NGOJA NILEWE 9

Emmanuel Lee
By -
0

 NGOJA NILEWE 9


MTUNZI: Mbogo Edgar


WHATSAPP +255743632247


ILIPOISHIA SEHEMU YA 8 : 

ata chumba cha George, kilishidana na vyumba vyao, maana alikuwa amesaidiwa vya kutosha na Mdogo wake Sebastian, ambae ametoka kumfukuza muda mfupi uliopita, na kumchungulia dirishani alipokuwa anaondoka, na alimwona akiitwa na binti wakazi wa nyumba kubwa la yule mwanamke Vanesa, ambae pale mtaani, wali mwita dada anae jisikia, maana akuwa na mazowea na vijana wa pale mtaani, iwe wakiume au wakike, na ata kisema apitie pale kwa mama Eva uwa ni hivyo hivyo, anakaa kwenye meza ya peke yake, na akikuta pamejaa, uwa anaptiliza na kuelekea nyumbani. ,…… . ENDELEA……..


“yule mwanamke nae, sijuwi anaongea nae nini yule fala” alisema George, ambae toka siku za nyuma, alikuwa anatafuta nafasi ya kumnasa yule dada wakazi anaeitwa Shani, lakini akupata nafasi ata ya kumkaribia, labda aliomba kazi za ndani, kwa yule dada, siunaona anaenda kule kule, na yule dada amepta sasa hivi” alisema Adija, kisha wakacheka kwa pamoja, tena kwa dharau kubwa, “najuwa yule awezi kwenda Namabengo, sababu anaona aibu, jinsi alivyo kuwa anajidai na kagari kake” alisema George ambae kiukweli akutaka kujiangaisha kukumbuka msaada aliopewa na ndugu yake huyo, “ndugu yako nae, sasa kwanini akaamua kucjizoelea wamawake wa hovyo, usikute mwanamke mwenyewe mbayaaa” alisema Adija, kwa sauti flani yakubedha, huku akikunja mdomo wake kwa dharau, sasa kama ungebahatika kuona wakati akifanya hivyo, na ungelinganisha na anacho ongea, sijuwi kama ungeweza kujizuwia japo kwa sekunde moja, ili ukachekee chooni, “yani mama akisikia kilicho mkuta Seba, atafurahi sana, juzi alipofika tu nakunieleza upuuzi alio ufanya, nikaandika barua alafu nikaenda kuituma kwenye magari ya huko, kwa hiyo mpaka sasa kila mtu anafahamu kilichotokea” alisema Geroge, ambae ata yeye kama ungemwuliza ni kwanini alimchukia vile ndugu yake, asinge kupa jibu la kulidhisha.


Kwahiyo hapo unapata picha ya Geroge kuondoka siku ile toka asubuhi, akidai ameenda kufanya kazi, kumbe kazi yenyewe ni kupeleka umbea kijijini, na lengo la kumtimua ndugu yake ni kwamba akadhalilike huko kijijini, “huyu mshenzi akibakia hapa mjini anafaya kazi ya uhouse girl nitaandika tena barua kwa mama ni mweleze, ili mama yake akisikia achanganyikiwe kabisa” alisema George, ambae alijifanya kuwa amesahu kale kamsemo ka wema ni mfuko wa rambo, kwamba auhozi, “kwanimama yake semeji aliwafanya nini?” aliuliza Adija, ambae kiukweli, alijikuta anamchukia Seba, kwakufwata mkubo wa mume wake mtarajiwa, “wanadharau sana, awa washenzi, yani wanajifanya wao ndio wao, ata kipindi yupo huko dar, ndio tulikuwa atusemi” alisema George, ambae pia kama utakaanae mna kumwomba akueleze dharau na majidai ya Seba na mama yake, usingeweza kusikia ata moja, ata kidogo lenye ukweli.*****


Yap! wakati George ana panga yake, huku anasubiri ale ubwabwa toka kwa dada wakazi, ubwabwa, ambao kunamwanaume ameutafuta kwaajili ya familia yake, na yeye kupenyezewa na Adija, ikiwa ni sehemu ya maisha yake, huku nako nyumbani kwa Vanesa, Sebastian na Vanesa mwenyewe wenye nyumba yake, walikuwa wametulia kule kwenye sebule ya mwenye nyumba, wakiendelea kupata mvinyo taratibu, maongezi yakiwa ni mala moja moja, maana mawazo yao yalikuwa yamezama kwenye movie, lakini tayari kilevi kilikuwa kimeshaanza kuchukuwa nafasi vichwani mwao, Vanesa akiwa akijari kijigauni chake mbacho sasa kilikuwa inainuka kiasi cha kufikia eneo na karibu na shamba la bibi, wakati mwingine Sebastian aliweza kuona kitambaa kidogo chekundu kikiwa kimezuwia mbele ya eneo la shamba, kwamaana ni nguo aina ya bikini, iliyo valiwa na mwanadada huyu, ambae kiukweli nikama alibarikiwa sehemu hiyo ya kutafutia na kupatia watoto, maana Seba aliweza kuona mtuno wakitumbua, kama vile kichuguu cha mfinyanzi.


Huku safari za chooni zikiwa zimeshaanza kwa Vanesa, ambae uinukaji wake, ulikuwa ni mgumu sana kwa Sebastian, ambae kila Vanesa alipoinuka, alilazimika kuona vyombo vyandani, siyo kwamba Seba akuwa ameshikwa na aja, ila ukweli ni kwamba, kutokana na matamanio aliyokuwa nayo, yaliyosababishwa na Vanesa mwenyewe, na kufanya mnazi wake ushindwe kukaa sawa ndani ya kaptulah yake, nakufanya unyanyuke, kiasi cha kutaka kutoboa kaptulah yake.


Ilikuwa kimya macho kwenye TV, ila nawazi kila mmoja alikuwa anawazajambo jambo kichwani mwake, atujuwi ni lipi, “yani mwenzio niliporudi tu huku, nilikaa miezi minne tu nikaanza kufungua kampuni yangu, mwezi wa tano nikaja dar, nilipanga nifikie kwako, nilikuwa nimefwata vifaa vya mashine ya kuchakata arizeti, nakuzalisha mafuta, kuyafunga na kukuweka nembo, lakini ndio hivyo sikukupata” alisema Vanesa, huku anatazama kwenye paja ya Sebastian, ambae alikuwa analazimisha kukunja nne, yani mguu juu ya mguu, ilikuwa ni kwaajili ya mambo mambo mawili, moja mkojo ambao sasa ulikuwa umemfika shingoni, na pili ni msimamo wa mwiko wake, “niliamaga pale, nikaenda kukutana na mkosi” alisema Sebastian ambae alionekana wazi kuwa katika hali mbaya, “lakini uwezi juwa, pengine ilibidi tupitie kwanza magumu, iitujifunze, kabla ya kukutana tena” alisema Vanesa, ata mimi sijuwi alimaanisha nini.


