwa wanaongea, Sebastian ambae alijuwa kilicho mtokea siyo kosa lake, ila nimaagizo ya manabii na mitume, kwamba tupenda na tusaidiane, aliendelea na kazi zake, huku mawazo yake ni namna gani mama yake ataweza kukabiri ukweli atakao mweleza, ukweli ambao ata mama yake alisha wai kuota siku za nyuma.

Naam, baada ya kumaliza kupika chai, Sebastian aliweka chai mezani, huku bado George akiwa amelala, akanywa chai taratibu, huku picha ya tukio la Vanesa, ambae ata akuwa anamjuwa jina, likiwa lina mjia kichwani, ata alipojaribu kulipuuzia, na kulichukulia kama tukio la kawaida, lakini ilishindikana na kuzidi kumtia machungu, alitamani akamkmbushe yule dada juu ya namna alivyo msaidia na ile ahadi yake ya kwamba, anatamani yeye ayapate malipo ya wema alioutenda na kwamba Vanesa mwenye awe njia ya kulipa malipo hayo, lakini Sebastian mwenyewe alajisemea moyoni, “malipo ya wema ayaombwi” na ukiomba inageuka kuwa deni, “Seba unazani utakaa mpaka lini bila kazi hapa mjini?” aliuliza George, na kumoa Seba akatika mawazo yake, ukweli Seba alishindwa kutoa jibu la swali la George, akaamua kutulia kimya, siyo kwamba alikosa jibu, ila ukweli ni kwamba jibu lisinge mpendeza George, ambae alionekana kuwa na hali flani ya ugomvi, “kukaa kimya ni kiburi, we fanya uondoke bwana, mimi siwezi kulala kwa kujibana wakati chumba ni chakwangu” alisema George huku anajiinua toka kitandani, na kuchukuwa mswaki na kikombe cha maji.


Ilitia uchungu, japo ni kweli alikuwa na mpango wa kuondoka, lakini siyo kwa kusimangwa namna ile, ukichukulia ni ndugu yake kabisa, na ukiachana na ilo ni mtu ambae alimsaidia sana, “kama ndugu ananifanyia hivi, kwanini nimshangae yule mwanamke” alijiuliza Sebastian, ambae licha ya hivyo, lakini bado alikuwa anaugulia maumivu moyoni mwake.


Naam Seba anamaliza kunywa chai, wakati huo George ana anaingia ndani, akiwa amemaliza kupiga mswaki, “najuwa unashindwa kurudi kijijini, sababu wakati ule hupo kazini, ulikuwa unajiona wewe ndio wewe, ukawatambishia na kagari kako, bwanaeee, kama uwezi kurudi kijijini, basi tafuta sehemu ya kuishi nashindwa kulala na demu wangu kwaajili yako” alisema George, huku anaweka kikombe na mswaki kwenye sehemu yake.


Safari hii Seba alishindwa kuvumilia, “asante kaka, wewe ni mwalimu mzuri sana, endapo nitaweka kamambo yangu sawa, sitorudia makosa” alisema Sebastian kwa sauti yachini yenye utulivu, “bwanaeee ata ukijifanya unaongea kisomi sijuwi hooo mwalimu mala hoo kurudia kosa, iloshauri lako, mimi nachotaka uondoke bwana” alisema George, huku anajifuta maji usoni, na kutoka nje, akimwacha Seba akiwa anawaza ilina lile, mpaka alipopitiwa na usingizi.******


Naaam Sebastian alinajikuta anapokelewa na mama yake tofauti na alivyo fikiria, mama yake aonekana mwenye furaha kubwa sana kumwona Seba, mama ambae amepika vyakula vingi sana, kama kuna wageni, anaonekana akiwa amevaa vizuri, “mchumba wako yupo wapi?” anauliza mama Seba, pengine ingemtia unyonge, lakini ukweli aionyeshi kumshtua seba, nikama akuna kilicho tokea, “yupo kwenye gari mama siunajuwa kuna utaratibu wa wewe kumtoa kwenye gari..” anajibu seba, huku ameachia tabasamu, lakini wakati huo huo anatokea George, ambae aijulikani alifikaje kijijini, anamwita Seba kwa hasira, “Seba we Seba” anaita George, kwa sauti yenye jazba, huku anamsogelea Seba kwa hatua za haraka, Seba anashangaa, ajuwi kwanini ndugu yake amekasirika kiasi kile.