Lakini wakati wanaendelea na maongezi yao, ndipo Vanesa akashindwa kujizuwia kuongea, “seba, mbona kama unaangaika, mkojo umekubana?” aliuliza Vanesa, huku akimtoa mkono Seba juu ya mapaja yake na kumvuta mguu pembeni, hapo nikama ndani ya kaptulah kulikuwa na nyoka, aliekuwa amebanwa, maana dudu ilifyetuka na kujikunjua, ikaaunua kaptulah, na kuwa kama mnara wa mawasiliano, jamani simpaka inauma sasa, ebu nikupeleke chooni, alisema Vanesa huku anainuka, kwauinukaji wake ule ule, ambao mudawote unamwingiza Seba kwenye shida.


Nae akainuka na kumfwata mwenyeji wake, ambae alimwongoza mpaka chooni, ambako walipofika mlangoni tu, Seba akaingia mwenyewe, na Vanesa akarudi sebuleni, nakuendelea kutazama filamu, huku Vanesa ambae kiukweli anaifahamu ile dudu, ambayo aliwai kuiona kwamacho yake mwenyewe, aliendelea kutazama filamu, akimsubiri mgeni wake atoke chooni, akiamini kuwa atarudi akiwa safi, yani dudu imepoa, huku wakato huo anawaza jinsi mwiko wa mwenyeji wako ulivyokuwa umesimama utazani hipo kwenye atua za mwisho, tayari kuingia kwenye chungu, “lakini inawezekana bwana, mbona alioa kwani huyo manamke aliwezaje” alisema Vanesa kwa sauti ya chini sana, sijuwi alikuwa anamaanisha nini.


Naam dakika mbili baadae Sebastian akaingia ndani ya Sebule, huku akiwa anaachia tabasamu flani, kama anaona noma flani, “naona sasa hupo fresh, nilikuambia uwe huru Seba” alisema Vanesa ambae pia aliachia tabasamu, huku anashusha macho kwenye kaptula, usawaa zip, ambapo alimwona mdudu akiwa amelala kwa kuja juu kitovuni, akionyesha wazi amebanwa kwanguvu, ili asinyayuke kwa juu, Vanesa anamwona Seba anakaachini haraka, lakini ukaajiwake unaonyesha wazi kuwa mwanaume huyu kunakitu kati yake kimebanwa, hapo pasipo kujiuliza anacho kifanya waa madhara ya kile anachokifanya, Vanesa alishika tishert ya Seba na kuipandisha juu, “jamaniiiiiii, kwanini sasaaaaaa” aliuliza Vanesa kwa sauti ya Mshangao, macho ametatoa kuelekea kwenye eneo la kitovu cha Seba.


Macho ya Vanesa, yaliweza kuona jinsi kijana huyu, alivyobana ibana dudu yake kwa mkanda, huku dudu ikichungulia kwa juu na kulala tumbo, sasa kwa jinsi ilivyo tutumka, unheweza kuona jinsi mishipa ilivyo chomoza pembeni ya dudu, mzizi wa mpingo, huku kitu kama kichwa cha koboko, kikiwa kime chaa usawa tumbo la kijana huyu, juu kidogo ya kitovu, “inasumbua” alisema Sebastian, huku anashika tishert na kulishusha haraka, “Seba jamani, sasa kwanini imekuwa, mbona ulikuja ikiwa vizuri tu?” aliuliza Vanesa kwa sauti yenye kujawa na huruma, huku analaza mkono wake kwenye paja la mgeni wake huyu, ambae ni leo ni mala ya pili wanakuwa pamoja, mala ya kwanza, ikiwa ni miaka mitatu iliyopita, “ata mimi mwenye nashangaa, aijawai kufanya hivi?” alisema Sebastian, huku anajiweka sawa, na kuchukuwa grass yake ya wine, “kwahiyo inakuwa hivyo sababu yangu, basi itakuwa imenitamani” alisema Vanesa, huku acheka kwa aibu, “itakuwa hivyo?” alijibu Seba nae akicheka kwa asibu kidogo, maana kuongea pumba mbele ya Vanesa ni kazi ngumu, “jamani Seba, sasa niifanyaje itulie?” aliuliza Vanesa kwa kisauti flani nyololo, kama cha kulalamka hivi, ungesema amepewa juku zito kulifanya.


Kwamaongezi yale Sebastian alijuwa fika kuwa, kunakoelekea, ni mwichi wake, kupewa ridhaa ya kutwanga kwenye kinu cha mrembo huyu, “mh! kwani we unazani utafanye Vanesa, niache tu nitamivulia” alizuga Sebastian huku akitamani kusikia neno zaidi toka wka Vanesa, “utawezaje kuvumilia kila siku, maana siutakaa hapa wakati unafanya kazi kwenye kampuni yangu mafuta” alisema Vanesa, huku anajaribu kupeleka mkono wake kwenye usawa wa mle ilimolala dudu, akiazia kwenye shina, na kupanda juu mapaka ilipoishia, usawa wa tumbo.


Kauri hii ilimpa furaha kubwa sana Sebastian, kusikia kuwa anapewakazi kwenye kampuni ya mwanadada huyu, ya kutengeneza mafuta ya alizeti, “kumbe unanipa kazi Vanesa, asante sana” alishukuru Sebastian, ambae huku akiusikilizia mkono wa dada huyu, ambao sasa, nikama aliona aitoshi, akaingiza ndani ya tisheti kwa chini, “ndiyo Seba, nimefurahi sana utakuwa jilani yangu” alisema Vanesa huku kiganja cha mkono wake kikilala juu ya kichwa cha koboko, na kikikmbata, nacho kinakutana na maji maji yanayo teleza, anakitoa haraka, “jamani Seba, inazidi kutamani, basi #NGOJA_NILEWE, alafu niifanya itulie” alisema Vanesa, huku anajifuta mkono wake kwenye gauni lake, na kuchukuwa wine, yake kisha akaiweka mdomoni, akimwacha Seba anashindwa kupiga kelele za kushangalia.


Naam wawili awa waliendelea kunywa wine, huku muda flani wakiongeza chupa zadi, pamoja na mipande ya kuku iliyokuwa kwenye oveni, kipindi hicho walikuwa wanaita kuku wa kuzunguka, nao walikula huku wanakunywa, na kuzidi kusogeleana kiasi kwamba ilifikia wakati akuna alie mwonea mwenzie aibu, maana ata walithubutu, kufanyiana michezo midogo midogo ya kimahaba, kama kuegemeana, kugusana sehemu shawishi, kama vile mapaja ata vifua, muda huu ndio muda mbao Vanesa aliutumia kumsimulia maisha yake kwakifupi.


Vanesa ambae ni mtoto wa mzee Danford, wazazi wake ni matajili wakubwa sana mjini Songea, ata Sebastian nae alikuwa anawafahamu matajiri hao, ambao siyo tu kumiliki magari aina ya land rover 110 yaliyofanya safari kwenye barabara ngumu za tunduru na ile ya kwenda mbinga, wakati huo azijawekwa lami, pia safari za mipaka ya msumbuji, kwenye machimbo ya dhahabu na sehemu zote mbazo barabara ilikuwa mbovu na ngumu kupitika kwa bus, pia wazazi wake walikuwa wanajiusisha na ununuaji mdomdogo wa dhahabu, kama ilivyofahamika, ila ukweli walikuwa wananunua dhahabu nyingi kwa bei ndogo, pia mzee huyu alikuwa anamiliki kiwanda cha sababu, na maduka makubwa ya nguo yaliyo simamiwa na mke wake, achana na mashamba na majumba ambayo aliyajenga ungesema anampango wa kuzaa watoto wengi, ila alibahatika kupata watoto watatu tu, wakike Vanesa akiwa ndie wakwanzana wadogo zake wawili, mmoja kiwa nchi Afrika ya kusini, alikoenda mwaka juzi kuchukuwa degree ya ufundi wa ujenzi, na mwingine ameondoka chini miezi miwili iliyopita, akiwa ameelekea nchini inia kusomea Ushirika na Mausiano ya kibiashara.


Ukweli nivigumu sana kuwafahamu watoto wa tajiri huyu, tofauti na wakina mzee Mahamud, ambao waliwaweka wazi sana watoto wao, huyu akuitaji watoto wake washindwe kuishi kwa uhuru, kutokana na utajiri wake, mfano huyu Vanesa, ambae licha ya kusoma vyuo vya kawaida, sasa licha yakumii nyumba hii anayoishi, akiwakama mmiliki wa kiwanda chake mwenyewe, pia alikuwa na majumba sehemu mbali mbali ya mji huu wa songea, huku akifanya kama wazazi wake, kwakununua mshamba huko Likalangilo pembeni ya mji kabisa, na kujijengea nyumba mbili, moja kuwa ikiwa nu kubwa kidogo, ambayo ilikuwa na wafanyakazi sita wa shamba ilo lenye mazao mbali mbali, pamoja na miti ya matunda, na mifugo, kila mfanyakazi akiwa anashugurika na kitengo chake, huku etar kama mia moja zikiwa ni za alizeti.


Nyumba nyingine ni ndogo nzuri, ambayo uitumia yeye mwenyewe, anapoamua kwenda kulala shambani, japo akuwa mpenzi wa kulala shambani, kama wazazi wake, toka amejenga nyumba ile yapata miaka miwili sasa, lakini alilala mala tatu tu, muda mwingi anakuwa mjini au safarini dar es salaam ambako alikuwa na tawi au kituo kikubwa cha kuuzia mafuta yake ya alizeti, maarufu sana, yanayoitwa V SUN OIL, akiwa amenunua nyumba mbili, moja mbezi na nyingine kibamba kwa mangi, zote akiwa amewaweka wafanyakazi wake, huku ile ya mbezi yenye ghorofa tatu, ghorofa ya tatu ikiwa ni makazi yake mwenyewe, wakati huo huo, alikuwa anamiliki ghara kubwa la kuifadhia mafuta, kule kibaha kwa mfipa.


“Mwenzio nilishawai kuwa na mwanaume, lakini niliachana nae” alisema Vanesa, ambae alisimulia kuwa alikuwa na mwanaume wake, wakati akiwa kidato cha tano, huku mwanaume wake, akiwa anasoma chuo kikuu cha mlimani, kilichotokea kati yao, ndicho kilicho sababisha yeye kupata matokeo mabovu ya kidato cha sita, yaliyo mkosesha alama za kwenda chuo kikuu cha mlimani, maana ilimlazimu kutumia pombe ili kuasahau maumivu aliyo pewa na mwanaume huyo, “mala kwa mala aliomba nimtumie ela, kumbe alikuwa anamwanamke mwingine, na fedha yangu alikuwa anatumia na mwamke wake, niliumia sana, na nilihapa nitaishi mwenyewe” lakini nilipokuona wewe na jinsi ulivyo mstaarabu, na siku ile nililala kwako kitanda kimoja, mpaka asubuhi, kitu ambacho ata Venance akuwai kulala nae hivyo, lakini wala ukutumia ulevi wangu kuniingilia” alisema Vanesa, huku anamtazama Sebastian kwa jicho laki pekee, “Venance amesha jaribu kuja kwangu kuomba turudiane, lakini nimekatalia, sitaki ata kumsikia mshenzi yule” alisema Vanesa, huku anachukuwa wine na kuinywa kidogo, kisha akaiweka chini.


Naam Vanesa anamtazama Sebastian kwajicho legevu, nae alikuwa anamtazama, wote wanatabasamuliana, “pole sana Vanesa, najuwa maumivu yake” alisema Sebastian kwa sauti tulivu, hapo Vanesa anazidisha tabasamu, “nilipoa sikuile asubuhi, nilipogundua kuwanimekutana na mwanaume anae niheshimu sana, mwenye utu na upendo, ilipelekea nikanunua nyumba Kibamba, nilizania itakuwa lahisi kukupata” alisema Vanesa, huku anajiegemeza kifuani kwa Sebastian, ambae kuna wakati alikuwa anajishtukia, pengine Vanesa angepatwa na arufu ya jasho lake, “kwahiyo ulikuwa unanitafuta sana?” aliuliza Sebastian ambae mambo yake huko duduni, yalikuwa ni zaidi ya hatari, “nazani ningekupata mapema, yasinge kukuta yaliyo kukuta” alisema Vanesa huku anajigeuza kidogo na kutazamana uso kwa uso na Sebastian, ile macho yao kutazamana kwa sekunde chache, kila mmoja ammoja akajikuta analegea, na kusogeza mdomo kwa mwenzie na ha kuanza kulambana midomo yao, kitendo ambacho kiliwasababishia waanze kupapasana viungo ya siri, ambayo vimetubatisa majina, ya kike na kiume.