Wakati Sebastian anajiuliza kulikoni, mala George anamfikia na kumshika mguu, “wewe inamaana usikii bwana ebu amka bwanaaaa” Sebastiana anashtuka toka usingizini, masikini Seba, kumbe alikuwa anaota, anapo tazama vizuri kujikuta alikuwa amevitwa mguu, na sasa nusu ya kiwli wili chake kilikuwa kina ng’inia nje ya kitanda, bado mguu umeshikwa na George, ile anataka kuupapatua mguu wake toka kwa George, nae akamvuta kwanguvu, na Sebastian akajibwaga chini, na hapo ndipo Seba alipo gundua kuwa George akuwa peke yake, “jamani George, utamuumiza” alikuwa ni Adija, mchumba wa George, alie ongea huku anaziba mdomo kuzuwia kicheko kisiwe kikubwa.


Ilimuuma sana Seba, alijikuta anapatwa na uchungu mkubwa sana, machozi yakamlenga, akaona sasa niwakati wakuondoka kabisa kwa kaka yake, kam ni kusubiri muda kausubirie mbele ya safari, kuliko kukaa hapa, hivyo Seba aliinuka pale chini kiunyonge na bila kusema kitu, akachukuwa mfuko wake, akaweka nguo yake na bahasha yake yenye vyeti, kisha akamtazama Geroge kwa macho ambayo yalikuwa yanachuluzika machozi, “kaka asante sana, lakini naomba wewe ndie uwe wakwanza kueleza haya unayo nifanyia” alisema Sebastian kwa sauti ya unyonge kabisa, “nenda bwana, na ni atafanya ujinga kama huo, mimi nimekuambia toka muda mrefu uondoke, wewe unakaa tu” alisema George, huku anaweka vizuri shuka juu ya kitanda.


Naaam Seba akatoka mle chumbani taratibu, akisindikizwa na vicheko vya dharau toka kwa wapenzi wawili waliobakia mle chumbani, naen akashika njia yake, huku wapangaji wengine wakimtazama kijana huyu, kwa macho ya huruma, ni wazi walisikia maongea yao, na kujuwa kilicho tokea, ata wakati akiondoka zake taratibu, nao waliendelea kumsindikiza kwa macho, hakika Sebastian alijihisi aibu kubwa sana, lakini aikuzidi maumivu na uchungu, aliokuwa nao, zaidi alitembea taratibu mpaka alipo ikuta barabara, wakati huo huo akaliona gari la yule mwanamke, yani Vanesa, likija mbio mbio, nikama aliongeza mwendo, baada ya kumwona, safari hii alipofika usawa wake, akusimama, ila alimkata jicho moja, na kutazama mbele, akiendelea na safari yake.


Sebastian akasimama na kulisindikiza gari lile kwamacho, mpaka liliposimama mbele ya nyumba ile ya mwanamke huyu mrembo, na kupiga honi, na sekunde chache geti likafunguliwa na yule mwanamke, anaefunguaga kila siku, seba akamwona yule dada akisogelea mlango wa gari, ambalo lilikuwa limesimama pale kwenye geti, ni kama alikuwa anaelezwa jambo flani, Seba akaona aimhusu, hivyo akaachana nao.


Sasa Sebastian akiwa mwenye machungu moyoni, akusubiri zaidi, aligeuka na kuitazama ile nyumba aliyotoka, akawaona wapangaji wenzie na George wakigeuza shingo zao haraka, ili isionekane kama walikuwa wanamtazama, hakika Sebastian aliona kuwa dunia ime mgeukia, walmwengu wote wanamempa kisogo, “Ee mungu mwenyezi, kama kweli mimi ndie nilikuwa na makosa, basi hii adhabu iendelee kwangu, lakini kama iki kikombe akikuwa stahili yangu, basi naomba uniondolee, na yaliyopita yawe funzo kwangu” alisema Sebastian, kwa sauti ya chini, huku anageuka na kuanza kutembea, kushika uelekeo wa upande wa kushoto, yani njia ya kuelekea mjini.


Lakini basi, wakati anapiga hatua ya tano, akasikia nyayo za mtu aliekuwa anakuja mbio upande wake, akageuka kwa haraka kutazama, maana alihisi kuwa anaweza kuwa George, anakuja kumvamia, lakini alipotazama akaona kuwa akuwa George, ila alikuwa ni mwanamke, ambae kwa haraka haraka pasipo kuitazama sura, ambayo akuwai kuiona vizuri, akagundua kuwa ni yule dada anaemwonaga anafungua geti kwa Vanesa, aliekuwa anakuja mbio mbio usawa wake, “we! Kaka nimekuita mudawote huo ulikuwa unisikii” alisema yule mwanamke ambae alikuwa anatabasamu, kwanza nikama Sebastian alishangaa kidogo, “ulikuwa unaniita mimi?” aliuliza Seba, huku anatazama kule kwenye geti la nyumba ya Vanesa, akuona kitu zaidi ya geti ambalo lilikuwa wazi, “ndiyo, nimetumwa na dada Vanesa nije nikuite” alisema yule dada, na kumfanya Seba, ajihisi kama yupo kwenye ndoto, kama aliyotoka kuiota muda mfupi uliopita.