Naaam dakika tano mbele, akuna kati yao aliekuwa amebakiwa na nguo mwilini, kwa hamu waliyokuwa nayo wote wawili, hakika sito weza kukusimulia, maana walicho kifanya, humo ndani, ndio maana Vanesa alimwondoa dada wakazi yani dada Shani, aende kusalimia, ili yeye apate nafasi ya kuwa na mwanaume aliekuwa anamuazia kila siku, huku Sebastian akiamini kuwa yupo kwendoto sawa na ile aliyoiota wakati ule chumbani kwa George, kabla ajavutwa mguu, na kutimuliwa, lakini ukweli siwezi kueleza kilieendelea mahari hapa, ambapo kama ungekuwa nje, usawa wa sebule hii, pale dirishani, basi ungesikia miguno na vilio vya raha kama vilivyosikika toka huko ndani.********


Wakati huo huo, nyumba inayofwata, pale kwakina George, geroge ambae alikuwa makini sana, kutazama dirishani, ilikuhakikisha kama atamwona Sebastian, akitoka upande ule wa nyumba ya Vanesa, na kuondoka zake, lakini mpaka giza linaanza kuingia, zaidi ya kumwona Shani, ambae alipita akiwa amebeba begi dogo mkononi, akumwona mtu mwingine akitoka kwenye geti la jumba lile, wakati huo Adija alikuwa amesha enda nyumbani, maana maboss wake lazima wangerudi leo ijumaa, kama ilivyo kawaida yao, “huyu ni kweli ameajiliwa kama house girl (house boy) ndio maana yule dada ameondoka, dah! kweli huyu ni mbwa kachoka, toka kwenye uboss mpaka mfanyakazi wa ndani” alisema George, ambae kutokana na hakiri yake fupi na dhana potofu, aliona kuwa mwanaume awezi kufanya kazi za ndani, aliona vyema kuwa kama yeye, anaeishi kwa sahani ya ubwa bwa anayo yafuta mwanaume mwenzie.


Naam saa moja ikaingia, giza likatanda, lakini bado George akumwona Sebastian akitoka kwa Vanesa, “yani kesho lazima wajuwe kama unafanya kazi yandani, wewe siutaki watu wajuwe kilicho kukuta” alisema George, huku anachukuwa peni na karatasi, na kuanza kuandika barua kwa mama yake, barua iliyokuwa inauliza kama Sebaamesha fika kijijini, au la, ilikesho akaikabidhi kwenye magari ya kwao, huku akisisitiza majibu. ********


Yap! nyumbani kwa Vanesa, paligeuka bustani ya Adeni, maana wawili awa licha ya kumaliza kupeana dudu kwa mitindo mbali mbali, lakini awakurudisha nguo zao kwenye miili yao, kwahiyo walibakia kama walivyo zaliwa, ata chooni walipelekana, na kusubiriana, milango yote ilikuwa imefungwa, akuna ambae angevumilia kila pale dudu ilipoonekana imesimama, lazima ingeingizwa kitumbuani, mwendo ulikuwa popote wakati wowote, ingetokea bafuni sebule kubwa au jikoni wao twende kazini, ungesema wametoka jela leo leo, kwajinsi walivyo shambuliana, ata muda wakulala walilala kule sebuleni, na na kuamka asubuhi, wakiwa wamechoka, huku kila mmoja akimwonea mwenzie aibu.


Lakini aibu aikudumu kwa muda mrefu, wakajikuta wakienda kuoga pamoja chumbani kwa Vanesa, na huko wakajikuta wakipeana tena, sasa ikiwa live live, kwamaana  kila mmoja akiwa anajitambua, na kutambua kile anacho kifanya, walifurahia sana, kiasi cha kujikuta wakiamishia mchezo kwenye kitanda kikubwa cha mle chumbani, wakikumbushia ile mitindo ya jana, waliyo ifanya wakiwa wamelewa, japo walishambulia kwa kiwango kilicho karibiana na kile cha jana, kwahiyo ni kweli mapenzi uchizi, “mpenzi, sijuwi hatima ya penzi letu, lakini mimi sijisikii kuachana na wewe” alisema Vanesa, wakati wakiwa wamemaliza kunyanduana, na kuoga, “kwangu uwa sinaga kujaribu mapenzi, alafu sizani kama niaujasiri wa kuusaliti moyo wangu ambao umekupenda sana” aljibu Sebastian huku wanafutana maji miilini mwao kwakutumia matauro mazuri, “alafu Seba mwenzio ninawazo, unaonaje week ijayo ukasalimie mama yako, bila shaka atakuwa na asi wasi juu yake, siulizema auja mwona muda mrefu sasa” aliema Vanesa, “ni kweli ni muhimu, ila wacha kwanza nipate kazi, nipate mshara ata wa mwezi mmoja ndipo niende kumwona” alisema Sebastian, lakini Vanesa akukubaliana nae, “hapana bwana, tutaenda ijumaa, tunashinda jumamosi jumapili tunageuka, tukae na mama week end yote, au atatukata kulala chumba kimoja” alitania Vanesa, wote wakacheka.


Ukweli wazo ilo lilikuwa zuri sana, maana Sebastian alikuwa ajawasiliana na mama yake muda mrefu zaidi ya kumpelekea zile zawadi, “ni sawa, lakini kampuni itabidi iniazime fedha kidogo, ili niweze kujiandaa kwa safari hiyo, nitarudisha kwenye mshahara wangu” alisema Sebastian, na hapo Vanesa akamgeukia Seba, na kumtazama kwa macho yenye kuchukia, lakini kwa kudeka, “inamaana mimiindie nilie panga safari, kwani ni wewe, sasa mimi ndio nita gharmia safari hiyo pamoja na kula kitu, mpaka zawadi za mama na watu wengine” alisema Vanesa, kama vile anatoa amri flani, iliyojaa deko na mahaba mazito.


Naaaam siku hiyo walishinda pamoja, wakifanya kila kitu pamoja, walisaidiana kupika kuosha vyombo, na kunywa wine, ata baadae Vanesa akapiga simu dukani kwa mama yake na kuagiza wamletee jozi kadhaa za nguo na viatu, ikiwa ni zakila aina, zote za kiume, mashati suruali nguo za ndani, kaptulah, bukta na matishert.


Lisaa limoja baadae tayari nguo, viatu na mikanda vilikuwa vimesha letwa, na Sebastian akavijaribu, hakika vilimpendeza, ata Vanesa akasema “umerudi kwenye ubora wako” ukweli japo ngozi ya mwili wake ilikuwa katika hali ya mpauko, lakini alipendeza sana, nautofauti kati ya jana na leo ulionekana, sababu leo alikuwa amepaka mafuta mazuri, ata ngozi aikuonyesha kupauka sana, japo ilikuwa bado aija nga’aa.


Maisha matamu ya liendelea mpaka siku ya jumapili, wawili awa ungesema wapo kwenye fungate, kwajinsi walivyo gusa kila idara ya mapenzi yao, ata alipofika Shani, wao walikuwa wakijifungia kwenye sebule yandani, huku Vanesa akifwata huduma ndogo ndogo walizo itaji, “Shani ulikuwa unaniuliza kwanini siolewi, sasa huyu hapa, ndie alie nifanya nisiolewe kwaajili ya kumsubiri, nilisha wai kukusimulia habari zake” alisema Vanesa akimtambulisha Seba kwa Shani, ikiwa pamoja na kumsisitiza asiwe mwepesi wa kutoa habari za mle ndani.********


Geroge akiwa chumbani jumapili hii, akiwa amesha peleka barua kijijini kuulizia habari za Seba, leo jumapili alipata majibu kuwa Seba akuwa amefika kijijini Namabengo, yani mama yake amekosa amani baada ya kusikia kuwa mtoto wake amefukuzwa kazi, na amadhurumiwa kila kitu, sehemu ya barua ilisema hivyo, hapo George alizidi kuumiza kichwa, asa baada kuona mwanamke ambae anammezea mate akiwa amesha rudi, wakati anahisi kuwa Sebastian yupo mle ndani na aenda kufanya kazi na mwanamke huyu, “nayule alivyo nabahati, anaweza kumchukuwa yule demu” aliwaza Seba ambae kiukweli siku zote za week end uwa ngumu kwake, maana upata mlo mmoja tu kwa siku, vinginevyo atunze chakula anacholetewa usiku, kwaajili ya kunywea chai asubuhi, vingenevyo ni usiku kwa usiku, maana Adija anashindwa kumletea chakula, sababu maboss wake wapo, labda nyakati za usiku, ambapo wanakuwa wamelala, ndipo Adija uiba chakula kwenye bakuri na kukipeleka getoni kwa George, ambae angemkuta anahesabu ambao za kenchi.


Jumatatu ilifika, Sebastian aliongozana na Vanesa mpaka ofisini, ambako alikabidhiwa ofisi yake, kama msimamizi msaidizi wa uzalishaji, akiadiwa kuwa, alipewa nafasi hiyo kama sehemu ya mafunzo, ili siku zijazo awe msimamizi mkuu, nae akaanza kazi mala moja akipokea maelekezo kwa msimamizi mkuu, mida ya chai na chakula cha mchana waliongozana na Vanesa, kwenda kula, aikuishia hapo siku ya ahl khamis, Vanesa alimpeleka Seba nyumbani kwao bomba mbili, mida ya jioni, kwakuwa walisha toa taarifa, ya ujio wa mgeni, maandalizi makubwa yalifanyika, nao wakapokelewa vizuri.


Vanesa alimtambulisha Sebastian ambae ni wazi alisha wapa habari zake, toka mwanzo, yani kuhusu kipindi kile alipo msaidia, na pia kuhusu kilicho mtokea, mpaka kupoteza kazi yake, mwisho Vanesa akawaomba wazazi wamluhusu Sebastian amuoe, wazazi nao awakuwa na mambo mengi, waka toa angalizo lao, kwamba wanaitaji taratibu zifanyike, na Sebastian akamtambulishe binti yao kwa mama yake, na mwisho wao pia wakutane na mama yake Sebastian, ili wafahamiane katika kuunganisha familia zao.


Ilikuwa ni fulaha kubwa sana kwa Sebastian na Vanesa, ambao toka siku ile wakaanza kufanya maandalizi ya kwenda kijijini, kwa mama yake Sebastian, wakati huo Sebastian alishaanza kunawilina kupendeza, huku ngozi ya mwili wake, ikizidi kungaa na kuwa na afya njema, sasa alianza kusahau maumuvu ya zamani, japo akuweza kusahau kilichotokea.********


Kitu ambacho Vanesa na Sebastian walikuwa awakijuwi ni kwamba, tayari George alisha kutana na Shani, akimulizia uwepo wa Seba nyumbani kwao, “jamaa yangu anaendeleaje hapo kwenu” aliuliza George, alipokutana na Shani aliekuwa anaenda dukani, “jamaa yako gani?” aliuliza Shani kwa mshangao, “Sebastiam yule jamaa ulie mwita…” kabla ata ajamaliza kueleza, tayari Shani alikuwa amesha mwelewa George, “hoooo yupo anaendelea vizuri, kumbe ni ndugu yako?” alisema Shani akionyesha kuwa mchangamfu, “ndiyo ni mtoto wa mama yangu mdogo, ata hapa alikuwa anaishi kwangu” alisema George, ambae alikuwa na malengo ya maswali yake, “kwani hapo nyumbani kwenu anafanya kazi gani?” aliuliza George, akipnyesha wazi ajuwi lolore kuhusu ndugu yake, na hapo ndipo shani alipokumbuka onyo la boss wake, kwamba astoe habari za nyumbani kwao, “we juwa yupo kwtu basi inatosha” alisema Shani, huku anaanza kutembea kuelekea dukani, “vipi naweza kuja kumchek?” aliuliza George ambae alikuwa na hamu ya kumwona jamaa yake anavyo angaika kazi ndani, au kufyeka nyasi kwenye jumba la Vanesa, “ukienda tu utaitiwa mwizi” alisema Shani, huku anaendelea kutembea.


George ambae kiukweli akuwaza, wala kujiuliza, kwanini anazuiliwa kuingia mle ndani, alijipa uhakika wa kuwa ndugu yake yupo mle ndani, na anafanya kazi za ndani kuweza kufukuri kuwa kijana mwenzie, anapika kwenye chungu ambacho yeye ajawai kuota, “huyu mshenzi ameanza kutembea na Shani nini, mbona shani amekuwa mkali ghafla hivi, dalili ya wivu ilimshika George, alihisi moyo unamchoma vibaya sana, “ngoja kwanza nika likoroge mpaka mama yake afunge safari kuja kumtoa hapa” alisema Geroge ambae licha ya miaka yake kukaribia ishilini na nane, lakini hakilizake zilikuwa ndogo kama za panzi.


Toka jumatatu siku ambayo Geroge alikutana na Shani, kijana huyu alianza kuangaika kusaka ela ya usafiri, huku siku zote licha yakujuwa kuwa Sebastian yupo kwenye nyumba ya Vanesa, lakini akuwai kubahatika kumwona, siku ya ijumaa, Geroge alifanikiwa kupata shilingi mia nne, toka kwa Adija, ikiwa ni matokea ya kubana na kupunguza fedha za matumizi kiasi cha shilingi elfu moja, alizoachiwa na boss wake, na ijumaa hiyo hiyo mchana sebastian akaondoka kuelekea Namabengo, akiwa na nauri yake ya kurudia, huku kichwani mwake akiwa amepanga vizuri mpango wake, kwamba akamvuluge mama Seba, mpaka afunge safari yakuja mjini, kujamchukuwa kijana wake.