Alimtazama huyu dada, kwa mshangao wakutoamini, kisha akatazama kule kwa Vanesa, alafu akamtazama tena yule dada, “una uhakika kuwa ananiita mimi?” aliuliza Seba, ambae ni wazi kabisa akuamini alicho kisikia, “ndiyo, amesema nije kukuita, kuna kitu anataka kuongea na wewe” alisema yule dada, huku anaanza kuondoka kurudi alikotoka. 


Sebastian akusubiri yule dada afike mbali, hivyo akiwa na mfuko wake akaanza kutembea kumfwata yule mwanamke, huku akikatiza pale alipokuwa amefikia, na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye geti la lile jumba, la kifahari, ambalo geti lilikuwa wazi, na kumfanya kijana huyu, aweze kushuhudia magari manne yaliyo simama upande wakushoto, wa jumba moja kubwa zuri na la kifahari, lenye kupambwa na mauwa mazuri na jamvi la sementi, lililowekwa mbele ya jumba, na kwenye vinjia vya kuzunguka jumba lile la kifahari.


Seba alitembea taratibu kuingia ndani na kusimama kidogo, akimsubiri yule dada funge geti, wakati huo yeye akiwa anatazama mandhari ya mle ndani, karibu ndani” ilisikika sauti toka upande ulipo mlango wa jumba lile, Seba akatazama upande huo ilikotokea sauti, akamwona yule mrembo, akiwa amesimama mlangoni, huku amevalia gauni lililoshonwa kwa kitenge, ambalo lilikuwa limemkaa vyema na kuonyesha vizuri kabisa, umbo lake zuri la kuvutia, aliekuwa anatabasamu, “asante sana dada” aliitikia Sebastia, huku anapiga hatua, kusogelea mlangoni, “vipi kunasehemu ulikuwa unaenda, maana nimekatisha kazi zangu ofisini, kwaajili yako, au nitakuchelewesha” alisema mwanamke huyu, ambae sasa Sebastian analifahamu jina lake kuwa anaitwa Vanesa, ni baada ya dada wakazi kulitaja, “hapana dada yangu, nilikuwa niende kupoteza muda huko mjini, kabla sijaondoka kurudi kijijini” alisema Sebastian ambae sasa alikuwa amesha mfikia mrembo Vanesa, ambae sasa hivi alionyesha kuwa mwenye tabasamu, japo uso wake ulionekana wazi kuwa alikuwa ametoka katika zimanziflani.


“hoooo! kumbe unaenda kijijini, sasa unatajia kurudi lini?” aliuliza Vanesa, huku anachukuwa mfuko toka kwa Sebastian, na kuingia nao ndani, huku Sebastian mwenyewe akivua viatu vyake, akimfwata yule dada kuingia ndani ya jumba ili la kifahari lenye thamani za anasa na gharama kubwa, “mh! kurudi huku ni mwisho wa mwezi, maana ndio wakati viwanda vingi vina ajiri wakati huo” alisema Sebastian, ambae alikuwa amesimama karibu kabisa na makochi ya kifahari, akimtazama dadayulembae alikuwa amenda na kukaaa wenye kochi moja dogo la mtu mmoja, “kwanini usinge subiria hapa hapa mjini?” aliuliza Vasena huku akiwa amesimama ameushikilia mfuko wa Sebastian.


Swali lilikuwa jepesi, lakini jibu jepesi la swali ilo, lilikuwa na ugumu kulitoa, maana lilijaa udhaufu na machungu makubwa sana, wakati huo yule dada alikuwa anaingia mle ndani, kabla Sebastian ajajibu, Vanesa akamgeukia yule dada, “dada niandalie kule sebuleni kwangu” alisema Vanesa na yule dada akalifwata kulido la moja kati ya tatu zilizomo mle ndani, “ujuwe toka nime toka dar, sijaenda kumsalimia mama, pia nimuhimu kwenda kumweleza kilicho nikuta” alisema Sebastian, aliekuwa bado amesimama huku anazungusha shingo yake kila kona ya sebule kutazama ufahari wa ile sebule, “Seba karibu ukae kaka yangu, tusubiri dada atuandalie sehemu tupige story vizuri, wacha niweke huu mfuko ndani, unisimulie kilichotokea maana sielewei, japo kwachochote ulicho kifanya naamini mimi siyo sababu, na wala aiingiliani na kujuwana kwetu, naamini utanipa muda wako leo” alisema Vanesa, huku anatembea kuelekea upande lilipo kolido, pengine ndio kiliko chumba chake cha kulala, maana ndio upande wenye hiyo sebule, inayoenda kuandaliwa, wakati kolido la upande wa pili lilikuwa na vyumba vinne.


Sebastian alitulia pale sebuleni, kwa dakika kadhaa, akiwaza na kutafakari jinsi mambo yalivyotokea, maana tayari alikuwa amesha sahau kile alichokuwa anamuwazia dada wawatu, sasa alianza kuona dalili ya kuweza kusaidiwa kupata kazi, ambayo japo isingemrudisha kwenye hadhi yake, ya mwanzo, mala akamwona mwenyeji wake anarudi, lakini akukaa, alipitiliza jikoni, ambako alirudi na vyombo kadhaa, alivyopitiliza navyo kwenye meza ya chakula, “pole, naona nimeakuacha peke yako” alisema Vanesa, huku anarudi tena jikoni, “hapana dada wala usiniofie” alisema Sebastian ambae aliona dalili za kuandaliwa chakula.


Naam chakula kiliandaliwa, huku Vanesa akimtupia tumaneno twa utani wenye kuchangamsha, “vipi ukufanikiwa kudaka mrembo wa chuo kule kigamboni?” aliuliza Vanesa wakati flani wakati wanakula, “hapana dada yangu, kule niliama” alisema Seba, “najuwa uliama, maana kuna wakati nilikuja kule, na kukuulizia, nikaambiwa umeama, na akukuwa na mtu anae fahamu ulipoamia” alisema Vanesa, wakiendelea kula chakula ambapo ilikuwa ni saa tano asubuhi, lakini ungesema nichakula cha mchana, tena wenye maandalizi yakipekee, “niliamia kibamba, ambako kuliniaribia maisha yangu” “tena itakuwavyema ukinikinisimulia kilichotokea, kama autojari” alisema Vanesa, huku wakiendelea kula, “usijari nitafanya kama ilishapita, wakati nakusimulia” alisema Sebastian, ambae alianza kumsimulia Vanesa mkasa mzima, akianzia toka siku amemkumkuta Adellah, gengeni kwa Baraka, akiomba akopeshwe chakula, kwamadai ya kwamba familia ilikuwa aijala toka asubuhi, na yeye kuamua kumsaidia.

 Sebastian aliendelea kumsimulia Vanesa jinsi Adelah alivyo mwingiza mtegoni, na kumsingizia mimba, huku akiwaidia Sophia na mume wake, ata alivyo mleta songea kwa mama yake, na yeye kuwatembelea wazazi wa Adellah, Seba alisimulia ndoto ya mama yake, yani kwa kifupi alisimulia kila kitu, ata ujio wa bwana Daniel waliemtambulisha kama kaka yao, na jinsi alivyo shtukia kuwa Adellaha anaujauzito mwingine, wakati yeye alikuwa anamiezi nane ajatembea nae, na jinsi walivyo mtegea bangi ofisini kwake na yeye kukamatwa, “nilikaa miezi minne mahabusu, nikashinda kesi huku ikibainika kuwa alie nifanyia vile ni Daniel, na nilipotoka mahabusu, nikagundua kuwa waliousika ni Daniel Daellah, na Sophia, ambae waliamia mbali kabisa, ili nisiwapate, maana walisha uza nyumba yangu na gari” eleza Sebani, katika hadithi yake, uku akieleza jinsi alivyo angaika kutafuta kazi bila mafanikio, na kuchukuwa uamuzi wa kuja songea, ambako licha yakukaasiku chache, lakini aliona wazi jinsi ndugu yake alivyo mnyanyapaa, na jinsi alivyo angaika kusaka kazi bila mafanikio.


Mwisho wa simulizi iliwakuta wawili awa wamekaa kwenye ukumbi wa chakula, lakini bado walikuwa wamesha maliza kula, “pole sana Seba, nazani kwa mala ya kwanza ulijutia tabia yako, ya kupenda kusaidia watu” alisema Vanesa, ambae ni wazi aliudhunishwa sana na kile alichofanyiwa Sebastian, “hapana sijawai kujuta, ila nimejifunza kutokana na ilo” alisema Sebastian, ambae akuonekana kunyongea, wala kuudhunishwa, “tabia ni kama ngozi, kuibadiri ni kujitia kilema” alisema Vanesa, na wakati huo dada wakazi aliingia kwenye ukumbi wa chakula, “dada ukumbi hupo tayari” alisema yule dada wakazikwa sauti ya upole, huku Seba akimtazama kwa macho ya kuibia, na kuona jinsi alivyo umbika, kiukweli siyo kwamba alikuwa mzuri kama Vanesa, ila kwa nafasi yake, alikuwa mzuri aswaaaaa, na kama ungemfananisha na Adellah, Adellah asinge mfikia ata nusu yake, na hiyo ni baada ya kupewa matunzo ya hali ya juu, na bwana Sebastian, ila yote kwa yote, dada wakazi nae alikuwa wamoto, siyo kama yule mwanamke wa George. 