Saa tisa jioni, ndio muda ambao Geroge alifika nyumbani kwa mama yake, kijiji namabengo, , wamasukana huku wanaongea ili nalile, “baba huyooooo” mama George alimkpokea kijana wake, ambae akuwa na mzigo mwingine, zaidi ya mfuko wa rambo, wenye nguo chache, ambazo angetumia mpaka jumatatu, siku ambayo alipanga kurudi mjini, “jamani kaka yani ata zawad kidogo” alisema Joyce mdogo wake wamwisho, aliekuwa anatokea ndani, akiongozana na Ester, dada yake, “yani afadhari ata kaka Seba, juzi ametuma nguo nzuriiii” alisema Ester, ilimgusa kidogo George, na hivi ndiyo moja ya vitu ambavyo avipendi, unamwulizia zawadi, wakati yeye mwenyewe chakula chake anategemea kiibwe kwenye nyumba ya watu, “weweee! acha kunifananisha na house girl” alisema George kwa dharau, kiasi kwamba wale wakina mama waliokuwepo pale uwanjani, wakashangaa na kumtazama George, wakitamani kumwuliza kama anauhakika na kile anachosema, “we! Geroge hivi una uhakika na unachokisema?” aliuliza mama George, kwasauti ya kujifanya ameshtuka, na kuudhunika, kumbe alikuwa nataka Geroge aongee pale pale mbele ya wale wakina mama, ili habari zisambae kwa haraka, sasa je, mimi nilimshauri arudi kijijini, yeye akaniona mjinga hivi sasa anaosha mivyombo kwenye nyumba ya watu” alisema George, kwa sauti yenye uhakika na anacho kisema, “jamani yule kijana wa mama Seba ndie mnae mzungumzia?” aliuliza mama nyoni, kwa sauti yenye masikitiko.


Hapo ndipo George akaona ndiyo nafasi ya kumwaga hadithi yake, “huyo huyo, tena anafanyia kazi karibu kabisa na ninapo kaa, yani anavyo pelekeshwa anatia aibu” alisema George, safari hii akuendelea kusimama, ila aliingia ndani na mfuko wake wa rambo, akiacha wakina mama wanajadiri swala lile kwa sauti za masikitiko, “jamani yule mtoto alikuwa anamsaidia sana mama yake” alisema mmoja huku mingineakidakia, “sijuwi atakuwaje mama Seba” wote walionyesha kusikika, ata mama George pia alionyesha kuumizwa, japo moyoni mwake, alikuwa anachekelea, kwa aanguko la Sebastian, “angalau alimjengea ile nyumba nzuri na kumfungulia duka” alisema mwingine na hii ilimkela mama George, japo akuonyesha usoni, lakini alichangia neno, “mh! mngemuona alivyonyongea, yani huyu mtoto ujinga wake umemtesa sana mama yake” alisema mama George, na hapo wakina mama wengine wakaitaji habari kamili, “kwani imekuwaje mpaka akafukuzwa kazi, na sasa anafanya kazi za ndani?” aliuliza mmoja kati ya wakina mama wale, “kuna kingine basi, ni pombe bangi na wanawake” alisema mama George, na wote wakatazamana kwa mshangao, “weee! Usiniambie, kumbe kisa ni ujinga wake” alisema mmoja wao.


Ukweli wakina mama wale, walianza kuona kuwa Seba alikuwa ni mjinga sana, na kwamba alikuwa wanamsikitikia bule, wakati kilicho mkuta ni haki yake, waliongea mengi ya kumsimanga kijana huyu, huku George aliekuwa ndani akiwasikiliza wanakina mama hao, ambao awakujuwa kama wanafwata mkumbo usio wahusu.

Mida ya saa moja kasoro, mama Geroge na wenzake, wakiwa wamesha maliza kusukana, waliongozana moja kwa moja kwa mama Seba, ambae walimkuta yupo dukani, anaendelea kuhudumiawateja wake kwa msaada wa taa yake ya chemri, “hooo dada! Karibu jamani, ndio maana niliona jicho linacheza sana, kumbe ni kwaajili ya ugeni huu” asema mama Seba, huku anawatazama wakinamama wale kwa macho ya tahadhari, maana aikuwai kutokea wao kumtembelea namnaile, “asante mama Seba, kwanza pole sana, nasikia seba…” kabla mama mmoja kati yawale walio ongozana na dada yake mama George, ajasema lolote, mala wakashtuka wakimulikwa na mwanga wataa zagari, lililokuwa lina kuja upande ule, lakini wakaona kama lilikuwa na fari zake nyingine, “jamani kuna nini mbona mnanitisha, eti dada kunanini kimetokea, au ni zile habari za george kufukuzwa kazi?” aliuliza mama Seba ambae alionekana kuingiwa na wasi wasi, “sasa unaambiwa mwanao ana fanyakazi ya kuosha vyombo, kwenye majumba ya watu” alisema mama George, kwa sauti ya kubedha, huku anatazama pembeni, wakati huo gari lilikuwa linazidi kusogea upande waliokuwepo.


Baada ya kusikia hivyo, hapo mama Seba anashusha pumzi kidogo, “kumbe ni hivyo tu, wala akuna shida, ni afadhari apate fedha kwa nguvu yako, kunavijana wapo mjini na awana kazi yoyote” alisema mama Seba, kwa sauti yenye uafadhari, hapo wakina mama wakatazama kwa mshangao, “kweli mama Seba umepatikana, kwahiyo kusoma kote kule, ndio kusie kwenye kuosha vyombo, aliuliza mama George, na wale wengine wakacheka, ukweli mama seba alishangaa sana, inamaana dada yake smewabeba wenzake kuja kumsimanga, “dada kumbuka seba huyo huyo ndie alie mpangia mwanao chumba kule mjini na kumnunulia kila kitu, kumbuka seba alikuwa anajitaidi kuwanunulia zawadi na kutatuashida zenu, pale mnapo muomba msaada, leo hii, unakuja kunisanifu namna hii” alisema mama Seba kwa sauti yenye masikitiko, huku anamtazama dada yake, ambae toka utotoni alikuwa anapenda kuonekana bora kuliko mwenzie, “ilikuwa enzi hizo, sasa atamsaidia nani, au yeye ndie anae itaji msaada wetu, kwataarifa yako Geroge ndie alimwifadhi kabla aja pata kazi ya kuosha vyombo hapo hapo jilani yake” alisema mama George, kwa sauti yenye nyodo za hali ya juu, na wakati huo huo wakaliona gari lile likikata kona kuja pale nyumbani.