Sebastian ambae alikuwa miezi mingi ajagusa wala kukiona kitumbua, alijikuta akiwaza ujinga, “sawa dada Shani, wewe kajiandae, ukasalimia wazazi liwena, utarudi jumapili, sawa? Nitakupa fedha ya kuwanunulia zawadi wakina mama” alisema Vanesa, kwa sauti iliyojaa upendo wa hali ya juu, sambamba na tabasamu laini, lililo nurulisha uso wa mrembo huyu, lakini hapo mwanamke huyu alieitwa Shani, alionekana kushtuka kidogo, nakutoa macho, yaliyouliza “kwani nimekosa nini” niwazi alihisi kuwa anafuzwa kazi, lakini nikama Vanesa alisha hisi fikla za Shani, “lakini hiyo ni nje ya mshahara wako, nyumba nitaitunza mwenywe” alisema Vanesa, akiendelea kuachia tabasamu mwanana.


Hapo Shani akaonekana kutabasamu, “asante dada, nibora kama kunakazi ya kufanyaniifanye kabisa, iliniwai gari la mwisho” alisema Shani, akionekana kufurahi sana, muda huo Seba alikuwa anafwatilia maongezi hayo, huku kwaumakini mkubwa, akiudifu mwili wa mwanamke ambae alianza kupanga moyoni kuwa akifanikiwa kupata kazi, aongee na Vanesa, ili amuoe Shani, maana isingewezekana kwa yeye kumtamani Vanesa, ambae ni mzuri kuliko neno uzuri linavyo andikwa, sababu ata alisha potedha ile nusu hadhi aliyokuwa nayo ya kuwa na mwanamke huyu, “hakuna kazi yoyote leo, nitashughulika mwenywe, wewe maliza kujiandaa, mimi naingia bafuni, nikitoka nikupe fedha uwai” alisema Vanesa, huku anainuka toka kwenye kiti, Seba, karibu huku tafadhari” alisema Vanesa, na Seba ainuka na kumfwata Vanesa, ambae alikuwa anaongoza kufwata kolido, fupi lenye milango mitatu, na kabati la viatu, lililo sheheni viatu vingi sana vya kike, vyote vikiwa vizuri vya kisasa, na vya gharama kubwa, sambamba na kioo kikubwa pembeni ya kabati lile, ambacho kilikuwa kinaonyesha kuanzia kichwani mpaka miguuni.


Kwa dokezo dogo ni kwamba, kati ya milango ile mitatu kwenyekolido la upande wakushoto, mmoja ulikuwa wachumba chake, iliotanguliwa na mlango wa ofisi yake ya Vanesa ya hapa nyumbani, na mlango ambao ulikuwa mwishoni kabisa mwa kolido ukitaazama mbele, huo ndio mlango walio ingia, wawili awa, na kujikuta wakiwa ndani ya sebule flani ndogo yenye set moja makochi na meza ndogo, choini ikiwa imetandikwa zuria la sufi, kwamaana ya kitu kama manyonya flani yenye rangi ya samawati, na dhahabu, ukikanyaga unajishi nyayo zinatekenywa, mbele kulikuwa na TV moja kubwa ya nchi alobaini nambili, sambamba na seti ya music.


Kingine kilicho mvutia seba, ni vilevitu walivyo vikuta mle ndani ya sebule, yani mbele ya makochi chini kwenye zuria, kulikuwa na chupa moja kubwa ya mvinyo toka #mbogo_land, maarufu kama #mbogo_land coco wine, sambamba na grass mbili zenye shingo ndefu, maanarufu kama mwanamke kiuno, pia kulikuwa sahani yenye korosho toka kusini mwa tanzania, ndani ya sebule hii iliyowekewa madirisha makubwa ilikuwa inanusikia vizuri, na panzia zilikuwa zime shushwa kwenye yale madirisha, na kufanya kuwe na hali flani ya giza, huku kukiangaziwa na rangi ya blue yenye mwanga afifu, ungesema kulikuwa na tukio moja muhimu lilikuwa linaandaliwa kufanyika mle sebuleni.


Karibu seba, naamini mazingira ya umundani utayapenda, maana wewe ndei ulie nifundisha kufanyahivi, alisema Vanesa, huku akimwelekeza Sebastian kwamba akae pale chini kwenye zuria, ambapo pia kulikuwa namito mikubwa minne, seba naakusubiri aambie mala mbili, akaa chini, taratibu, huku anaendelea kutazama kile chumba kizuri, ambacho ata wakati ule yupo kazini akufikilia kuwa anaweza kuweka sebue ya nyumba yake kuwa kama hivi, “Seba naomba uwe huru, yani jisikie kama hupo nyumbani kwako, alafu mimi ndio mgeni wako” alisema Vanesa, ambae sasa alikuwa anamimina wine kwenye grass moja na kuiweka, “asante sana” aliitikia Sebastian ambaealikuwa anajaribu kutazama mwanamke huyu kwamacho yawizi, nakuona jinsi umbo lake lilivyo kaa vizuri, huku moyoni kijipa onyo kuwa, kama asipo angaika kupata kazi, basi warembo kama awa ataishia kuwaona kama hivi, na pengine akaangukia kwa mwanamke kama yule wa George, ambae kwa yeye ata kwa ukame aliokuwanao, asingeweza kumaliza ata mzunguko mmoja, juu ya chungu kile cha Adija,


Naam Vanesa, alimpatia Sebastian grass ya wine na “najuwa ujaacha bado” alisema Vanesa, wakati anampatia Sebastian ile Grass, nae akaipokea ile grass, “sijuwi kama niliacha au nilisimma au sababu nimefilisika” alisema Sebastian na wote wakacheka kwa pamoja, “Seba bwana, bado ujaacha vituko vyako” alisemaVanesa, huku anasogelea Tv na kuiwasha, nakuweka CD ya music ya mwanamusic Shania Twain, “sasa Seba naomba akika chache, nikatoa jasho usije ukanikimbia” alisema Vanesa, huku ameachia tabasamu moja matata sana, “mh! kwajasho gani dada Vanesa, wakati mimi nasikia arufu nzuri ya manukato” alisema Sebastian ambae kiukweli akijifanisha na yeye, ambae akuwa na mpango wa kwenda kuoga, na huyu anaesema anaenda kupunguza jasho, ungesema anamthanifu, wote wakacheka huku Vanesa akiwa anatoka nje ya ile sebule, akimwacha Sebastian anapata wine yake taratibu, huku anatazama music laini kabisa.*********


Yap! dakika ishilini baadae Vanesa alirudi mle sebuleni, akiwa amevalia kijigauni flani chepesi balaa, yani chepesi alafu kifupi mpaka kati kati ya mapaja, ila kiliachia flani, japo aikusaidia kitu, maana Seba alijikuta akiinua mnazi, sawa na paka ane tamani maziwa ndani ya fliji, na wakati anajuwa fika kuwa awezi kuyapata ata kwa bahatimbaya, labda kwa huruma ya bwana wake, “pole nimekuacha peke yako” alisema Vanesa, huku anakaa kwenye dhuria, karibu na sebastian, wakiwa wametenganishwa na grass na chupa ya wine, “hapana, nilikuwa pamoja na TV, alisema Sebastian wote wakacheka kidogo, “lakini TV sio sawa na mimi nikiwepo, sindiyo?” aliuliza Vanesa, kwa namna flani hivi kama ya kudeka, asauti ambayo ilimsisimua kidogo Sebastian, na kujikuta akikosa jibu kwa sekunde kadhaa, wakati Vanesa, akiwa busy anamimi na wine kwenye grass, “yaah ! yaah ! ni…nisawa nikweli kabisa” alisema Sebastian, kwamsauti iliyo kwama kwama, “sasa je nilitaka nishangae yani usinimiss kwaajili ya TV, alisema Vanesa kwa utani, kisha akanywa wine kidogo na kuiweka chini grass.