Wote wakageuka kutazama linakotokea lile gari, kila mmoja akiwa na swali lake kichwani, alilitazama lile gari mpaka lilipokuja kusimama mbele ya nyumba ya mama Seba, ambae pia alikuwa anajiuliza huyu mgeni ni nani, swali ambalo kila mmoja alijiuliza, ata hivyo jibu lake awakuchelewa ulipata, asa ni pale gari, lililposimama tu, akashuka Sebastian akiwa mwingi wa tabasamu, na kuilipua furaha ya mama yake, huku wale wakina mama wengine wakiacha kumtazama Seba, ambae ukimtazama uwezi amini kama alikuwa ametoka kwenye mkasa mkubwa wakufukuzwa kazi, nakupoteza kila kitu,nikuanzia mavazi na mwonekano wa afya ya ngozi yake, ukiambiwa ametoka mjini kweli unasema ametoka mjini, na ni mfanya kazi, nao wakamtazama mama George, ambae alikuwa ametazama chini, “shiamoni wakina mama” alisamia Sebastian, na wale wakina mama wakaitikia kwasauti za wagonjwa, huku shingozao zimeelekezwa pembeni, kwa aibu, kitu ambacho licha ya kukiona na kukigundua, lakini Seba akukijari, na kujifanya kama ajakiona.


Wakati mama Seba alitoka nje ya duka, na kumfwata mwanae akamkumbatia, “mwanangu umeudi salama, karibu nyumbani kikubwa uzima” alisema mama Seba, kisha akamwachia Sena na kumshika mkono kijana wake, majilani huyu ndie Seba tulie kuwa tuna mzungumzia, kama anacho kifanya ni kwajasho lake, sina wasi wasi nae” alisema mama Seba, kisha akataka kumwongoza Seba kuingia ndani, lakini Seba akamzuia, “mama nimekuja na mchumba wangu” alisema Seba kwa sauti ya kunong’ona, “we mtoto sasa kwanini unashuka mwenyewe, na kumwacha mkwe wangu ndani ya gari” alipaza sauti ya furaha mama Seba, huku anafwata mlango wa abiria wambele, na kuufungua, huku akitarajia kumwona Adellah, akiwa amebeba mtoto.


Hapo mama Seba anashikwa na mshangao, baada ya kumwona mwanamke mrembo, kupita kiasi, ambae anashuka haraka toka kwenye gari, na kupiga goti moja huku anasalimia, “shikamoo mama” alisamilia mwanamke huyu mrembo, “marahaba mwanangu karibu ndani” alisema mama Seba, huku wale wakina mama wakikodoa macho, kumtazama mwanamke yule rembo, ambae pia aliwasalimia kwa kupiga nusu goti, nao wakaitikia kwa macho ya kujisuta, “mama Seba sisitunaenda, waliaga wale wakina mama wengine, kasoro mama mkubwa peke yake, “mama mkubwa waambie wakina Joyce kesho wake kuchukuwa zawadi zao” alisema Sebastian, baada ya kuona mama mkubwa anaondoka zake, wakati huo mama Seba akiwa amesimama pembeni karibu na mkwe wake mpya, akitabasamulia pembeni.


Naam mama seba Seba na Vanesa, walisaidiana kushusha mizigo na kuingiza ndani, kisha akaa na mama yake, na kumtambulisha Vanesa kwa mama yake, kama chmba wake, huku akimsimulia kilichotokea, kati yake na Adellah, akumficha chochote, ila pia akuacha kueleza chanz cha kufahamiana na Vanesa miaka mitatu iliyopita, “karibu sana mwanangu, nawaombea muishi vizuri, msiingie tena katika matatizo, kwanza nimefurahi sana, kuona kuwa mmependa toka moyoni” alisema mama Sebastian ambae alisimulia jinsi alivyoletewa taarifa za kufukuzwa kwake kazi, taarifa ambazo mama George alikuwa anazisimulia kama taarifa za burudani kwake, zenye kupendeza zinapomtoka mdomoni, “yani ata awa mliowakuta hapa walikuwa wananisimanga, kwani ukuona jinsi walivyo shushuka?” alieleza mama Seba, na wote wawili yani Seba na Vanesa wakakili kuona jambo ilo, kwa wale wakina mama, “ndio maana mama mkubwa aliondoka bila kuaga kama wenzake” alisema Sebasbastian, kwa sauti ya mshangao, huku akimweleza mama yake jinsi mapokezi ya George yalivyokuwa juu yake.


Waliongea mengi na mwisho wakapanga wakakubariana kuwa, kilichotokea kimekuwa funzo kwao, na nikosa kubwa sana kurudia kosa, ata kama nidogo. *******


Kama kunasiku George alijihisi aibu ya mwaka, basi nisiku ya ijumaa hii, maana alipo ambiwa kuwa, Sebastian amekuja na mchumba wake, naaonyeshi kama amefukuzwa kazi, nae akaenda mpaka kwa kina Seba, yani kwa mama yake mdogo, japo alisimama mbali, lakini aliweza kumwona Seba akiwa na Vanesa, tena Sebastian alionekana kubadirika kimavazi na kimwonekano, ilimshangaaza saba George, ambae alishindwa kumaliza usiku ule pale kijijini, na kuamua kuondoka zake, kuelekea barabara kuu, ambako alipata usafiri wamagari yanayotoka wilaya ya tunduru, kuelekea songea mjini.


Ata kulipokucha akuna alie juwa George, ameelekea wapi, lakini wadogo zake walienda nyumbani kwa mama yao mdogo, yani mama Seba na kumsaidia kupika vyakula vuzuri kwaajili ya wageni, ambao ni wakina Seba na Vanesa, ambao walijumuika nao pamoja, na jioni wakaenda kwao wakiwa na zawadi zao, walizo bebewa nakaka yao Sebastian.


Jumapili jioni, Vanesa na Seba walirudi mjini, kwaajili yakazi jumatatu, maisha yalikuwa mazuri yenye furaha na amani, japo yalichukuwa furaha ya George na mama yake, huku bwana George akishinda ndani, amekosa amani kabisa, ata alipo fwatilia habari za Seba, na kugundua kuwa, siyo tu kumpata Vanesa, pia amepewa kazi, tena katika nafasi nzuri, hapo ndio alijikuta anachanganyikiwa kabisa.