Baada ya hapo, kikapita kimya kifupi, wakiachia music utawale, nikama kila mmoja alikuwa anatafuta aanzishe hadithi gani, “nime kumbuka, kuna movie moja hivi niliinunua sijaitazama aSebastian, afadhari leo nimepata kampani” alisema Vanesa, huku anaweka grass chini na kujiinua, katika kuinuka sasa nakile, kigauni kilivyo kifupi, dah! na bahati mbaya zaidi kwa ukaribu waliokuwa nao, Seba akuwa na ujasiri wa kuzuwia macho yake, kutazama maeneo ya karibu na uvungu wa mwanadada huyu, japo mapaja yake manene yalizuwia macho kufika kwa bibi, lakini kwakile alichokiona kilitosha kabisa kuinua winchi yake, bahati zaidi nikwamba, Vanesa akuakuangaika kabisa kuzuwia nguo ile isiachie utamu wazi, yeye akiinuka na kuelekea kwenye TV ambako aliinama kwaajili ya kutoa CD kwenye deck, hapo ndipo mambo yalipozidi kuaribika kwa Sebastian, ambae alijihisi kuwa pengine mda wowote anaweza kushusha watoto kwenye nguo, “ni move nzuri sana hii sema inaitwa #UTAKUFA_NA_SIRI_YAKO, ni ya #mbogo_land Studio, alisema Vanesa wakati anabadiri CD, huku akimwachia Sebastian ajitazamie Video nyingine, aliyo iachia mwenyewe, maana kigauni kilikuwa kimepanda juu na kuachia anekubwa la nyuma ya mapaja mpaka mwanzoni mwa makalio, likionekana wazi wazi. 


“nawakubari sana awa jamaa, movie zao zina visa vizuri sana” alisema Sebastian, wakati huo anakwepeshamacho na kuzuga kwamba akuwa anatazama video ya hasiri, ni baada ya kumwona Vanesa, akichukuwa remote, na kurudi alipokaamwanzo, “asawaaa awa jamaa, wanamovie nzuri sana, yani kila zinapotoka uwa siachi kununua, alisema Vanesa wakati anakaa, kisha akaicheza ile CD na filamu ikaanza kuonyesha, nao wanaendelea kutazama huku wanaendelea kunywa wine, na kushushia korosho.*******


Naaam nimuda mrefu sana atuajaangazia dar es salaam, ambako sasa tutaanza kuangazia kule chanika, ambako tunaanzia pale njia panda ya mvuti, kwenye duka la bwana Philipo, ambae tuna mkuta akiwa amekaa kwenye kiti chake, huku mala moja akipokea mteja na kumhudumia, mala nyingi sana mida hii uwa na wateja wachache, labda kwa siku za weekend za, mwisho wa mwezi, bwana Philipo anasinzia kidogo, anaamshwa na muayo wa njaa, maana leo mke wake akumletea chai kama ilivyokaida, lakini ilo alikumshtua sana, sababu asubuhi alikuwa anafua, ata hivyo alitegemea kuwa, mke wake ambae ni sophia angewai kumletea chakula cha mchana, kutokana na kukosekana kwa chai.


Lakini licha ya kusubiri mpaka saa saba, akuna chakula kilicho letwa, saa nane kasoro ndio muda ambao, Philipo alipomwona mke wake akiingia pale dukani, ameongozana na Adellah mdogo wake, alie kuwa na watoto na watoto wawili, yani Samuel na mwingine mchanga ambae kama alijitaidi sana, basi alikuwa anakaribia mwezi wa pili, “naomba elfu ishilini” alisema Sophia, mala baada ya dellah, kusalimiana na Philipo, hapo Philipo bila kuuliza ile la ni yanini, akazama kwnye drow ya meza kubwa ya pale dukani yenye kujaa noti kadhaa za fedha, na sarafu, Philipo anaanahesabu noti kadhaa mchanganyiko, mpakazinapotimia elfu ishilini, anamkabidhi mke wake.


Mwananzo alizania kuwa mke wake kuna kitu anaenda kununua kwaajili ya dukani, “Adellah, mi nakushauri huyo mwaname kama akufai achana naewakati bado mambo ayajawa mabaya zaidi, aiwezekai ela zote zile azichezee kwenye maulevi na umalaya, alafu wewe bado unamng’ang’ania, bola uchukuwe maamuzi mapemaaaa” alisisitiza Sophia huku anamkabidhi ile fedha, “sawa dada lakini nitafanyaje, maana yeye ndie baba wawatoto awa, nikisema niachane nae nitaishi wapi?” alisema Adellah, ambae kimwonekano alionekana kamwakati ule anakutana na Sebastian pale gengeni kwa Baraka, tena pengine na zaidi, maana achilia lile umbo alililo chanua akiwa na Sebastian, pia ata ngozi ya mwili wake ilisha chujuka na kuwa kama zaidiya vile alivyo kuja dar akitokea huko Lungwe, “sehemu ya kuishi wala usiwe na wasi wasi, ata kwangu utaishi, kwani ulipofika toka Lufilyo aulifikia wapi?” alisema Sophia, huku Philipo akiwasikiliza kwa maumakini, na ufahamu kuwa tayari mambo yalisha aribika kwa upande wa Adellah, lakini kilichomuuma ni fedha ambayo ilikuwa imetoka, maana ata toka asubuhi mpaka hii saa nane alikuwa ameingiza kiasi cha kama elfu sita au saba tu, kitu ambacho kilimfanya ashindwe kutuumia fedha wenda kula, lakini kilahisi tu, mtu anapewa elfu ishilini, ambayo yeye ameikusanya tokea jana, wakati miezi michache iliyopita walikuwa na milioni za fedha.


Baada ya maongezi yale ambayo yalichukuwa dakika tano, Adellah, akaondoka huku akisaidiwa na dada yake kumbeba mtoto mmoja maana ata afya ya Adellah na watoto wake, ilionekanakuwa dhaifu, Philipo alikuwa ametoa macho ya mshangao, akimtazama mke wake, ambae alikuwa anamsindikiza mdogo wake, kilicho mshangaza na kumduwaza ni kitendo cha mke wake kuja na kuondoka bila chakula, wakati anajuwa fika kuwa yeye ajala toka amekula jana usiku, “hivi huyu anaakili kweli?” alijiuliza Philipo, huku anaendelea kumtazama mke wake kwa macho ya hasira.


Kutoka pale dukani mpaka Stendi ya dala dala, siyo mbali, hivyo dakika baadae tayari Sophia alikuwa amesha rudi pale dukani, “hivi mimi nilizania utakuja na chakula, unajuwamwenzio toka jana sijala?” aliuliza Philipo, huku anamtazama mke wake kwa namna ya kumshangaa, “kwahiyo wewe unajari tumbo lako, mwenzio amekuja nanjaa ananyonyesha, toka jana ajala, amekuja kuomba ela kidogo, ndio amekuta chakula nilichotaka kukuletea, nikaamua nimpatie, wewe nnaenda kukupikia japo kitachelewa kidogo, maana mboga yenyewe amemaliza Adellah, alisema Sophia, huku anataka kuondoka zake, “ebu subiri kwanza, inamaana naitajika kusubiri zaidi ya hapa, alafu hii tabia ya kuchukuwa ela za dukani na kuwapatia wakina Adellah, mwisho wake nini, hapa mwisho wake ni kurudi kule kule tulikotoka, kushindia mlo mmoja na kukaa kwenye kijumba cha kujibana” alisema Philipo, kwa sauti yenye kuonya na kutahadharisha.


Wakati Philipo anazania kuwa maneno yake yangesaidia kumpatia tahadhari mke wake, kumbe alikuwa tofauti kabisa, “kwani we hii ela inakuuma nini bwana, siuliiona tu imesha kuja, huyo ambae unasema tusimpe ela ndie aliefanya ela ikaja” alisema Sophia na kumfanya Philipo aachame mdomo kwa mshangao, “na kwataarifa yako, yule ni mdogo wangu, siwezi kumwacha apate tabu wakati mimi jnauwezo” alisema Sophia, ambae safari hii akubakia tena pale, akaondoka zake, kufwata uelekeo wa nyumbani kwake, akimwacha Philipo ametoa macho ya kuto kuamini alicho kisikia toka kwa mke wake, “mh! kilicho mtokea Seba, ndio kinakuja kwangu” alisema Philipo kwa sauti ya chini, huku anatazama ndani yauka, kama vile anakagua bidhaa.**********


Naaam turudi Songea mji mwema, mita kama hamsini au sitini toka kwenye nyumba ya bibi Vanesa, hapa tuna zungumzia sehemuiliyopo ile nyumba kubwa ya wapangaji, nyumba ambayo mchana ungewaona wanawake watupu, na mida ya saa kumi na mbili ndio ungeanza kuwaona wanaume wanarudi makazini, kasoro mwanaume mmoja tu, ambae mudawote ungemwona pale nyumbani, lakini maisha yake hapo mwanzo yalikuwa mazuri zaidi ya wale wapangaji wengine, ambao kwa ratiba zao ni wafanyakazi, wasehemu mbali, mbali ata chumba cha George, kilishidana na vyumba vyao, maana alikuwa amesaidiwa vya kutosha na Mdogo wake Sebastian, ambae ametoka kumfukuza muda mfupi uliopita, na kumchungulia dirishani alipokuwa anaondoka, na alimwona akiitwa na binti wakazi wa nyumba kubwa la yule mwanamke Vanesa, ambae pale mtaani, wali mwita dada anae jisikia, maana akuwa na mazowea na vijana wa pale mtaani, iwe wakiume au wakike, na ata kisema apitie pale kwa mama Eva uwa ni hivyo hivyo, anakaa kwenye meza

 ya peke yake, na akikuta pamejaa, uwa anaptiliza na kuelekea nyumbani.


Itaendelea

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)