Nambaya zaidi kila siku ziivyozidi kusonga mbele, ndivyo Seba alivyo zidi kuwa bora zaidi, na kuzidi kueewana nwatu wengine, kitendo kilichozidi kumuumiza George, ambae sasa alikuwa anamwina Seba kwambali tu, akiwa anapita na gari pamoja na mke wake, ilimuuma zaidi wakati Sebaliponunua gari dogo aina ya toyota merk 2.********


Siku miezi ikapita, ikatimia miezi sita toka Seba na Vanesa wawe wapenzi, jumamosi moja ndani ya jiji la dar, Sophia ambae sasa alikuwa anampeleka mume wake Philipo anavyo taka akashauliwa kwenda kumtembelea Adelah, ambae sasa alikuwa na miezi kama minne ajawatembelea, mshauri akiwa ni bwana Philipo, Sophia akajibeba, na kuelekea Kimara, akujiuliza kwanini mume wake ameshauri kitukama hicho, maana aliondokamida ya saa tatu asubuhi.


Sophia alipofika kule alimkuta mdogo wake mzima, lakini afya yake ikiwa imeporomoka vibaya sana, amechoka atamaniki ata kidogo, usoni kovu kama nguo ya kuchomea mkaa, inavyojaa viraka, Adellah, ndiyo kupenda gani huko jamani, yani unamakovu namnahii na bado una ng’ang’ania mwanaume, utajuta kumfanyia vile Sebastian, alisema Sophia huku wakati Daniel mwenyewe anasikia, “kama huyo fala nimzuri sana siaende kwake” alisema Daniel, kwa sauti iliyojaa jeuri, “Adellah, ebu chukuwa nguo zake chache na watoto, twende ukakae kwangu, mpaka upate nafuu” alisema Sophia, ambae alimsimamia mdogo wake akiwachukuwa nguo zake, kisha wakandoka zao, “sijuwi Philipo alishtuka nini, hivi unajuwa yeye ndie alie nisisitiza nije kukuona” alisema Adellah, huku wakiwa kwenye daladala wanalekea chanika, hii iliwashangaza wote wawili mambao kila mmoja alikuwa amekaa na mtoto mmoja, jibu laswali ilo walilipata baada ya kufika chanika


Kwanza kabisa wanapitia dukani wanakuta duka limefungwa, “nilijuwa, tu huyu mshenzi aliniambia nije kwako aende kwa mahawara zake, sasa leo ata nitambua, anakuta virago vyake nje, akuchangia ata shilingi moja, kupatika hizimali” alisema Sophia kwa hasira, huku wanaongoza njia ya nyumbani, ambako angetegemea kukuta watoto, lakini anakuta mlango umefungwa, Ile anataka kuwa tafuta watoto, mala anaitwa na dada wajilani yao, ambae alikuwa ame shikilia fuko la shangazi kaja, “mumeo amechukuwa vitu vyote, amesma yeye amesha tangulia kule mnako amia, wewe uende na begi lako ili hapa” kusikia hivyo Sophia na Adellah wakaanza kuangua kilio cha mwaka, wakijaza watu maali pale, “jamani nimeibiwa, mume wangu weeeee, yalikuwa nimambo ya kusameheana jamani, kwanini umenifanyia hivi jamani” alilia Sophia, sasa watoto nao wakaanza kuwasaidia kulia, walijaza watu kwa masaa matatu, ata wakapata wazo la kurudi kimala kule kwa Adellah, ambako walimwacha Daniel, pasipo kujuwa kuwa walikuwa wamechelewa, 


Maana ile wanafika pale wanakuta watu ndio wanatawanyika, kutoka kwenye mnada wavutu vyote vyandani vilivyo kuwa vimebakia, maana vingine vilisha uzwa toka zamani, leo aliuliza aya nguo za Adellah, ambazo alikuwa amezibakiza, na mteja wa mwisho, alipewa opunguzo la kumalizia kodi ya chumba kwa miezi mitatu iliyokuwaimebakia.


Mpaka hapo wakina Adellah walijiona kuwa wenye mikosi, hivyo wakachukuwa uamuzi kwa kwenda kibamba chama, kwa jenifer, dada ambae alimpokea Sophia kwa mala ya kwanza alipokuja dar.


Dada yule ambae alikuwa anafanya kazi kama mhudumu katika bar moja kubwa ya panama, pale kibamba chama, akawapokea na kuanza kuishi nao huku Sophia akijipatia kazi panama, na Adellah akipata elfu mbili za kuanzishabiashara ya kuuza ndizi kwenye sinia, mida ya jioni, ili aweze kuwalisha watoto wake.******** 


Huku Songea nako mambo yalikuwa simchezo, Sebastian alizidi kunawili, huku akikabidhiwa tena nyumba yake ya kibamba kwamangi, maana ndiyo nyumba ambayo Vanesa aliinunua kwaajili ya wafanyakazi wake, na sasa wafanyakazi aliwanunulia nyumba nyingine, mala kwa mala Seba na mke wake walikuwa wanafanya safari za Dar es salaam kukagua mauzo, na mwenendo wa biashara, tayari Vanesa alikuwa mjamzito, kitu kilichopelekea wakimbize taratibu za kufunga ndoa.


Siku moja ikiwani siku ya jumamosi, siku ambayo, kama kawaida maboss wa Adija wanakuwa nyumbani, George ambae alisha kubari yaishe kuhusu maisha ya Seba, ambae akujiusisha nae, huku na yeye akiona aibu kumsogelea ndugu yake japo alimtamani, George akiwa amesinda na njaa kutwa nzima, mida ya saa tatu usiku, Adija aliingia ndani ya chumba cha George, akiwa na bakuri lililojaa chakula, George akalipokea na kuanza kupiga mchapuo mmoja mkubwa, ambalo alliweka mdomoni, na kulimeza, kitendo kilicho fwata ni kelele za ghafla, ambazo zipigwa na kijana huyu, “maaaaaa nakufaaaaaaa, Adja unaniuwaaaaaaa” alipiga kelele George, huku anatafuta maji, ya kunywa, ata alipoyapata, na kuyanywa, lakini aikusaidia kupunguza uchungu nkubwa ulio kuwepo kwenye chakula kile, “mamaweeeeee Adija umeniwekea nini” alilia George, kama mtoto mdogo, mdomo wazi, uchungu mkubwa na mkali ulijaa mdomoni, koo lake lilikuwa linawaka moto, kwa kitu kikali kama pili pili, hukuulimi na midomo yake ikihisi uchungu kali, zaidi ya mchunga au shubiri, Adija alimpatia kikopo cha sukari ambacho kilikuwana sukari kidogo, aliyo ibakiza Seba.


ITAENDELEA...

Post a Comment

0Comments

Your Thoughts

Post a Comment (0)